Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Be serious mkuu hao wanawake wenye maadili zama hizi mnawatoa wapi labda muumbe wa kwenu, wangekuwepo basi kusingekuwa na malalamiko ya wanaume kila siku, kwamba wanawake wanawaigizia kwenye uchumba halafu kwenye ndoa wanafungua makucha yao halisi

Unajua tofauti yangu mimi na wewe mimi naongelea reality wewe unaongelea fantasies, wanaume bado mko kwenye zile ndoto za kupata wanawake decent na full package mnaowataka mnasahau hakuna binadamu mkamilifu, kama ninyi mmeshindwa kuwa na maadili basi msitegemee hilo kwa wanawake wa sasa

Fuatilia hali halisi iliyopo kwa vizazi vya sasa kuanzia Gen X na Gen Alpha halafu fuatilia viongozi wa dunia wanachotabiri kuhusu vizazi vijavyo, ndio utapata picha halisi ya wapi tunaelekea inasikitisha kwamba kuna wanaume ambao bado mnaziota enzi za babu zetu, mnatakiwa kuamka kutoka kwenye huo usingizi na kukubaliana na ukweli uliopo kwenye dunia ya sasa acheni kujifariji kwamba tunaumia
We jua tu kuwa to each her own and to each his own. Kila m'moja atapata wa kufanana nae. Wewe kwa hizi kauli zako inaonyesha wazi umezungukwa na role models wenye past relationships trauma na toxic mindset kwenye ndoa.

Ni ngumu kwa church girl kuwa around company ya hood rats sababu hawaendani kimaadili.

Wanawake wenye discipline wapo, so am sorry to bust your bubble.
 
Aah mkuu why nitume picha siyo zangu Are you sure?, and why useme uliona tu siyo picha zangu inamaana ulikua na picha yako kichwani ama? Sawa watu tuna mapungufu but lawama zingine mtupunguzie jamani [emoji2296]

Factor ya uchumi haijawahi kuwa kikwazo kwangu as long as tunapendana, pesa zinatafutwa tu. Kuna watu walianza zero pamoja now wako somewhere.
Mmmmmmhmn miaka hii ni ngumu sana mwanamke kuishi nae kama kipato ni cha wasi wasi sishauri kuishi na mwanamke kama mambo yako hayapo sawa.
 
nakuomba sana mtu akija kwako kwa nia nzuri usimpuuze, nina uhakika umetukosa wengi tuliokuwa na nia nzuri na wewe, ila wengi wetu umetukatisha tamaa kabla hata hatujatangaza nia, ule wakati wa kujiona wewe ndio wewe ushakutupa mkono, kwa sasa kwenye suala la mahusiano fana kama unabeti tu waweza kushinda bingo ujishangae
Mmmmmmhmn bro mbona umekaza statement hivi au unataka kupiga kijanja?
 
Haya sio maoni mazuri. Nyie ndio mnawaponza wanawake wanaingia kwenye mfumo wa hovyo wa maisha halafu wakiwa wanalalamika wanasema wanaume ndio wametushauri kumbe sio wanaume wanaojitambua.
30's mdada huna mtoto binafsi nawaona mko katika risk sana.

Huna Mpenzi hilo its okay,Umeshindwa jipambania ukapata mtoto? Taa nyekundu iwake kichwani mwako.

Ugumba/Utasa vipo wala sio hadithi za kusimulika. Ila make sure unapata myu sahihi wa kukupa Mtoto.

Acheni kuwaza kuhusu Mapenzi sana,kuna muda ufike muwaze kuhusu familia na familia sio Mume tu Familia ni Wewe na Mwanao/wanao.

Mume anaweza kukuacha anytime ila mtoto ndio familia yako,shida mnawazaga sana kuhus Mume, na bado mnachagua sana na mnaishia kupata macheck bob wanawaumiza na no mimba. Badilikeni.

30's usi relax upo hatarini labda kama Plan zako ni kuwa na mtoto Mmoja its Okay.

ila kama ni zaidi ya mmoja 30's alarm ishaanza kulia ...
We umeona wapi au kwa mafundisho ya kitamu au mila za wapi familia ikaanza na mama na mtoto, wewe umefundishwa na nani huo uhuni?

Hebu msiwe mnatoa maoni yenu binafsi katika kujibia hoja za msingi.
 
Sasa ujuaji unahusiana nini na mwanamke kuwa na wanaume watano, mwanamke siku zote hajui ni nani atakayemuoa kwa sababu ndoa haamui yeye sasa unataka awe na mwanaume mmoja huyo asipomuoa je, bora awe na zaidi ili asipoolewa na huyu anaweza akaolewa na yule je ni wanawake wangapi wanakuwa na mwanaume mmoja na bado hawaolewi wanaachwa vile vile
Ndio maana watu wanalala na kuwaacha unaendelea kuwa cha wote hadi uzee unakuvaa.
 
Hayo ya burudani kwa wote ni mawazo mliyoyatengeneza vichwani mwenu tu, kwani unaweza kunijibu mwanamke akiwa na mwanaume mmoja anafaidika nini, na akiwa na zaidi anapungukiwa nini physically
Dah aisee we mtu sijui umelelewa na kukuzwa na nani ila unasikitisha sana MUNGU akusaidie hii akili chafu isiwe serious uwe tu unaongea hapa kufurahisha jukwaa.
 
Ungekuwa serious usingeandika haya uliyo andika hapa. Ila kwakuwa haupo serious wacha nikwambie machache ambayo yatakusaidia.

Unahisi wewe na hao wenzako ambao mnahisi mnashindana na wanaume mnamkoa nani zaidi ya kuteseka na kuishi kwa huzuni na upweke?

Wanaume hawalalamiki sababu hii kitu inawatesa wao ila ni huruma juu yenu wenyewe na pia kutazama ustawi wa jamii.

The worst that is yet to happen kwa jamii ya mwafrika ni yale yale yanayotokea mataifa ya kimagharibi huko (am not sure if unajua au kufuatilia kinachoendelea mataifa ya magharibi kwa sasa).

Furaha yako ni illusion uliyobeba kichwani ukidhani kila mtu anajali au upo entitled kupewa au kuona unachokitaka.

Sasa wewe ukizeeka ukachoka na ukawa na fatherless kids mimi kama mwanaume inanizuia nini kutafuta mwanamke younger than you ambaye hana mtoto tukaanzisha familia ?

Au wewe kuwa na kazi ambayo mapato yake hayatanisaidia tukiishi pamoja ina tofauti gani na nikiwa bila wewe?

The point is mkiharibu hii jamii kwa viburi, ego, utoto na uzembe wenu hasara itaanza watafuna ninyi kwanza.

Nakwambia hivi kwasababu mkilea watoto bila baba wakiwa majambazi nani atakuwa kwenye risk kubwa ya kushambuliwa kati ya mwanaume na mwanamke, si unakumbuka "Panya Road" habari yake, nani walikuwa wanakabwa kila uchao?

Haya tuje makahaba na Wadangaji, hawa watoto wa sasa hivi wa mwaka 2000 tu tazama wanavyovamia wanaume za watu rika za babu zao, nani ana athirika hapo si ninyi wanawake maana vibinti vinawazidi kete, dada wa mwakan1980 utakompete kimvuto na binti wa mwaka 2000 shughuli yake utaiweza?

Haya kulea watoto bila mwanaume, kodi, matunzo, gharama za utility ndani ya nyumba, zote utazibeba na bado mtoto akikua anasepa utabaki pekee yako nani aliyekwambia hiyo inamuathiri mwanaume kuliko mwanamke?

Upweke wa maisha bila mwenza wa maisha ni kichochezi kikubwa cha magonjwa ya akili na afya ya mwili kama kisukari, stroke, kiharusi kwa wanawake miaka hii, ulizia data za wataalamu ujifunze acha kuleta petty arguments hapa.

Wanawake single ndio mnaoongoza kurubuniwa na wanasiasa na kuchagua viongozi wa hovyo na hii inaathiri sana maendeleo ya jamii in the long run, fuatilia utajionea hizi tafiti zipo na zinasema ukweli?

Madhara ni mengi kuliko faida ila sababu unahisi ni ujanja kushindana, then "continue to Fuuck around then you will find out".
Kumbe kuwa single mothers ni kitu mnachagua kwa hiyari yenu sasa mbona kwenye vyombo vya habari mkihojiwa huwa mnasema wanawake wananyanyasika sababu wanaume wanawapa mimba kisha kuwatelekeza?

Unajua inabidi muwe specific badungu? [emoji23][emoji23][emoji23]

Hii statement yako itakuja kukuhukumu siku moja.
We jua tu kuwa to each her own and to each his own. Kila m'moja atapata wa kufanana nae. Wewe kwa hizi kauli zako inaonyesha wazi umezungukwa na role models wenye past relationships trauma na toxic mindset kwenye ndoa.

Ni ngumu kwa church girl kuwa around company ya hood rats sababu hawaendani kimaadili.

Wanawake wenye discipline wapo, so am sorry to bust your bubble.
Mkuu kwanza kabisa futa hiyo kauli kuwa wanaume wanalalamika kwa sababu ya kuwahurumia wanawake futa kabisa, HAKUNA mwanaume anayefanya jambo kwenye mahusiano kwa maslahi ya mwanamke narudia HAYUPO acheni kuwadanganya wanawake kwenye hili, ukiona mwanaume analalamikia jambo kwenye mahusiano ujue linamuumiza yeye ila ni vile tu huwa mnatumia kitu kinaitwa self serving reverse psychology trick ili ionekane kama vile mnawasaidia wanawake ili wafanye mnachotaka

Tuanze kwanza na hili kama mngekuwa mnawahurumia wanawake basi mngekuwa mmeshaacha kuwatongoza kwa lengo la kuwachezea lakini kwa bahati mbaya mkiambiwa hivi mnakimbilia kusema, "oo mwanaume hawezi kujizuia mwanamke akitongozwa ndiye anatakiwa akatae sababu yeye ndiye anayeumia zaidi" kitendo cha kutoa hiyo kauli maana yake hamna huruma kwa wanawake, kwa sababu kama ninyi mmeshindwa kujizuia mnategemea mwanamke aweze vipi kwani yeye ameumbwa na kitu gani special cha kumfanya ajizuie na majaribu na vishawishi kwani naye si binadamu

Tukija kwenye suala la ndoa waliosusa ndoa ni wanaume na siyo wanawake maana vinara wa campaign ya kataa ndoa ni wanaume na lengo la wao kufanya hivyo siyo kwamba hawataki ndoa kweli, ila wanataka eti kuwakomoa wanawake ili wajirudi wawe wife materials ndio waolewe sababu wanajua wanawake wako desperate na ndoa hivyo wako tayari kufanya chochote ili waolewe sasa mimi ndio nawaambia kwamba hao walikuwa ni wanawake wa zamani, hawa wa siku hizi mkiwasusia ndoa hawahangaiki bali nao wanatafuta namna ya kuwa na furaha bila ndoa na kama ni pesa siku hizi mbona wanawake wengi tu wanajitafutia pesa wanachangamkia fursa kwenye kazi na biashara au unaishi sayari gani mkuu

Kama ni upweke na matatizo ya akili haviwapati wanawake tu tena wanaume wakikosa wanawake ndio wanakuwa wapweke kuliko wanawake wakikosa wanaume na tukiangalia uhalisia wanaume ndio wanaihitaji sana ndoa kuliko wanawake, ila hawataki kuadmit kama nilivyosema wanatumia self serving reverse psychology trick ili kufanya ndoa ionekane ni muhimu kwa wanawake tu, ila ukiuliza huo umuhimu ni upi hasa ambao kwa mwanaume haupo hakuna jibu la maana utapewa lakini tukija kwenye uhalisia kisaikolojia wanaume ndio wanaihitaji sana ndoa kuliko wanawake

Ni kwa sababu wanaume huwa mnaitafuta furaha kwa wanawake na siyo kwa watu wengine au kwenye vitu vingine tofauti na wanawake ambao wao wanaweza kupata furaha toka kwa watu wengine kama watoto na vitu vingine kama pesa, ndio maana kwenye ndoa mke akizingua tu kidogo mwanaume anavurugwa akili na ni ngumu kumvumilia na kusamehe badala yake atatafuta furaha kwa mchepuko ambaye naye pia ni mwanamke, wakati mwanaume akizingua ni rahisi mwanamke kumvumilia na kusamehe na atatafuta furaha kwa watoto wake na watu wengine wa karibu au kazi au biashara yake

Wewe hujawahi kusikia huu msemo kwamba mwanaume kadiri anavyozidi kupata pesa ndivyo anavyozidi kutaka kuwa na wanawake wengi ila mwanamke anavyozidi kupata pesa ndivyo anavyozidi kutaka kujiweka mbali na wanaume, mkuu kwenye mahusiano au ndoa wanaume ndio mnapenda kupetiwa kubembelezwa na kauli kama "pole na uchovu mpenzi" sijui "karibu chakula mume wangu" na huwa mnategemea kuzipata toka kwa wanawake tu, na kuna wanaume seriously kabisa wanachepuka kisa tu hawapati romantic gestures kama hizo toka kwa wake zao wakati wanawake mara nyingi huwa hawajali kuhusu hizo gestures

Sasa unaposema kwamba utazalisha mwanamke halafu utamuacha awe single mother kisha utaoa binti mbichi una uhakika gani huyo binti ndio atakuwa decent na hatakusaliti unataka kuniambia wanaume wote wazee waliooa vibinti wanafurahia ndoa zao kuliko waliooa single mothers, na kama mnajua kuwa wanawake decent wapo sasa mbona malalamiko ni mengi kwamba siku hizi wanawake wameharibika si muwaoe hao hao wanawake mnaowaona decent ujue mkuu ifike mahali wanaume muache kuishi kwenye fantasies mje kwenye reality, mkubaliane na ukweli kwamba wanawake hawatarudi tena enzi za bibi zetu na huko tunakoelekea hali ndio itakuwa mbaya zaidi acheni kujifariji it is either ninyi ndio mkubali kucompromise au muendelee kulalamika hadi mwisho wa dahari
 
Ndio maana watu wanalala na kuwaacha unaendelea kuwa cha wote hadi uzee unakuvaa.
Dah aisee we mtu sijui umelelewa na kukuzwa na nani ila unasikitisha sana MUNGU akusaidie hii akili chafu isiwe serious uwe tu unaongea hapa kufurahisha jukwaa.
Si kila ninachojadili humu basi maana yake mimi nakifanya au kimenitokea mimi naandika hali halisi iliyopo kwenye jamii sitoi maoni yangu binafsi kama ninyi, mimi naongelea reality siongelei fantasies sawa jamii imeharibika so what anayelalamika ni nani ni mwanaume au mwanamke, kama wanawake ndio wanaoumia zaidi kwanini wengi wameacha kulalamika badala yake wanaume ndio mmepokea microphone na ninyi sasa ndio mmeanza kuchana mistari ya malalamiko so what next then..
 
Back
Top Bottom