Je, umewahi kubadili mtazamo juu ya kitu fulani ambapo hapo awali uliuamini sana? Kwanini?

Je, umewahi kubadili mtazamo juu ya kitu fulani ambapo hapo awali uliuamini sana? Kwanini?

Hizi varieties za races kwa binadamu zilitokea wapi ikiwa kwa mujibu wa Biblia ni watu wawili tu (Adam na Hawa) ndio walioumbwa?
🤣Atakuambia mnara wa babel watu walichanganywa lugha wakasambaa dunia nzima...🤣au baada ya Noah's flood. Inategemea anasoma chapter gani
 
Embu nisaidie hili swali mkuu kwa mujibu wa sayansi.
Ni ipi asili ya mwanadamu?
Unataka asili ipi ya kipindi binadamu tumekuwa binadamu au kipindi tulikuwa tunashare ancestors na sokwe au kipindi hamna binadamu wala sokwe bali wakina komba au kipindi hamna mamalia kuna chura tuu au kipindi cha wazee wetu walikua samaki au twende kabisa kipindi maisha duniani yalikuwa unicellular?
 
Nadhani utakuwa umeshamjibu yule aliye uliza kuhusu Mungu hayupo kwa sababu haonekani.
Milango yetu ya fahamu ina limit macho hayawezi kuona kila kitu, masikio hayawezi sikia kila kitu n.k vipi sasa kutaka kuyalazimisha macho mpaka yamuone Mungu ndio useme yupo??
Hasira, Woga, Akili ni vitu vipo iwe kwa dhana ya kufikirika kama unavyodai lakini vipo na hatujawahi kuviona why sasa tuseme vipo? Mngeitimisha tu havipo Kama mnavyoitimisha kuwa Mungu hayupo.
Mungu hayupo katika uhalisia.

Yupo kwa kufikirika.

Mungu ni dhana ya kufikirika.

Na wewe umesha jijibu kwamba Mungu hayupo kwenye uhalisia ila ni mawazo yako tu ya kufikirika.
 
🤣Atakuambia mnara wa babel watu walichanganywa lugha wakasambaa dunia nzima...🤣au baada ya Noah's flood. Inategemea anasoma chapter gani
Ndio namsubiri hapa anipe hiyo logic yake tuijadili hapa
 
The same hoja yako pia haionyeshi Mungu hayupo kwani ili Mungu awepo ni lazima atoe mali kwa watu wote?
Haya chukulia ndio katoa kwakuwa umeamua kupinga uwepo wake bado ungesema hizo mali watu wote wametafuta kwa juhudi zao.
Hapa ni vizuri kuelewa kuwa jitihada hazizidi kudra, Mungu ndio mmiliki wa hali zote, zote kwa maana ya zote na yeye ndio aliyesema tokeni mkatafute riziki hapa ndio watu huchanganya mambo wengi hudhani kuwa rizki ni mali tu, Kumbe rizki ni mjumuisho wa mambo mengi kama elimu,Afya,mali, n.k
Ndio maana utakuta mtu ana elimu lakini hana mali mungine ana mali lakini hana afya, Sasa usichukulie Mungu anagawa mali tu uka hitimisha kwa kuwa watu wengine hawana mali basi hayupo my friend logic ya wapi hiyo ? Mungu kuwa muweza wa yote na mwenye upendo wote sio sasa ndio watu wasife, ndio watu wawe na mali wote n.k, Yeye anabaki kuwa muweza wa yote tu hata kama wewe hauna mali, hata kama mtoto wako kafa kwenye ajali n.k
Alafu maswali yote hayo Mungu mwenyewe kashayajibu kwenye vitabu vya dini kuwa Yeye ndie Mola wa ulimwengu, Ametuumba wanadamu ili tuishi katika hii dunia na akatupa akili ili tuitumie kudhibiti matamanio yetu hivyo tumuamini yeye na kumuabudu, baada ya hayo ndio kuna maisha ya umilele na furaha kwa waliotumia akili zao vyema kumuabudu Mungu na hapo ndio hayo maswali yako yanapojibika kwa urahisi kuwa.. Baada ya kukuumba na kukuweka duniani kisha ukafa sasa unaenda kuishi tena katika umilele huko hakuna hizo ajali unazolalamikia huku duniani, Huko kuna mali unazoziangaikia huku duniani.
Mungu kashajibu maswali kwenye vitabu vya dini vinavyo tofautiana maelezo na mitazamo?

Yani kwenye kitabu cha dini hii anasema hivi, kwenye kitabu cha dini nyingine anasema kingine?

Yani anaji changanya changanya mwenyewe, Hana msimamo.

Ni Mungu gani huyo?
 
Mungu kashajibu maswali kwenye vitabu vya dini vinavyo tofautiana maelezo na mitazamo?

Yani kwenye kitabu cha dini hii anasema hivi, kwenye kitabu cha dini nyingine anasema kingine?

Yani anaji changanya changanya mwenyewe, Hana msimamo.

Ni Mungu gani huyo?
🤣Kila dini inasema Mungu wake kajibu maswali ambayo Sayansi haiwezi jibu
 
🤣Kila dini inasema Mungu wake kajibu maswali ambayo Sayansi haiwezi jibu
Dini imefeli kwa miaka mingi sana, mpaka sayansi ilipokuwa kuleta majibu mengi kwa binadamu.

Dini ni Psychotherapy kwa watu wengi, inawapa pleasure of illusion.

Mtu akitaka ku avoid uhalisia basi dini ndio kitulizo.
 
Niliamnini sana, tena sana ukristu, baada ya kugundua ni biashara nimesepa na kuingia katika imani yangu ya asili. Hakika Mungu wa kweli anapatikana kupitia imani ya jadi. Mfalme Costantine alipokea ukristu ili apige biashara.
 
Dini imefeli kwa miaka mingi sana, mpaka sayansi ilipokuwa kuleta majibu mengi kwa binadamu.

Dini ni Psychotherapy kwa watu wengi, inawapa pleasure of illusion.

Mtu akitaka ku avoid uhalisia basi dini ndio kitulizo.
🤣Ukiwaambia watakuambia tu angalia miti afu jibu ilipotoka..ukisema hujui..bac we ndo mjinga, ye anajua. Ni Allah au Yahweh au yesu
 
Mungu hayupo katika uhalisia.

Yupo kwa kufikirika.

Mungu ni dhana ya kufikirika.

Na wewe umesha jijibu kwamba Mungu hayupo kwenye uhalisia ila ni mawazo yako tu ya kufikirika.
Mimi sijasema Mungu hayupo.. wewe ndio umesema usinisingizie mkuu.
 
Mungu kashajibu maswali kwenye vitabu vya dini vinavyo tofautiana maelezo na mitazamo?

Yani kwenye kitabu cha dini hii anasema hivi, kwenye kitabu cha dini nyingine anasema kingine?

Yani anaji changanya changanya mwenyewe, Hana msimamo.

Ni Mungu gani huyo?
Kitabu gani hicho Mungu anasema tusimuabudu.?
Mada hapa ni uwepo wa Mungu na hakuna kitabu kinachopinga uwepo wa mungu.
Kama unataka mambo ya utofauti wa vitabu vya dini hiyo ni mada nyingine ambayo wewe itakuwa haikuhusu kwa sababu wewe haukubali uwepo wake, Hizo tofauti inabidi wajadili waislamu, wakristo na wayahudi wanaoamini katika Mungu.
 
Unataka asili ipi ya kipindi binadamu tumekuwa binadamu au kipindi tulikuwa tunashare ancestors na sokwe au kipindi hamna binadamu wala sokwe bali wakina komba au kipindi hamna mamalia kuna chura tuu au kipindi cha wazee wetu walikua samaki au twende kabisa kipindi maisha duniani yalikuwa unicellular?
Asili ya mwanadamu yaani where we come from?? I.e what is our origin ? Kitu gani huelewi apo?
 
Mimi sijasema Mungu hayupo.. wewe ndio umesema usinisingizie mkuu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Una hofia kuchomwa moto, ukisema kwamba Mungu hayupo.

Anyway hukatazwi kuwa na imani yako, ila ukianza kusema imani yako ina ukweli tutabishana sana.

Kila mtu abaki na mtazamo wake.
 
Hizi varieties za races kwa binadamu zilitokea wapi ikiwa kwa mujibu wa Biblia ni watu wawili tu (Adam na Hawa) ndio walioumbwa?
Nikuongezee tu sio biblia tu imesema Mungu Kaumba Adam na hawa ata Qur an ya waislamu na talmud za wayahudi zote zinasema Mungu aliumba adam na hawa tu.
Sasa nije kwenye swali lako ilikuwaje kukawa na hizi varieties za races ... Adam na Hawa waliishi mashariki ya kati na walipata watoto wakazaliana sana tu. Lakini Hapa watu wote walikuwa ni wa race moja ya Adamu Lakini watoto wa Adamu walisambaa sana kuna walioenda kuishi palestina wengine iraq na Iran wengine maeneo ya sham na maeneo mengine kumbuka hapa watu wote Ni race moja lakini washatawanyika hivyo mazingira ndio yaliyo sababisha hizo races zikazaliwa kwasababu mazingira yanaweza kumshape mwanadamu na mazingira yanaleta athari kwa mwanadamu mfano mtu anayeishi maeneo ya baridi ni tofauti na anayeishi maeneo ya joto nywele zao na rangi lazima zitofautiane hivi ndiyo races zilivyoanza.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Una hofia kuchomwa moto, ukisema kwamba Mungu hayupo.

Anyway hukatazwi kuwa na imani yako, ila ukianza kusema imani yako ina ukweli tutabishana sana.

Kila mtu abaki na mtazamo wake.
Sio nahofia nitachomwa ni hakika ukisema Mungu hayupo utachomwa.
Ok wacha tukubaliane kutokukubaliana.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Una hofia kuchomwa moto, ukisema kwamba Mungu hayupo.

Anyway hukatazwi kuwa na imani yako, ila ukianza kusema imani yako ina ukweli tutabishana sana.

Kila mtu abaki na mtazamo wake.
Sio nahofia nitachomwa ni hakika ukisema Mungu hayupo utachomwa.
Ok wacha tukubaliane kutokukubaliana
 
🤣Atakuambia mnara wa babel watu walichanganywa lugha wakasambaa dunia nzima...🤣au baada ya Noah's flood. Inategemea anasoma chapter gani
Kumbe unajua habari ya mnara wa Babeli na Safina ya Noah inaonekana unapenda kusoma maandiko, Jitahidi mkuu kuna za Mussa na farao, Daudi na Goliathi alafu kuna ya huyo Muhammad Hapo Makka very educative and interesting vipi nikutumie pdf usomesome kuongeza ufahamu??
 
Back
Top Bottom