Je, ungependa nini kiwemo kwenye Katiba Mpya? Mimi napendekeza Ruzuku ya Vyama vya Siasa iondolewe!

Dira ya taifa na mambo yote ya kipaumbele kwa nchi na watu wake vitamkwe wazi wazi kwenye katiba. Vyama vya siasa wakati wa uchaguzi, vijinadi jinsi ya kutekeleza vipaombele hivyo vilivyo ndani ya katiba badala ya kila chama kuwa na ilani ya uchaguzi.
 
Asante, namba moja ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa. Hata wanunuapo bidhaa pia walipe kodi kama wananchi wengine.
Namba 9 nayo ni muhimu sana, tumekwisha toka kwenye serikali 3 hatuwezi kurudi nyuma, sasa iwe serikali moja.
 
posho za wabunge zikatwe kodi
 
Naongeza kidogo;
1. Viongozi wa Mashirika ya umma wafanyiwe "public vetting" ili wachaguliwe kutokana na uwezo wao unaoendana na taaluma aliyosomea na hitaji la shirika lenyewe.
2. Viongozi wa Mihimili yoote wawe wanachaguliwa kwa kupigiwa kura siyo kuteuliwa na Rais. Jaji Mkuu akiteuliwa na Raisi basi sheria lazima itapindishwa. Na iwe marufuku Jaji Mkuu kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
3. Hata Spika wa Bunge si lazima atoke chama Tawala, kuwepo utaratibu wa kumpata spika ambye hahusiki n chama chochote cha siasa.
4. Wakuu wa Mikoa wawe wanagombea nafasi na wapigiwe kura Mikoani mwao hali kadhalika wakuu wa Wilaya.
5. Wakurugenzi wa Mikoa na Wilaya wapitie public vetting, wachaguliwe kwa uwezo na asiwe mfuasi wa chama chochote cha siasa.


...... huenda nitaendelea
 
Ni vyema ukashukuru kwa neema ya Akili uliyopewa na Mola wako ndugu yangu yohana, hivi kweli mbali na chama chako kupora, kufuja na kutapanya mali za umma kwa kigezo Cha "chama cha Mapinduzi" bado unaweza kuwa na hasadi kwa vyama vichanga ndani ya karne hii ya domo cratia? Viwanja lukuki vya mipira, maeneo ya wazi , majengo ya umma, fadha kutoka kwa mifuko ya umma bado unawaonea gere wanyonge? Ikowapi mantiki ya wazee wetu kupigania uhuru wa Taifa hili? Kwakweli hii Inakuwa kama laana umeni disappoint bwana John
 
Kambaya atuhumiwa kujenga ghorofa kwa Fedha za Ruzuku!

Niishie hapo
 
1. Mawaziri wasiwe wanateuliwa na rais bali ziwe za kuomba, ili kila wizara iwe na waziri ambaye ana fani husika, kama ni wizara ya Kilimo iwe na waziri pamoja naibu wake ni wataalam wa kilimo hivyo hivyo wizara ya afya, uvuvi, Ulinzi na Usalama.

2. Kiongozi aliye madarakani au amestaafu akiwa amefanya makosa pawe na uwezekano wa kuwajibishwa na kushitakiwa.

3. Ardhi isiwe mali ya serikali bali raia wawe na mamlaka na ardhi ikitokea mwekekezaji, huyo mwekekezaji ataelewana malipo na mwenye ardhi ambaye ni raia.
4. Bidhaa za zinazotoka Zanzibar kuja Tanzania bara au zinazotoka Tanzania bara kwenda Zanzibar zisitozwe kodi hata bidhaa za matumizi ya nyumbani kutoka Zanzibar ushuru uondolewe.
5. Wabunge wa bunge la jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mishahara yao ipungue na posho zao pia, haiwezekani Daktari aliyesomea fani yake miaka saba au wanajeshi wanaolinda nchi kwa jasho, damu na uhai wanazidiwa mishahara na wabunge wengi wao elimu ya la saba au form four.
Pia watozwe kodi kama raia wengine kwenye nchi hii, haiwezekani muuza nyanya atozwe mbunge asikatwe kodi.
 
Idadi ya wizara isizidi 15
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…