Je, wajua Djibouti walivunja mkataba na DP-World?

Je, wajua Djibouti walivunja mkataba na DP-World?

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Haya mijadala inaendelea kuhusu uwekezaji wa bandari, hoja nyingi zikitolewa kutokana na masharti ya mkataba huo ambao unaonekana utaathiri uchumi wa Tanzania badala ya kuuendeleza.

Kampuni ya Dubai inayosimamia bandari Zaidi ya 78 katika nchi 40 duniani imekuwa na kashfa kadhaa za ukwepaji kodi na rushwa. Mwaka 2008, Kampuni ya DP World ambayo ni kampuni ya tatu kwa ukubwa katika kampuni zinazoendesha bandari duniani iliingia Mkataba na Jamhuri ya Djibout wa miaka thelathini (30) kuendesha bandari ya Dorahel (Dorahel Container Terminal-DCT).

M
waka 2014, kulitokea mgogoro kutokana na madai kwamba Kampuni ilitoa rushwa kwa mkuu wa Mamlaka ya Bandari wa wakati huo na hivyo kusababisha kuwepo Mkataba wenye masharti yanayoipendelea Kampuni ya DP World.

Serikali ya Djibout kwa kuona kuwa Mkataba huo ni tishio kwa mamlaka ya nchi (sovereignty of the state) na tishio kwa uchumi wa nchi (economic independence), iliamua mnamo tarehe 22 Februari, 2018 kuvunja huo Mkataba na kuichukua bandari ya Djibout.

Kampuni hiyo ilifungua kesi kudai fidia ya dola milioni 148 kupitia usuluhishi dhidi ya Jamhuri ya Djibouti baada ya mzozo huo.
 
Hizi mishe aliwezaga Magu tu, wengine wakisikia sauti ya mweupe tu wanakunja mikia ka nyau chotara!
Hata alifeli, Mimi nawapongeza wasiasa wa mlengo wa kushoto(wapinzani). Wako Vizuri, japo ni sahihi, anayeona ndo anayeweza kukosoa ufanisi wa anayefanya, issue wamwambie nae FANYA, atabolonga panaposhangaza
 
IMG-20220725-WA0016.jpg
Mzilankende, Chuma, Jiwe, Ngosha
 
Hata alifeli, Mimi nawapongeza wasiasa wa mlengo wa kushoto(wapinzani). Wako Vizuri, japo ni sahihi, anayeona ndo anayeweza kukosoa ufanisi wa anayefanya, issue wamwambie nae FANYA, atabolonga panaposhangaza
Kwa hiyo tumwachie anayeharibu aendelee kuharibu???!!!!
 
Huyu Rais hatufai hata kidogo.

Anatuingiza kwenye matatizo makubwa sana kila siku kuna jipya kubwa zaidi.

A very incompetent president toka tumepata uhuru.
Halafu anauza Tanganyika tu
 
magufuli alisema tutamkumbuka, aisee naona kama tumeanza kumkumbuka. hivi kweli unampa mtu bandari ya dsm ambayo imeshajengwa na unampa kama karanga tu, badala ya kumwambia aende akajenge bandari yake pale bagamoyo? na ipo wazi kabisa dubai wanaishika hii ili wachina wasihamishie mizigo yao Bagamoyo toka dubai? tumelala usingizi? au kwasababu baadhi ya watu wana undugu na waarabu?
 
Hii Kampuni siyo kongwe, haina zaidi ya miaka 18.
Ni kampuni ambayo serikali ya Dubai ndiyo yenye hisa nyingi, sasa mbona sisi hapa akili zetu ni kuuza tu kila tulicho nacho na kusema serikali isijihusishe na lolote, bali awaachie wengine kila jambo?

Kama hawa waarabu wanaweza kuwa na kampuni yenye ufansi kiasi hicho, kwa nini nasi tusiwe 'inspired' tujifunze wanachokifanya kwa ufanisi ili nasi tukifanye?

Sisi inaelekea tunachoweza pekee sasa hivi ni kutegemea tu watu watoke nje waje watufanyie sisi kwa gharama kubwa. Sisi tunajitoa kabisa kwamba hizi kazi hatuziwezi, kwa nini?

Nirudi kwenye swali nililouliza kwenye kichwa cha mada: Hawa DP World, bado wapo Kwenye ile bandari ya Djibouti (Doraleh Container Terminal) au hawapo? Kama hawapo, ni nini kiliwatokea huko?
Je wakati sisi tunawatafuta kwa udi na ubani, tumejiridhisha na baadhi ya mifano juu ya kazi zao wanazozifanya takribani kwenye nchi kama kumi hivi? Hapo Rwanda, jirani napo wapo, tumewatembelea hapo na kuona kazi zao zinavyokwenda na kujiridhisha?

Lakini yote kwa yote, hii mikataba ya kuingia kama watu tusiokuwa na akili kichwani ni ujinga wa hali ya juu sana.
 
Wewe jiulize kwanza nikikuachia biashara uiendeshe na mimi nikasafiri miaka 3
Je nikirudi ntaikuta imekua na umeajiri watu zaidi au utakuwa umeiba na kujenga nyumba zako?

Sisi ndio tuko hivyo, ukipata nafasi unaona ni mali yako
Wenzetu CEO yuko Dubai au Geneva na kazi zinafanyika nchi 150 na faida zinasoma

Sasa niambie wewe fungua duka moja Dar mpe mtu na lingine Moro mpe mtu uone
 
Hii ni sawa na inaweza kuwa mfano wa Zimbabwe Gold Mafia. Kwenyewe tunaona jinsi matapeli wa kimataifa wanavyojipenyeza na kuwashawishi viongozi wa kitaifa kufanya nao dili. Dili kama hizi, hazianzi hivi hivi. Ndio maana utaona vocal person kama Msukum, walipelekwa Dubai ili kuzibwa midomo. Kwa ufupi, kuna hidden agenda ya kufaidisha wachache kwa kisingizio cha kukusanya mapato.
View attachment 2650651
 
Wewe jiulize kwanza nikikuachia biashara uiendeshe na mimi nikasafiri miaka 3
Je nikirudi ntaikuta imekua na umeajiri watu zaidi au utakuwa umeiba na kujenga nyumba zako?

Sisi ndio tuko hivyo, ukipata nafasi unaona ni mali yako
Wenzetu CEO yuko Dubai au Geneva na kazi zinafanyika nchi 150 na faida zinasoma

Sasa niambie wewe fungua duka moja Dar mpe mtu na lingine Moro mpe mtu uone
Zitaje hizo nchi 150 hata 5 na faida zake tuzijue!!¡??
 
Hii Kampuni siyo kongwe, haina zaidi ya miaka 18.
Ni kampuni ambayo serikali ya Dubai ndiyo yenye hisa nyingi, sasa mbona sisi hapa akili zetu ni kuuza tu kila tulicho nacho na kusema serikali isijihusishe na lolote, bali awaachie wengine kila jambo?

Kama hawa waarabu wanaweza kuwa na kampuni yenye ufansi kiasi hicho, kwa nini nasi tusiwe 'inspired' tujifunze wanachokifanya kwa ufanisi ili nasi tukifanye?

Sisi inaelekea tunachoweza pekee sasa hivi ni kutegemea tu watu watoke nje waje watufanyie sisi kwa gharama kubwa. Sisi tunajitoa kabisa kwamba hizi kazi hatuziwezi, kwa nini?

Nirudi kwenye swali nililouliza kwenye kichwa cha mada: Hawa DP World, bado wapo Kwenye ile bandari ya Djibouti (Doraleh Container Terminal) au hawapo? Kama hawapo, ni nini kiliwatokea huko?
Je wakati sisi tunawatafuta kwa udi na ubani, tumejiridhisha na baadhi ya mifano juu ya kazi zao wanazozifanya takribani kwenye nchi kama kumi hivi? Hapo Rwanda, jirani napo wapo, tumewatembelea hapo na kuona kazi zao zinavyokwenda na kujiridhisha?

Lakini yote kwa yote, hii mikataba ya kuingia kama watu tusiokuwa na akili kichwani ni ujinga wa hali ya juu sana.
Jibu ni moja sisi wabongo ni wezi wezi wezi mpaka tunajiibia wenyewe hatuna trust na honest kwenye biashara, ndo maana tunashindwa kuendesha hata mradi mdogo kama wa masi muendo kasi, unasuasua ineja sikendo nyingi sana.
 
Jibu ni moja sisi wabongo ni wezi wezi wezi mpaka tunajiibia wenyewe hatuna trust na honest kwenye biashara, ndo maana tunashindwa kuendesha hata mradi mdogo kama wa masi muendo kasi, unasuasua ineja sikendo nyingi sana.
Hata kama tukiwa wezi, lakini hatuwezi kuwapa waarabu sehemu ya bandari yetu kwa terms za kijinga kama zile halafu tunyamaze tu, huo ni upumbavu.

Kwanza inakuwaje mnakuwa na wezi halafu mnashindwa kuwashughulikia? hii kitu niite nini?

Mnamaanisha tumekuwa na wezi mpaka tumeshindwa kuwafanya chochote? sasa tunawaogopa tumeamua kabisa kuwaacha watufanyie chochote watakacho?

Bora mkoloni arudi tu.
 
Wewe jiulize kwanza nikikuachia biashara uiendeshe na mimi nikasafiri miaka 3
Je nikirudi ntaikuta imekua na umeajiri watu zaidi au utakuwa umeiba na kujenga nyumba zako?

Sisi ndio tuko hivyo, ukipata nafasi unaona ni mali yako
Wenzetu CEO yuko Dubai au Geneva na kazi zinafanyika nchi 150 na faida zinasoma

Sasa niambie wewe fungua duka moja Dar mpe mtu na lingine Moro mpe mtu uone
Umeongea jambo la akili sana
Mwenye akili ataelimika hapo
 
Hata kama tukiwa wezi, lakini hatuwezi kuwapa waarabu sehemu ya bandari yetu kwa terms za kijinga kama zile halafu tunyamaze tu, huo ni upumbavu.

Kwanza inakuwaje mnakuwa na wezi halafu mnashindwa kuwashughulikia? hii kitu niite nini?

Mnamaanisha tumekuwa na wezi mpaka tumeshindwa kuwafanya chochote? sasa tunawaogopa tumeamua kabisa kuwaacha watufanyie chochote watakacho?

Bora mkoloni arudi tu.
Wizi umekua sehemu ya system hamna wa kuushugulikia, mkataba unaweza kurekebishwa ila sio kuachia sisi wa bongo, wewe angalia, mtaji ulio wekwa kwenye mashirika ya serikali na performance zake, ATC, TTCL, BRT, nk hiyo Air Tanzania ingepewa wazungu wa fast jet tungekua kwenye Air transport revolution.
 
Umeongea jambo la akili sana
Mwenye akili ataelimika hapo
Tatizo uadilifu mkuu
Mtu anawaza kuiba tu au kuuliza rushwa
Hao wanakuja kuwekeza kwa sababu wamepewa ahadi hawatasumbuliwa na makanjanja

Kungekuwa na wawekezaji wengi sana tangu zamani ila tatizo wengi walikimbia baada ya kuulizwa cha juu.
 
Back
Top Bottom