MIXOLOGIST
JF-Expert Member
- Mar 1, 2016
- 14,311
- 36,056
DP World in pornographic movies enthusiasts' perspertives means double penetration world. Huku bandari ya DSM, kule airport ya KIA
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ndicho tulichoweza kufikia.DP World in pornographic movies enthusiasts' perspertives means double penetration world. Huku bandari ya DSM, kule airport ya KIA
Kupewa mzungu au mwarabu chochote akiendeshe sio tatizo, tatizo linakuja pale huyo anayetoa anapokuwa hajielewi, anafanya mambo ya msingi kwa akili ya mtoto mdogo, huyu hatufai kabisa, hafai kutetewa kwa jina lolote iwe system au vinginevyo.Wizi umekua sehemu ya system hamna wa kuushugulikia, mkataba unaweza kurekebishwa ila sio kuachia sisi wa bongo, wewe angalia, mtaji ulio wekwa kwenye mashirika ya serikali na performance zake, ATC, TTCL, BRT, nk hiyo Air Tanzania ingepewa wazungu wa fast jet tungekua kwenye Air transport revolution.
Mkataba umeuona kwani?.Hii Kampuni siyo kongwe, haina zaidi ya miaka 18.
Ni kampuni ambayo serikali ya Dubai ndiyo yenye hisa nyingi, sasa mbona sisi hapa akili zetu ni kuuza tu kila tulicho nacho na kusema serikali isijihusishe na lolote, bali awaachie wengine kila jambo?
Kama hawa waarabu wanaweza kuwa na kampuni yenye ufansi kiasi hicho, kwa nini nasi tusiwe 'inspired' tujifunze wanachokifanya kwa ufanisi ili nasi tukifanye?
Sisi inaelekea tunachoweza pekee sasa hivi ni kutegemea tu watu watoke nje waje watufanyie sisi kwa gharama kubwa. Sisi tunajitoa kabisa kwamba hizi kazi hatuziwezi, kwa nini?
Nirudi kwenye swali nililouliza kwenye kichwa cha mada: Hawa DP World, bado wapo Kwenye ile bandari ya Djibouti (Doraleh Container Terminal) au hawapo? Kama hawapo, ni nini kiliwatokea huko?
Je wakati sisi tunawatafuta kwa udi na ubani, tumejiridhisha na baadhi ya mifano juu ya kazi zao wanazozifanya takribani kwenye nchi kama kumi hivi? Hapo Rwanda, jirani napo wapo, tumewatembelea hapo na kuona kazi zao zinavyokwenda na kujiridhisha?
Lakini yote kwa yote, hii mikataba ya kuingia kama watu tusiokuwa na akili kichwani ni ujinga wa hali ya juu sana.
Kumbe shida ni Uarabu!.Upuuzi.Hata kama tukiwa wezi, lakini hatuwezi kuwapa waarabu sehemu ya bandari yetu kwa terms za kijinga kama zile halafu tunyamaze tu, huo ni upumbavu.
Kwanza inakuwaje mnakuwa na wezi halafu mnashindwa kuwashughulikia? hii kitu niite nini?
Mnamaanisha tumekuwa na wezi mpaka tumeshindwa kuwafanya chochote? sasa tunawaogopa tumeamua kabisa kuwaacha watufanyie chochote watakacho?
Bora mkoloni arudi tu.
Duuh wee ndo akili kisoda kweli,baada kusema tupeleke wataalamu kusoma warudi na ujuzi wa hio technology eti wapewe tuMi naona wapewe tu, dunia ipo kitechnolojia zaidi sisi tupo ki maneno zaidi, mifumo yetu ya kizamani sana
Yes, maarabu majizi hayatakiwi na terms za hovyo kwenye mikataba.Kumbe shida ni Uarabu!.Upuuzi.
Tumepeleka sana tu mkuu, lakini wote wanarudi kama walivyoenda na wanakuwa wametumia pesa ndefu..Duuh wee ndo akili kisoda kweli,baada kusema tupeleke wataalamu kusoma warudi na ujuzi wa hio technology eti wapewe tu
Tatizo letu Watanzania linaanzia kwenye uongozi na sheriaWizi umekua sehemu ya system hamna wa kuushugulikia, mkataba unaweza kurekebishwa ila sio kuachia sisi wa bongo, wewe angalia, mtaji ulio wekwa kwenye mashirika ya serikali na performance zake, ATC, TTCL, BRT, nk hiyo Air Tanzania ingepewa wazungu wa fast jet tungekua kwenye Air transport revolution.
Ukweli ni kwamba Tz hatuwezi kuendesha shirika lolote kiufanisi sisi niwezi, masikini ni wezi matajiri ni wezi.....achani wenye maadili wa tufanyie biashara.Tatizo letu Watanzania linaanzia kwenye uongozi na sheria
Wanaosema tuna hitaji katiba mpya naungana nao. Katiba ya sasa ina ubaguzi mwingi inawapa watawala nguvu kubwa sana.
Watawala wanatumia mwanya huo huo kujilinda,hebu fuatilia miswaada inayopelekwa Bungeni yote imeangalia upande mmoja tu ambao ni kuwalinda watawala hata kama watafanya makosa gani na upande wa pili inawabana wananchi kupindukia.
Matokeo yake watawala wanateua watendaji bila kuzingatia weledi wa mtu, unaweza kuta mtu hana uwezo kabisaa lakini ndiye boss,huyo unategemea wa chini yake watakuaje. Boss wa hivyo ukienda na mawazo chanya anakuona adui wake.
Watanzania wenye uwezo wapo sana tu shida inaanzia kwenye sheria zetu.
Umeuliza swali nzuri sana, miongoni mwa watu wanaopambana sana kuwekeza kwenye biashara na mitaji ya kawaida wanayo ni wafanyakazi. Lakini kinachowaangusha sikuzote ni wasimamizi coz mfanyakazi Hana muda wa kutosha kuisimamia biashara. Sasa licha ya wengi kufail lakini wapi wanaofanikiwa. Kwani hakuna watanzania wenye biashara zaidi ya mkoa mmoja na biashara zinaendelea? Hivi nauliza huko kwa wenzetu Hakuna wapigaji yaan Sheria zao mbovu kama za kwetu na watu hawapigi? Lakini mswahili anamheshimu sana mzungu, wahindi, waarabu lakini sio mswahili mwenzake ukitaka kujua Hilo nenda kawaone waswahili wanaofanya kazi kwenye maduka ya wahindi/waarabu wakiitwa na boss wanavyokimbia fasta na kwa nidhamu, angalia wanavyotukanwa lakini kesho yake lazima aje kazini. Sasa nenda kwa mswahili kwa mswahili ni tabu tupu. Hili taifa linawatu wa hivyo sana hususani vijanaWewe jiulize kwanza nikikuachia biashara uiendeshe na mimi nikasafiri miaka 3
Je nikirudi ntaikuta imekua na umeajiri watu zaidi au utakuwa umeiba na kujenga nyumba zako?
Sisi ndio tuko hivyo, ukipata nafasi unaona ni mali yako
Wenzetu CEO yuko Dubai au Geneva na kazi zinafanyika nchi 150 na faida zinasoma
Sasa niambie wewe fungua duka moja Dar mpe mtu na lingine Moro mpe mtu uone
Kufanya biashara kubwa hapa Tz ni pasua kichwa, TRA wezi, watumishi wako wezi bandarini wezi, wizara na mamlaka husika wezi hamna unafuu popote, wengi wanao pinga hiyo tenda ndo walio kua wanafaidi na ubomvu wa utendaji wa bandari.Umeuliza swali nzuri sana, miongoni mwa watu wanaopambana sana kuwekeza kwenye biashara na mitaji ya kawaida wanayo ni wafanyakazi. Lakini kinachowaangusha sikuzote ni wasimamizi coz mfanyakazi Hana muda wa kutosha kuisimamia biashara. Sasa licha ya wengi kufail lakini wapi wanaofanikiwa. Kwani hakuna watanzania wenye biashara zaidi ya mkoa mmoja na biashara zinaendelea? Hivi nauliza huko kwa wenzetu Hakuna wapigaji yaan Sheria zao mbovu kama za kwetu na watu hawapigi? Lakini mswahili anamheshimu sana mzungu, wahindi, waarabu lakini sio mswahili mwenzake ukitaka kujua Hilo nenda kawaone waswahili wanaofanya kazi kwenye maduka ya wahindi/waarabu wakiitwa na boss wanavyokimbia fasta na kwa nidhamu, angalia wanavyotukanwa lakini kesho yake lazima aje kazini. Sasa nenda kwa mswahili kwa mswahili ni tabu tupu. Hili taifa linawatu wa hivyo sana hususani vijana
Umesema vyema sana. Mfumo uliopo nchini ni wa wizi wa dola (KLEPTOCRACY) toka juu hadi chini. Ndio maana wako tayari kuua ili wasiachie madaraka.Wizi umekua sehemu ya system hamna wa kuushugulikia, mkataba unaweza kurekebishwa ila sio kuachia sisi wa bongo, wewe angalia, mtaji ulio wekwa kwenye mashirika ya serikali na performance zake, ATC, TTCL, BRT, nk hiyo Air Tanzania ingepewa wazungu wa fast jet tungekua kwenye Air transport revolution.
Kani Kalamagamba, kuhani mkuu wa Magufuli umesikia akitia neno lolote hapo?magufuli alisema tutamkumbuka, aisee naona kama tumeanza kumkumbuka. hivi kweli unampa mtu bandari ya dsm ambayo imeshajengwa na unampa kama karanga tu, badala ya kumwambia aende akajenge bandari yake pale bagamoyo? na ipo wazi kabisa dubai wanaishika hii ili wachina wasihamishie mizigo yao Bagamoyo toka dubai? tumelala usingizi? au kwasababu baadhi ya watu wana undugu na waarabu?
Geuza upande wa pili, utaona sura mbovu zaidi ya hiyo uliyoieleza hapo.Kufanya biashara kubwa hapa Tz ni pasua kichwa, TRA wezi, watumishi wako wezi bandarini wezi, wizara na mamlaka husika wezi hamna unafuu popote, wengi wanao pinga hiyo tenda ndo walio kua wanafaidi na ubomvu wa utendaji wa bandari.
Magu tutamkumbuka sana,Hizi mishe aliwezaga Magu tu, wengine wakisikia sauti ya mweupe tu wanakunja mikia ka nyau chotara!
Kwani ninahitaji "kuuona mkataba" kabla sijatoa maoni yangu kama nilivyoyawasilisha hapa?Mkataba umeuona kwani?.
umenikumbusha nilikuwa najenga nyumba nikaanza kufyetua matofali nikampa jamaa mmoja kazi ya kuyefyetua nikimuamini vile ni jirani yangu.Wewe jiulize kwanza nikikuachia biashara uiendeshe na mimi nikasafiri miaka 3
Je nikirudi ntaikuta imekua na umeajiri watu zaidi au utakuwa umeiba na kujenga nyumba zako?
Sisi ndio tuko hivyo, ukipata nafasi unaona ni mali yako
Wenzetu CEO yuko Dubai au Geneva na kazi zinafanyika nchi 150 na faida zinasoma
Sasa niambie wewe fungua duka moja Dar mpe mtu na lingine Moro mpe mtu uone