Dkt. Gwajima D
Minister
- Nov 28, 2015
- 966
- 6,019
'Bila Kunyukwa'😀 ishakuwa Imani tena. Nahisi tunahitaji huduma ya ushauri nasihiSisi wa africa bila kunyukwa hatuendi jamii nyingi tunazotamani kuziiga nao wana mambo yao ya ajabu , sio kitu cha ajabu watoto wakizungu kuwaambia wazazi wao wanavutiwa na mahusiano ya jinsia moja na kwao ni kawaida tu.
Mda mwingne tusipuuze desturi zetu na kuiga za watu ambazo kiundani zina madhara yake pia.
Hawa watoto wanaolelewa hivi ndio mwisho wazazi wakipata ajali ghafla wakafa huishia kutaabika sana na duniaMambo ya daddy ,mammy ,junior ni hatari. kwa lyfe style za kibongo unless uwe na Mtonyo wa kwenda.
Na hayo yote yazingatie 👇Kupiga mtoto at first hand naona haijakaa sawa isipokuwa tu kwenye attempts za uzembe. Mtoto alishafanya kosa hilo hilo mara mbili au zaidi hizo ni signs of negligence of which sio tabia nzuri kwa mtoto kukua nazo. Mara zote ulishamkanya ila anakuwa mzito kuelewa ni lazma umshtue kidogo.
Africa genetically tuna hizo element za kufanya mambo ya uzembe ikiwa hakutakuwa na gharama za maumivu kwa namna fulani.
Wazungu wao wana condition watoto in another way round. Hawa impose physical disturbance ila psychologically kama ku deny mtoto kufanya michezo flani kama way of punishment. Hawaruhusiwi kupiga ila adhabu wanatoa.
Mlete kwenye huduma ya marekebisho ya tabiaMimi nilishapigwa sana, sasa ni zamu ya watoto wangu kuchezea mbalata hasa first born ni mtundu kinoma. Nawaza tu kama na mimi niliwasumbua wazazi kama yeye anavyonivuruga mimi basi Mungu awabariki wazazi wangu 😁
Uoga na unafiki si mfumo uliotengenezwa na waasisi wa nchi. Ile dhana ya mkubwa hakosei huwa naipinga kwa nguvu zote. Bindamu hatuna perfections ni lazima kuna point utafeli tu.Jamii yetu ina maadili au ina uoga na unafiki?
Ulitusumbua sana kijana mshukuru mungu mzee Ndomba alikupeleka kikamanda.Nashukuru mzee wangu kwa kunipa kipondo kilali pale nilipotoka nje ya mstari. Bila hivyo leo hii ningekuwa pusha au teja.
Zipi zitaje kwa manufaa ya wengiWatoto wengi waliolelewa Kwa vipigo hawana maadili . wazazi wale wakali , wazee wakufoka foka wametoka 0-0 hawajafanikiwa kuandaa kizazi bora
Kuna njia za kulea mtoto ambazo zinaweza kumfanya akawa na Utii. Heshima na maadili mazuri.
Mtoto mfanye awe na usikivu mzuri na mpatie na EI
Amini nakuambia...mzee aliekuchapa katika njia ya kukuelekeza uishi kwenye miiko na ukaja fanikiwa lazima utarudisha fadhila kwa kumtunz vzur...labda kama huyo mtt hajitambui..vivyo hivyo kwa mwalimu aliekuwa mnoko lkn alikuwa na nia njema kwakoAhsante Sana kwa mada yako. Ndiyo Iko x usiku kucha jana na inaendelea.
Naongezea; tuna wazee wengi hawatunzwi na watoto wao waliowachapq Sana kwa madai ya kuwatengeneza. Je hii siyo MOJAWAPO ya athari ya mpasuko wa mahusiano ya watoto na Wazee ? Kwamba nguvu kubwa ilitumika kuumiza mwili badala ya ku transform akili ya ndani ya mtoto? Sasa mtoto kawa mkubwa, Tabia zake zilizokandamizwa kwa hofu ya kipigo, sasa zinaanza kushamiri na kumea maana hakuna wa kumpiga tena?
Nini maoni yenu?
Ukizungumzia kina mama hapo nakubaliana na wewe kabisa. Wengi ni wakatili hasa wale waliozalishwa bila kuolewa na kisha kuachwa wahangaike na watoto huwa wana uchungu sana wa kuachwa hasira wanamalizia kwa mtoto.Ni kweli mkuu wengi hawakubali na kusema ooh tunawadekeza hell no
Mtoto kuonywa na kupigwa kidogo ni sawa ila sio mpaka unamchoma moto mikono kisa kadokoa nyama au kaiba mia
Kuna wazazi washenzi mkuu na hao ndio sikubaliani nao kabisa
Unamfunga kamba mtoto masaa na kumfungia chumbani siku nzima
Mkuu kuna ukatili wa watoto we acha tu
Hata humu unaweza kukuta watu wanapiga hivyo
Tuendelee kutoa darasa ili nao wabadilike
Mzazi hata siku moja hutembei barabarani na mwanao bali kuwakunjia uso tu
Akikuomba buku unamtukana
.aisee tunaona mengi sana mitaani
Wengine wanasema wazungu hawapigi sio kweli wakiwa wadogo wanawapiga kwa kuwafundisha ingawa wanajua wanaweza kunyang"anywa watoto
Ila nidhamu ipo
Kina mama kwa afrika ndio wanaongoza kwa ukatili wa watoto sasa sijui kisa mimba za nje ya ndoa sijui
Hakika, umesema vyema waziri.Sisi huku watoto siyo wanachapwa, wanapigwa na kupigana na wazazi wao. Ngumi, mateke, wengine wanafungwa kwenye miti, wengine wamwagiwe maji ya moto, sad... Halafu mtu huyu anasifiwa na jamii....
Wanasahau kuna kliniki za malezi na makuzi na 👇
Mkuu hapa ndo unakosea...uchumi haulingani kwa wote...na haya ndo yanaleta makuzi tofaut ktk jamiiNunua vitu vya jumla weka ndani acha kumtuma mtoto vitu rejaja dukani mara sukari robo, mara kiberiti kimoja, mara chumvi pakiti moja n.k
Uko sahihi...pia hata hiyo kumtuma mtoto inamjengea hali ya kuish maziringira yyte ya kudekezwa na kupiga kazi piaMkuu hivyi unadhani ulivyo wewe namimi tunalingana kiuchumi?
Hujui Kuna familia Kila siku hununua mafuta 300 na sabuni ya kufulia na kuogea ndo hiyo hiyo? Kwa comment Yako inaonyesha wazi hujui hata uchumi wa watanzania walio wengi
Tufanye Hivi muheshimiwa ninyi waleeni Watoto wenu kama Yai vile mbona inafaa nasisi tuwalee vile tunaona inafaa. Elimu Zenu Bado hajawahi kutusadia wa Africa Kila kitu mnafanya Kwa ku copy then mna paste. Akili Zenu zimedumaa na kukaririshwa na WA magharibi eti Kila wanachofanya wao ni sahihi tu.'Bila Kunyukwa'😀 ishakuwa Imani tena. Nahisi tunahitaji huduma ya ushauri nasihi
Kutoa huduma ni kufuga mtoto. Ni sawa na mbwa unampa chakula na chanjo ila anajiongoza mwenyewe😁Nyakati hizi, wazazi hatulei watoto Bali tunatoa huduma.
Nashangaa sana sijui ni lini tutaanza kujiamlia na sisi mawazo yetu. Kama na kuleta napo tufundishwe Nini maana ya kuwa mzazi sasa.Naona wameanzisha sijui programs zao za child protection..ila ukiziangalia kwa jicho la tatu ni kutaja kutuaribia tu hiki kizazi....wanapitia sijui mashuleni na kuwaambia watt kuwa hairuhuisiwi kuadhibiwa kwa namna yyte ile ..huko huko wanapitisha na ajenda zao za ushoga....serikali inatakiwa uwe makinii sanaa na Hawa wanajileta kama NGO's
Kupiga mtu yeyote yule(hasa asie na uwezo wa kukurudishia) ni hatua ya juu kabisa ya uonevu.
Jiulize, wewe ukikosea, ni nani huwa anakupiga?
Hiyo clinic ni Kubwa kiasi gani?Mlete kwenye huduma ya marekebisho ya tabia