TANZIA Jecha Salim Jecha afariki dunia akipatiwa matibabu hospitali ya Jeshi Lugalo

TANZIA Jecha Salim Jecha afariki dunia akipatiwa matibabu hospitali ya Jeshi Lugalo

Team imekamilika huko,mkapa,jpm,maalim seif,nyerere,Membe,sitta aiseh uongozijarabu kabisa huko kwao!!

RIP mtumishi mwaminifu wa jamhuri YETU!!!
 
Aache uzembe na yeye. Kama aliweza kufuta uchaguzi na watu wakapoteza maisha bila sababu inakuwaje akashindwa kufuta/kukata hicho kifo?
Jecha alitangaza kufutwa kwa Uchaguzi yeye kama yeye hana ubavu wa kufuta sema ndio raha ya Siasa …alieyafuta ni Mzee Mjanja mjanja wa Mjini anaejua kusimama eneo salama wakati wote wa vimbunga
 
Mnamuonea tu Jecha. Tatizo ni Kikwete na Mkapa. Kikwete alihairisha hadi Safari navkuwahi Zanzibar pamoja na Mkapa. Na kumuonya Jecha asitangaze. Dkt Sheni alishakubali kumkabidhi maalim lakini mkapa na Kikwete wakamuambia haiwezekani aache upuz.

Ni Kikwete na Mkapa ndo walifuta hule uchaguz.
Upo sahihi kabisa.
Madhalimu hawajifunzi.
Mauti ni mawaidha kama wasemavyo ndugu zetu waislamu.
 
Mnamuonea tu Jecha. Tatizo ni Kikwete na Mkapa. Kikwete alihairisha hadi Safari navkuwahi Zanzibar pamoja na Mkapa. Na kumuonya Jecha asitangaze. Dkt Sheni alishakubali kumkabidhi maalim lakini mkapa na Kikwete wakamuambia haiwezekani aache upuz.

Ni Kikwete na Mkapa ndo walifuta hule uchaguz.
Hapo naweza kuungana na wewe hapo ni nadharia
 
Kumbe Na wao wanakufa,hahhaahha halafu kafia Tanganyika. Haya kashindwa kufuta kifo chake?Rot in hell wewe kibabu Jecha.
Wewe siyo wa kusema hivyo jameni. Kumbuka yule kipenzi chako ndiye aliinjinia yote haya aliyofanya Jecha
 
Kula nafsi ana mauti. Kila Nafsi itapata umauti/kufa.
Tutende mema hapa Duniani ili tupate pepo kesho yake. Tusijisahau. R.I.P.
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) aliyefuta uchaguzi 2015 na kupata umaarufu mkubwa, Jecha Salim Jecha leo amefariki Hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam na mwili wake utapelekwa Zanzibar kwa maziko.

Jecha Salim Jecha alipata umaarufu mwaka 2015 baada ya kufuta matokeo ya uchaguzi Zanzibar. Zaidi soma Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yafuta Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu

Aprili 17, 2018 Salim Jecha Salim aling'atuka rasmi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC) baada ya kuhudumu katika nafasi hiyo kuanzia Mei 4, 2013. Zaidi soma Hatimaye 'mtemi' Jecha Salim Jecha ang'atuka

Mwaka 2020, Jecha Salim Jecha alichukua fomu ya kuwania Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM), jambo ambalo lilizua utata ukizingatia mwaka 2015 alikuwa ni Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar yenye dhamana ya kusimamia chaguzi zote kisiwani humo. Zaidi soma Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC), Jecha Salim Jecha achukua fomu ya urais Zanzibar

Mola amsamehe makosa yake alipoteleza.

View attachment 2691725
Picha maarufu ya Jecha Salim Jecha enzi za uhai wake​
Looooooooooooo! Alievujishiwa jamani nyeti atabugia bia mpaka azame kwenye chupa.
 
Hivi hospital ya Mnazi mmoja Zanzibar ina hadhi sawa na hizi rufaa za mikoa huku Tanganyika au ni zahanati kubwa.

Tuvunje tu muungano tupige na pesa za "utalii wa matibabu".
 
Back
Top Bottom