Jeff Leah: Yanga itafungwa 3-0 na Marumo na nina uhakika haitofuzu Fainal wala kuchukua kombe

Quality ni kigezo cha msingi chakuangliwa.

Huwezi ukawa unajifananisha na timu ambayo inafunga timu kubwa zenye proffesional players na timu ambayo inafunga regular clubs kuwa ni sawa.

Mfano angalia tu katika hizo timu zote ambazo Yanga amekutana nazo, ni timu gani ambayo ilikuwa inapeleka pressure kwenye lango la Yanga kama Marumo tena Yanga akiwa nyumbani?

Angalia nafasi walizotengeneza Marumo halafu fananisha na timu zingine ambazo Yanga alikutana nazo utaona hizo timu zilikuwa na ubora sawa na Marumo?
 
Uwe na nguvu usiumie maana ata Mimi nilishabikia Simba siku Ile mlipo kuwa Morocco
 
Nabi akipanga kikosi kwa formation aliyocheza na Rivers Nigeria marumo sio tu hawatapata goli wataongezwa zaidi
 
Ukisikia uchawi ndio huu Sasa.
Utafaidika nini Yanga ikifungwa?
Mkitaka ushindi jipangeni mwakani sio kuombea wengine mabaya.
 
Una hoja nzuri na hii ndio iliyopaswa kukaa mezani ijadiliwe badala ya kuanza kuwashutumu wachambuzi

Ni kwamba hivi, Marumo walipokuwa wanacheza na Pyramids walikuwa na nidhamu ya hali ya juu kwasababu walielewa ubora wa mpinzani wao na kujua kiasi gani makosa madogo yanaweza kuja kuwa gharimu.

Mechi ya Marumo na Yanga utaona kabisa Marumo walikuwa wame lose some respect na ndio maana walikuwa wana over confidence ya ajabu hata wakiwa wamezingirwa na washambuliaji kwenye lango lao wao walikuwa wanauchezea mpira.

Na hili nimelizungumza frequently wakati wa mechi updates, Marumo walionekana ni watu ambao wanacheza kwa ku relax na confidence ya hali ya juu.

Sasa wachambuzi perception yao ni kwamba hawa Marumo wakija na intensity yao ile walioionesha kwenye mechi kubwa dhidi ya Pyramids hilo wanaloliona huwenda likatokea.

Japo uwezekano wa kuja ndivyo sivyo pia upo, mpira ndio ulivyo inaweza ikaja tofauti na Yanga hii ikaja na plan nyingine matokeo yakaja tofauti.

Hivyo kinachoonekana saizi ni kwamba Yanga akicheza vile kwa namna alivyocheza hapa halafu Marumo wakaongeza fighting spirit ile waliyokuwa nayo kwenye match over giants wanaweza wakapata hayo matokeo.
 
Aya, tuje kwenye Quality kwa kuangalia mechi ya awali baina ya Yanga na hao Marumo.

Kitu pekee ambacho Marumo alimzidi Yanga ni Ball possession tu. Yanga akiwa na 48, Marumo 52.

Kwenye on target, Yanga alipiga 8 huku Marumo 3. Golikipa wa Marumo alifanya Saves 6, huku wa Yanga akifanya 3 tu. Maana yake Yanga alikuwa mkatili zaidi kuliko huyo Marumo. Wangetulia angeoga nyingi.

Turudi sasa Mazembe vs Yanga.
Mazembe alipiga on target 4 huku Yanga 2. Kipa wa Yanga alifanya Saves 4 huku wa Mazembe 1. Japo Yanga alishinda lakini alishambuliwa zaidi.

Kwa uhatari, Mazembe alionyesha kuwa na njaa zaidi ya Marumo. Hapa tunaenda kwa takwimu za wazi.
 

Ni kipimo gani kinachopima kiwango cha kujiamini? Au imetumika hisia tu?
Mpira ni mbinu mkuu, unaweza kuja na intensity ya kiwango cha juu ndio ikawa ni advantage kwa Yanga, wakakupiga magoli ya counter attack. Hizo mnazoongea ni utabiri na wala sio kulinganisha mizani kiufundi.
 
Hivyo kinachoonekana saizi ni kwamba Yanga akicheza vile kwa namna alivyocheza hapa halafu Marumo wakaongeza fighting spirit ile waliyokuwa nayo kwenye match over giants wanaweza wakapata hayo matokeo.
Na kwa nini useme Yanga akicheza vile huku ukisema Marumo wakaongeza fighting spirit?

Waweke katika mzani sawa kisha wapime. Kama Marumo wataongeza upambanaji, sema Yanga nao wakiongeza upambanaji. Kila mmoja ana approach yake. Si kumuona kuwa mmoja pekee ndiyo ana njaa na matamanio zaidi ya mwingine.

Na wala usiseme kuwa Marumo waliingia pasipo kuwaheshimu Yanga. Kipindi cha kwanza, Marumo walicheza kwa nidhamu ya hali ya juu sana. Mechi ilikuwa iishe 1-0, shukuru ya goli la BM dakika za jioni.

Kwa ngazi hii ya nusu fainali, ni kichekesho kusema timu fulani haikuheshimu nyingine.

Kwamba Yanga wao watakuwa wamefungwa kwenye stagnant mode wacheze kama walivyocheza?
 
Unabishana na hater, huyo hawezi kukubali kuwa Yanga sasa ina timu nzuri, atatafuta sababu yoyote ya kuhalalisha hisia zake
 
Mazembe alikuwa na on target 6 sawa na Yanga with poor performance

Hiyo ndio jnayokuja kutofautisha

Angalia

Marumo wao wako vizuri kwenye counter attack na pia kwenye kupora mipira na hard pressing

Mechi ambayo walitoa sare na Pyramids walizidiwa maeneo mengi ilikuwa ni 69 over 31 percent.

Na mind you kwenye uzuiaji wako vizuri sana na hata hilo bao walilosawazisha Pyramids ilikuwa ni penati.

Sasa jaribu kufanya evolution hapo, kwamba hii timu ambayo ikizidiwa umiliki wa mpira na timu kubwa iliweza kupata matokeo mazuri.

Kwanini hii mechi ambayo ilikuwa na possession kubwa kuliko Yanga ikaruhusu mabao?

Ndio hapo unaangalia nidhamu ya mchezo kwanza kupima na ile waliyokuwa nayo kwenye mechi dhidi ya giants unaona kuna utofauti.

Sasa hiyo inaweza kuwa sababu ya watu kuamini Marumo wanaweza kufanya hicho kitu iwapo watacheza kwa intensity ile ile ya kumheshimu mpinzani. Kwasababu sababu kubwa ya wao kufungwa ilisababishwa na kutoheshimu mpinzani
 
Yanga game ya hapa home alikuwa na upambanaji mkubwa kwa shauku ya kutaka kumaliza mechi hapa hapa nyumbani.

Mimi nimempima Yanga kupitia ubora huu ambao nimeuona, lakini pia kupitia kwa mpinzani mwenye ameonesha challenge ya kiupinzani kuliko wale waliotangulia.

Kwa hiyo kama umenisoma kwenye post mbili zilizopita nimeonesha uwezekano wa matokeo kuja ndivyo sivyo.

Nilichojaribu kuki address mimi ni kwamba Yanga alicheza kwenye ubora, wakati Marumo akikosa nidhamu.

Ni ubora gani ambao unautegemea kuuona kwa Yanga zaidi ya ule?

Kumbuka unapotaja reference ya mechi fulani ya Yanga kuwa bora uwe unaangalia na mpinzani wa hiyo mechi alikuwa nani

Mimi nimeona mechi ambayo Yanga alicheza kwa ubora zaidi ni hiyo ya Marumo na sababu nimeshazitoa.
 
Kwa maelezo niliyosoma hapo, umedhihirisha kuwa wewe umeiheshimu pyramids na kuidharau Yanga.
 
Unabishana na hater, huyo hawezi kukubali kuwa Yanga sasa ina timu nzuri, atatafuta sababu yoyote ya kuhalalisha hisia zake
Wale wale watu wa kuendeshwa na hisia.
 
Kwa maelezo niliyosoma hapo, umedhihirisha kuwa wewe umeiheshimu pyramids na kuidharau Yanga.
Kwa maelezo uliyoandika hapa umedhihirisha kwamba umeidharau Marumo na kuiheshimu Yanga kwasababu ni timu yako.
 
Natamani ukiwa unaquote, kama itakupendeza tutumie taarifa rasmi za CAF wenyewe. Nilikuwa natumia za Livescore ila sasa baada ya kuangalia za CAF, zinatofautiana.

Hata hiyo uliyoweka wewe ni tofauti pia.
Ndugu,

Kila mechi ina approach tofauti kulingana na aina ya mpinzani, uchezaji wa timu, uwanja na hata muda wa mechi kuchezwa.

Huwezi kutumia approach ya game ya Pyramids katika kila mechi. Huwezi kusema kwa sasa alicheza vile dhidi ya Pyramids basi anapaswa kucheza hivyo hivyo dhidi ya Yanga.

Mfano, Yanga kwenye mechi za Uarabuni alifungwa magoli ya kichwa sababu ya ufupi wa Wachezaji wao. Akawaweka wachezaji ambao wana uwezo wa kwenda juu na kucheza mipira hiyo kwa usahihi. Approach ya mchezo huo haipaswi kuwa sawa na mechi zingine zote.

Kutomheshimu mpinzani huwa inapimwaje? Timu icheze vipi ili ujue kuwa haijamheshimu mpinzani? Kama labda kulikuwa na wachezaji kadhaa wa kikosi cha kwanza hawakuchezeshwa kwa sababu waliona mechi ni nyepesi, basi nitakubaliana nawe, vinginevyo hizo ni story tu.
 
Kwa maelezo uliyoandika hapa umedhihirisha kwamba umeidharau Marumo na kuiheshimu Yanga kwasababu ni timu yako.
Unaacha kuzungumzia Yanga vs Marumo unazungumzia Marumo vs Pyramids. Utafikiri Yanga hakucheza bado na Marumo. Weka takwimu zao wenyewe kwa wenyewe na uzungumzie mapungufu kwa kila mmoja ila wewe unajizungusha zungusha kwa Pyramids huko. Wacha tusubiri tu hiyo jumatano
 
Unajichosha tu mkuu hapo
 
Kazi ya malaya ni kuuza (sijataja)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…