Jenerali Mabeyo amuaga Rais Mwinyi. Ajiandaa kustaafu June 2022

Hivi hatujapeleka watu Siberia?
====
Hongera CDF kwa utumishi wako uliotukuka.
 
anakaa ofisini miaka sita anatunzwa hadi afe, halafu nesI aliyetumika miaka 45 anaambulia kiko kotoo
Huyu wa miaka 6 ametumikia na kushuhudia mazito ya nchi hii
 
Moja ya Wakuu wa jeshi niliyetokea kumu 'admaya' sana. CDF Mabeyo tutakuheshimu na kukuenzi daima kwa mchango wako katika jeshi,kanisa,jamii na taifa kiujumla.Vitabu vyako ulivyoandika ni kumbukumbu njema sana.Salute Soldier [emoji870]
General venance mabeyo ni mfano wa kuigwa
 
Akapumzike mzee wetu aliachiwa nchi ktk sintofaham nadhani hakuna Jeneral aliyepata changamoto km yeye katika historia ya nchi hii
Je, angekua amepoteza Battalian nzima siku moja vitani Ungesemaje?
 
Kwanini amuongezee Muda, hakuna wanajeshi wengine wenye sifa? Miaka 65 Bado anakitu kipya Cha kufanya.?
Kitu kipya cha kufanya bado anacho ndiyo mimi naamini kabisa hivyo; ila sema tu kwa namna Jeshi letu lilivyo, naamini kabisa wapo pia vijana wengine chini yake wanaoweza kufanya vizuri kwenye nafasi hiyo kama alivyifanya yeye; hivyo kuendelea kumpa ashikilie nafasi hiyo kutawavunja moyo wengine wenye sifa za kushika nafasi hiyo. Mimi napendelea apumzike kwa sababu hiyo, awaachie na wengine walio na sifa za kuifanya kazi hiyo
 
Kitu kipya cha kufanya bado anacho ndiyo mimi naamini kabisa hivyo; ila sema tu kwa namna Jeshi letu lilivyo, naamini kabisa wapo pia vijana wengine chini yake wanaoweza kufanya vizuri kwenye nafasi hiyo
Hata Marekani hiyo haipo nafasi kubwa hiyo hushikwa na wakongwe wa vita hiyo post siyo ya internship

Hiyo ya kiongozi mpiganaji hasa mwenye track record ya vita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…