Jengo refu zaidi Duniani la Burj Khalifa - Dubai lapambwa kwa picha za Bendera ya Tanzania

Jengo refu zaidi Duniani la Burj Khalifa - Dubai lapambwa kwa picha za Bendera ya Tanzania

Kwanini wasingweeka picha/videos za vivutio vya utalii, Madini, mazao ya kilimo vinavyopatikana TZ?
Hili jengo ni kubwa, refu, zuri na la gharama kubwa mno. Lina mfumo wa taa za rangi ambao unaweza kuwekwa kwa mfano wa picha za vitu mbalimbali.

Kama kuna tukio kubwa linafanyika Dubai, basi muonekano wa rangi za jengo hili nyakati za usiku huashiria tukio hilo. Muundo wa mfumo wa taa zake ni kama ule uwanja maarufu wa Ujerumani ukulikanao kama Olympic Arena.
View attachment 2134617View attachment 2134618View attachment 2134619View attachment 2134621
 
Kwanini wasingweeka picha/videos za vivutio vya utalii, Madini, mazao ya kilimo vinavyopatikana TZ?
mkuu Mazao na madini yanapatikana kila sehemu ya ulimwengu na ni ngumu kubaini kuwa haya madini au mbuga ni ya Tanzania au laaa!!! wasipokuwa specific kwa kutaja eneo husika watarii au watu wengi wangeshindwa kuelewa maana yake, Ila bendera ya taifa ni unique kila mtu akiiona lazima ajue hii ni bendera ya taifa fulani .

Lakini pia tambua kuwa bendera yetu kwa hizo rangi zake inawakilisha vitu vingi ukijumuisha madinu,water bodies nk. Ambavyo viko Tanzania

Hongera rais wetu Samia
 
Tanzania sasa imekua ni ya kushindana na kina Huddah the boss Chick kuwekwa kwenye majengo ya Dubai.

Kwamba Tanzania inaenda kujitangaza Dubai na kujiweka kwenye majengo?

Tanzania sasa inajilinganisha na kina Christiano Ronaldo kina The Rock nk.

Hivi mtu atasema kuna mtu haijui Tanzania? Matatizo ya Tanzania ni kutokujulikana ana sera na uongozi mbovu wa ccm kwa miaka zaidi ya 60?

Aisee.
 
Tukio la muonekano wa rangi ya bendera katika jengo hili la Burj Khalifa lina gharama zake, ambazo zinapaswa kulipwa na serikali ya Tanzania. Kutokana na chanzo cha habari cha Arabian Business kinasema "real news have value"

"The cost to place a promotional advert or message on the façade of the Burj Khalifa starts from AED250,000 ($68,073) for a single three minute display, according to the marketing agency which manages the lighting displays.

Prices range from AED250,000 for the three minutes during weekdays from 8pm to 10pm, rising to AED350,000 at weekends. For two three minute impressions any night between 8pm and 10pm the price is AED500,000 and for AED1 million you can get five three minute impressions any night between 7pm and midnight.

The displays are managed by Dubai-based marketing agency Mullen Lowe MENA and the content must be submitted four weeks before the promotion goes live, in order to be approved by Burj Khalifa’s owner Emaar Properties"

Kwa hiyo ni lazima tutambue muonekano wa bendera yetu katika jengo hili ilikuwa ni huduma ya matangazo ya biashara ambayo ilinunuliwa na kulipiwa kwa fedha za kigeni.



Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Mbona kawaida tu,
Ila muda siyo mrefu jiandaeni twiga kupandishwa ndege.
Eti ajira laki 2 aisee...!
 
I think Kama unaweza kutumia milioni 157 kujitangaza then ukapata watalii kutoka Dubai naamini sio tatizo since huwezi kupata hela kama hauna hela.

Ukiacha mambo ya mkataba wa Loliondo, waarabu wanaokuja kula maisha mngekuwa mnaona Ile convoy yao Wala isingekuwa hii million 157 ni ishu kabisa.

Mswahili usipotangaza yanakuwa maneno mkasema mbona Kagame anatangaza visit Rwanda kule Arsenal, Mara Kenya wanatangaza kwenye CNN, hivi unajua Tangazo moja CNN inalipiwa bei gani???

Kwa namna hii ya thinking tuna safari ndefu sana, nadhani wamefanya kazi nzuri mno wakati mwingine tusiwaze kwa kuangalia myopically.

Kama Kuna 10% hiyo anayejua aje aseme otherwise wacheni kazi ifanyike wandugu tutamtumia Mrisho Mpoto au Wanne Star mpaka lini? Kwanza alipwe milioni sita Yani nanii anamjua??? Unapoweka tangazo watu wanauliza hii bendera ya wapi? Then anapogoogle anakutana na Mt. Kilimanjaro, Serengeti etc hata agents wa watalii wanaona.

Let's be positive. Wakati mwingine ukiwa kiongozi halafu unafanya mema watu wanaibuka namna hii ndio unajikuta unasema wacha nipige hela zangu nimalize muda nikastaafu kwa raha.

Let's show appreciation kwa kufikiria positively, imagine Will Smith, Angelina Jolie wanapokuja wanalala Grumeti kule Serengeti wanaacha bei gani? Chumba kulala dola 2000 per night hapo hajataka kiwe customised ambapo huwa mpaka 12,000 dollars per night.

Sasa lazima tujiulize mtu mwenye hela zake aliyezoea kwenda Hawaii, Malibu, Malta, Santorini nk anaanzaje kujua mlima Kilimanjaro, Serengeti nk wakati agents wake wanachojua ni Alps mountains, Niagara falls nk? Lazima tukubali tutumie pesa ndio pesa itakuja, the fact tuna hivi vivutio haimaanishi kwingine hakuna, yaani Malaysia wanajitangaza CNN, Croatia, Switzerland yenyewe, Netherlands, sisi ni nani tusitangaze ili wajue? Tukiacha wataenda Kluger National park au Nairobi National Park or Masai Mara nako Kuna Simba, chui etc then tutaanza kulalamika.

On my side, Dubai is the best spot kwa kutangaza kwa sasa Tena tunapaswa kufungua information centre pale ambayo TIC na ministry ya utalii kwa maana ya Tanapa na foreign affairs wawepo pale Kama tourist information centre maana matajiri wa dunia na watu wengi sana wapo pale kustarehe so wanapata muda wa kuangalia na kuuliza hii ni wapi? Then atajiuliza Kuna nini huko mbona wameweza kutangaza?? I believe ni wazo zuri sana na la kupongezwa forget about gharama ya Tangazo 157 million think about Return On Investment.

Najua nitashambuliwa Ila tuwe positive sometimes.
Umeelezea vizuri sana.Ukitaka upate faida(profit) kwenye pesa ulionayo,lazima uifanyie biashara yako matangazo.
 
Ana kimuhemuhe tu juzi kati tu Ronaldo aliwekwa hapo siku ya birthday yake. Hamna maajabu kuwekwa bendera ya Tanzania wakati rais yupo huko.
Dubai ni Waarabu smart,ukiona hivo Kuna kitu wamekiona...Uchumi!
 
Ana kimuhemuhe tu juzi kati tu Ronaldo aliwekwa hapo siku ya birthday yake. Hamna maajabu kuwekwa bendera ya Tanzania wakati rais yupo huko.
Majitu yasiyo na exposure yanakurupuka na ulimbukeni kudhani ni jambo la ajabu.
 
Tanzania sasa imekua ni ya kushindana na kina Huddah the boss Chick kuwekwa kwenye majengo ya Dubai.

Kwamba Tanzania inaenda kujitangaza Dubai na kujiweka kwenye majengo?

Tanzania sasa inajilinganisha na kina Christiano Ronaldo kina The Rock nk.

Hivi mtu atasema kuna mtu haijui Tanzania? Matatizo ya Tanzania ni kutokujulikana ana sera na uongozi mbovu wa ccm kwa miaka zaidi ya 60?

Aisee.
Mkuu ni kweli kuna watu hawaijui Tanzania,usibishe ...hili la CCM ni chanzo ,ila ukweli ndio huu!
 
Lengo refu zaidi duniani linalofahamika kwa jina la #Burj Khalifa lililopo #Dubai, likiwa limenakshiwa na rangi ya bendera ya Tanzania, jana Februari 28, 2022.

IMG_20220301_061334.jpg
 
Huu ni uongo. Picha hapo haiwekwi sababu ya mahusiano mazuri, bali huwekwa kwa kuwa umelipia na ni mil 160 kwa dakika 3.
Jamani chunguzeni. Kama huu ni ukweli basi nchi hii imejaa wapuuzi wenye mamlaka kupita wakati mwingine wowote. Jee kama tukio hilo lilifanyika kwa nusu siku ni kiasi gani nchi imelipa? Na faida gani imepata kwa rangi ya bendera kuonekana hapo? Ujinga mtupu.
Kiasi hicho kikitumika vizuri kinaweza kufanya mambo mangapi ya maana?
Bado mavuvuzela ya mbogamboga yanashangilia!
 
Back
Top Bottom