Jeshi la Kenya dhidi ya M23: Je, Kenya itaweza kufanya kile ilichofanya Tanzania mwaka 2013?

Jeshi la Kenya dhidi ya M23: Je, Kenya itaweza kufanya kile ilichofanya Tanzania mwaka 2013?

Jeshi la Kenya hawajawahi kupigana vita kwenye mazingira ya misitu mikubwa na migumu kama ya Kongo. Unapigana na watu waliozaliwa na kukulia kwenye hiyo misitu!

Ni jaribio kwa KDF ambalo mabwana vita wa ukanda huu wametega sikio kutokana na uzoefu mdogo wa jeshi la Kenya kwenye vita vya msituni! Pengine hata kuhusisha Uganda lengo ni kuchota uzoefu wao kwenye misitu ya Kongo.

Meja General (mstaafu) Mwakibolwa atakuwa na cigar yake anaangalia majirani wanatokaje na hii mbugi [emoji2]
Kama jeshi la Kenya lilishindwa kuwadhibiti vijana wawili pale katika uvamizi wa maduka ya east gate mchana kweupe na camera zikiwa wazi, je wataweza kuwadhibiti maelfu ya vijana walioshiba mazoezi, wenye mioyo migumu iliyotoboka na isiyojali chochote kuhusu kufa au kuishi.

Bila backup kubwa ya kimataifa Kenya lazima itaomba poo mapema sana.
Ngoja usikie kina mama wa Kenya wakiandamana kutaka watoto wao warudishwe nyumban baada ya kupokea vichapo kila upande.
 
Watume magaidi au wamuundie makundi ya waasi au magaidi kama walivyomuundia Gadafi na Saddam
Mkuu inaonekana wewe sio mfuatiliaji wa mambo yanayoendelea katika nchi za East Afrika.

Rwanda tayari ina waasi wanaopambana na serikali yake toka mwaka 2015. Waasi hao wanaishi katikati ya msitu wa Burundi na Rwanda. Siku za nyuma walikuwa wanaingia Rwanda kufanya mashambulizi ya kushtukiza afu wanakimbia.

Sasa kwa bahati mbaya mkubwa wa lile kundi aliingia kwenye 18 ya wana usalama wa Rwanda na hapo ndo ikawa mwisho wa kundi hilo. Kwa sasa hapo lipo lkn halina nguvu kivile maana jeshi la Rwanda liko macho sana kwa upande wa usalama wa nchi yao, tofauti na Congo unakuta colonel anasikiliza mziki wa fally pupa na kukata mauno ofisini huku vijana wake aliowatuma vitani wakiendelea kufa.
 
😄😄 Sasa hapo ni ukikaa nchale ukisimama nchale,itabidi wapigane nao tu maana itakua aibu wasipopigana nao,mbwembwe walioingia nazo Congo zilikua za hatari..

Hao M23 Jana wamesema wamesitisha mapigano,lkn hawatatoka kwny maeneo waliyoyashikilia na wakishambuliwa na jeshi la Kenya then watajibu mashambulizi ipasavyo.
Kenyata na Ruto wamewaponza watoto wa wenzao 🤣🤣🤣
 
Kenya na Ruto wamewaponza watoto wa wenzao 🤣🤣🤣
Twitter Kule wakenya kibao wanasema jeshi Lao lirudishwe nyumbani 😄😄,huku Wacongo nao Twitter wakilalamika wakisema walidhani KDF wakifika tu watawatoa wahuni wa M23 lkn wanashangaa kuwaona KDF huko Kwny mahotel ya Goma wakila Maisha na totozi tu.
 
Inakuaje brothers and sisters,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Leo ndio siku ya mwisho waliopewa waasi wa Congo ili kusalimisha silaha zao kwa serikali, kinyume na hapo hatua kali za kijeshi zitachukuliwa kwa kundi lolote la waasi ambalo limekaidi amri hiyo. Na oparation hiyo itahusisha majeshi ya Afrika mashariki kutoka Burundi, Congo, Uganda na Kenya huku Kenya ikionekana kuongoza oparation hiyo ambayo kundi kuu la waasi nchini Congo la M23 likisema kwamba haliitambui oparation hiyo na kwamba yeyote atakaethubutu kwenda kuwachokoza katika maeneo yao wata deal nae.

Tusisahau kwamba mwaka 2013 nchi za Malawi, South Africa zikiongozwa na jeshi la Tanzania ambalo lilisimamia oparation zote za chini ziliweza kulisambaratisha kundi hilo la M23 katika kipindi kifupi cha week kadhaa tu, na kusababisha waasi hao kukimbia ng'ome zao na kuacha silaha zao na kwenda kuomba hifadhi katika nchi jirani za Rwanda na Uganda.

Sasa baada ya miaka 9 ya ile oparation kabambe iliyoongozwa na Tanzania, leo waasi hao wamerudi tena kwa kasi ile ile huku Kenya ikionekana kutaka kuchukua nafasi ya Tanzania ili kurudisha tena amani katika maeneo hayo ya mashariki mwa Congo.

Sasa tukiachana na hizi nchi zingine zilizoshiriki au zinazoshiriki katika oparation hizo kama vile SA, Malawi, Burundi na Uganda.

Swali langu je Kenya itaweza kufanya kile ilichofanya Tanzania?

Au jeshi lake linakwenda kupokea kichapo kile inachopokea serikali ya Congo?

Lets wait to see what's gonna happen. Maana yamebakia masaa matano tu ule muda waliyopewa waasi uishe.

God bless Congo,
God bless Tanzania,
God bless our continent Africa.

Thank you 🙏
Sidhani kama ni muda muafaka kuuliza swali lako. Ulivyoliweka ni kwamba nia yako ni kulinganisha uwezo wa jeshi la Kenya na la Tanzania. Muda huu inabidi tuelekeze juhudi zetu katika kuondoa uasi unaozifanya nchi za Afrika kupoteza muda na mali katika migogoro isiyo na kichwa wala mkia badala ya kujikita katika kuleta maendeleo ya nchi.
 
Bila hata Sheria za kimataifa ni Nani Kati Yao ana uchumi wa kupigana Vita?Nchi maskini hizo zingepambana kutafuta Maisha Bora kwa wananchi wake tu.
Uchumi wa Rwanda unategemea zaidi vita vinavyoendelea huko Congo.

Yale maeneo yanayodhibitiwa na M23 yana utajiri mkubwa wa rasilimali, kwahiyo Askari wa Rwanda wanaingia kimya kimya wanachukua rasilimali na kupeleka nchini kwao na baadae kusafirisha katika nchi zinazohitaji hizo rasilimali kwa bei chee.
 
Twitter Kule wakenya kibao wanasema jeshi Lao lirudishwe nyumbani [emoji1][emoji1],huku Wacongo nao Twitter wakilalamika wakisema walidhani KDF wakifika tu watawatoa wahuni wa M23 lkn wanashangaa kuwaona KDF huko Kwny mahotel ya Goma wakila Maisha na totozi tu.
Leo wamepeleka troops zingine Goma! Wanajipanga tu isitokee aibu! Ukiona jambo TZ wamejikalia pembeni ogopa [emoji2]
 
Twitter Kule wakenya kibao wanasema jeshi Lao lirudishwe nyumbani 😄😄,huku Wacongo nao Twitter wakilalamika wakisema walidhani KDF wakifika tu watawatoa wahuni wa M23 lkn wanashangaa kuwaona KDF huko Kwny mahotel ya Goma wakila Maisha na totozi tu.
Kwa upande wa wakenya washajua fika kwamba ndugu zao wamepelekwa kuuwawa kwa faida ya viongozi waliopo madarakani.

Kwa upande wa wacongo wanajua vizuri kwamba jeshi hilo la Kenya halitawaweza vijana hao.

Kwanza ile kujivinjari na totozi ndani ya mahotel ni mtego mkubwa uliyotegwa na hao M23.

Wengi wa hao totozi wanaolala na askari wa Kenya ni watutsi ambao wako kwenye mission maalum ya kufuatilia nyendo za wanajeshi wa Kenya. Wasipokuwa makini watapigwa ambush 1 kali sana ambayo itasababisha maafa makubwa kwa askari wa Kenya, na huo ndio utakuwa mwanzo wa mkakati wa akina mama wa Kenya kuomba watoto wao warudishwe nyumban.

We subiri muda utaongea.
 
Sidhani kama ni muda muafaka kuuliza swali lako. Ulivyoliweka ni kwamba nia yako ni kulinganisha uwezo wa jeshi la Kenya na la Tanzania. Muda huu inabidi tuelekeze juhudi zetu katika kuondoa uasi unaozifanya nchi za Afrika kupoteza muda na mali katika migogoro isiyo na kichwa wala mkia badala ya kujikita katika kuleta maendeleo ya nchi.
Ya ni kweli mkubwa, wote tunaomba amani itawale katika ukanda wetu wa Afrika mashariki.
 
Leo wamepeleka troops zingine Goma! Wanajipanga tu isitokee aibu! Ukiona jambo TZ wamejikalia pembeni ogopa [emoji2]
😄😄 Kama Western wasipoingilia kwa kutishia vikwazo na blah blah nyingine then Kenya inaweza kupatwa na aibu isiyoitegemea mkuu.

Bongo wanajua wanachokifanya,acha tuone Kenya kwny medani nae yukoje.
 
Uchumi wa Rwanda unategemea zaidi vita vinavyoendelea huko Congo.

Yale maeneo yanayodhibitiwa na M23 yana utajiri mkubwa wa rasilimali, kwahiyo Askari wa Rwanda wanaingia kimya kimya wanachukua rasilimali na kupeleka nchini kwao na baadae kusafirisha katika nchi zinazohitaji hizo rasilimali kwa bei chee.
Hebu tuwekee hapa records kuonyesha uchumi wa Rwanda ulitetereka kwa kiasi gani kuanzia kile kipindi cha 2013 ambako M23 walibondwa na kuachia maeneo hayo mpk hii majuzi walipoanza kupigana tena ili tuone ktk kipindi hicho chore Cha miaka 8 uchumi wa Rwanda ulikuaje.

Maana miaka yote hio ya 2013-2022 hao M23 wakiwa wamenyang'anywa hayo maeneo bado hao Rwanda walikua Kwny fastest growing economy in Africa na Wala hawakutetereka.
 
Congo isha setiwa kabla hata ya uhuru ili ije kuwa shamba la bibi kwa wakubwa kutoka dunia ya kwanza waje kujichotea na kuondoka. Kwa maana hiyo hakuna mtu wala nchi itakayoweza kuleta amani pale Congo

Acha ujinga wewe mkata tamaa!
Usiidharau nguvu ya wana nchi wakiamua walahi!
SA dunia nzima ili sema haiwezekani lakini ikawezekana!
Kukata tamaa ni dhambi kubwa sana hapa duniani!
Jiamini!
 
Hebu tuwekee hapa records kuonyesha uchumi wa Rwanda ulitetereka kwa kiasi gani kuanzia kile kipindi cha 2013 ambako M23 walibondwa na kuachia maeneo hayo mpk hii majuzi walipoanza kupigana tena ili tuone ktk kipindi hicho chore Cha miaka 8 uchumi wa Rwanda ulikuaje.

Maana miaka yote hio ya 2013-2022 hao M23 wakiwa wamenyang'anywa hayo maeneo bado hao Rwanda walikua Kwny fastest growing economy in Africa na Wala hawakutetereka.
Waasi walipokimbia usidhani kuwa walikimbia mikono mitupu, wanaweza kuwa waliacha migobole lkn wakakimbia na dhahabu, almasi na rasilimali zingine ambazo zilikuwa rahisi kwao kubeba. Na nchi ambayo iliwapokea kwa wingi hao vijana ni Rwanda ikifuatiwa na Uganda.

Sasa hivi ishapita miaka 8 au 9 kwahiyo zile rasilimali walizokimbia nazo huko Rwanda zimeisha, kwahiyo wameamua kujipanga tena ili wakapambane na ikiwezekana wachote zingine.

Kwahiyo kwa sasa inawezekana na Burundi nayo imeamua ikatumie njia wanazotumia majirani wengine kujineemesha kupitia shamba la bibi kwa kujifanya kutuma jeshi la kupambana na hao M23 pamoja na Red tabara. Uganda yeye tayari ana sehemu yake ya kuchota since alipoingiza majeshi yake Congo kupambana na kina Joseph Kony nk.

Kenya inatoka mbali na haijui vizuri nini kinachoendelea katika eneo hilo. Imeingia kichwa kichwa na sasa itashangaa jinsi itakavyopokea kichapo huku wenzake Burundi na Uganda anaowategemea washirikiane wakiwa katika mashimo yao ya kuchimba dhahabu wakitorosha mzigo fasta fasta usiku kupitia katika mipaka yao inayopakana na Congo 😂😂😂
Kifupi Kenya yuko katika vita hii peke yake na atahenyeshwa kweli kweli.
 
Back
Top Bottom