Pre GE2025 Jeshi la Polisi: Hatujakubali au kukataa maandamano, tutawapa majibu tarehe 23

Pre GE2025 Jeshi la Polisi: Hatujakubali au kukataa maandamano, tutawapa majibu tarehe 23

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sheria ziko wazi kuhusu taratibu za kufuata kufanya maandamano, lakini kwa kwakuwa jeshi la polisi letu ni unprofessional, linasubiri maelekezo kutoka kwa wanasiasa walioingia madarakani kwa wizi wa kura. Hakuna kipindi nchi imekosa uongozi na muelekeo kama awamu ya sita
 
DJ ni DJ tu, sasa alikuwa anawahi wapi huyu jamaa,kawajaza ujinga wafuasi wake,maandamano hayapo,labda yafanyike kitandani
Yaani, anataka kuwaingiza chaka vijana wakavunjwe miguu badala ya kufanya shughuli zao za kiuchumi
 
Mbowe kaona hana jipya kaamua kutunga uongo eti polisi wemekubali bila hata kuwaonesha nyumbu kibali. Sasa watalalamika kwamba wamenyang'anywa kibali. Kumbe hakukuwa hata na mtu wa kuandamana.
FYI maandamano hayahitaji kibali.
 
ila maandamano yakikataliwa wakati ya Bawacha yalikubaliwa watakuwa wanalenga kumwangusha mama kidiplomasia na kisiasa. wacha waandamane imjenge mama kidemokrasia na 4R zake. CDM hata wakiandamana hawafanya lolote
 
Huu ndio ukweli wenyewe , Nimemhurumia sana Mulilo , yaani hana uwezo wa kuamua chochote !
Hivi chadema akili yenu huwaga iko sehemu gani ya mwili? Eti mtaandamana hadi ofisi za umoja wa mataifa (UN) ili umoja huo wa mataifa uiondoe hiyo miswada ya sheria za uchaguzi na za tume ya uchaguzi tunazotarajiwa kupelekwa bungeni?

Hivi hamjui taratibu za kufikisha suala lo lote kwa Umoja wa Mataifa na ni mtu gani au kikundi gani kinaruhusiwa kufikisha suala hilo ili likajadiliwe na umoja wa mataifa na kupigigiwa kura ya kuwa azimio la umoja wa mataifa?

Kama hamjui si mungalimuliza hata hata Zelenski au yule kiongozi wa Palestine namna walivyofikisha masuala yao Umojawa Mataifa? Kwani walifanya maandamano kuyafikikisha masuala yao huo UN?

Hivi mbajua kweli maana ya demokrasia? Kwa kifupi demokrasia maana yake ni wengi wape hata kama hukubaliani nao. Walio wachache kamwe hawawezi kushinikiza mambo yao yakubaliwe na walio wengi kwa kuandamana au kwa namna nyingine yo yote ile la sivyo mtaumia na baadhi kubaki kilema au hata kupoteza uhai kabisa.

Ushauri kwenu ni kwamba kazaneni kupata kuungwa na wengi kwa chaguzizi zijazo ili mkamate dola. Mkishakamata dola hayo mambo ya katiba mpya mnayoitaka, ya serikali tatu, serikali ya majimbo, tume huru ya uchaguzi mnayoitaka na kadhalika, mtayapata bila shida yo yote.
 
Huu ndio ukweli wenyewe , Nimemhurumia sana Mulilo , yaani hana uwezo wa kuamua chochote !
Mbona mapendekezo ya Kamati ya Haki Jinai iliyoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mhe Othman ilishauri Jeshi la Polisi liundwe upya! Ila utekelezaji wake naona . ni mgumu kwa sababu: ya kusemwa na ya kutendwa ni mambo mawili tofauti. Kwa hiyo usishangae juu ya uwezo wa polisi wa leo kutenda mema yanayostahili kwa mujibu wa wajibu wao. Ila baadhi ya polisi wanapoamua kufanya yasiyostahili, ubunifu wao hauna kifani! Kuna siku Mwenyezi Mungu atatupa kiongozi mtekelezaji atakayewezesha utawala bora hapa nchini. Inshallah!
 
Mbowe anataka kuwatoa chambo nyumbu wake itakuwa kama ya lipumba kilichomkuta maana hii nchi sio ya vyama vingi vya siasa ni ccm 4rever
 
Mbombo ngafu.....jidanganye kwamba maandamano yamekubaliwa!!!!
======

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limesema limekutana na Viongozi wa CHADEMA na kuwahoji kuhusu maandamano waliyopanga kuyafanya January 24,2024 na wamekubaliana kuwa watawapa majibu kimaandishi kesho January 23,2024 kama maandamano yawepo au yasiwepo na kusisitiza kuwa hadi kufikia sasa Polisi hawajakubali wala kukataa uwepo wa maandamano hayo.

Akiongea na TBC, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro amesema “Baada ya kuwaona Katibu Mkuu wa CHADEMA akitangaza kwa kutumia Vyombo mbalimbali kwamba tarehe 24 lazima atafanya maandamano suala hili tumelifuatilia kwa ukaribu na leo January 22,2024 tulimuita Katibu Mkuu wa Chama hicho lakini akatuma ujumbe wa Naibu Katibu Mkuu akiwa na wenzake na tumefanya nao mahojiano mbalimbali kwa kina kulingana na suala walilotangaza”

“Mimi nikiwa na Maofisa wa Kamisheni mbalimbali baada ya kuwasikiliza kwa kina na sisi kufuatilia kwa kina dhamira yao na kwasababu walituletea taarifa yao kimaandishi sisi hatujakubali au kukataa maandamano yao, majibu yao tumekubaliana kwamba tutawaapa kimaandishi kesho January 23,2024”

“Hatujaawambia maandamano yapo au hayapo kwasababu walituandikia barua kwenye Himaya zao na sisi majibu watayapata kwenye Himaya walizoandika barua hizo ambapo utakuwa ndio mwongozo wa nini kinafanyika huku tukizingatia masuala ya kiusalama na Maslahi ya Taifa kwa ujumla, tumezingatia suala la amani na majibu yao watayapata kesho”

Pia Soma; Mbowe: Makubaliano na Jeshi la Polisi yamefikiwa kuwa maandamano yataendelea kama yalivyopangwa

Pia Soma; CHADEMA yatangaza Maandamano Kupinga Miswada ya Sheria za Uchaguzi iliyowasilishwa Bungeni
Zigzaga Crew 🐒
 
Ccm huwa ni waoga mno, CHADEMA yenyewe mmeivunja vunji miguu lakini mnaigopa balaa
kama CHADEMA hawana woga si waendelee na masndamano January 24 kuliko hii kwenda kushoto kulia yaani hamjielewi kabisa....
Useless kabisa 🐒
 
Katibu mkuu ameogopa nn kwenda kituo cha polisi.?
 
..kamanda polisi atakuwa amepigiwa simu na kutishiwa kuyazuia.

..kungekuwa hakuna makubaliano Chadema wangeanza kupiga makelele bila kuchelewa.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa Chalamila atakuwa amempigia simu baada ya majadiliano na vyombo vya usalama.
 
Ni lazima uombe ulinzi wa polisi ili walinde amani katika maandamano yako. Bila polisi chawa wanaweza kujipenyeza na kuanzisha vurugu na uvunjifu wa amani ikawa ndiyo precedent ya kupokonywa hiyo haki ya kikatiba.

Polisi nao wana haki ya kukataa hasa wakiwa na taarifa za kiintelijensia kwamba kutakuwa na uvunjifu wa amani.

Ni haki ya kikatiba ndiyo lakini ni lazima kuwe na utaratibu!
Kwa akili zetu ndogo hao polisi ndio wanaokuaga chanzo cha vurugu.
 
Back
Top Bottom