Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi kuwekeza kwenye Research za HIV, COVID, Nuclear, Balistic Missiles, Ndege Jeshi, Submarines, wao wana hangaika na mitumba za Marehemu Wa Kizungu. Kiwanda chao cha Nyumbu kimeshindwa hata kuzalisha Bajaji za Abiria.
mkuu matusi ya nguoni hayaruhusiwi humu.😅😅😅
 
Watanzania uzuzu wetu umeanzia kuonekana hapa hapa kwenye huu uzi. Yaani kabisa kuna watu wanamdhihaki na kumwona Mwambukusi kama amekosea. Watu kama hao unatarajia kuna siku watakomboka na kuwa huru kifikra???
Watu wajinga Sana hata Mimi nimeshangaa Sana najiuliza asipojitolea mtu kusema Hali sijui itakuwaje .... Daah kazi ipo kweli
 
WAKILI MWABUKUSI ANATAKA MKUU WA MAJESHI AZUIE UVUNJIFU WA KATIBA.

"Nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kazi ya kukamata wa halifu ni ya Jeshi la Polisi. Jeshi la wananchi halina mamlaka kisheria na kikatiba kuingia kufanya msako mitaani kwa kisingizio cha kutafuta sare zao. Jukumu lao ni kulinda mipaka ya nchi. Cha ajabu hawajatuambia walizipeleka lini huko mitaani au zilichukuliwa na nani au waliibiwa lini? This is more than a comic [Huu ni usanii]!

Mwanajeshi hana mamlaka ya kupekua mtu katika makazi yake au maungo ya raia. Hii ni kazi ya Polisi wetu. Isipokuwa pale kunapokuwa na hali ya hatari au tishio dhahiri la mapinduzi.

Sheria inaruhusu kukataa ukamataji haramu na iwapo jeshi litaingia kwa namna hii ni haki ya wananchi kukataa ukamataji au upekuzi haramu usiofuata sheria ikiwemo kumshtaki Mwanasheria mkuu na Mkuu wa Majeshi ili kulinda sheria na Katiba ya Nchi na kudai fidia ya usumbufu.

Kama jeshi limeibiwa sare zake likaripoti Polisi. Polisi wafanye uchunguzi na wakibaini kosa Polisi ndiyo wenye utaalamu wa kupeleleza uhalifu wa wizi. Jeshi au wanajeshi hawako juu ya sheria [hivyo] wapunguze mihemko.

Kumekuwa na ujasiri wa uvunjaji katiba na sheria na kuwatisha wananchi katika taifa letu katika uongozi huu wa sasa na kwa hili hatutakubali na tutalitolea tamko rasmi kupinga vurugu hizi katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Majeshi awajibike haraka kuzuia ukora huu wanaotaka au kupanga kuufanya!

Najisikia aibu sana kuishi na kushuhudia viroja hivi. Mungu bariki Watanganyika! Mungu ibariki Tanzania! Mungu waadhibu na kuwakemea madhalimu wote.

Boniface Kajunjumele Mwabukusi!
Yupo sawa
 
Kuna kitu naanza kuhisi

Ukifikiri kwa makini lile tamko la JWTZ kuhusu sare za jeshi naliona kama lina mlengo mwingine tofauti na ambavyo limewasilishwa.

Kwanini kusalimisha sare kuambatane na msako wa nyumba kwa nyumba kukagua watu ambao hawajakabidhi sare?

Vipi kama hao wanajeshi wana agenda yao nyingine?

Kupitia sakata la bandari na jinsi upinzani walivyo chachamaa kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ubovu wa mkataba.

Huku wakihamasisha wananchi waukatae pamoja na kuongeza nguvu ya kudai katiba mpya, na mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa.

Vipi kama ujio wa wanajeshi mtaani hauna lengo la kukusanya sare bali kuwatisha raia ambao hivi karibuni wamekuwa wakihamasishwa kufanya maandamano ya kupinga mkataba?
Aisee, acha ondoa kabisa mawazo haya kichwani mwako...

Raia mpaka hatua hii hatuogopi cha polisi wala jeshi la wananchi (JWTZ)
 
Afrika wajinga wengi sana. Huyo atakuumiza akili.
Kusaka sare za jeshi, ni kazi ya polisi na siyo jeshi.
Ukiwa na bunduki kwanini wanakufuata polisi na siyo jeshi la wananchi?
Jwtz imekosa kazi.
Kweli kabisa. Unakumbuka kesi ya ugaidi ya mbowe na walinzi wake. Je uniform na silaha zilitolewa ushahidi na aliyezikamata ni jeshi au polisi. Sheria Zina mipaka yake
 
Watanzania kweli tuna safari ndefu. Ukisoma hoja za watu humu, unashangaa kuwa bado Kuna ujinga wa kiwango hiki!!
Mwabukusi yuko sahihi 100%. Hata mimi nilishangaa sana nilipomsikia yule msemaji wa jeshi na vitisho vyake.
Hivi huko Kenya wanakosumbuliwa na alshabab kila mara, huwa wamevaa sare za jeshi la Kenya?
Na kama ni kosa kwa nini wasitumike polisi? Kwanza ni aibu sana eti mwanajeshi anapekua nyumba ya mtu kwa kisingizio eti cha kutafuta sare za jeshi.
Ni uonevu mkubwa kwa raia waliokosa mtetezi.
Jeshi la ulinzi lina mipaka yake, na raia wamekuwa wakiliheshimu sana jeshi lao. Sasa wanajivunjia heshima kirahisi kama hivyo kusumbua raia!!
Na wananchi kwa sababu ya kujaa woga wa kijinga wanamshambulia Mwabukusi!!!
Jeshi linayo mambo ya msingi ya kufanya, kama ugunduzi, na ubunifu wa zana za kijeshi na siyo kuhangaika na vitu vidogo vinavyoshusha heshima ya jeshi.
Mbona hata wao wakitenda jinai wanakamatwa na polisi?
Nchi iendeshwe kwa utaratibu na kufuata sheria.
 
Eti jeshi kazi yake kusaka sare teh teh teh hili litakuwa Jeshi la zama za mawe za kale.

Wanaacha mambo ya msingi kama vile research and development linakwenda kusaka sare. Ndiyo maana lilikuwa likitoa show za kuvunja tofali kwa vichwa badala ya kuonyesha limegundua au kutengeneza silaha gani
 
Kweli kabisa. Unakumbuka kesi ya ugaidi ya mbowe na walinzi wake. Je uniform na silaha zilitolewa ushahidi na aliyezikamata ni jeshi au polisi. Sheria Zina mipaka yake
Jeshi la wananchi lina majukumu makubwa sana ya kulinda amani yaani litaaingia mtaani km kutakuwa na viashiria vya kuleta vita.
Polisi kazi yake kuhakikisha sheria inafuatwa ndiyo maana ina mahakama na magereza.
Jeshi linaingia mtaani kusaka sare za jeshi kwa raia ambaye hana bunduki?
Hiyo ni kazi ya polisi.
 
Namheshimu sana Mwabukusi na ninamuunga mkono katika baadhi ya mambo kama DPW. Au kupinga badndari zetu kugawiwa bure kwa DPW.
Ila ktk ili nadhani hatofautishe utendaji wa kazi za jeshi na polisi. Pia hatofautishe sheria zetu jinai na taratibu za kijeshi.

Ajiulize, kwanini jeshi lina mahakama yake ya kijeshi. Kwanini mwanajeshi akivunja sheria lazima kwanza taratibu zao za kijeshi zifuate avuliwe uanajeshi ndipo taratibu za kawaida za kijinai zifuatwe.

Anatakiwa ajue taratibu za kijeshi na intelligency za kijeshi. Jeshi halikurupuki kufanya jambo. Si mara ya kwanza jeshi kufanya zoezi kama hili. Nakumbuka miaka ya nyuma mkoa fulani zoezi ili lilifanyika na lilisaidia kuzuia uharifu. Yaani ukichekea watu hati sheria za kijinai unaweza shangaa unajeshi lisilo rasmi nchini. Au watu tayari wanamiliki silaha.

Na zoezi ili ufanywa na Military police. Wanajua taratibu tuache wafanye kazi.
H vs A kwenye ubora wake
 
WAKILI MWABUKUSI ANATAKA MKUU WA MAJESHI AZUIE UVUNJIFU WA KATIBA.

"Nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kazi ya kukamata wa halifu ni ya Jeshi la Polisi. Jeshi la wananchi halina mamlaka kisheria na kikatiba kuingia kufanya msako mitaani kwa kisingizio cha kutafuta sare zao. Jukumu lao ni kulinda mipaka ya nchi. Cha ajabu hawajatuambia walizipeleka lini huko mitaani au zilichukuliwa na nani au waliibiwa lini? This is more than a comic [Huu ni usanii]!

Mwanajeshi hana mamlaka ya kupekua mtu katika makazi yake au maungo ya raia. Hii ni kazi ya Polisi wetu. Isipokuwa pale kunapokuwa na hali ya hatari au tishio dhahiri la mapinduzi.

Sheria inaruhusu kukataa ukamataji haramu na iwapo jeshi litaingia kwa namna hii ni haki ya wananchi kukataa ukamataji au upekuzi haramu usiofuata sheria ikiwemo kumshtaki Mwanasheria mkuu na Mkuu wa Majeshi ili kulinda sheria na Katiba ya Nchi na kudai fidia ya usumbufu.

Kama jeshi limeibiwa sare zake likaripoti Polisi. Polisi wafanye uchunguzi na wakibaini kosa Polisi ndiyo wenye utaalamu wa kupeleleza uhalifu wa wizi. Jeshi au wanajeshi hawako juu ya sheria [hivyo] wapunguze mihemko.

Kumekuwa na ujasiri wa uvunjaji katiba na sheria na kuwatisha wananchi katika taifa letu katika uongozi huu wa sasa na kwa hili hatutakubali na tutalitolea tamko rasmi kupinga vurugu hizi katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Majeshi awajibike haraka kuzuia ukora huu wanaotaka au kupanga kuufanya!

Najisikia aibu sana kuishi na kushuhudia viroja hivi. Mungu bariki Watanganyika! Mungu ibariki Tanzania! Mungu waadhibu na kuwakemea madhalimu wote.

Boniface Kajunjumele Mwabukusi!


Alichosema ni ukweli, na naheshimu watu wa kweli na walionyoka, Je atapata mazara? Pengine atapata, Ila misingi, uhuru na Amani tuliyonayo sasa ililipwa na watu kama Mwabukusi miaka ya nyuma, ni Mpumbavu tu atakaye acha kupongeza hatu za Mwabukusi.
 
Back
Top Bottom