Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Namheshimu sana Mwabukusi na ninamuunga mkono katika baadhi ya mambo kama DPW. Au kupinga badndari zetu kugawiwa bure kwa DPW.
Ila ktk ili nadhani hatofautishe utendaji wa kazi za jeshi na polisi. Pia hatofautishe sheria zetu jinai na taratibu za kijeshi.

Ajiulize, kwanini jeshi lina mahakama yake ya kijeshi. Kwanini mwanajeshi akivunja sheria lazima kwanza taratibu zao za kijeshi zifuate avuliwe uanajeshi ndipo taratibu za kawaida za kijinai zifuatwe.

Anatakiwa ajue taratibu za kijeshi na intelligency za kijeshi. Jeshi halikurupuki kufanya jambo. Si mara ya kwanza jeshi kufanya zoezi kama hili. Nakumbuka miaka ya nyuma mkoa fulani zoezi ili lilifanyika na lilisaidia kuzuia uharifu. Yaani ukichekea watu hati sheria za kijinai unaweza shangaa unajeshi lisilo rasmi nchini. Au watu tayari wanamiliki silaha.

Na zoezi ili ufanywa na Military police. Wanajua taratibu tuache wafanye kazi.
Military Police, Martial court si kwa ajili ya raia.
Vyote hivyo vimeundwa huko huko jeshini kushughulikia maswala ya kijeshi.
Mnyororo wa utoaji haki kwa jamii hakuna pahala jeshi linaingia kwenye mnyororo huo. Wahusika wa mashtaka hapo utakuta ni polisi au takukuru lakini mwisho yataishia mahakama za kiraia kutoa haki.
Uwe na amani, hakuna sheria inayoizidi katiba KIMAMLAKA
 
Military Police, Martial court si kwa ajili ya raia.
Vyote hivyo vimeundwa huko huko jeshini kushughulikia maswala ya kijeshi.
Mnyororo wa utoaji haki kwa jamii hakuna pahala jeshi linaingia kwenye mnyororo huo. Wahusika wa mashtaka hapo utakuta ni polisi au takukuru lakini mwisho yataishia mahakama za kiraia kutoa haki.
Uwe na amani, hakuna sheria inayoizidi katiba KIMAMLAKA
[emoji106][emoji2956]
 
MARTIAL COURTS si muhimili wa dola....

Military courts inahusika na mambo ya jeshi tu....

Mwambukusi anaongelea sheria ambayo mhimili wake wa kuitafsiri uko MAHAKAMANI....

JWTZ waheshimu katiba ya nchi.....ninashangaa wana wanasheria wao...hawawasikilizi ?!!! [emoji15][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kazi ya jeshi ni kufanya oparesheni kubwa za kivita sio kusaka majambazi nimeona pia kama hapa kwa Matias kibaha wanajeshi wanaongoza magari kama traffic wakiwq na kombati
 
Watanzania uzuzu wetu umeanzia kuonekana hapa hapa kwenye huu uzi. Yaani kabisa kuna watu wanamdhihaki na kumwona Mwambukusi kama amekosea. Watu kama hao unatarajia kuna siku watakomboka na kuwa huru kifikra???
Hayo majitu ya hivyo ndio yanatuchelewesha mkuu, akili zao ziko matumboni. yakishashiba hela za kifisadi yanelewa kabisa!

yanafanya hizi nchi zinakuwa shithole!!!!


JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Watu wakikosa KAZI za kufanya ndio matokeo yake. Huwez acha shughuli zako ukaanza kupitapita mitaani kutafuta nguo za kijeshi.

Pia watu hawajui sheria ndio maana kuna huu ujinga ujinga.

Mie ninabegi la kijeshi kbs na kofia navaa muda wote na nikisafiri nabeba hilo begi. Nasubiri waje
 
Ukiwa na Akili na ukawa ni Msema kweli popote pale utakuwa ni target [emoji457]

Ukweli huwa Unauma !!
[emoji1787][emoji1787]
Ila mwenye akili na msema kweli huwa hasemi KWELI popote tu...chukua hii

#Karibu wanzuki hapa ubandani kwa mama Lily Sondombwa[emoji120]
 
Kuna kitu naanza kuhisi

Ukifikiri kwa makini lile tamko la JWTZ kuhusu sare za jeshi naliona kama lina mlengo mwingine tofauti na ambavyo limewasilishwa.

Kwanini kusalimisha sare kuambatane na msako wa nyumba kwa nyumba kukagua watu ambao hawajakabidhi sare?

Vipi kama hao wanajeshi wana agenda yao nyingine?

Kupitia sakata la bandari na jinsi upinzani walivyo chachamaa kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ubovu wa mkataba.

Huku wakihamasisha wananchi waukatae pamoja na kuongeza nguvu ya kudai katiba mpya, na mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa.

Vipi kama ujio wa wanajeshi mtaani hauna lengo la kukusanya sare bali kuwatisha raia ambao hivi karibuni wamekuwa wakihamasishwa kufanya maandamano ya kupinga mkataba?
Una hoja,utafika mbali,,,hii ndyo inaitwa kuwaza kwa sauti,hongera kwa kutumia vema ubongo wako,
 
Watanzania uzuzu wetu umeanzia kuonekana hapa hapa kwenye huu uzi. Yaani kabisa kuna watu wanamdhihaki na kumwona Mwambukusi kama amekosea. Watu kama hao unatarajia kuna siku watakomboka na kuwa huru kifikra???
Kabisaa aisee
 
WAKILI MWABUKUSI ANATAKA MKUU WA MAJESHI AZUIE UVUNJIFU WA KATIBA.

"Nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kazi ya kukamata wa halifu ni ya Jeshi la Polisi. Jeshi la wananchi halina mamlaka kisheria na kikatiba kuingia kufanya msako mitaani kwa kisingizio cha kutafuta sare zao. Jukumu lao ni kulinda mipaka ya nchi. Cha ajabu hawajatuambia walizipeleka lini huko mitaani au zilichukuliwa na nani au waliibiwa lini? This is more than a comic [Huu ni usanii]!

Mwanajeshi hana mamlaka ya kupekua mtu katika makazi yake au maungo ya raia. Hii ni kazi ya Polisi wetu. Isipokuwa pale kunapokuwa na hali ya hatari au tishio dhahiri la mapinduzi.

Sheria inaruhusu kukataa ukamataji haramu na iwapo jeshi litaingia kwa namna hii ni haki ya wananchi kukataa ukamataji au upekuzi haramu usiofuata sheria ikiwemo kumshtaki Mwanasheria mkuu na Mkuu wa Majeshi ili kulinda sheria na Katiba ya Nchi na kudai fidia ya usumbufu.

Kama jeshi limeibiwa sare zake likaripoti Polisi. Polisi wafanye uchunguzi na wakibaini kosa Polisi ndiyo wenye utaalamu wa kupeleleza uhalifu wa wizi. Jeshi au wanajeshi hawako juu ya sheria [hivyo] wapunguze mihemko.

Kumekuwa na ujasiri wa uvunjaji katiba na sheria na kuwatisha wananchi katika taifa letu katika uongozi huu wa sasa na kwa hili hatutakubali na tutalitolea tamko rasmi kupinga vurugu hizi katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Majeshi awajibike haraka kuzuia ukora huu wanaotaka au kupanga kuufanya!

Najisikia aibu sana kuishi na kushuhudia viroja hivi. Mungu bariki Watanganyika! Mungu ibariki Tanzania! Mungu waadhibu na kuwakemea madhalimu wote.

Boniface Kajunjumele Mwabukusi!
Huyu hajui kama jeshi pia wana Polisi wao.
 
Back
Top Bottom