Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Ni vizuri upitie sheria za jeshi ujue military polisi ana wajibu gani na wakati gani anaweza fanya majukumu yake. Na majukumu yake nipamoja na nini. Natumai uwezi niuliza tena hilo swali!

Jeshi (JWTZ) lipo kwa ajili ya raia. Halipo kwa ajili yake binafsi. Lipo kulinda amani ya nchi na mipaka ya nchi. Sasa ikitokea uniform za jeshi zimeenea mtaani unadhani nini kinafuata?

Nimeishi Ethiopia, uniform za polisi ilitokea zikaenea sana kwa raia. kuna muda ilikuwa ngumu kutambuia polisi halali ni yupi kwa kuangalia. Hii ilileta madhara makubwa ktk amani ya nchi.

Walichelewa kuchukua hatua hivyo ilibidi wabadili mavazi ya jeshi la polisi nchi zima. japo madhara yalikuwa tayari yameisha tokea.

Kazi ya polisi ni maswala ya jinai na si vinginevyo.

Ebu nitajie kifungu cha sheria za jinai kinachoeleza kukutwa na mavazi ya jeshi la wananchi. Hapo ndo utajua kuwa unapokutwa na magwanda ya jeshi ufikishwi mahakamani. Bali magandwa ya JWTZ ni mali yao wanachofanya ni kuyachukua na kurejesha kwao.

Kwa maswala ya amani ya nchi ebu tuache siasa na ushabiki. Waacheni jeshi wafanye zoezi la kurejesha magwanda yao. Na uzuri wameomba watu warejeshe wao wenyewe.

Ila wale wabishi ndo wao jeshi watawafuata majumbani au kokote waliko kuyarejesha. Shida hiko wapi?
Ujumbe mzuri kasoro tu hilo neno 'hiko wapi'..maana yake nini mkuu?
 
Kwa hiyo jeshi likipekuwa likakuta chupi za mabakamabaka nayo itakuwaje sasa?

Jeshi lisilo na kazi linapekuwa nguo za watu. Huu ni ujinga mtupu.

Wanataka kuliguza jeshi letu kuwa below vikundi vya ulinzi shirikishi. Ni aibu sana
 
Ujumbe mzuri kasoro tu hilo neno 'hiko wapi'..maana yake nini mkuu?
Na maanisha wale wanao lalamika jeshi kutoa tamko kuwataka walio na magwanda kurejesha. Mbona ni jambo la kawaida tu. Unagwanda rejesha.
Mara ngapi watu wamerejesha siraha walizo nazo isivyo kihalali bila kuchukuliwa hatua?
Jeshi wamesema usiporejesha watakuja wao wenyewe kuchukua kwani wanajua. Sioni shida jeshi kutoa tangazo. Kinachotakiwa watu waatii.
 
Na maanisha wale wanao lalamika jeshi kutoa tamko kuwataka walio na magwanda kurejesha. Mbona ni jambo la kawaida tu. Unagwanda rejesha.
Mara ngapi watu wamerejesha siraha walizo nazo isivyo kihalali bila kuchukuliwa hatua?
Jeshi wamesema usiporejesha watakuja wao wenyewe kuchukua kwani wanajua. Sioni shida jeshi kutoa tangazo. Kinachotakiwa watu waatii.
Silaha huwa zinarejeshwa polisi, sio jeshini.
 
Namheshimu sana Mwabukusi na ninamuunga mkono katika baadhi ya mambo kama DPW. Au kupinga badndari zetu kugawiwa bure kwa DPW.
Ila ktk ili nadhani hatofautishe utendaji wa kazi za jeshi na polisi. Pia hatofautishe sheria zetu jinai na taratibu za kijeshi.

Ajiulize, kwanini jeshi lina mahakama yake ya kijeshi. Kwanini mwanajeshi akivunja sheria lazima kwanza taratibu zao za kijeshi zifuate avuliwe uanajeshi ndipo taratibu za kawaida za kijinai zifuatwe.

Anatakiwa ajue taratibu za kijeshi na intelligency za kijeshi. Jeshi halikurupuki kufanya jambo. Si mara ya kwanza jeshi kufanya zoezi kama hili. Nakumbuka miaka ya nyuma mkoa fulani zoezi ili lilifanyika na lilisaidia kuzuia uharifu. Yaani ukichekea watu hati sheria za kijinai unaweza shangaa unajeshi lisilo rasmi nchini. Au watu tayari wanamiliki silaha.

Na zoezi ili ufanywa na Military police. Wanajua taratibu tuache wafanye kazi.
Huko shuleni mlisomea ujinga?

Mahakama ya jeshi ni maalumu kwa ajili ya wanajeshi!.Military police wanahusika zaidi jeshini.

Unapohalalisha wanajeshi kuingia mtaani "kusaka sare zao " inamaanisha

1)Polisi hawatekelezi majukumu yao
Ama 2)Wanaamua kuingilia mipaka ya polisi.

Kazi ya jeshi ni kutulinda wananchi ndiyo maana linaitwa LA WANANCHI
,na jukumu la polisi ni kulinda raia na Mali zetu.

Mwenye akili na asikie
 
Unaelezea uzoefu wako wa nchi mbalimbali kwa ajili ya kujibu swali la matumizi ya military police kwa raia!! Nikikwambia uzoefu wangu pengine hutarudia tena kujibu swali namna hiyo. Mafunzo na weledi wa Jeshi lo lote katika nchi inayoendeshwa kidemokrasia hayaelekezwi kwa raia. Raia ye yote ambae ana afya na mzalendo ni jeshi la akiba endapo nchi inaingia vitani. Nadhani ulikuwepo na ulikuwa unajitambua yaliyofanyika Tanzania ilipombana na Idd Amin wa Uganda. Kwa sababu hiyo nguvu za jeshi kwenye nchi yo yote inayojitambua na inayothamini utawala wa sheria haiwezi kuelekezwa kwa jeshi lake la akiba. Suala la sare za Jeshi lishughulikiwe na polisi vinginevyo ni kulidhalilisha wanajeshi wetu na jeshi lenyewe. Serikali ilikuwa wapi mpaka sare za jeshi zinazagaa? kama zinakuja kama mitumba au zinaagizwa au kushonwa hapa nchini Serikali ndiyo inaweza kuwachukulia hatua wahusika. Governance! Governance. Governance!
Nadhani hujui pengine demokrasia ni nini na Governance ni nini? Wazungu walio kudanganyeni na demokrasia jiulize huko kwao kuna demokrasia? Je Rais wa Marekani anachaguliwa na nani? Ni nani hutoa maamuzi kuwa sasa huyu ndo Rais? Na hiyo demokrasia inataratibu zake. Unajua Marekani kuna maeneo Jeshi ndo wanatumika kuzuia vitendo fulani. Mfano kuna maeneo uwezi piga picha. Na hayajaandikwa. wakikukamata wanauwezo kuchukua hatua yoyote.
Kwanini wasiite polisi wafanye wao jeshi? Si Marekani tu ni katika nchi nyingi duniani. Military domain uwezi ukaichanganya na polisi au demokrasia.

Sijaona wapi raia kanyanyaswa. Tangazo limesema wenye uniform za jeshi rudisheni. Huo ni unyanyasaji? Huko ni kuharibu demokrasia? Tena wakasema msiporejesha tutakuja wenyewe kuchukau. Unyanyasaji huko wapi?

Unadai raia ni jeshi la akiba kwani polisi si jeshi la akiba? Hivyo kwa maelezo yako polisi akihusika si nae atakuwa anamnyanyasa jeshi la akiba aliye raia? Ha ha ha ha!

Jeshini tu wanajeshi akikosewa anashitakiwa na anauwezo kufungwa au kuvuliwa ujeshi si wangesema wananyanyasa jeshi? Yaani raia ahatarishe amani ya nchi muwache ati ni jeshi la akiba! Ha ha ha!

Si kweli kwamba raia ni jeshi la akiba. Kwa sababu ajachukua mafunzo yoyote ya kijeshi na kuthibitishwa kuwa mwanajeshi kwa kiapo.
Nadhani hujui maana ya jeshi la akiba. Hakuna raia aliye pigana vita ya Iddi Amini. Ili upigane vitani kwanza lazima upokee mafunzo ya kijeshi, kukuwezesha kujua mbinu za kivita. Kulinda na kujilinda kisha unapelekwa vitani. Hapo utakuwa umekuwa mwanajeshi.

Hata wakati wa Idd Amini watu waliingia Mgambo wakafundishwa. Ndo maana Mgambo ni jeshi la akiba ambalo liko chini ya JWTZ. Uwezi sema kila raia ni jeshi la akiba. Ndo maana kuna raia na jeshi.
 
Sana tu, katukana viongozi kimyaa, kamtukana Rais kimyaa, Kawatukana police kimyaa sasa anataka kutest maji, Nadhani atawataja walioko nyuma yake very soon. Ana act kama vile ndio kahamia Tanzania juzi wakati jitu lina miaka 60 huko. Nchi zote duniani watakosoana lakini siku zote wanalipa jeshi lao heshima hata kama kuna mapungufu. USA walisema hakuna mwanajeshi wao atashtakiwa kwa kuvunja haki za binadamu japo wao ni machampion wa mambo hayo. Israel alikataa wanajeshi wake kushtakiwa.. na wengine wengi. Hawa sio wajinga. Sasa huyu kafika sehemu anataka kuhatarisha amani ya nchi. shida hapa ukiwakashifu jeshi au police na wakakulia kimya unafungua mlango na kufunga itakuwa too late. Mshughulikieni huyu haraka.
Katukana tusi gani?kwanini wasimchukulie hatua?Jeshi lifuate sheria za nchi,mambo ya kukaa kambini bila kazi ndio matokeo yake haya.
 
Tunahitaji wananchi wote wawe na uelewa, wajue majukumu ya kila taasisi na yao pia kisheria, waweze kutambua haki zao ili waweze kupambana katika dunia yya ushindani.
Umasikini wa nchi una uhusiano mkubwa sana na kujielewa kwa jamii na raia kwa ujumla.
Hoja za Mwabukusi ni za msingi sana katika kujenga uzalendo kwa sababu hakuna mzalendo wa kweli ambaye ni muoga kwa sababu ya ujinga au kutojielewa.
Raia wengi wa nchi tajiri wana uelewa na siyo waoga ambapo katika nchi masikini ni kinyume chake.
Kuwa na raia wasio waoga, wenye uelewa na majasiri ni manufaa kwa nchi na kinyume chake ni hasara kwa nchi na dunia kwa ujumla.

Hakika!
 
90% Kwa wanaopinga operations nguo jeshi wanahisia za uharifu! Ni zoez la kawaida sanaaaa kwahy unahitaji polisi ndio wafanye kazi hiyo kwakuwa mnawamudu? Ukumbuke vazi la jeshi la ulinzi la wananchi hata hao polisi wanavaa na nikosa pia, kwahyo tuache watu wafanye kazi tupunguze uraiya ambao hauna afya Kwa taifa letu,,, tusitete uharifu ukumbuke hata mwanajeshi akivaa uniform/ Kombat nje ya muda wa kazi ni kosa ,, Sasa Kwa raia inakuwaje? Tuache kuiga mataifa mengine!
 
Ila jamani gharama za maisha zimepanda mno, mafuta juu, vyakula bei navyo juu, dola imepanda, corona ilitutisha sana, watu wana ugumu mno, sasa na JWTZ itutie hofu hivyo jamani, tutaishi vipi lkn? Mwananchi wa kawaida si atakufa kwa stress na hofu kila kona, uanze kupekuliwa nyumba kwa nyumba, haya maisha gani? Mkuu wa Jeshi azuie hii hofu maana JWTZ wakiingia mitaani itazua taharuki sana sana, waacheni watu wapambane na maisha sio kupambana na JWTZ..
Kupekuliwa nyumba kwa nyumba ni maisha fulani ya kikomunisti yaliyopitwa na wakati.

Sheria za nchi zilizoendelea zinatakiwa kuwa na vipengele vya kukataza "unreasonable search".

Yani mpaka nyumba yako isachiwe, inatakiwa iwepo warrant ya mahakama, jaji kaitoa kwa kuridhika kuwa kuna sababu maalum ya kui convince mahakama kutoa ruhusa nyumba yako isachiwe. Nyumba yako kama nyumba moja, si katika fungu la mkumbo wa kutafuta nguo za polisi.

Na warrant inatakiwa iwe specific kinachotafutwa ni nini, warrant ya kutafuta nguo za jeshi hairuhusiwi kukamata madawa ya kulevya.

Mwabukusi anaelimisha jamii kwamba, kadiri tunavyotoka kwenye mifumo ya kipolisi inayoongozwa na sheria na mahakama na kupeleka habari za search kwenye jeshi, ndivyo tunavyoondoka kwenye hiyo due process iliyowekwa kisheria na kwenda kwenye mfumo wa shaghalabagala ya kuendeshwa kijeshijeshi.

Watu wanaoishi nchi zenye kufuatilia sheria dhidi ya unreasonable search, kama Marekani, watamuelewa sana Mwabukusi hapa.
 
Ila jamani gharama za maisha zimepanda mno, mafuta juu, vyakula bei navyo juu, dola imepanda, corona ilitutisha sana, watu wana ugumu mno, sasa na JWTZ itutie hofu hivyo jamani, tutaishi vipi lkn? Mwananchi wa kawaida si atakufa kwa stress na hofu kila kona, uanze kupekuliwa nyumba kwa nyumba, haya maisha gani? Mkuu wa Jeshi azuie hii hofu maana JWTZ wakiingia mitaani itazua taharuki sana sana, waacheni watu wapambane na maisha sio kupambana na JWTZ..
Hutakiwi kuwa na hofu kama sio muarifu!
 
Wewe ndo hutumii akili kwa sababu hujui majukumu ya jeshi. Mmekariri vita tu. Ha ha ha! Ingekuwa jeshi linasubiri vita kwanini mabalozi wengi duniani ni wanajeshi.

Kwa nini maofisa wengi balozini ni wanajeshi. Si wangekaa kambini kusubiri vita kama unavyomaanisha.

Kwanini kamati za usalama za nchi nyingi hata hapa Tanzania kamati za usalama zinajumuisha wanajeshi, anzia wilayani, mkoa hadi Taifa. Unajua vikao vya ulinzi na usalama vinajadili maswala gani?

Ati serikali! Unajua hiyo serikali inavyoendeshwa? Unajua mambo yote unayoyaona kuanzia kijinini kwenu, wilayani, mkoani hadi Taifa jeshi wanahusikaje?

Kwa taarifa yako humu duniani serikali zote zinategemea jeshi. Si maswala tu ya vita hata na mengineyo.

Kagame, na ethiopia wanaongoza kwa kuwa na wanajeshi wengi nje hawako kivita wapo kwa kazi maalum. Marekani, Uingereza, Ufaransa, na nchi zinginezo wanajeshi ndo maintellijensia wa uchumi. Jeshi linakazi zaidi ya vita.

Tafakari ndugu yangu. Unajua mambo unayoyaona nje ni tofauti na inavyokuwa ndani.
Mfano tu wakati Rais Magufuli amefariki kulitokea matafaruku nani ashike nchi, kuna baadhi ya viongozi waliosema Makamu wakati huo Samia hawezi. Ili liko wazi. Mama Samia alilisema na Mkuu wa Majeshi wakati huo aligusia kidogo.
Ni Mkuu wa majeshi ndo alie toa msimamo kuwa katiba ifuate wote wakaufyata! Kwanini Mkuu wa jeshi aliingia katika kikao cha serikali si angekuwa kambini kwa msemo wako.

Narudia jeshi si vita tu!
Acha bang3 wewe. Unadhani tungekua na serikali ya mseto na mpinzani akiwa ameshikilia ile nafasi ya VP huyo Mkuu wako wa Majeshi angetoa ule msimamo? Jeshi ilikua enzi za Nyerere, hawa wasasa ni wachumia tumbo na VIBARAKA WA CCM. Kazi yao ni kuhakikisha chama twawala kinaendelea kusalia madarakani bila bugdha
 
UKIKAMATA TURUFU ITUMIE VYEMA!
1694251470374.png
 
Nadhani hujui pengine demokrasia ni nini na Governance ni nini? Wazungu walio kudanganyeni na demokrasia jiulize huko kwao kuna demokrasia? Je Rais wa Marekani anachaguliwa na nani? Ni nani hutoa maamuzi kuwa sasa huyu ndo Rais? Na hiyo demokrasia inataratibu zake. Unajua Marekani kuna maeneo Jeshi ndo wanatumika kuzuia vitendo fulani. Mfano kuna maeneo uwezi piga picha. Na hayajaandikwa. wakikukamata wanauwezo kuchukua hatua yoyote.
Kwanini wasiite polisi wafanye wao jeshi? Si Marekani tu ni katika nchi nyingi duniani. Military domain uwezi ukaichanganya na polisi au demokrasia.

Sijaona wapi raia kanyanyaswa. Tangazo limesema wenye uniform za jeshi rudisheni. Huo ni unyanyasaji? Huko ni kuharibu demokrasia? Tena wakasema msiporejesha tutakuja wenyewe kuchukau. Unyanyasaji huko wapi?

Unadai raia ni jeshi la akiba kwani polisi si jeshi la akiba? Hivyo kwa maelezo yako polisi akihusika si nae atakuwa anamnyanyasa jeshi la akiba aliye raia? Ha ha ha ha!

Jeshini tu wanajeshi akikosewa anashitakiwa na anauwezo kufungwa au kuvuliwa ujeshi si wangesema wananyanyasa jeshi? Yaani raia ahatarishe amani ya nchi muwache ati ni jeshi la akiba! Ha ha ha!

Si kweli kwamba raia ni jeshi la akiba. Kwa sababu ajachukua mafunzo yoyote ya kijeshi na kuthibitishwa kuwa mwanajeshi kwa kiapo.
Nadhani hujui maana ya jeshi la akiba. Hakuna raia aliye pigana vita ya Iddi Amini. Ili upigane vitani kwanza lazima upokee mafunzo ya kijeshi, kukuwezesha kujua mbinu za kivita. Kulinda na kujilinda kisha unapelekwa vitani. Hapo utakuwa umekuwa mwanajeshi.

Hata wakati wa Idd Amini watu waliingia Mgambo wakafundishwa. Ndo maana Mgambo ni jeshi la akiba ambalo liko chini ya JWTZ. Uwezi sema kila raia ni jeshi la akiba. Ndo maana kuna raia na jeshi.
Kwa sababu wewe unajihesabu kama unajua basi hufundishiki. Jeshi kwenye vita huwa ni watangulizi tu; nchi ikiwa kwenye vita raia ye yote anakuwa mpiganaji ila nani na anakwenda kwa kipindi kipi jeshi ndilo linaratibu. Hiyo demokrasia nyeusi au nyeupe unayotaka kutuambia Tanzania inaweza kuigundua sasa unarudia tu propaganda za watu wasiofikiri au wanaotaka kuturubuni. Demokrasia ilikuwepo hata kabla ya Wagriki waliisemea. Hiyo demokrasia ya Tanzania unayoijua wewe ni ipi? Ya kuwaacha watu wabaki wajinga ili uendelee kuwatawala? Unakumbuka Tanzania ilifikia kiwango cha demokrasia kiasi cha wasomi wa kimataifa kuja kujifunza hapa. Sasa ile demokrasia bado ipo? Ndiyo maana huelewi kuwa Jeshi letu lilianzishwa kama Jeshi la Wananchi na ndiyo maana tunasema lichukue hadhari linapokuja kwa wananchi kwa sababu mafunzo ya namna ya kushughukikia jinai au madai ni polisi ambao wamefunzwa, siyo Jeshi. Ni sawa vita itokee ukasema IGP ndiye atakayepiganisha vita. Kama huelewi ninachosema basi nimekata tamaa; bila shaka wewe una uzoefu na ni msomi kupita wote hawa ambao wana maoni tofauti na wewe.
 
Sana tu, katukana viongozi kimyaa, kamtukana Rais kimyaa, Kawatukana police kimyaa sasa anataka kutest maji, Nadhani atawataja walioko nyuma yake very soon. Ana act kama vile ndio kahamia Tanzania juzi wakati jitu lina miaka 60 huko. Nchi zote duniani watakosoana lakini siku zote wanalipa jeshi lao heshima hata kama kuna mapungufu. USA walisema hakuna mwanajeshi wao atashtakiwa kwa kuvunja haki za binadamu japo wao ni machampion wa mambo hayo. Israel alikataa wanajeshi wake kushtakiwa.. na wengine wengi. Hawa sio wajinga. Sasa huyu kafika sehemu anataka kuhatarisha amani ya nchi. shida hapa ukiwakashifu jeshi au police na wakakulia kimya unafungua mlango na kufunga itakuwa too late. Mshughulikieni huyu haraka.

Ushamba na akili za kitumwa! Bora muendelee kuwa masikini wa kutupwa maana mnastahili!
 
Back
Top Bottom