Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Daah story ni tamu sana kuna vitu vingi sana nimejifunza your the best bro sema umekata Tamaa haraka sana
Uwezi AMINI watu wengi wanafatilia huu Uzi ujui ni wangapi wanajifunza kutokana na hicho ulichoandika

Usisitishe kile ulichokianza kama Kuna kitu umekusudia watu wajifunze endelea Tu
Maneno Huwa yapo Tu yasikufanye uache kutusimulia kile ambacho ulitaka hasa tujifunze kama haters ni 2 Kwa 200 wanafatilia uoni kama hutendei haki wale wenye Nia ya dhati ya kutaka kujua nn kimejili
Usikate Tamaa kiboya be strong move on bro
 
Dah kwahiyo umeamua kuwasikiliza mbweha walio wachache kuliko sisi wadau wako, mkuu umetuangusha[emoji21]
 
[emoji23] nyie sio watu wazur mmetuharibia Uzi wetu aisee
 
Ukiangalia watu mnaojifanya kujua literature criticism ni wale mme join 2014-2020 , means they are matured people who in one way or another Wana ka frustration ya maisha after what magufuli did to them financially...Sasa Wana hasira na yeyote anaye onekana kuwa au kuzungumzia maisha Bora... Shida si sisi wenyewe kwa wenyewe ...ni CCM ndio imetufikisha hapa tulipo...tupeleke/ tuelekezeni frustration zetu huko.
 
Sure, thread ikikosa critisim haiwezi toboa ht, kwnz insider anatakiwa ajivunie maana wafuatiliaji wamekua Ni active na wengi,
 
Jf ilikua nzuri sana miaka ya nyuma kidogo kabla vijana wengi maJobless hawajaanza kumiliki simu, ambazo wamekua wakizitumia vibaya kutokana na stress za ukosefu wa ajira [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wewe fala kasome.vizuri jamaa amelipa dollar 6500 sawa na million 17.

Aliyetaka kumbaka iryn.

Hivi million 17 mnaijua nyie.

Halfu insider akampa mlinzi elfu 50 chai chai
Kuna siku nilikuwa kijiji kimoja usukumani kwetu. Simu niliyokuwa nayo ilikuwa ni infinix hot 10 play. Kuna jamaa akaniuliza ni bei gani. Nikamwambia nimenunua laki tatu na hamsini. Akashangaa sana akanijibu hao si mbuzi karibu 10. Sasa yeye alikuwa na tecno ya button, nikamuuliza yako sh ngapi? Akaniambia ef 40. Nikamwambia nawe ni sawa na kuku 10. Akacheka sana, ila tukaelewana.

ukielewa utofauti wa mazingira na uthamani wa fedha wala haikushangazi.

Wewe ukiingia bar hapo ukatumia 50 wala si ajabu, ila nenda kijijini hela hiyo tumia kwe pombe pale 'senta', kijiji chote kitapata taarifa zako.
 
Sijawahi ku comment huku hata siku moja ila nimegundua huku kuna watu wana mambo ya ajabu saaba any way

Maisha yako usinifananishe na maisha ya mtu mwingine ukiona kwako haiwezekani kwa mwingine inawezekana.

Bwana insider kaamua kusitisha story hata kama ndo mimi ningefanya hivo.

Asante sana bwana insider nimejifunza vingi.
 
Bwana mdogo na ukali wote wa maneno kumbe fundi uashi, embu jaribu kuwa mstaarabu kwenye nyuzi za watu. Pia kumiliki pasi ya kusafiria sio ujanja, unaweza kuwa nayo na usiitumie ipasavyo kama inavyotakiwa.
Mfano mm Nina leseni ya gari Ila mpk Leo hii sijaendesha gari coz I'm not interested [emoji23]
 
3. Aliomba msaada maana akikutana na dem wake anakojoa haraka, aliomba ushauri humu JF. [emoji23]
 
Mdugu zangu nitamalizia hii story sababu ya heshima ya JF. Kuna watu wengi wamenitumia ujumbe na watu ambao nawaheshimu wameomba nimalizie story.

Nimegundua story inafuatiliwa na watu wengi sana mpaka sasa tuna views almost 400k ni watu wengi sana.

Nitawapa mwendelezo na huu mwezi 8 story yetu itakuwa imeisha yote.

Kitu kingine sitajibu swali lolote kwa mtu atakayeuliza, ila nitajibu maswali yote baada ya kumaliza kuandika story.

Naomba heshima iwepo kwenye uzi kusiwepo na watu kutukanana sio jambo jema sisi sote ni Watanzania japo kuna foreigners pia wanapitia huu uzi. Kwa mtu ambaye atakiuka na kuleta taharuki nitamreport kwa mods waangalie namna ya kudeal naye.

Kama unaona huwezi kwenda na hii story unaweza uka ignore huu uzi, ukaacha watu ambao wako tayari kusoma.

Nilikua naomba mfanye maamuzi nyinyi wenyewe;

1. Niandike Epsode zote then nizipost?

2. Ndani ya week niwe napost episode 3?

Option ipi kwenu itafaa?

BY INSIDER MAN
 
hahahaha watu wameshavurugwa...
 
Mkuu kwanza nashukuru umézingati maombi ya sisi wasomaji wako kuturudishia burudani hii nzuri.

Pili, option ya kwanza ni nzuri zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…