Ndugu Mwandishi,
Mosi, naona umeanza kumuweka Mwanadamu kwenye kundi la Primates yaani viumbe jamii ya manyani na masokwe n.k n.k, ni kweli tupo humo lakini kuna kitu kimoja ambacho kinatutofautisha licha ya ufanano wetu kwa asilimia 99, nacho ni UTASHI WA KUAMUA JEMA NA BAYA, Je huoni kuwa kwa kuwa amekosa utashi ndio anaamua kuoa majike mengi.
Pili, naona umesema kuna manabii waliona faida ya kuwa na wake wengi, na declare interest mie ni Mkristu na naomba unisaidie kunitajia hao manabii, just curious... Nimeshuhudia ndoa nyingi za mitala hasa za waislamu asilimia kubwa wanazidiss, wanasema uke wenza ni kazi.
Tatu, umesema tuzingatie law of demand and supply lakini umesahau kuwa hii law inatumika under certain conditions either being "ceterius paribus" ama ile ya "mutatis mutandis", Je unadhani ni sahihii kutumia hii law na ikawa effective katika hoja tajwa.
Mwisho, umeongelea kitu MVUTO au UZURI, nadhani hapa pia inabidi uwe specific unapoongelea uzuri una maanisha nn, mm ninachoelewa inawekana ukamuona mwanamke X mzuri kwako lakini mtu mwingine akamuona huyo mwanamke X si chochote, kwa muktadha huo am sure wanawake wote wanaweza kupata wenza regardless of mvuto unaoongelea ww.
Hitimisho, KAMA IMANI YAKO, UTASHI WAKO NA UWEZO WAKO UNAKUAMBIA MUME MMOJA KWA WAKE WENGI NI SAWA THEN GO FOR IT, MASUALA YA KUCOMPARE NA PRIMATES, MANABII SIJUI LAW OF DEMAND AND SUPPLY SIDHANI KAMA NI SAWA.