Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Ndugu zangu wana JF kwa heshima ya watu wote humu ndani naomba kuisotisha hii story iishie hapa sitoimaliza maana inaonekana ni chai. Na mimi siwezi kupoteza muda kuandika kitu ambacho watu wanasema ni uongo.

Nina mambo na majukumu mengi ya kufanya na hakuna anayenilipa kwenye hii story, napoteza muda wangu kuwapa watu story kilichonitokea na mpaka nikaamua kuandika lakini inaonekana ni 0,

Nafikiri kila mtu aendelee na mambo yake kwa stage iliyofikia kumaliza story itakua ngumu, nafikiri tuishie hapa. Kama mtu ameshasema story ni chai kuna haja gani ya kuendelea kuandika?.

Kwa wale tuliokuwa pamoja ahsanteni kwa muda tulionza pamoja ila mimi binafsi nimeshindwa kuendelea kuandika, maana watu wanakatisha sana tamaa.

Story haijaisha hapo niko na matukio ya March, lakini mtu kashaaanza kutukana, haters wamekua wengi, lakini hii ni JF kila mtu anahaki ya kuongea. Ustaarabu mngesubiri story iishe hapo ndo muanze kujudge, maana hivi vyote nilivyoandika na ushahidi navyo kwa picha, Contracts nilizoingia nawateja zangu zote ninazo mpaka Iryn.

Story haijaisha mtu watu wameanza kukosoa anyway ndo wabongo walivyo, sinaga muda na JF ila haya matukio yalinitokea ni kweli na nilikua ndo nimeanza kuingia kwenye kiini cha story na nilikua nimepanga kuandika Epsodes 30 tu.

Wabongo tunakosa kitu kinaitwa patient hapa ndo tunafeli sana, story haijaisha hata mjue lengo la kichwa cha story lakini watu wameanza kushout. Siwezi endelea kuandika kwa style hii inakatisha tamaa, ndomana story nyingi za JF zinaishia njiani.

Wale ambao tunawasiliana PM na tumebadlishana namba tutaendelea kuwasiliana tuko pamoja, ila niseme biashara ya Uber ilinipa mafanikio sana na mpaka sasa naendelea kunufaika.

ALL THE BEST
Hao wanaosema hii story ni chai ni asilimia ngapi ya wasomaji wote wa hii story?..

Mimi kama mwanaume siwezi kukubembeleza uendelee kuandika story..ila jua ulichokiamua ni uamuzi usio na busara.
 
Nasikitika Sana kumkosa kijana makini anayestahili kila heshima.

Nashindwa kuelewa jambo moja kwa nini usibaki na wastaarab wanakukubali kuliko kujibizana na watoto wajinga? Maamuzi ni yako INSIDER MAN

Kama ni mkeo kwa jinsi ulivyomuelezea ni make Bora, unafanyakazi nawadada Bora Irini kwetu sie wamama tunaelewa kuna kuzidiana urembo.

Una wazaz wenye hekma umetumegea visehemu vya heshima na busara nyingi zimo kwenye Uzi wako kwanini umeshindwa kupima kwanba viewers Wengi Sana tunakukubali, uamuzi ni wako kaka
 
Jamani hebu tuachane na hizi kelele, tutumie muda huu kumshawishi mwandishi aendelee na story au mnasemaje? Kila mmoja wetu aende pm ya insider man tumuombe aendelee na story maana alishafika pazuri sana. Lakini pia tusimpinge medecin kwa anacholalamikia nae tumuombe aache mada iendelee.
 
Daah! Arosto niliyokuanayo kwa BM X6,nakutana nayo na apa tena...(iryn kama carryn kwa mbaliii)
Kumbe ya BM X6 uliisoma Mkuu! ebu zipe max ipi kali kati ya story hii na ya BM?

Then kwa hao warembo (Caryn & Iryn) yupi unadhani machacha zaidi na aliyekukosha?
 
Jamani hebu tuachane na hizi kelele, tutumie muda huu kumshawishi mwandishi aendelee na story au mnasemaje? Kila mmoja wetu aende pm ya insider man tumuombe aendelee na story maana alishafika pazuri sana. Lakini pia tusimpinge medecin kwa anacholalamikia nae tumuombe aache mada iendelee.
Kwann mnamuabudu medecin
 
Jamani hebu tuachane na hizi kelele, tutumie muda huu kumshawishi mwandishi aendelee na story au mnasemaje? Kila mmoja wetu aende pm ya insider man tumuombe aendelee na story maana alishafika pazuri sana. Lakini pia tusimpinge medecin kwa anacholalamikia nae tumuombe aache mada iendelee.
Pm imefungwa labda wale ambao mnaaccess nae mfanye hivyo
 
Kwann mnamuabudu medecin
Hatumwabudu ila hoja yake ina mashiko, hoja yake ni kuwa story sio ya kweli na watu wamekiri kuwa katika kusimulia lazima kuna mambo utaongeza kunogesha story sasa hapo kuna tofauti gani na story ya kutunga?

Insider aseme kweli kuna matukio kachezesha ila hayana ukweli.
 
Ametoa mawazo nyie mnamjaza upepo...

Tumekosa Sasa ndio atakuwa na amani?

Ukisikia uchawi ndio huo, nyote wachawi.

Wadada tunahangaika kuachna na umbea nashangaa wanaume wanaubeba
Basi cha kufanya tuwaambie mods wamblock medecin asipate access ya kucomment japokuwa haitakuwa haki maana hili ni jukwaa huru na hajavunja sheria yoyote sana sana katoa mawazo yake tu.
 
Hivi unapata shida gani huko moyoni juu ya hii story? Mbona ccm inakudanganya Kila siku na bado unaitikia hewala🤲.

Kama mnaona hii story inauongo Basi mtuambia ukweli ni upi.
Rafiki yangu mi naishi uhalisia hiyo ccm unayoitaja naijua rangi ya bendera yao tu ni kijani, kiufupi sifuatilii siasa hata chembe, hivyo hapo unansingizia fuatilia hata comments zangu huwezi kuta nimeshobokea siasa sijui bandari sijui kuuzwa kama kuuzwa tushauzwa kitambo hapo ni kubadilishiwa mteja tu.
Sema mi napenda uhalisia usitupange simulizi ya ukweli afu ndani uhalisia hamna, na katika kazi ya fasihi inatakiwa iburudishe, ielimishe ili watu waifuatilie lazima isisimue sio unasoma story za mtu za daily routine ye kila siku ni anakutana na zali la mentali tu, hata wanaotumia ndumba (hata masonia) au wanaomtegemea mungu kuna ups and down za kutosha, kujisifu kwingi sijui gentlemen sijui mstaarabu hizo promo tunazijua. Mi mwenyewe nikiamua kukufunga kamba kwa story nakufunga na hamna boya anashtuka ila ukiona mtu kashtukiwa na watu wawili watatu ujue kuna walakini
 
Back
Top Bottom