Jinsi Introverts wanavyopata tabu kuingiliana na watu wanaowazunguka

Jinsi Introverts wanavyopata tabu kuingiliana na watu wanaowazunguka

Hivi kushindwa kusamehe ni tabia ya introvert pia au ni litabia langu tu libaya?. Binafsi huwa sio mtu wa kukasirika kirahisi, mtu anaweza kunifanyia kitu kibaya sana na nikawa namchekea tu. Ila ikitokea siku nikakasirika, hiyo ndo nitolee....hata atembee kwa magoti kutoka kwake hadi nilipo siwezi hata kifikiri kumsamehe.


Huu ni mwezi sasa tangu rafiki yangu wa karibu sana (jinsia ke) anitamkie kauli ambayo sikuipenda (si kauli mbaya sana kiasi hicho na nadhani alisema katika hali ya kunitania), kuanzia siku hiyo nilamfungia vioo. Ametuma meseji kibao akiniomba lakini sijajibu hata meseji moja na sina mpango wa kujibu, amepiga simu sana lakini sipokei na sina mpango wa kupokea. Mpango nilionao ni kumwondoa mbali kabisa na maisha yangu.


Yeye ndiye alikuwa alikuwa rafiki yangu wa pekee wa kike. Tumepitia nyakati nzuri sana na yeye tukiwa kama marafiki wa karibu.


Sasa hivi nimebaki mwenyewe tena, nikiwa alone ni mwendo wa kubadili vifaa tu. Mara nishike simu, mara nishike peni na daftari, mara nitupe peni nichukue penseli, mara nishike pc, mara nishike kitabu.


Ila napenda jinsi nilivyo.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kauli gani hiyo
 
Hiyo hali ya kuulizwa 'mbona unaonekana una mawazo sana!?' ishanitokea mara nyingi sana; kwenye daladala, darasani, nk.

Nakumbuka kuna kipindi nilikiwa na utaratibu wa kwenda kukaa kwenye lile daraja la wapita kwa miguu la pale ubungo mida ya usiku. Nilikuwa naenda kukaa sehemu ambako movement za watu sio nyingi na kuanza kutafakari kuhusu mambo mbalimbali.

Sasa kuna siku moja dada mmoja akanifuata na kuanza kuniuliza nina shida gani mbona nimekaa mpweke na inaonyesha nina matatizo. Nikamwambia mi niko fresh wala hata asiwaze sana kunihusu. Lakini yeye akaendelea kunikazia kuwa nina shida so nimwambie, nikaona kama ananizingua, Nikanyanyuka nikasepa nikaenda kukaa sehemu nyingine huku yeye akiona.

Ni kama ukichaa flani hivi, ila ni ukichaa ambao binafsi naufurahia.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] huyo dada alikuwa anakufahamu
 
Yes offcourse hata mimi ndio nilivyo.
Kwa mfano mtu akiniletea dharau huwa narekodi halafu namvizia baada ya muda mrefu sana wakati kashasahau namfanyia kitu ambacho kitamtesa miaka yote.
Yaani niko very strategic nikimuwekea mtu mtego anakuja kunasa mzima mzima lazima kamasi zimtoke.
kitu gani hicho?[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Mi binafsi nipo hivyo na najifahamu muda mrefu.
Hata marafiki huwa ni wale tunaokutana katika tukio fulani, michezo au kazi ila nje ya hapo napenda kutafakari vitu vipya nikiwa mwenyewe.
Mahusiano ni hadi mtu nimzoee sana na nimjue nje ndani ndio nakuwa nae.
Mimi ukitaka hata namba yako niifutilie mbali niletee habari ya "kuna mtu anakusema hivi na vile" ntakuchukia daima. Nafurahi na najikubali japo watu kunielewa huwa wanapata tabu sana.
introverts hawawezi unafki
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kauli gani hiyo
😂 😂 😂
Nilimuuliza yuko job au amesharudi home...aka ijibu "niko home shoga angu"...Aisee nilimimind kinoma...ila yeye akakazia tena "shoga angu usinune bwana". Nikawaza au kwa sababu niko karibu naye sana (hadi kuna watu kibao walijua yeye ni demu wangu, pia hata yeye alikuwa anajitangaza kwa baadhi ya watu kuwa ni demu wangu) na hata siku moja sijawahi kuonyesha dalili ya kumtaka kingono so landa ndo ananiona mi ni kama demu mwenzie...nikaamua kupiga 'tinted'.

Leo yenyewe mida ya saa tatu amenitext akiendelea kuni'apologize lakini sijisikii kabisa hata kuwasiliana naye.
 
Dah yaan Mimi nahisi Niko tofauti Sana na watu wengine Kuna mda huwa sipendi kabsa kuongea na mtu yyte na kupokea simu wat husema Nina kiburi ,
Pia naweza kujifungia ndan kwa mda mrefu .
nikiwa o level wat walisema sizan kama nitafauru sabab sichangamani na watu lakni tangia nmeanza kusoma cjawahi toka top4 .

ndugu upande wa baba ndo atuna ukaribu kabsa wanaishia kusema tu malezi ya kimaskini ya single mother ndo yemeniathiri,. Sometime huwa natami nichangamane nao lkni huwa nahofia Sana kwamb watahisi nafuata msaada kwao naishia kwapotezea tu.

Tatzo jingie kubwa sana huwa sipendi kabsa kusifiwa yaan mtu akinisifia huwa nafadhaika Sana cjui kwanini (God help me) huwa nahisi kama ananikejer hiv nahisi sababa y kukulia kweny umaskin na kukataliwa.
Kweny mahusiano naweza nkampenda mtu kwa mda mfupi tu lkni baada ya mda staki hata kumuona nikiwa alone nakuwa na furaha Sana
Napenda kusikiliza mziki hasa old skul unanikumbusha mmont flan za kitamb afu naenjoy.
Sometime nkiwa chuo napenda kwend club na mziki nacheza (japo sio Sana)

Nauwez wa kusoma alama za nyakati sna nikiona sehem wat Kam hawapend uwepo Wang huwa nasepa kimya kimya, afu Nina mtindo wa kuhukumu mtu kimya kimya siwez kumchana live,
Kwhyo hkumu yake nakuwa naijua mm tu yy ajui atakuta mtu nmebadirika tu. Popote napoishi watu hu feel kama mm nateseka ,najifanyisha na kiburi
Wengine husema najifanya mkimya kumb mhuni tu huwa naumia na kutoa hukumu kimyaa kimya .
Mamangu tu na baadhi y ndugu upande wa mama ndo pekee wanajua jinsi ya kuishi n mm
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Nilimuuliza yuko job au amesharudi home...aka ijibu "niko home shoga angu"...Aisee nilimimind kinoma...ila yeye akakazia tena "shoga angu usinune bwana". Nikawaza au kwa sababu niko karibu naye sana (hadi kuna watu kibao walijua yeye ni demu wangu, pia hata yeye alikuwa anajitangaza kwa baadhi ya watu kuwa ni demu wangu) na hata siku moja sijawahi kuonyesha dalili ya kumtaka kingono so landa ndo ananiona mi ni kama demu mwenzie...nikaamua kupiga 'tinted'.

Leo yenyewe mida ya saa tatu amenitext akiendelea kuni'apologize lakini sijisikii kabisa hata kuwasiliana naye.
[emoji3][emoji3][emoji3] umekuwa naye rafiki kwa muda gani?
 
Hebu fanya kuziweka nione mkuu.. Hafu niambie motive behind ya kuukiza hvo
Paul mccartneyView attachment 1643498John Lennon
images%20(5).jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wengine wanatumia hii mambo ya introvert kama gia ya kupata mademu hahaaaaaaa....
Utakuta mtu anajiita introvert ila mkute ktk nyuzi sasa kila demu ana flirt naye.....
Mwingine akisikia introvert wana vijiakili akili basi anenda Mawasiliano getini pale kwa bonge kununua miwani ili aende na biti hahaaa tunawachora tuuuuu.....

it's easy sunday relax
 
Back
Top Bottom