Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Inaendelea,

Sasa bhana pale chuoni kulikuwa na warembo balaa ila kwa sababu sina mkwanja nilikuwa napita pembeni japo nilikula wawili waliojileta wenyewe. Hawakuwa pisi kali wala nini, ni wale wanaoweza kulika tu. Pisi kali nilikuwa nazipita kama sizioni maana niliona nitajiongezea stress tu. Stress za Khumbu zilikuwa zinanitosha kabisa hadi nilikuwa nahitaji kuzigawa maana zilikuwa kama zimamwagikia hahahahah! Ila kuna pisi kali moja matata ilikuwa pisi ya mshikaji nasoma nae ilinipenda yenyewe ilitaka kuingia kwenye 18 zangu nikaikosa kosa. Mtanikumbusha niwape ID yake inayotumia facebook muiview. Iko njema hatari.

Khumbu aliendelea kunibania sana. Alikuwa anakuja mara moja sana. Na akija atalala siku moja kesho anasepa.
Kuna siku alikuja, hiyo siku ilikuwa kipindi cha mitihani. Kama nilivyowaambia kipindi cha mitihani watu kibao walikuwa wanataka kujisomea na mimi. Mpaka kuna msemo walikuwa wanauongea "If you can't beat Konda msafi, join him". Siku hiyo Khumbu alinipigia simu akaniambia leo atakuja kulala. Sasa ikawa mtihani maana tulikuwa tunajisomea hadi saa 6 za usiku. Dah ikabidi niwape excuse hao watu wanaotaka kujisomea na mimi. Nikawaambia leo ni emergency siwesi kukaa mpaka usiku. Nitasepa ikifika saa 11 jioni ili nikamsubirie Khumbu. Watu wakanielewa ila kuna mshikaji wangu mmoja anaitwa Sandile na demu mmoja anaitwa Pontsho wakasema Konda msafi tutaenda wote kwako kujisomea, dah nikaona hii sasa shughuli. Nikafikiria, nikaona watu wawili hakuna shida, twendeni tukajisomee home kwangu.

Itaendelea..
 
Uzamwamwa huo tangulini dumu akamuita dume mwenzake kipenzi naona mmemsahau makonda nyie

Basi nilipoangalia dp yako ikanipelekea kusema hayo plus na mundende ninaopiga hapa ndiyo kabisa, nisamehe mzee baba hapo vp? [emoji481][emoji481][emoji481][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482][emoji481][emoji481][emoji481][emoji481]
 
Tangu mwanzo nilishaanza kuhisi Khumbu atakua tu ni Mama wa mtoto au watoto,kusema la ukweli wanawake waliozaaa hawa tunaowaita single mothers au vyovyote vile huwa 90% ni visu tena viwembe kweli kweli.

Khumbu deserves kuwa mzuri, sema siku hizi nikiona tu toto lina figure ya kueleweka huwa najiongeza maana najua panga pangua hakosi mtoto.

Japo si wote wenye figure wana watoto ila wengi wao ni hivyo
 
Inaendelea..

Mapenzi yetu yaliendea vizuri tu japo Khumbu alianza chenga chenga ninapomhitaji siku za weekends. Ilipoingia 2009 nilianza mchakato wa kuingia chuo. Kama mnakumbuka hapo awali nimeelezea kuwa nilipata ufadhili flani japo ulikuwa ni kwa amount ambayo haikidhi tuition fee kwa ujumla wake. Mie target yangu ilikuwa kwanza nipate admission. Vyuo vya South wanaruhusu kulipa kidogo kidogo. Kikubwa tu uwenze kulipa registration fee ili uweze kusajiliwa.

Ukishasajiliwa sasa unaanza kupambana kuhakikisha unamaliza deni lako kabla mwaka haujapinduka, maana usipomaliza deni lako huwezi kusajiliwa kuingia mwaka unaofuata. Siku ya usajili nilienda na Khumbu, dah! ilikuwa ni fahari sana kutinga viwanja vya chuo nikiwa na Khumbu pembeni. Khumbu alikuwa what is called "centre of attraction" Elimu yake ni high school tu lakini alivyo chuma na avyotembea utadhani ana Phd. Mambo ya kujisajili nikayakamilisha, nikaenda workshop kwa masela, na Khumbu akasepa kwao. Wiki kama mbili baada ya usajili masomo yakaanza rasmi. Ilibidi niachane na issue za kuuza viatu, na pia nikawa nimepewa sehemu ya kuishi na hao wafadhili wangu.

Kilikuwa ni kikuwa ni kijumba kidogo chenye chumba na sebule, jiko, bafu na choo. Kule wanaita cottage. Nikawa nimeanza maisha mapya ya kishule shule. Kule workshop nikawa naenda mara moja moja kuwatembelea masela. Masela wakanitungia na jina nikawa naitwa "wakusoma". By the way kule wabongo wote wana majina mapya. Ukienda kule unamtafuta mtu kwa jina unalomjua kutokea bongo huwezi kumpata. Watu wanaitwa wakina "Bozeni, Jakama, the game, etc.

Nilipoanza chuo hela za kuspend na Khumbu zikakata. Ikawa kumuona Khumbu lazima nitumie nguvu sana. Inaweza kukata hata wiki mbili sijamuona. Anyway nilianza kuizoea hiyo hali japo kwa kujilazimisha sana. Masela wangu wa workshop nikawa nawasiliana nao mara moja moja, japo nilipokuwa nafulia ile sana walikuwa wananiungia.

Chuoni nikaanza kupata marafiki wapya. Course niliyokuwa nachukua ilikuwa ya miaka 3. Darasani nilikuwa njema kinoma, kipindi cha tests na mitihani nilikuwa nazungukwa na warembo balaa, wote wanataka kusoma na mimi. Maana kila test tukifanya lazima niongoze, hivyo kila mtu akanijua. Mpaka nilishawahi kula kimashara demu mmoja aliyepata supp hivyo alihitaji nimfundishe hadi night kali.

Itaendelea..
Sasa hapo kwenye hilo neno kula kimasihara mods wangetuekea linki ya ule uzi wetu pendwa kama refference
 
Back
Top Bottom