Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Lete hizo chapati za chaduma mzee
Screenshot_20210211-163043.jpg
 
Tuendelee...

Mshikaji wangu Sandile alikuwa ni mpiga picha wa gazeti linaitwa Sunday tribute/tribune (nishaanza kusahau), kwa hiyo alikuwa anasoma huku anafanya kazi. Pontsho sasa hivi ni metro police lakini kipindi hicho alikuwa anafanya kazi bank. Hivyo wote wawili walikuwa na usafiri. Ilipokaribia saa 11 Khumbu akapiga simu kuniulizia nipo wapi? Nikamwambia bado nipo chuo ila anielekeze tu yuko wapi tuje tumchukue tusepe nyumbani. Akaniambia yupo stand. Hiyo taxi rank ilikuwa karibu na chuoni kwetu. Hivyo nikawashitua Sandile na Pontsho kuwa tuondokeni, kuna mtu inabidi tumpitie. Tukakubaliana tutumie gari ya Sandile, ya Pontsho tuiache tu huko parking maana italeta usumbufu usio wa lazima. Tukawaaga wana group wenzetu, tukaelelea parking kuchukua usafiri wa Sandile.

Picha linaanza,
Nikawaeleza kuhusu Khumbu kuwa inabidi tumpitie yupo stand, bila hiyana Sandile akawasha gari tukashuka kituoni tukamchukua Khumbu. Khumbu alipoingia kwenye gari nikafanya utambulisho na safari ya kwenda maskani ikaanza. Tukiwa njiani Sandile na Pontsho wakashauliana tupie KFC tununue chakula kabisa maana huko tuendako hakuna mpishi. Basi chakula kikanunuliwa na safari ikaendele. Pale nilipokuwa nakaa kulikuwa na nyumba nyingine inatumika kwa ajili ya mikutano na funguo zake mimi ndio nilikuwa nazo. Tulipofika nikampeleka Khumbu getoni kisha nikaenda kufungua ile nyumba ya mikutano kwa ajili ya kupiga kitabu. Chakula tukagigawa, tulichukuwa kinachotutosha sisi na kingine nikapelekea Khumbu.

Wadhamini wakaanza, Sandile na Pontsho wakawa wananidadisi kuhusu Khumbu. Of course waliona nakula chakula grade one ila nikiwaangalia kwa jicho la tatu nawaona kama wananiona nimepatikana. Khumbu alikuwa demu classic hivyo walikuwa na wasiwasi nimewezaji kummiliki. Nadhani walianza kuunganisha matukio ya mizinga niliyokuwa nawapiga, hivyo walipata jibu hiyo mizinga nilikuwa nagawana na Khumbu. Na kuna siku Sandile alinichana live kwa kuniambia "Konda msafi mie nakusupport financially ila siafiki mahusiano yako na Khumbu, sikupangii nani um-date ila siafiki mahusiano yako na Khumbu". Mie niliamua kumpotezea maana niliona kama ananichuria tu, naanzaje kuiacha ngozi tamu kama hiyo, kama kufa acha nife tu. Maisha menyewe mafupi.

Tulianza kujisomea lakini akili yangu ilikosa utulivu kabisa, maana nilikuwa nawaza kwenda kumtawanya miguu Khumbu. Naona jamaa waliona sina concentration kama wanavyonifahamu, wakaamua tuachane tu na discussion waniache niende nikacheze na makalio ya dada yao.

So discussion ikafa, wakaingia kwenye gari wakasepe, na mie nikachoma ndani.
 
Inaendelea...
Siku niliyotoka na boxer mpaka barabarani kama mtu aliyechanganyikiwa.

Baada ya Khumbu kuendelea kunibania, yaani mpaka nitumie nguvu sana kumfanya akubali kuja kuliwa, niliona napata stress zisizo na faida yoyote. Nikaamua nifanye mazoezi ya kumpotezea ikiwezekana niachane naye kabisa. Sikumbuki vizuri kama nilikuwa bado niko mwaka wa kwanza chuoni au nilikuwa nimeingia mwaka wapili. Khumbu alikuwa haji tena kunitembelea, ilipita karibia miezi miwili sijamuona. Kila nikipiga simu hata haeleweki kabisa.

Kuna siku jamaa zangu wa workshop walinipigia simu wakaniambia Khumbu kapita hapa akiwa na rafiki yake. Wananiambia huenda Khumbu kapata jamaa mwenye cash chafu maana amezidi kupendeza sana. Hayo maneno yaliniumiza sana. Dah! Kumbe Khumbu yupo tu hapa town ila nikimhitaji hataki kuja. Basi nikajikuta mpango wangu wa kutaka kumpotezea umefeli vibaya sana.

Nikaanza kumpigia simu mfululizo ili kumbembeleza japo aje tu nimuone maana nimemmiss ile mbaya plus machungu yakujua kabisa jamaa wenye hela zao wanamla na kushiba. Majibu yakawa yale yale, sometimes hapokei simu au akipokea anakuambia nitakupigia.

Kipindi hicho msela wangu muuza viatu alikuwa tayari keshaingia kwenye biashara ya sembe, na lile goli kamuachia mdogo wake. Sasa kuna siku nilikutana naye mitaa ya home akiwa kwenye rada zake. Anaendesha BMW kali, hata sikumbuki ilikuwa inaitwa jina gani maana hizi gari zina majina yake.

So, tulipokutana nikamkaribisha getoni maana alikuwa hajawahi kufika tokea nimehama kule Rossburg. Baada ya stori mbili tatu akaniachia mpunga wa kutosha. Dah! Nikajisemea moyoni, huu mpunga tunagawana na Khumbu. Swali likabaki Khumbu atajuaje kama nina mpunga? Nikimpigia simu lazima ataleta nyodo zile zile za siku zote. Nikaamua kesho acha niende kwao kabisa, nimfuate huko huko nije naye.

Itaendelea...
 
Baada ya hapo mapenzi yaliendelea. Khumbu alionyesha kunijali. Kama nilivyosema nimedate na wasouth wengine tofauti na Khumbu ila treatment aliyokuwa ananipa huyu mwanamke ni tofauti sana. Kuna siku nikiwa bado nipo Rossburg, maana baada ya kuanza chuo nilihama huko. Nilimuomba aje mjengoni maana tulikuwa hatujaonana karibia wiki hivi. Nilikuwa nimemmiss kinyama. Akasema atakuja lakini hakutokea. Usiku wake nikawa nampigia hapokei, baadae nilipozidi kupiga simu akazima.

Basi nikajua tu hapa yupo na msela mwingine. Ukimpenda mtu wivu hauwezi kukosekana, so nikawa namtumia msg ili akiwasha simu azikute. Simu haikupatikana mpaka kesho asubuhi. Mawazo yalikuwa mengi sana, ile kufikiria tu demu alikuwa analiwa ilikuwa inaniumiza sana. Siku hiyo sikuweza hata kufanya kazi, nilienda kufungua goli lakini baadae nikarudi mjengoni kupumzika. Kule mjengoni alikuwepo demu wa baba Isa, alikuwepo kama wiki hivi. Huyo demu alikuja na sijui baba ake.

So, nilivyofika nikamkuta demu wa baba Isa yupo sebleni anaangalia tv. Kumbuka apartment ilikuwa ya vyumba vitatu. Sebule, jiko na bafu la kushare. Nilipomkuta demu wa baba Isa nikawa nimemjoin hapo sebuleni. Tukawa tupiga story mbili za hapa na pale. Baadae mie nikaamua kuingia chumbani kupambana na stress zangu, hivyo nikamuacha demu wa baba Isa akiendelea kuangalia TV. Nilipoingia chumbani sikuufunga mlango wangu.

Nikiwa nimejilaza nikaanza kusikia makelele hapo sebleni, nikakurupuka kuelekea sebleni kujua nini kinaendelea. Ile kutoka nikakuta yule demu wa baba Isa hayupo ila kuna demu mwingine wa baba Isa yupo jikoni anatukana kwa kizulu huku anatembea tembea, na kugonga mlango wa baba Isa. Harakaharaka nikajua hapa kuna fumanizi. Mademu wote wa baba Isa nilikuwa nawafahamu maana walikuwa wanakuja kila mmoja kwa wakati wake.

Nadhani kuna mmbea aliamua kuchoma utambi siku hiyo. Basi yule demu aliyekuwa anaangalia tv alikuwa kajifungia ndani, halafu mle ndani kulikuwa na baba ake pia, we acha tu. Sasa picha linakuaje hapa. Yule demu mwingine ndio anagonga mlango kwa nguvu akimtaka mwenzie afungue wapambane. Hapo mie nimeduwaa tu sijui hata cha kufanya.

Huyu anayegonga mlango sijui alifikiria nini, mara nashangaa kaingia jikoni sijui kabeba jiwe, sijui alibeba kitu gani mara vuuu kaingia chumbani kwangu na kukipasua kile kidirisha nilichokuwa nawaambia hapo awali. Basi vipande vya glass vikawa nimetawanyika kila sehemu mle chumbani kwangu. Kile kidirisha ndio kikawa kimebomolewa.

Sasa hapa nikawa namuwazia Khumbu, sijui akija atakubali kulala kwenye hiki chumba kisichokuwa na dirisha, maskini mimi Khumbu akigoma kulala humu nitampeleka wapi? Gharama za kulala guest kwa South Africa nitaziweza kweli?
Lakini bwana konda hicho chumba si ulikihama ukapata nyumba nyingine baada ya kwenda shule?
 
Waulizeni mods kama inaruhusiwa kutupia picha ya mtu hapa. Kuna moja nataka niitupie yupo na bikini tu. Tulikuwa kwenye swimming pool. Wale masela niliokuwa naishi nao waliingia kwenye business ya sembe hivyo hela ikawa sio shida tena tukahamia kwenye nyumba bab kubwaa yenye swimming pool na kila kila kitu ndani, maeneo ya watu wanene.
Itupie tu mkuu hawa moderator nawafahamu vizuri.
Ukiomba ruhusa hawakupi ila ukituma hawana noma
 
Back
Top Bottom