chikutentema
JF-Expert Member
- Dec 10, 2012
- 7,694
- 4,954
Hawajui lolote vijana wetu hawa, akiazimwa smart phone na Kaka yake anakimbilia kuandika anachokiwazaMsimulie Kuhusu..historia ya bunduki pendwa AK 47
Sent using Jamii Forums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hawajui lolote vijana wetu hawa, akiazimwa smart phone na Kaka yake anakimbilia kuandika anachokiwazaMsimulie Kuhusu..historia ya bunduki pendwa AK 47
Mkuu Russia ilianguka baada ya kuvunjika kwa USSR ......but kuingia kwa Vladimir Putin......miaka ya 90 kumeirejesha Russia....kwenye nguvu zake dunianNajua tafauti baina ya USSR na Russia lakini usijidanganye kwamba Russia imepungua nguvu zake.
Bado anao mkono wa chuma kwa yale mataifa yote yaliyokuwa chini ya himaya ya USSR na hawafurukuti kwa lo lote lile.
Mkuu....labda Kama haujaelewa..chanzo cha huu mgogoro......... Russia haitaki influence ya Ukraine kiuchumi .....but ni interest za kiusalama ...kutokana na baadhi ya mikataba waliyoweka ...kumaliza Vita baridLeo hii nchi kama china ana nguvu kwa sababu ana influence kubwa sana kiuchumi nchi nyingi zinamtegemea azalishe bidhaaa wakanunue kwake
Marekani technologia ndo inayombeba, Sasa Putin anataka influence kupitia mtutu wa bunduki he has nothing to offer in economy point of view, ndo maana nchi kama Ukraine wanaona wawe upande wa ulaya kuliko urussi
Kabisa mkuu.......Sasa..mfano ...Russia atengeneza allience yake ...+ China. + Irani. + North korea....vip mizan itakaajeNATO ni mjumuiko wa mataifa zaidi ya matano yaliyo jiunga ili kumkabili urusi... sasa huu wa nato ndio uoga sasa...
Daaah ...Basi walimfanyia ukatiliUnajua yule Mzee wa Ak 47 Mikhail Kalashnikov ameishi maisha ya kimaskin sana japokua silaha aliyoivumbua ni maarufu
mwaka 2012 alikua analalamika silaha aliyoitengeneza yeye hafaidiki nayo hata cent moja ana wish angekua western world
Upo deep mkuuSijajibuje ananunua kwa local manufactures ambapo serekali Ina share na anawekeza kwenye research and development kote huku ni ela inatumika au unadhani zile silaha zinashushwa kutoka mbinu hakunaga cha bure ndugu
Haya ndo baadhi ya makampuni ya urussi
Almaz-Antey – air defense systems
United Aircraft Corporation – fixed-wing airplanes
Tactical Missiles Corporation – air- and naval-based missiles
Russian Helicopters – helicopters
Uralvagonzavod – main battle tanks
United Shipbuilding Corporation- submarines, corvettes, frigates, aircraft carriers.
nyie nchini mwenu ambapo sio wajamaa mupo busy na nn?Ukiangali kwa percentage ya gdp ni ndogo, tofauti na russia ukiangalia ela anayotumia kwenye silaha na percentage ya gdp ni kubwa
Na marekani ana balance kipato Cha marekani mmoja ni kikubwa maradufu ya nchi kama Russia, nchi za kijamaa kama korea kaskazin vipato vya wananchi wao ni vidogo lakin nchi iko bize na nyuklia
sasa wewe umepataje hizo taarifa?Hata wakifa na njaa hapana atakayesubutu kunyanyua mdomo wake. Anaweza kuishia kupigwa na lile zinga la kudungulia ndege.
wala uchumi sio kil kitu kwenye kuifanya nchi ama taifa fulani liwe upande fulani kama unavyodai mbona CUB VENEZEVUELA wapo karibu na US ila wapo upande wa RUSSIA?Leo hii nchi kama china ana nguvu kwa sababu ana influence kubwa sana kiuchumi nchi nyingi zinamtegemea azalishe bidhaaa wakanunue kwake
Marekani technologia ndo inayombeba, Sasa Putin anataka influence kupitia mtutu wa bunduki he has nothing to offer in economy point of view, ndo maana nchi kama Ukraine wanaona wawe upande wa ulaya kuliko urussi
Kuna watu wanaona miaka 100 ijayo Putin anaona miaka 200 ijayo ya taifa lake..MSM haziwezi eleza ukweli huo.Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
Sasa Venezuela si sawa na somalia Hana faida yeyote yaan sio potentialwala uchumi sio kil kitu kwenye kuifanya nchi ama taifa fulani liwe upande fulani kama unavyodai mbona CUB VENEZEVUELA wapo karibu na US ila wapo upande wa RUSSIA?
mmemezeshwa prooaganda[emoji23][emoji23][emoji23]
na Tanzania imempita nani?Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
sasa mkuu,kati ya nchi ulizotaja ukilinganisha na russia nani anaheshimika na kuogopwa zaidi,mipaka yako ni muhimu sana..Nchi inaheshimika kwa kuwa na uchumi imara na wala sio una Nuclear Warheads ngapi.
Leo hii China, Japan na South Korea zinaheshimika zaidi duniani kwa kuwa na uchumi mkubwa na wala sio kwa kujilimbikizia silaha nyingi na itakumbukwa kwamba miaka 40 iliyopita Urusi ilikuwa mbele ya hayo mataifa kiuchumi lakini leo yameiacha Russia mbali kwa sababu Russia haijui vipa umbele vyake ni nini.
Wao wangejishughulisha na maendeleo ya watu wao wakaachana na ndoto za kutafuta umaarufu wa kuuza silaha kwa sababu hiyo ndiyo imewafanya leo hii wawe maskini pamoja na akili nyingi walizonazo.
Angekuwa amejenga taifa lenye nguvu angekuwa haogopi Ukraine kujiunga na EU na NATO. Halafu maisha ya watu ni ya hali ya chini sana; kuna matajiri wachache tu. Alipopota mafuta na gesi, pesa yote akapeleka kwenye jeshi. Nchi haina barabara za maana za kuunganisha miji. Ni sehemu chache tu zilizoko Magharibi maneo ya Moscow na St Petersbug ndiko kuna maisha; ukishafika Ufa kutokea Mosco unakutana na barabara za hovyo sana kuliko hata za Burundi. Kwa mfano angalia hizi Highway za kutoka Ufa kwenda sehemu nyingine ispokuwa kwenda Moscow.Unazima moto wa msitu, lakini bado unawaka," yalisoma maandishi juu ya picha ya mwanamke mchanga wa Kirusi, akitabasamu huku akiwa nusu uchi. Kama hii, picha zingine 11 zenye maneno ya kuudhi zilitengeneza kalenda ya mwaka 2011 iliyohusisha wanafunzi wa uandishi wa habari wa Chuo Kikuu cha Moscow na kuitolea kwa sanamu yao.
Kiongozi wa kisiasa wa Urusi Vladimir Putin, ambaye katika majira ya joto ya mwaka 2010, alikuwa ameongoza binafsi helikopta ya zima moto ili kukabiliana na moto huo uliokuwa umeutishia mji wa Moscow.
Zawadi za kupendeza za kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Putin, ambaye amekuwa madarakani nchini Urusi kwa zaidi ya miongo miwili, ni sehemu moja tu ya utekelezaji kimila wa umma wa sifa ya kiongozi huyo wa Urusi.
Putin amekuwa kielelezo cha ubabe na kuwatia moyo wanasiasa duniani kote, kama vile Mmarekani Donald Trump, Mhungari Viktor Orban na Mbrazil Jair Bolsonaro, ambaye aliondoka Jumatatu wiki hii kwenda Moscow kwa lengo la kukutana na rais huyo wa Urusi.
Mbali na kipindi cha helikopta ya zima moto, Putin tayari amejiruhusu kupigwa picha katika mfululizo wa hali za kiume. Aliwaangusha wapinzani kwenye mkeka katika mechi za judo. Alichunguza meno ya dubu katika Aktiki na chui huko Siberia, wote wawili wakiwa wamelala.
Aliendesha nyambizi na mashua. Alipiga picha akiwa na bunduki mkononi (na bila shati) alipokuwa akiwinda Siberia. Aliibuka akiwa utupu akiwa amepanda farasi na kuvua samaki. Alijionesha na bastola kwenye safu ya risasi. Au tu alionekana akiwa amevalia mavazi ya michezo alipokuwa akifanya mazoezi ya misuli ya kifua chake kwenye ukumbi wa mazoezi.
'Nguvu za ubabe duniani'
Baada ya kuingia madarakani mwishoni mwa miaka tisini, Putin alichukua uongozi wa nchi inayojaribu kuinuka kutoka kwa vifusi vya Umoja wa Kisovieti. Umoja wa Kisovieti ulikuwa umesambaratika mwaka wa 1991, na Warusi walikabiliwa na maswali ya utambulisho, wakilazimika kuzoea ubepari, kushughulikia mgawanyiko wa eneo na upotezaji wa hadhi ya nguvu ya ulimwengu.
"Kulikuwa na hali ya kushindwa kwa ujumla, kuyumba kwa uchumi, na kushuka kwa thamani ya sarafu ya Urusi, na kushindwa katika Vita Baridi. Udhaifu huo ulionekana wazi zaidi kati ya wazazi wa Urusi, watu wa miaka 30, 40 na 50 ambao walipoteza maisha yao, akiba na kazi, kwamba hawangeweza tena kutunza familia zao huku akashuhudia vijana wakitajirika katika biashara mpya, na kwamba alikuwa mlengwa wa kukosolewa waziwazi, kwa kutokuwepo kwake katika maisha ya familia, kwa unyanyasaji wa nyumbani na kwa shida kama vile ulevi, anasema Amy Randall, profesa wa historia katika Chuo Kikuu cha Santa Clara huko California na mhariri wa toleo maalum "Masculinities Soviet" wa jarida la Masomo ya Historia ya Kirusi.
CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Kwa mujibu wa Randall, udhalilishaji na aibu ya Kirusi kwa ulimwengu katika miaka ya 1990 iliishia kufananishwa na kiongozi wa nchi hiyo wakati huo, Boris Yeltsin, alinaswa akiwa amelewa na katika mitazamo ya aibu katika hafla za kimataifa. Hata alijifanya kuongoza orchestra kwenye sherehe ya kijeshi na kutoa taarifa juu ya tamaa ya kutokomeza silaha za nyuklia za Kirusi baada ya kulewa.
Bila kujulikana kwa umma, Putin anaonekana kwenye uwanja wa kisiasa wa Urusi mikononi mwa Yeltsin, ambaye alikuja kumrithi. "Putin anawapa Warusi picha ya ajenti mkali wa sanaa ya kijeshi kutoka KGB (shirika la ujasusi la Soviet). Anasema Sperling.
Chini ya amri yake, jeshi la Urusi lilipata tena udhibiti wa Chechnya, lilivamia Georgia na kuteka Crimea. Sasa nchi inakabiliana na uwezekano wa mzozo wa silaha na Ukraine. Tangu mwishoni mwa mwaka jana, Putin ameweka zaidi ya wanajeshi 100,000 kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili na akitaka Ukraine isiingizwe kwenye Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi, NATO, muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani na Ulaya Magharibi ambao Putin anaona kama tishio kwa usalama wa nchi yake.
CHANZO CHA PICHA,REUTERS
"Chini ya uongozi wa Putin, Urusi imejiimarisha kama nguvu ya uanaume duniani, ikionyesha nguvu zake za kisiasa, kujitegemea kiuchumi, na uwezo wake wa kiteknolojia na kijeshi. Putin anatumia umaarufu wake na uwezo kubaki madarakani kwa muda mrefu , mifumo kama vile utaifa wake wa kiume, nia yake ya kuifanya Urusi kuwa kubwa tena, matumizi yake ya maadili ya mfumo dume na dhana ya tofauti katika majukumu ya kijamii kati ya jinsia, pamoja na chuki ya wazi ya jinsia moja", anasema Randall, ambaye Trump pia alipata msukumo wa Kirusi kwa kauli mbiu yake ( "ifanye Marekani kuwa kubwa tena") na sio tu mtangulizi wake Ronald Reagan.
'Sifa bora za kiume'
Ilikuwa kutoka kwa mtazamo huu ambapo Putin alisema, mnamo Novemba 2020, kwamba Jair Bolsonaro alikuwa na "sifa bora za kiume" kwenye usukani wa Brazil. Pongezi hizo zilikuja wakati wa hotuba ya rais wa Urusi kwenye mkutano wa BRICS, kundi linaloundwa na Brazil, Urusi, India, Uchina na Afrika Kusini, na kurejelea jinsi Bolsonaro alishughulikia janga la covid-19.
"Hata wewe binafsi uliambukizwa na ugonjwa huu na ulistahimili mtihani huo kwa ujasiri mkubwa. Najua wakati huo lazima haukuwa rahisi, lakini ulikabiliana nao kama mwanaume halisi na ulionyesha sifa bora za kiume, kama vile nguvu na utayari", Putin ilisema kulingana na nakala ambayo serikali ya Brazil yenyewe ilichapisha.
Wiki moja iliyopita, Putin alivutia hisia za ulimwengu kwa taarifa ambayo alimsuta Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, mkosoaji wa makubaliano ya amani ya Minsk.
"Upende usipende, mrembo wangu, lazima uvumilie," Putin alisema, akitumia msemo wa kike kuhutubia kiongozi wa Ukraine. Bolsonaro, katika kilele cha majadiliano yake na Rais Emmanuel Macron kuhusu moto katika Amazon mnamo 2020, alichapisha tena chapisho ambalo lililinganisha Mama wa Taifa Michelle Bolsonaro, 39, na Brigitte Macron, 68. Chapisho hilo lilisema:
"Unaelewa sasa kwa nini Macron unamtesa Bolsonaro?" Na rais mwenyewe akatoa maoni yake "Usidhalilishe jamani lol".
CHANZO CHA PICHA,REUTERS
Mbinu nyingine ya kawaida ni kufanya "utani" kuhusu ubakaji na chuki dhidi ya wanawake. Mnamo 2014, katika majadiliano na mwenzake wa PT Maria do Rosário, naibu Jair Bolsonaro alisema kuwa "Sitakubaka kamwe, kwa sababu haustahili." Bolsonaro alielezea kuwa Rosário atakuwa mbaya sana kwa yeye kumpenda.
Putin, mwaka wa 2006, aliripotiwa kumwambia mwandishi wa habari wa Israel, kuhusu tuhuma za ubakaji dhidi ya Rais wa wakati huo wa Israel Moshe Katsav: "Msalimie rais wako. Alitokea kuwa kijana mwenye nguvu sana. Alibaka wanawake kumi, sote tunashangaa, sote tunamuonea wivu." Baada ya msukosuko wa kipindi hicho, Kremlin ililaumu dosari katika tafsiri.
Mnamo 2014, wakati Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Merika Hillary Clinton alilinganisha uvamizi wa Crimea na shambulio la Mjerumani Adolf Hitler dhidi ya Poland, Putin alisema kwa ufupi: "Bora hata usibishane na wanawake." Pia alisema kuwa maoni ya Hillary yalifichua "udhaifu".
Na kwamba "udhaifu sio lazima liwe jambo baya kwa wanawake". Bolsonaro, mnamo mwaka 2017, alisema kuhusu binti yake Laura: ""Nina watoto watano kuna wanaume wanne, kisha katika mtoto wa tano nilikuwa na udhaifu na mwanamke akakuja".
Tofauti na Brazili, nchini Urusi ndoa ya watu wa jinsia moja ni kinyume cha sheria. Wanandoa wa jinsia moja hawawezi kuasili watoto pamoja. Ikiwa itafanywa, itasajiliwa kwa jina la mmoja tu wa wazazi.
Kuhusu suala la mizozo nyumbani, nchini Brazili, Sheria ya Maria da Penha ilikamilisha miaka 15. Katika Urusi, unyanyasaji dhidi ya wanawake ulikataliwa mwaka 2017.
Kuanzia wakati huo, unyanyasaji tu wa waume ambao husababisha madhara makubwa ya mwili kwa wake zao ndio wanakabiliwa na adhabu ya kisheria. Mabadiliko ya sheria yaliwakilisha faida kwa serikali ya Putin, ambayo imekuwa ya kihafidhina zaidi kwa miaka.
"Putin na Bolsonaro wanatazamana na kwa pamoja wanaimarisha hisia hii ya kujivunia uanaume. Bolsonaro amejaribu kwa uwazi kumuiga Putin katika misimamo yake ya chuki dhidi ya wanawake na ushoga, na katika makabiliano yake na uongozi wa Ulaya na wa kimataifa. Anamwona wazi Putin kuwa mtu mwenye nguvu na picha hii ya mtu mwenye nguvu imekuwa maarufu zaidi na imeenea ulimwenguni nyakati hizi, "anasema Randall
Source bbc news
View attachment 2123944
Ndiyo utasema iliyumba kipindi cha Boris Yeltsin kwa vile yule hakuwa na muelekeo wo wote na kuna wakati fulani Georgia ilikuwa na nguvu sana lakini sasa kimya.Mkuu Russia ilianguka baada ya kuvunjika kwa USSR ......but kuingia kwa Vladimir Putin......miaka ya 90 kumeirejesha Russia....kwenye nguvu zake dunian
Tangiapo US wananunua silaha za mrusiYaani Urusi anunue silaha?
Kweli tunashida na elimu yetu.
Ni rahisi kwa marekani kununua siraha ila sio Urusi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hii barabara ni kama Arusha-Moshi, hamna tofauti. Eti hii ndio Highway na hawa ndio wanawakomalia nchi za magharibi.Angekuwa amejenga taifa lenye nguvu angekuwa haogopi Ukraine kujiunga na EU na NATO. Halafu maisha ya watu ni ya hali ya chini sana; kuna matajiri wachache tu. Alipopota mafuta na gesi, pesa yote akapeleka kwenye jeshi. Nchi haina barabara za maana za kuunganisha miji. Ni sehemu chache tu zilizoko Magharibi maneo ya Moscow na St Petersbug ndiko kuna maisha; ukishafika Ufa kutokea Mosco unakutana na barabara za hovyo sana kuliko hata za Burundi. Kwa mfano angalia hizi Highway za kutoka Ufa kwenda sehemu nyingine ispokuwa kwenda Moscow.
View attachment 2125684
View attachment 2125687
Kama zipi.Tangiapo US wananunua silaha za mrusi