Jinsi tunavyoishi wakristo hapa Zanzibar kipindi hiki cha mfungo

Jinsi tunavyoishi wakristo hapa Zanzibar kipindi hiki cha mfungo

Wazungu wanavalishwa kanga sehemu zisizokuwa za Watalii, hapa Unguja,..

Kuhusu kula Wazungu wako tafauti wao moja kwa moja wanakuwa wanaheshimu itikadi, mila na tamaduni wa sehemu wanazokwenda kutalii..
Mkunazi 1 ni sehemu ya kitalii?

Mwanakwerekwe, Ikipida, Mitaa ya Malawi Road (kwenye mitambo ya ZECO) ni maeneo ya watalii?

Huku kote nimekutana na Watakii wakiwa wanagida soda zao na wamevaa kama wapo ufukweni.
 
Hata akila hadharani wewe ina kuathiri vipi?

Ndio maana tunawaambia hamfungi mnalazimisha kuacha kula mchana badala yake mnakula usiku
Alibughudhiwa na nani?Huyo alikutana na vibaka,ndio wakamtisha tisha,na kwa vile muoga akatishika.Kwa vile wewe pia uko muoga na lege lege,wamuunga mkono.Huyu alikutana na vibaka,na inawezekana pia wamemchomoa hela,badala ya kwenda kwenye vyombo vya sheria,kutoa malalamiko anakuja jf,mbona yaonyesha mawenge wenge ya kutishwa tishwa anayo.
 
Naona umeshavimbiwa cha saa 12 sasa unasubiri uvimbiwe cha alfajiri saa 11 ili mchana ujifanye umefunga
Ndugu yenu kakutana na vibaka,wamemtisha tisha,na yaonyesha na hela wamemkwapuwa,badala ya nyinyi kumuelekeza njia sahihi ya kwenda kwenye vyombo vya sheria,kutoa malalamiko yake,mwazidi kuuunga mkono.
 
Pale CCM -Maisara walikuwa wanauza chakula, Mkuu wa Mkoa kaenda kupafunga.

Ajabu ni kwamba, mara zote nilizoenda kula St. Monica, Kambi ya Jeshi - Nyuki na hata hapo CCM nimekutana na Waislam wengi tu wakipata chakula.

Pia kwa observation nilizo fanya, heri Waislam wa Bara na funga yao kuliko hapa Zenji. Zenj unafki ni mwingi sana, ni watu wenye roho ya kwanini kwa ngozi nyeusi na sio kwa Mzungu.

Juzi nilikiwa Mkunanzini, kuna mzungu kanunua chakula pale Lukmaan na anakula huku anatembea wana muangalia tu na muda wa kufuturu ulikuwa bado, ila mswahili mwenzao hata ukishika chupa ya maji ni KESI.

Mitaa ya Raha Leo nimeona mtu akizongwa zongwa kisa yupo na mtoto anakula chakula nikabaki nashangaa hii ndio DINI YA MWENYEZI MUNGU KWELI ?
Nyinyi mnakutana na wajanja wa mjini,badala ya kwenda kwenye vyombo husika kulalamika,mnakuja jf.Hebu jiongozeni,tumieni akili.
 
Huyu kakutana na wahuni wa mitaani,wamemtisha tisha,na yeye akatishika.Kama ingekuwa ni watu wa waliotumwa kisheria,lazima wangekuwa na sare maalumu,na wangempeleka kwenye vyombo husika.Ndugu yenu,badala ya kumfahamisha,amekutana na vibaka wa mtaani,mwazidi kumuunga mkono.
Huu uzi haunihusu mimi na kumbuka kuna wengi tu hawana kipato cha kula hotel za kitalii. Ni upuuzi wa hali ya juu kumpa mtu leseni ya biashara ya chakula na kumlazimisha kufunga biashara yake eti kwa Ramadhan. Si ajabu watu kama huyu mleta mada wapo wengi Zenj ama wanashindishwa na njaa au wanaenda kula sehemu hatarishi tena kwa kujificha utadhani wametenda uovu wowote ule hadi wanyanyaswe kiasi hicho.
 
Hiyo ni hofu yako tu, mie mbona Jumamosi hii iliyopita nilikuwa nakula mgahawani mida ya saa 9 alasiri, watu waliniangalia pia na wale vijana wajinga wapitao kukamata wenzao wasile walikuwepo na waliniona. uzuri walijuwa kuwa mie ni mtu wa bara ila nilijiandaa kuua mtu iwapo wangenivamia. Kula nakula mie kwanini mtu akasirike, nani aliyewakataza kula? Ujinga huu mie mwiko kwangu, wapigane wenyewe kwa wenyewe kwa ujinga wao, HAKUNA aliyekatazwa kula kila mmoja ana uhuru wa kula. Mi naua mtu aje kunivamia kisa nakula kwa raha na hela zangu mwenyewe.
Wewe sasa unajielewa,hao wanaokamata watu,ni wajanja wajanja mitaani tu,ni vibaka,hakuna sheria katika uislamu inayomzuia mtu wa dini nyingine kula mchana wa Ramadhani, ndani ya uislamu na aliyemuislamu pia wapo
Wagonjwa,
Wazee wasiojiweza,
Watoto,
Waliojifunguwa,
Wanawake walio kwenye siku zao,
Wanawake wanaonyonyesha,
Wasafiri,
Wote hao hapo juu,wana ruhusa ya kutokufunga,na sharti mojawapo la kufunga katika uislamu ni kuwa muislam.
Nyinyi mnakutana na vibaka,wajanja wa mjini,huwenda pia ikawa ni wakristo wezenu walio wajanja wa mjini au wa sio na dini,wajanja wajanja,wanawatia mjini.Kama mngekuwa na akili,mngewafikisha kwenye vyombo vya sheria.
 
Mkunazi 1 ni sehemu ya kitalii?

Mwanakwerekwe, Ikipida, Mitaa ya Malawi Road (kwenye mitambo ya ZECO) ni maeneo ya watalii?

Huku kote nimekutana na Watakii wakiwa wanagida soda zao na wamevaa kama wapo ufukweni.
Mwanakwereke Watalii wamefuata nini?? Au wamefuata Tv na Mafrigi "Used" 😂🤣
 
Kiukweli sio Tabia nzuri kwa nchi ya aman kama Tanzania kuishi kama watumwa kwa kipindi kifupi kama hik ndio maan kuna dini mbili sio din moja itake dini nyingine ifuate wanachokifanya so tubadilike
 
huo mtazamo wako nenda Zenji kauze kitimoto chako mwanaharam mkubwa wewe hamtafaulu kunasibisha uislam na kitimoto ni wakristo tu ndio wanakula najisi hiyo ingawa bible inakataza
njoo kwa bibi janet hapa mbweni uone inavyolika mpaka na waislam tena maustaadh
 
Kwanini wakristo huwa mnasema waislamu hula kitimoto?

Kwa taarifa yako muislamu hata kama haswali swala tano au hafungi Ramadhan kamwe huwa hafanyi mambo yafuatayo:-
1.Kula nyamafu(hapa anaweza hata kukutoa uhai ukimlazimisha)
2.Kula nguruwe.
Muislamu yupo tayari kuacha kila kitu katika Uislamu ila hivyo vitu viwili kamwe huwa hawaviachi.

Propaganda ya wakristo kuhusu hili suala huwa inachekesha sana eti wanakwambia 'mwezi mtukufu biashara ya kitimoto haiendi kabisa'

Hata walaji wa kitimoto wenyewe ukifika mwezi mtukufu huwa hawaendi bar kula kitimoto!

Na maeneo wanayoishi waislamu wengi hata kumuona nguruwe tu ni nadra.
Binafsi nimekuja kumuona nguruwe 'live' nikiwa na miaka kama 15 au 16 hivi.Nilikuwa sijawahi hata kumuona.
Basi utakuwa wa ajabu sana. Mudy mwenyewe kawaambia mle mkiwa na njaa sasa sijui nani anakula wakati ameshiba!!!?
 
Kila sehemu kuna mila, taratibu, desturi, tamaduni, silka zake. Zanzibar ilitawaliwa na waarabu na kwa asilimia 99 ya wazanzibari ni waislam. Kama sikosei walitaka kujiunga na OIC miaka ya nyuma huko kitu ambacho kingeitambulisha Zanzibar kama taifa la Kiislam. Muungano wa Zanzibar na Bara ndio uliosababisha hadi leo hii Zanzibar kukwama kuwa taifa la Kiislam. Hivyo basi kulingana na maelezo hayo mafupi utaona ni jinsi gani Zanzibar ilivyo. Hivyo basi wapo Wakristo ambao nao pia wamezaliwa na kukulia Zanzibar lakini wanafuata mila, taratibu, desturi, tamaduni, silka za kizanzibar. Sasa basi ikiwa umekwenda ugenini kwa watu jaribu sana kuelewa ni kipi wenyeji wako wanapenda na kipi hawapendi ili kuweza kuendana na sehemu husika na sio kutaka kufanya vile unavyoona kwako inafaa wakati huo huo ukiwaudhi wenyeji wako.
Kama ukiona unashindwa au unanyanyasika unaweza kurudi nyumbani kwa maana hujafukuzwa. Lakini pia kwanini uteseke na una kwenu? Vile vile kuharibika kwa mila, taratibu, desturi, tamaduni, silka za kwenu kusisababishe ukataka na ugenini kwako kuwe hivyo hivyo.
Lakini sio mafundisho ya dini yanavyotaka, huu ni ukweli ysiopingika.

Ni wapi katika historia ya mtume S.w.a aliwabugudhi makafiri wa Makkah au Madina kisa kufunga?

Uislamu ni dini ya kisimamia maslahi ya kila mtu, ndiyo maana inaitwa dini ya haki. Uislamu unajali mpaka haki ya kuku anapotakiwa kuchinjwa.
 
Lakini sio mafundisho ya dini yanavyotaka, huu ni ukweli ysiopingika.

Ni wapi katika historia ya mtume S.w.a aliwabugudhi makafiri wa Makkah au Madina kisa kufunga?

Uislamu ni dini ya kisimamia maslahi ya kila mtu, ndiyo maana inaitwa dini ya haki. Uislamu unajali mpaka haki ya kuku anapotakiwa kuchinjwa.
Kumbuka pia mtume hakuwabughudhii watu wa Makka kwasababu kipindi alipokuwa alilingania Uislam kwa njia ya siri na hata baada ya kuwa Dhahiri ni miaka 10 tu ndio aliyokaa Makka, na sehemu kubwa ilibaki ya miaka 13 alikuwa Madina kwa maana alikuwa amejitenga na washirikina wa Makka. Kwa mantiki hiyo washirikina wa Makka hawakwenda kumbughudhi huko Madina alikokuwa, ijapokuwa Madina kulikuwa na watu ambao nao si waislam lakini waliiheshimu dini ya Kiislam na Waislam kwa ujumla wao. Ukiangalia Zanziba kiuhalisia imejitenga, ni kisiwani na ukiangalia kumejitenga na bahari sasa iweje wewe kutoka pande nyingine ukawabughudhi wazawa, wakati huo pia wapo Wakristo wazawa lakini hawawabughudhi Waislam? Hayo ni sawa na kusema leo hii mimi niende Mtwara then mila zao au ngoma zao usiku nitoke nje na kuwakataza kwavile kwangu mimi naona ni makelele.
NB
Ukiwa kwenye mji wa vipofu nawe jifanye Chongo.
 
Kwanini wakristo huwa mnasema waislamu hula kitimoto?

Kwa taarifa yako muislamu hata kama haswali swala tano au hafungi Ramadhan kamwe huwa hafanyi mambo yafuatayo:-
1.Kula nyamafu(hapa anaweza hata kukutoa uhai ukimlazimisha)
2.Kula nguruwe.
Muislamu yupo tayari kuacha kila kitu katika Uislamu ila hivyo vitu viwili kamwe huwa hawaviachi.

Propaganda ya wakristo kuhusu hili suala huwa inachekesha sana eti wanakwambia 'mwezi mtukufu biashara ya kitimoto haiendi kabisa'

Hata walaji wa kitimoto wenyewe ukifika mwezi mtukufu huwa hawaendi bar kula kitimoto!

Na maeneo wanayoishi waislamu wengi hata kumuona nguruwe tu ni nadra.
Binafsi nimekuja kumuona nguruwe 'live' nikiwa na miaka kama 15 au 16 hivi.Nilikuwa sijawahi hata kumuona.
Wewe ni msemaji wa waislamu ? Umetembelea grocery za Sinza, zinazouza kitimoto, ?/ waislam hawali nyama za porini? mfano nyati, viboko, tembo nk nani anachinja hiyo mifugo, uelewa wako ni mdogo kama ubongo wa mbu
 
Nchi yetu haina dini,kinachoendelea Zanzibar ni uvunjaji wa katiba na dola itawajibika
Mazingira ya maisha hapa zanzibar kipindi hiki cha mfungo wa ramadan kwa wakristo ni magumu sana hasa kuhusu suala la chakula,kwa sisi ambao tuko kikazi huku na familia zetu ziko bara ni shida, mfano kupata chakula inabidi uende kwenye lile kanisa ambapo zamani kulikua na soko la watumwa,ukiwa mwanakwerekwe napo inabidi uende pale kanisani,ukiwa maeneo ya mbweni itabidi uende kanisani ndio kuna kimgahawa hapo utapata chakula,ila kwa siku ya leo kuna kitu kimenikera sana baada ya kukosa chakula kanisani ikabidi nipelekwe sehemu ya mafichoni kunapouzwa chakula,nimefika na chakula nimepata ila mazingira ya kukaa pamoja ulaji sio mzuri kwa sababu unakula kwa hofu kwamba muda wowote mnaweza kamatwa.na kama unafamilia yako huku basi kama mkeo anataka kupika ni marufuku kupikia nje inatakiwa kila kitu amalize humo humo ndani na ukikamatwa unapelekwa jela mpaka mwezi uishe ndio unaachiwa,lakini hivi vitu vinafanyika kwa ngozi nyeusi kwa nyeusi,ngozi nyeupe aiguswi na hii zihaka mzungu wanakula na kunywa muda wowote na hotel/ mabaa yao yako wazi muda wote,ombi langu kwa waislamu ni kwamba waache tabia za unafiki wa kubagua maana kwa mtindo huu hata thwawabu sidhani kama mtapata.
 
Mazingira ya maisha hapa zanzibar kipindi hiki cha mfungo wa ramadan kwa wakristo ni magumu sana hasa kuhusu suala la chakula,kwa sisi ambao tuko kikazi huku na familia zetu ziko bara ni shida, mfano kupata chakula inabidi uende kwenye lile kanisa ambapo zamani kulikua na soko la watumwa,ukiwa mwanakwerekwe napo inabidi uende pale kanisani,ukiwa maeneo ya mbweni itabidi uende kanisani ndio kuna kimgahawa hapo utapata chakula,ila kwa siku ya leo kuna kitu kimenikera sana baada ya kukosa chakula kanisani ikabidi nipelekwe sehemu ya mafichoni kunapouzwa chakula,nimefika na chakula nimepata ila mazingira ya kukaa pamoja ulaji sio mzuri kwa sababu unakula kwa hofu kwamba muda wowote mnaweza kamatwa.na kama unafamilia yako huku basi kama mkeo anataka kupika ni marufuku kupikia nje inatakiwa kila kitu amalize humo humo ndani na ukikamatwa unapelekwa jela mpaka mwezi uishe ndio unaachiwa,lakini hivi vitu vinafanyika kwa ngozi nyeusi kwa nyeusi,ngozi nyeupe aiguswi na hii zihaka mzungu wanakula na kunywa muda wowote na hotel/ mabaa yao yako wazi muda wote,ombi langu kwa waislamu ni kwamba waache tabia za unafiki wa kubagua maana kwa mtindo huu hata thwawabu sidhani kama mtapata.
Mbona huku bara waislamu tuko nao maofisini, na muda wa lunch ukifika wanaendelea na mfungo wakati sisi tunakula, na wala sijaona hata mmoja aliyesema anakwazika sisi tunapokula? Tena mmoja rafiki yangu ananiambia anapofunga wakati wengine wanakula mbele yake anajisikia kweli amefunga kuliko ingekuwa kwamba wote hatuli ingekuwa ni kawaida tu.
Lakini kwa huko Zanzibar kwa kuwa ni sheria kabisa inasema hivyo hilo limeshakuwa jambo la kiutawala au kiserikali zaidi kuliko la kiimani, kwahiyo hata namna ya kulishughulikia ni ya kiserikali. Kupata au kutokupata thawabu hakuhusiani na sheria hiyo kwa sababu waumini wa kawaida wa kiislamu mnaoishi nao mitaani siyo wao walioweka hiyo sheria, kwenye suala la sheria ikishakuwa ya serikali basi sote inatuathiri tu hata kama hatukubaliani nayo. Inawezekana hata huko Zanzibar wapo waislamu ambao hawakubaliani na suala la kuwakataza wengine kula au la kuwawekea masharti, lakini sheria ndiyo hiyo iko hivyo na ni sheria rasmi ya nchi. Poleni wenzetu.
 
Ni kweli kabisa hamna wateja, wauza kitimoto nao wanalalamika biashara mbaya, wanatamani wafungue hata kesho ili biashara ya kitimoto irudi kwenye peak
Walaji wa kitimoto na wanywaji wa pombe ni walewale, kabla na baada ya Ramadhani. Kinachotokea wakati wa Ramadhani ni suala la kuheshimiana tu na ujirani, watu wanapunguza fujo ili wenzao wafanye ibada zao. Wanaepuka kuwakwaza wenzao. Ni hivyo tu. Mfungo ukiisha watu wanarudia bata zao
 
Back
Top Bottom