DOKEZO Jinsi ziwa Tanganyika lilivyo na maji mengi

DOKEZO Jinsi ziwa Tanganyika lilivyo na maji mengi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Weka sawa hapo mkuu ziwa Tanganyika ni ziwa la pili kwa kina kirefu duniani na sio ziwa kubwa kuliko ziwa victoria, ni ziwa lenye kina kirefu kuliko ziwa victoria ila sio kubwa kuliko ziwa victoria.
 
kwa kuwakumbusha tu pia TANGANYIKA ndio ziwa pekee samaki wanakufa kwa uzee na kuna samaki humo tangu kuumbwa dunia wanaishi humo
na kuna kina maeno tangu kuumbwa kwa dunia mpk leo hakuna mashua iliwahi fikia ikarudi salama
ni ziwa la pili kwa kina kitefu duniani


hvyo inahitajika MAARIFA ya ziada kuyatoa maji humo
hilo ZIWA lina mambo makubwa si mchezo ni moja ya milango ya kufikia HIDDEN WORD(kuzimu) ndio mana likawa afrca mashariki
na ndio mana NCHI yetu inaitwa NCHI ya MAZIWA MAKUU
hiyo TENDA ya kuyatoa maji humo labda apewe MCHINA

Kwani mchina yeye ni nani, tatizo watu mna akili za kitegemezi sana.
 
Km ni pamoja na umwagiliaji hapo sawa;Lkn je watu wote wanafanya umwagiliaji?, Vipi watoto,nao wanatumia hizo lita mia moja kwa Siku??.
Lita Mia moja ni ndoo tano za lita ishirini ishirini. Ni sahihi mtu mmoja kutumia ndoo tano kwa siku. Mfano kama anaoga asubuhi na jioni hizo ni ndoo mbili. Kama atafua nguo chache tu minimum ndoo mbili bado hajafanya mambo mengine. Ni sahihi mtu mmoja kutumia ndoo tano na zaidi kwa siku. Watu hawatumii kwa sababu wana pungufu wa maji
 
Lita Mia moja ni ndoo tano za lita ishirini ishirini. Ni sahihi mtu mmoja kutumia ndoo tano kwa siku. Mfano kama anaoga asubuhi na jioni hizo ni ndoo mbili. Kama atafua nguo chache tu minimum ndoo mbili bado hajafanya mambo mengine. Ni sahihi mtu mmoja kutumia ndoo tano na zaidi kwa siku. Watu hawatumii kwa sababu wana pungufu wa maji
Wewe na familia yako huwa mnatumia kiasi gani cha maji??.
 
Katika maziwa yote nchini, Victoria linaongoza kwa kunyonywa, mpaka limelala aisee
emoji3.png
emoji3.png
emoji3.png
emoji3.png
Linanyonyw Sana hadi limekuwa ndala.
 
Serikali haiwezi kutatua au kumaliza kabisa changamoto ya maji, umeme, huduma za afya, barabara kwasababu watakosa cha kuwadanganyia wananchi kipindi cha kampeni. Yaaani kwa kifupi hizi changamoto za wananchi ni mtaji wa wanasiasa [emoji119]. Kwa ujinga wa viongozi wa Tanzania na Afrika kwa ujumla kama ikitokea hakuna shida ya maji, umeme, barabara, zahanati (hospital) madarasa, wataongea nini majukwaani ili wapate kura???
 
Duniani ziwa Tanganyika ni la pili kwa ukubwa baada ya ziwa Baikal. Ziwa Baikal lina ujazo wa kilomita za ujazo 23,000 huku Tanganyika likiwa na 18,900. Nyasa lina 8,500 na Victoria lina 2,500. Ziwa Victoria linaingia kwenye ziwa Tanganyika karibu mara nane.

Ziwa Tanganyika lina asilimia 18.9 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia. Tanzania sisi tunamiliki 46% ya ziwa Tanganyika. Kwa maana hiyo, hilo linatufanya tumiliki asilimia kama 8.5 ya maji safi yote yaliyopo kwenye uso wa dunia. Ukijumlisha na sehwmu za ziwa Nyasa na Victoria utaweza kuta karibia asilimia 11 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia yapo Tanzania.

Ukitoa maji yote kwenye ziwa Tanganyika halafu ukasema mito yote duniani itiririke kulijaza, itatumia karibia miezi saba kulijaza. Mto mkubwa wa Amazon utatumia karibu miaka mitatu. Mto Congo utatumia miaka 13.

Ukisema mto Rufiji utiririke kujaza Ziwa Tanganyika utatumia karibu miaka 1,400.

Hili ziwa peke yake linaweza kunywesha kila jiji Tanzania nzima. Na kila mtanzania. Ukipiga hesabu ya watanzania wote milioni 60 na ukipiga hesabu ya kuwa kila mtu, mtu mzima hadi mtoto mchanga anatumia lita mia moja kwa siku utaona kuwa tunahitaji kilomita za ujazo 2.2 kwa mwaka. Kinadharia, kwa idadi hiyo tunaweza kutumia maji ya ziwa hilo kwa miaka 8,500.

Asitokee mtu wa kutuambia tuna upungufu wa maji.
Hapo hujaongelea maji yaliyopo chini ya ardhi (underground water), maana nayo ni mengi mno kila mahali!
 
Hii imekaa kitaalamu,hatuna akili,hatuna ubunifu,hatuna nia ya kutoka tulipokwama kila siku tuko palepale

hatuwezi kabisa kutumia rasilimali tulizobarikiwa....hili ziwa lingekuwa uswiss huko lingekuwa na manufaa makubwa sana kwa waswiss.

Ziwa Tanganyika unaambiwa tangu kuumbwa kwake walishavua asilimia 2 tu ya samaki wote waliohai ingekuwa huko mbele hili ziwa lingekuwa na faida kubwa sana kwa nchi,cha ajabu hata waishio jirani na ziwa hili hukosa maji mabombani,tumuombe Mungu atupe akili ya kuziona fursa na kuzitumia Amiin.
Kabisa!
 
... in its simplest definition, volume (V) = length (L) x width (W) x height (H); V = L x W x H. Now, since L x W = Area (A) then; V = A x H.

Lake Victoria: large A but small H hence small V.
Lake Nyasa: small A but large H hence large V.
Note: a small change in H has drastic effect on change of V.
Surely correct!
 
Duniani ziwa Tanganyika ni la pili kwa ukubwa baada ya ziwa Baikal. Ziwa Baikal lina ujazo wa kilomita za ujazo 23,000 huku Tanganyika likiwa na 18,900. Nyasa lina 8,500 na Victoria lina 2,500. Ziwa Victoria linaingia kwenye ziwa Tanganyika karibu mara nane.

Ziwa Tanganyika lina asilimia 18.9 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia. Tanzania sisi tunamiliki 46% ya ziwa Tanganyika. Kwa maana hiyo, hilo linatufanya tumiliki asilimia kama 8.5 ya maji safi yote yaliyopo kwenye uso wa dunia. Ukijumlisha na sehwmu za ziwa Nyasa na Victoria utaweza kuta karibia asilimia 11 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia yapo Tanzania.

Ukitoa maji yote kwenye ziwa Tanganyika halafu ukasema mito yote duniani itiririke kulijaza, itatumia karibia miezi saba kulijaza. Mto mkubwa wa Amazon utatumia karibu miaka mitatu. Mto Congo utatumia miaka 13.

Ukisema mto Rufiji utiririke kujaza Ziwa Tanganyika utatumia karibu miaka 1,400.

Hili ziwa peke yake linaweza kunywesha kila jiji Tanzania nzima. Na kila mtanzania. Ukipiga hesabu ya watanzania wote milioni 60 na ukipiga hesabu ya kuwa kila mtu, mtu mzima hadi mtoto mchanga anatumia lita mia moja kwa siku utaona kuwa tunahitaji kilomita za ujazo 2.2 kwa mwaka. Kinadharia, kwa idadi hiyo tunaweza kutumia maji ya ziwa hilo kwa miaka 8,500.

Asitokee mtu wa kutuambia tuna upungufu wa maji.
Ziwa Tanganyika ni la 2 duniani kwa kuwa na kina kirefu, kwa ukubwa Ziwa Victoria ni la 3 duniani na Tanganyika nazani ni la 5 au 6 kwa ukubwa
Tanganyika linamaji mengi kwasababu kwanza lina outlet moja tu kule Zambia inayopeleka maji mto Congo, pili lina kina kirefu. Disadvantage ya ziwa ni uwepo wa samaki wachache nazani inachangiwa na uwepo wa species chache za samaki
 
... uko sahihi. Hata hivyo, ukubwa wa Ziwa Victoria unaozungumziwa kwenye elimu yetu umezingatia zaidi ukubwa wa eneo (surface area) badala ya ujazo (volume). Ni suala la kuamua jamii inapaswa ipate ujumbe gani; ukubwa wa eneo au ujazo?
Naam!
 
Takwimu iliyonishangaza ni hii ya nyasa kulizidi victoria karibia mara tatu na ushee!
Jamani nikiangalia kwa macho mbona inakataa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ni ukweli kabisa, ziwa victoria linazidiwa ujazo na ziwa Tanganyika. Hata ziwa Nyasa bado lina maji mengi kuzidi Victoria.

Hii ni kwa sababu Ziwa Tanganyika na Nyasa yana kina kirefu kwa sababu yamepitiwa na bonde la ufa. Lakini ziwa Victoria limechukua eneo kubwa lakini lina kina kifupi.

Ziwa Victoria lipo kama sinia, lakini ziwa Tanganyika na Nyasa yapo kama bakuli.
 
Mkuu ni kweli ,juzi nilisema hapa TZ hatuna shida ya maji wala umeme maana tuna sources za kutosha sana za umeme na maji,tatizo ni kipaumbele cha watu waliopora madaraka,wanajiangalia wao tu bila kujali maslahi mapana na wananchi na vizazi vijavyo.

Wao wanangalia kutumia mabilioni kwenye kununua V8 ,kujijengea majumba ya kuishi wao officers ,kuishi kiflamboyant tu ,wao wanawaza kupiga madeal tu.

Tuwe na mpango ya muda mrefu ya kusambaza umeme na maji nchi nzima kwa kutumia resources za kutosha ambazo mungu ametupatia....Tuna Gesi Mtwara ,tuna makaa ya mawe ya kutosha mchuchuma/liganga ,tuna upepo wa kutosha singida ,tuna uranium sehemu nyingi sana TZ mf Namtumbo,tuna jua la kutosha sana nchi nyingine jua hawalioni ,tukitumia tu Nuclear Reactor kugenerate Umeme tungeweza kuzalisha MW za kutosha kutuwezesha kufunga umeme hadi kwenye mbuga za wanyama huko porini.

Ukija kwenye maji hapa sisemi kitu ushamaliza.
Hapo umenena kweli, kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu ni sisi wenyewe. Ina maana siri ya kuendelea au kukwama iko kwetu wenyewe, hususan kwa wenye dhamana ya kutuongoza!
 
Back
Top Bottom