Jirani anajenga Msingi wa ukuta katikati ya jiwe la mpaka la manispaa, Sheria ya Ardhi inaruhusu hii?

Jirani anajenga Msingi wa ukuta katikati ya jiwe la mpaka la manispaa, Sheria ya Ardhi inaruhusu hii?

Habari wadau,

Nina kiwanja changu kimepimwa na manispaa ya Ubungo.

Jirani yangu naepakana nae ameamua kujenga msingi wa ukuta wake kati kati ya jiwe linalotutenganisha..

Je, yupo sahihi? Sheria ya Ardhi inaruhusu hili kutokea?

Wataalamu na wazoefu naombeni ushauri

Tazama picha. Kiwanja changu ni upande wa kushoto na cha jirani ni upande wa kulia wa beacon

Beacon iliyowekwa na manispaa ndiyo hiyo pembeni ya mti (mti ameuweka ndani ya upande wa kiwanja changu) na hayo nyuma ndio matofali ya jirani

View attachment 2371564
Hebu weka site plan au ramani ya kiwanja ili tukusaidie.
 
Shida yako maelezo yako yamekaa kilayman kishamba, hujui vitu una lazimisha kujua

Tuna kuelekeza lakini wapi ubishi mwingi... wewe ndio chanzo cha migogoro... watu wa aina yako ndio chanzo cha migogoro...
Huwa mnajidai mnajuuuuuaaa!Mkifika eneo mnajijambia tu ushuzi wa ngomani.Twende site tukafanye kazi ujue hujui.😂😂😂😂
 
Hakuna kitu sikipendi duniani kama ugomvi wa Ardhi uwa haumaliziki salama.
 
Huu ukuta ni wa kishari shari ndio maana nauogopa.. maana viwanja vyetu ni vya mtaa wa mwisho. Nyuma yetu kuna majirani waliojenga kienyeji enyeji..

Hao watu wote watategemea mimi ndio niwaachie njia kubwa.. maana walikuja kuomba na tukaongea na jirani wote tuingie ndani mita chache ili wa nyuma wapate njia.

Sasa ghafla jirani kaanza jenga ukuta nyuma ya beacon kabisa
sio lazima kila baada ya kiwanja kunakuwa na uchochoro au barabara viwanja vingi tu uzio wa nyumba unakutana, suala la njia ni suala la mipango miji , kama wamepima kuna sehemu maalumu wanaacha njia , tambua kwamba sio kila baada ya kiwanja kilichopimwa wanaweka njia au barabara
 
Uchochoro haupaswi kuwa kila sehemu, kuna barabara za mitaaa
kabisa kiongozi huyo jamaa inaelekea hajatembeea maeneo yaiyopangwa vizuri kama mikocheni au masaki, kungekuwa kuna njia au uchochoro kila baada ya nyumba sijui kungekuwaje , sanasana ingeleta shida kwenye suala la ulinzi
 
Binafsi ninaishi kwenye nyumba ambayo ujenzi wa ukuta unaendelea. Na tumejenga ukuta katikati ya "uchochoro" - katikati ya beacon ya Halmashauri.

Hatujengi kwa shari, bali tunafuata maelekezo ya Idara ya ardhi. Idara ilituelekeza kuwa Sheria hazikatazi kujenga ukuta(fence) katikati ya ya beacon. Mita 1.5 ambayo watu wanazungumzia ni lazima uiache unapoanza kujenga nyumba (sio fence). Na chochoro zinazoachwa huwa wanasema zinaachwa kwaajili ya huduma za jamii n.k. lakini kwa mujibu wa idara ya ardhi - hakuna kitu kama hicho endapo viwanja vimepimwa na kuna barabara upande wa mbele wa kila block. Mara ya kwanza tulipeleka ramani ya fence ambayo inaacha mita 1.5 za uchochoro - wakagoma kui-approve, wakauliza hizi mita 1.5 mmeacha za nini?

Gari la zimamoto halipiti uchochoroni, ni mazoea tu kusema uchochoro ni kwaajili ya gari la fire au gari la wagonjwa. Septic tanks unatakiwa kujenga ndani ya kiwanja chako sio katikati ya beacon. Zaidi ya hayo, unapolipia kiwanja ramani haioneshi uchochoro: kwahiyo unalipia kiwanja chako chote bila kuacha hata hatua moja. Kwa maana hiyo, unaruhusiwa kukitumia chote bila kuacha hata hatua moja. Isipokuwa kuna taratibu zake kila unapotaka kuanza ujenzi ili upate vibali vya kujenga either fence au nyumba. Na kwasababu taratibu zinaanzia katika Serikali za mitaa, kibinadamu na ili kuepuka migogoro - basi huwa wanashauri kama unajenga ukuta katikati ya beacon zungumza na unayepakana nae ili mkubaliane na ikiwezekana mchangiane gharama.

Lakini ukijenga ndani ya beacon, si lazima umshirikishe jirani kwasababu unajenga NDANI ya kiwanja unacholipia.

Nyumba ninayozumgumzia ipo ndani ya Halmashauri ya Mji mmoja hapa nchini. Na wakati tunaanza kujenga ukuta majirani waliandamana, kesi ikafika mpaka kwa Mkuu wa idara ya ardhi. Akafika eneo la ujenzi na akasisitiza kwamba: kisheria fence haijakosewa, ila kibinadamu hayo ni maamuzi ya majirani kukaa chini ya kuyajenga ili kesho na keshokutwa yasije kutokea maafa ya visasi. Lakini nilichokiona ni kuwa sheria yenyewe haifahamiki na watu, kwahiyo tunaenda kimazoea zaidi kuliko kisheria.

NB: Hata mimi nasimamia huu ujenzi lakini Sheria yenyewe siijui, nafuata tu maelekezo ya Halmashauri ambayo wameyaweka kwenye kibali walichonipa.

Walichosisitiza ni kwamba; wanaruhusu kujenga ukuta katikati ya beacon kwasababu ukuta sio "permanent structure", inaweza kubomolewa kirahisi kama kukiwa na ulazima wa kufanya hivyo. Mwisho wa siku Serikali ndio inamiliki ardhi yote, yenyewe ndo inaweza kuja saa yeyote ikakwambia uondoe ukuta. Na Serikali inapozungumza, unapaswa kutii!
upo sahihi sana na ndivyo ilivyo, honera kwa mchango wako mzuri na wa ukweli
 
Huu ukuta ni wa kishari shari ndio maana nauogopa.. maana viwanja vyetu ni vya mtaa wa mwisho. Nyuma yetu kuna majirani waliojenga kienyeji enyeji..

Hao watu wote watategemea mimi ndio niwaachie njia kubwa.. maana walikuja kuomba na tukaongea na jirani wote tuingie ndani mita chache ili wa nyuma wapate njia.

Sasa ghafla jirani kaanza jenga ukuta nyuma ya beacon kabisa
Kama jiwe limewekwa na manispaa maana yake njia wataweka haohao manispaa, hivyo hapo hapapaswi kuwa na njia yoyote. Infact, sijaona kosa la jirani yako. Ukuta unaojengwa ndio mpaka wenu. Hakuna sababu ya kuja kuwa na kuta mbili kisa kuacha jiwe wazi.
 
Siyo kuombwa.Uchochoro kati ya nyumba na nyumba ni lazima uachwe kwa vipimo vyake kitaalamu.Ujenzi holela,ubishiubishi na maroho machafu huwa yanazua balaa.Mkalisheni chini mumueleze huyo mshari.Laa sivyo mbeleni atawasumbua zaidi.Wa wapi huyo jirani yako?
Viwanja vilivyopimwa huwa havina huo utaratibu ndugu. Hicho unachoongea ni taratibu za kimila lkn taratibu za ardhi iliyopimwa hazina hicho unachoongea kwasababu ardhi iliyopimwa huzingatia barabara hadi miundombinu mingine kama maji na umeme
 
Uliwahi kujenga Kate?Au ulijenga tu kwa sababu hakuna aliyekughasi ukaona upo sawa?Jielimishe "dugu yangu"?Unajua hata kuhamia kwenye nyumba yako uliyoijenga kunahitaji leseni?Uliwahi kudodosa au kuiona mkuu?
Vibali vya ujenzi huwa havioneshi hivyo vichochoro unavyosema wewe labda kama umeenda kujenga maeneo yasiyopimwa ndio vichochoro ni lazima kuacha. Maeneo yaliyopimwa yanazo barabara zake. Sisi tunaojenga maeneo yaliyopimwa tunafahamu
 
Kwan ile sheria ya kuacha nusu mita sijui mita moja kutoka kwenye mpaka wako unapo taka kujenge fensi imebadirika au mazaea mabaya?

Na wewe lounge hapo hapo kaishakusaidia ukuta wa upande mmoja
Sheria za zamani sana izo, huku nchi za watu ni ukuta kwa ukuta, hivyo vichochoro bongo mnavyovitengeneza vya kuacha mita mojamoja katikati ya mpaka wabongo mko na project gani mnayotaka kuileta au anzishavna hivyo vichochoro
 
Lazma uunge ndio
Master plan inaonyesha kichochoro?
Kama hamna we unaitoa wapi?
Inaonekana hawa jamaa wanajenga sehemu zisizo rasmi ambako hakuna mipango miji ndio maana wanaongea habari za kuacha hatua. Kwa tuliojenga maeneo rasmi tunajua kuwa hakuna utaratibu wa kuacha hata hatua moja
 
Hapana.Kuacha nafasi kati ya nyumba ya kiwanja kimoja na kiwanja kingine ni lazima kisheria za ujenzi.Na kuna vipimo vyake.Kila mmoja ataacha mita moja na nusu kutoka katika jiwe/bikoni yake.Akileta ubishi atabanwa kwa kuombwa yafuatayo kisheria za mipangomiji/halmashauri;-
1-Uhalali wa umiliki eneo(nyaraka halali),
2-kibali cha ujenzi kinachoenenda na muda(expire date)
3-Na kama amehamia/nyumba ipo,ataombwa leseni/kibali/ruhusa ya kisheria ya kuishi hapo,
4-Hana hivyo vitu;a,atapigwa faini kimojakimoja-b,atasimamishwa ujenzi-c,atavunja ukuta kwa muda atakaopewa kwa gharama zake-d,atapewa onyo kali aache ungedere.🙏🙏🙏😂😂😂😂
Haya ndo majibu ya msomi. Wengine porojo sana.
 
Back
Top Bottom