Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 70,785
- 186,690
Mimi sio Nabii ila huyo jirani yako lazma atakuwa ana vinasaba vya Kilimanjaro. Hao ndio wataalam sana wa kugombea mipaka 🤣Wakuu habari zenu,
Nipo kwenye changamoto na jirani yangu hapa anayetaka kujenga nyumba Yake Kwa kutumia fensi yangu. Upande mmoja na cha kushangaza analazimisha na Ujenzi umeshafikia level ya fensi sasa kimbembe anataka aongeze kozi kadhaa za tofali kwenye fensi yangu ambayo ninataka iishie hpo ilipo na niweke zile electric wire au urembo wa fensi ninao utaka Mimi.
Hivyo ananiharibia plan za kutengeneza fensi ninayoitaka Mimi, mbya zaidi Niko mbali na nyumbani, kwani nyumba nimeijenga huko kanda ya ziwa na Mimi Niko hapa mjin Dar. Ninapomuambia asubiri nirudi ili nione anachotka kufanya anakuwa haelewi...
Kwa mazingira haya nashindwa kumuelewa kabisa kwani kama kiwanja anacho kikubwa kuliko Mimi. Hebu nishaurini maana ugomvi sipendi lakni naona ananichokoza to the maximum.