JK: CCM Tujiandae kisaikolojia muundo wa serikali tatu

JK: CCM Tujiandae kisaikolojia muundo wa serikali tatu

Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.

Mkuu,dalili za kuchanganyikiwa hizo. Unaona ulichoandika ni sahihi? Atakuja wassira na kusema serikali tatu ndiyo ulikuwa msimamo wa ccm,maana kama una kumbukumbu japo sina imani na kichwa chako kama kipo sawa,wassira bila hata tone la aibu aliwahi diriki kusema wazo la katiba mpya ni ccm ilitoa. Yaani sielewi kama nyie magamba mnatumia akilia alizowazawadia MWENYEZI MUNGU,labda mnatumia za ibilisi.
 
Uwe unaota ndoto nzuri wakati mwingine,
Hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuchukua dola;
labda mpaka Kristo arudipo kwa mara ya pili.

Maumivu huanza taaribu mwisho yanageuka nakuwa kilio.
 
kama kweli unauliza ili ujue. basi naomba nikujibu.... HAPANA MIMI SIO MTOTO WALA BABA WA KIONGOZI WA CCM.. ila napigania maslahi mapaaaana ya taifa langu. poleni mnaochukuliwa na vimbunga vya wanasiasa. mimi ukiniuliza kwa nini naipigania tanzania ya serikali mbili nina sababu nzito za kutosha ila wewe nikikuuliza kwa nini unataka tanzania ya serikali tatu utaniambia'''''' mbowe/slaa wamesema''''

Zitaje hizo sababu.
 
Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.
chuki chuki chuki
 
This is simply stupid, Katiba sio ya CCM wala CHADEMA sio CUF ama NCCR katiba ni ya wananchi wa JMT.
 
Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.
Kama hujui maana ya utafiti bora kukaa kimya kuliko kuaibisha fani ya wenyewe.
 
Mambo mapya yameibuka huku mitaani hususani kwa wanachama wa CCM kuingiwa na hofu baada ya Jaji Warioba Kukabidhi Rasimu ya Pili ya Katiba kwa Rais.

Hofu ilitanda baada Kauli mbiu ya Viongozi wa Kitaifa wa CCM kama Bulembo Nape Kinana na hata Mzee Kingunge kukataa Mfumo wa Serikali 3 na kupigia chapuo mfumo wa seikali 2 na Rais kutopunguziwa Madaraka.

Hata hivyo baada ya Nape Nnauye na Kinana kufanya kampeni kuzunguka nchi nzima kuponda Wapinzani na Wanaharakati pamoja na Wale Waliopendekeza Serikali 3 bado Wananchi Wameipitisha Rasimu ambayo ina mambo ambayo ccm hawakupenda yaguswe ila yamepita kwa 64%.

Hapo ktk 64% ndipo wanaccm waliposhituka kuwa kwa takwimu hzo si nzuri kwao kwani ni kiashiria kwa wao kutokubalika kwa wananchi kama ilivyo kwa Wapinzani hasa cdm waliozunguka na mapendekezo yao wananchi wameyakubali kwa 64%.

Swali rahisi ni kuwa ccm kwa walivyojinasibu kuwa wanawanachama wengi kumbe sivyo ilivyo waliambulia 36% tu.

Watanzania sio wale wa zidumu fikira za fulani.

CCM nendeni na wakati na wala msipinge yale ya Wapinzani maana ni aibu mwisho wa siku.

nape alifikiri wanachi wa tz bado wako enzi za mwalimu? we subiri uone walikua wanakataa serikali tatu sasa watajiunga na wapinzani kuunga mkono hoja
 
Tanganyika yetu naitamani japo niione kabla siku zangu hazijakoma hapa duniani
 
Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.
Tuna kazi! Maoni yalikusanywa kutoka kwa Watanzania wote?! Labda kwa kukusaidia anamaanisha asilimia 64 kwa waliopata nafasi ya kutoa maoni ambao wametuwakilisha katika kusema tunapenda mfumo gani wa kuendesha nchi yetu tukufu!
 
Wewe 45M umeipata wapi wakati tunajua waislamu wote hawakuhesabiwa? Hiyo sensa tunajua ilichakachuliwa.

Mbona mimi na Faiza Fox na Ritz tulihesabiwa? Ina maana sisi ni Makadiani?
 
...walishaambiwa wajiande kisaikolojia wakatia pamba kweye masikio..."Kenge hasikii hada atokwe na damu masikioni"...

Kikwete ana machale kama nn.
Akili za kuambiwa Mara Rushwa itatuondoa sasa tujiandae kisaikolojia na hii katiba hata kama sio sera yetu.
 
Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.

dah! Mwalimu wako wa hisabati alipata tabu sana. Inapozungumziwa 64% ni asilimia inayotokana na idadi ya wananchi walioshiriki katika mchakato wa katiba na si idadi ya watanzania wote kwa ujumla. Sasa piga asilimia 64 ya 1.5 milioni utajua ni wananchi kiasi gani
 
Huo utafiti wa wanywa gongo Asilimia 64 ya Watanzania wote unaijua?
64/100x45,000,000=28,8000,000.
Wakati tume yenyewe imehoji watu Milioni 1.5 tu.

Utafiti wa wanywa gongo hauna Mashiko.
Tunataka serikali mbili.
You always speak in majestic plural as if you are in "the majority". Huu mwaka mtahama nchi hii mwende mtafute ya kwenu muwe na serikali mbili. Au tengeneza ya kwako chumbani, ya Watz lazima Tanganyika irudi na tayari imerudi, Zenji na Tanzania. Hupendi jiue!!!!!
 
Huu ndio upuuzi mwengine CDM majuzi tu hapa kulikuwa na thread wamefungua kanda ya ZnZ, hapo hapo kiongozi wao amenukuliwa mara nyingi akiponda wabunge wa ZnZ na muungano halikadhalika wao wanao wabunge wa viti maalumu kutoka huko huko (akiitwa kilaza aisye na ufahamu mnapinga).

Wewe huwezi ukawa na principles zako kichama halafu ukawa na kigeugeu kwenye maslahi ya kura ndio ujitie katikati, umeona wapi vyama vya siasa ambavyo havina msimamo. CDM na CUF hawana wanalolijua zaidi ya kusaka kura wao hata gongo kuhalalisha wapo tayari ilimradi kura, looser hapa ni CCM kwa kuburuzwa poor JK (what useless man) na huyu babu Mzee Warioba akapimwe akili kwanza maana umri umeenda mapendekezo ya kijinga kabisa.
 
Si kweli kwamba Watanzania 60% waliotaka serikali tatu wanaunga mkono Upinzani kumbuka pia kuna WanaCCM ndani ya hili kundi waliunga mkono pendekezo la kuwepo kwa serikali tatu na pia sio kweli kuwa katika lile kundi la Watanzania (30%) lililounga mkono serikali mbili wote ni WanaCCM ukweli ni kwamba kulikuwepo Watanzania wanaounga mkono Upinzani lakini walitaka serikali mbili.Get your facts right please!

Tamko la viongozi wa CCM ndiyo tamko la wanachama wote wa CCM.Mashambulizi ya Bulembo,Nape na Kinana dhidi ya Waryoba ni mashambulizi ya wanachama wote wa CCM dhidi ya Waryoba.Viongozi karibu wote wa CCM kasolo mwenyekiti wao walitoa tamko la kuzikataa serekali 3 na hilo ndilo tamko la chama na wanachama kwa ujumla wao.
 
Uwe unaota ndoto nzuri wakati mwingine,
Hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuchukua dola;
labda mpaka Kristo arudipo kwa mara ya pili.

Mamndenyi unaumwa au nini?
Mbona hakuna sehemu mtu kazungumzia upinzani kuchukua dola??
 
Back
Top Bottom