Joe Biden asinzia wakati Makamu wa Rais Dkt. Mpango akizungumza

Joe Biden asinzia wakati Makamu wa Rais Dkt. Mpango akizungumza

Unafikiri kwanini nchi ilimpenda?
Hivi sera, kauli zake hazikusaidia wananchi wengi kama Babu yako kijijini.
Nilitegemea nawe kumpenda, kama maudhui ya majadilano haya yalipo tukutanishia. Lakini naona taratibu unajiweka pembeni, umebaki tu kuwa mtu wa kupenyeza viswali hapa na pale, huku mjadala ukibadilika!
 
LOooooh!

Sasa mimi 'Kalamu', nami nimekuwa na "genge"?

Magufuli alikuwa 'strongman' asiye kuwa na busara ndani yake. Na ni kweli kuhusu hayo ya ukabila na kuendekeza makundi, tabia mbaya kabisa aliyo kuwa nayo.
Hapana. Sizungumzii "strongman" aina ya Magufuli, ingawaje yapo mambo ambayo 'instinctively' alikuwa akiyafanya kuonekana kuwa ya maslahi ya nchi; wakati huo huo aki-'sabotage' hata uzuri huo; kwa mfano kujenga uwanja wandege kwao na kupeleka raslimali nyingi huko isivyo kuwa na taratibu.

Lakini pamoja na haya yote, inashangaza sana kwamba alikoga roho nyingi za waTanzania. Na sababu yake ni hizo kelele alizo kuwa akifanya kuhusu "wanyonge".

Anahitajika kiongozi mwenye uelewa mzuri wa haya ya 'wanyonge' lakini pia asiwe mtu wa kuburuza tu watu katika maamuzi yake.

Sasa mkuu 'lookmasin'; kama kweli unataka kuniweka kwenye 'genge', basi nitafutie genge lisilo yumbishwa na chochote kuhusu maslahi ya Tanzania. Hilo genge nitalifurahia sana.. Vinginevyo, unanivunjia tu heshima.
N
Nilitegemea nawe kumpenda, kama maudhui ya majadilano haya yalipo tukutanishia. Lakini naona taratibu unajiweka pembeni, umebaki tu kuwa mtu wa kupenyeza viswali hapa na pale, huku mjadala ukibadilika!
Mjadala ni upi? Nini? Wewe mweyewe unetembea mbali.
 
Kababu kamechoka juzi kwenye mkutano wa G20 kule Brazil wakati wanataka kupiga picha ya pamoja kakawa kamechelewa kanabadilisha diaper

Viongozi wengine wakaona isiwe taabu wakapiga zao picha ya pamoja bila kababu kuwepo

View attachment 3169063
Angalia hii picha kwa makini sana. Hivi mtu aliyealikwa kwenye shughuli kihitifaki anatakiwa awe line ipi kwenye swala la picha ya pamoja.
 
Watu aina ya Biden, Philip mpango, mama presidenga na wanaofanana kitabia, hawafai kupewa nafasi ya mazungumzo ktk UMMA/mkusanyiko wa watu maana hawana Communication skills ya kutowachosha wasikilizaji wala kufikisha ujumbe kwa wasikilizaji bila kuicontrol attention ya wasikilizaji,

ni vile tu USA na kibabu Biden hakina madhara sababu ya Strong control ktk uongozi wa nchi Yao kuliko sisi ambao sidhani hata humu kama Kuna mtu anaweza kufurahia kusikiliza mazungumzo ya viongozi wetu Hawa wawili, Makamu na bosi wake, wote hawana mvuto ktk tasnia ya maongezi, Hawa kiuhalisa walitakiwa kupewa nafasi mahospitalini wawe ktk vitengo vya kuwatia moyo wagonjwa na watu wenye misongo ya mawazo.

Narudia Tena, mzigo tuliowabebesha madam presidenga na mwenzie Makamu, ni mzito sana kwao, kama huamini chukua clip ya dakika 10 ya Hawa viongozi wetu na clip ya dakika hizo hizo ya singeri/mwijaku/baba levo au doto magari alafu uone ni clip ipi utaitazama mpaka mwisho au ni clip ipi utaitazama bila kuskip.

Hata bwana yule aliyekwenda zake japo wapo wapinzani wasiompenda lkn maajabu yake mazungumzo yake yalifuatiliwa sana na mpaka Leo clips zake za maongezi nadhani ndizo zinaongoza kwa namba za viewers kuliko kiongozi wala mwanasiasa yeyote hapa nchi.

Kwa viongozi wetu suala la mawasiliano bado ni changamoto sana,
 
Hahahaaa hapana bana. Biden kachoka.

Analazimisha tu hiyo kazi ya urais.

Tofauti ya masaa kati ya Marekani na Angola ni kubwa vya kutosha.
Sasa mzee wa miaka zaidi ya 80 hivi mnatarajia afanyeje kweli kama siyo kusinzia?
 
Wakiwa Angola, Joe Biden anaonekana akisinzia wakati makamu wetu wa Rais akizungumza.

Babu Biden kachoka. Arudi kwao huko Delaware akapumzike na wajukuu wake.

Hii ni aibu.


View: https://youtu.be/3jqHuRkI6EE?si=Df4KXUIbUnRGzmxb

Video ndefu zaidi hii hapa….


View: https://youtu.be/Ikyt0nNX5lI?si=fj6waQjv-t4m6aC3

Philip Mpango afanyiwe rehearsal ya kuzungumza kwa kukaza sauti. Hata mimi kwenye speach hiyo ningeboreka na kusinzia kumuota cheupedawa wangu wa Kitunda😂😂😂
 
Kwa jinsi Tanzania ilivyo sasa,angeweza alale kabisa.Maana kuna mambo ukiskia ya Tanzania unatamani ulale kabisa au utumie dawa za usingizi
 
Back
Top Bottom