Joe Biden asinzia wakati Makamu wa Rais Dkt. Mpango akizungumza

Joe Biden asinzia wakati Makamu wa Rais Dkt. Mpango akizungumza

Nikukumbushe tu mkuu Kalamu, 2020 Kimei alivyoamua kugombea ubunge Vunjo, tulisoma maandiko mengi humu kuwa Mpango ajiandae kukabidhi wizara ya Fedha kwa Kimei.

Hayakuwa mawazo mabaya, lakini binafsi yalinishtua yalipotoka kwa wafuasi wa ccm na chadema. Inawezekana, hata leo, Mpango anaonekana si competent kwa kuwa tu hatokei kule tulikotaka atoke.

Mpango ni mpango wa Mungu. 2015 hakuwa na ndoto hata ya kugombea udiwani, leo ni makamu wa rais.
Kuna mambo ndani ya nchi hii, na baadhi ya watu wanao yasukuma kuwa mambo ya hovyo sana. Bado kuna waTanzania wanao amini anako tokea mtu (kabila, kanda, dini) ni muhimu zaidi na kumpa sifa ya juu kuliko wengine.

Tabia hii ilikuwa imeanza kufifia kwenye miaka ya 70; 80; lakini sasa haya mambo ndiyo yame pamba moto sana kila sehemu. Viongozi wa kisiasa ndio wanao yapa nguvu badala ya kuyakemea.

Hii inaifanya Tanzania kuwa hovyo zaidi hata pengine kulko Kenya tuliko kuwa tukiona mambo haya yakiwaumiza zaidi.
 
Yes, on speaking. Nyerere, Mkapa, Obama will not have such issue. Msikilize Rais wa Zambia hapo anavyotema madini. Sauti ya mamlaka, kauli thabiti anavyoongea kwa kujiamini. Akianza kuongea hata wewe huwezi kulala. Hakuna kujiumauma.
Sasa umejuaje kuhusu mimi mkuu 'Lookmasin'. Wewe unajuaje kuwa ninakogwa sana na hayo mawimbi ya sauti kuliko kilichomo kwenye hayo mawimbi?
Ni hivi. Wewe ulisema hapa kuwa mimi ni mbishi, lakini inaonekana wewe ni mbishi asiye kuwa na aibu. hata unapo ambiwa ukweli hutaki kuuelewa ukweli huo.
Kama una maswala yako mengine na Mpango, hayo ni mambo yenu, hatuyajui, lakini huwezi kusema Philip Mpango ni 'incompetent' kwa vile tu hukupenda sauti yake.

Sioni sababu ya kuendelea kupoteza muda na hili hapa. Tuendelee na m mengine.
 
Wakiwa Angola, Joe Biden anaonekana akisinzia wakati makamu wetu wa Rais akizungumza.

Babu Biden kachoka. Arudi kwao huko Delaware akapumzike na wajukuu wake.

Hii ni aibu.


View: https://youtu.be/3jqHuRkI6EE?si=Df4KXUIbUnRGzmxb

Video ndefu zaidi hii hapa….


View: https://youtu.be/Ikyt0nNX5lI?si=fj6waQjv-t4m6aC3

Biden sio anasinzia. Anashangaa aina ya hoja zinatolewa na Tanzania. Yeye amezoea kusikiliza hoja za nchi nyingine zimetayarishwa na marekani yenyewe😆
 
Biden sio anasinzia. Anashangaa aina ya hoja zinatolewa na Tanzania. Yeye amezoea kusikiliza hoja za nchi nyingine zimetayarishwa na marekani yenyewe😆
Mkuu, napenda kutofautiana na wewe kidogo kuhusu usinzifu wa Joe Biden.

Nadhani anachofanya huyu Mwamerika ni kulipiza kisasi kwa kile alichofanyiwa katika sekeseke na songombingo za uchaguzi wa urais Marekani.

Iko hivi: Japo Kamala na JB wanatokea chama kimoja cha Democrats, JB hakufurahia kufurushwa kwake urais halafu akapewa Kamala Harris.

Ndiyo maana JB alikuwa na furaha sana baada ya Kamala kupigwa chini na Trump, na hata hotuba yake ya kwanza kwa umma baada ya anguko hilo ilikuwa kemkemu kiasi kwamba hakuwa akijing'atang'ata na kugugumia kama tulivyomzoea.

Inadaiwa pia kwamba aliwaambia watu wake wa karibu kwamba kama angeingia yeye kwenye sanduku la kura angemshinda Trump kirahisi - katika namna fulani za kukebehi kushindwa kwa Harris.

Na wengine wametia chumvi kwamba huenda JB hata hakumpigia kura Kamala; kwamba kura yake alimpa Trump.

Sasa huu usinzifu wa kisasi unakujaje? Uhusiano wa karibu wa uswahiba kati ya Kamala na Dkt. Sa100 uko wazi kama mchana.

Si ajabu safari za rais zilikuwa nyingi nyingi kwenda Marekani sijui Q-ba, wakati wa uchaguzi wa Marekani, mpaka wengine wakasema anaenda kumfundisha Kamala jinsi ya kumshinda Trump kwa bao la mkono.

Kwa hiyo Kamala Harris na Sa100 ni chanda na pete, halafu Biden na Kamala haziivi. Halafu adui wa rafiki yangu (au rafiki wa adui yangu) ni adui yangu, siyo? Umeona? Patamu hapo!

Unakuja sasa mkutano muhimu kama huu. Biden, hasimu wake Kamala, ambaye Kamala ni swahiba wa Sa100 anategemea Sa100 awe mmoja wa wageni muhimu waalikwa mkutanoni.

Dkt. Samia, kwa sababu ya huba yake kwa Harris, anaamua kuususia kiaina mkutano wa JB.

Anamtuma makamu wake kwenda kumwakilisha. Kimsingi huku ni kususiwa, kwa sababu kwa cheo cha JB, mgeni mwalikwa alipaswa kuwa Sa100 na wala si Dkt. Mpango.

Sasa JB kuona hivyo kwamba amesusiwa, anaamua kupiga kaunta-attack ya Kiukreni! Naye anamsusia Dkt. Mpango (makamu wa Sa100, Sa100 swahiba wa Kamala, ambaye ni hasimu kwa sasa wa JB!)

JB anaamua kujisinzilisha bhana! Anajipigisha mbonji ya kutuma ujumbe kwa Sa100 na Kamala kinamna akiwaambia kimoyo moyo, Gotcha!
 
Mpango anavyoongea hata wewe utasinzia tu...
Una maana angalikuwa ni Samia mwenyewe hangalisinzia? Sababu wala siyo uzee kivile kwani kwa WHO definition uzee ni kuanzia umri wa miaka 80. Biden is just 81 years old, ndiyo tu kauanza uzee na ndiyo maana alipenda kuendelea kuwa rais.

Nadhani ni dharau tu ya Biden kwa nchi yetu. Kwa kuukataa ushoga katika utawala wa Biden, walifikiri wataua biashara yetu ya TAZARA na ya SGR huko DRC na Zambia. They are quite wrong. We are geographically in a much better position to compete by that Lobito route. On the contrary itatusaidia sisi kupeleka bidhaa na kuleta bidhaa kutoka Afrika Kusini.
 
Mentality ya kitumwa ingekuwa ni kiongozi mwafrika hakuna rangi angeacha kuona.Akifanya mzungu anatafutiwa sababu Inferiority complex ni tatizo kubwa sana.
Viongozi wote wa kiafrika walikuwa brilliant speakers. Kutoka Marcus Garvey, Kwame Nkurumah, Malcolm X, Luther King Jr, Nyerere, Mandela nk.

Ukiwa kiongozi hujajifunza kuongea na hadhira yako ndio utumwa, wenyewe.
Sasa umejuaje kuhusu mimi mkuu 'Lookmasin'. Wewe unajuaje kuwa ninakogwa sana na hayo mawimbi ya sauti kuliko kilichomo kwenye hayo mawimbi?
Ni hivi. Wewe ulisema hapa kuwa mimi ni mbishi, lakini inaonekana wewe ni mbishi asiye kuwa na aibu. hata unapo ambiwa ukweli hutaki kuuelewa ukweli huo.
Kama una maswala yako mengine na Mpango, hayo ni mambo yenu, hatuyajui, lakini huwezi kusema Philip Mpango ni 'incompetent' kwa vile tu hukupenda sauti yake.

Sioni sababu ya kuendelea kupoteza muda na hili hapa. Tuendelee na m mengine.
Kalamu, uwa maoni mazuri sana. Lakini wakati mwingine ukubali unakuwa mbishi.
 
Kuna mambo ndani ya nchi hii, na baadhi ya watu wanao yasukuma kuwa mambo ya hovyo sana. Bado kuna waTanzania wanao amini anako tokea mtu (kabila, kanda, dini) ni muhimu zaidi na kumpa sifa ya juu kuliko wengine.

Tabia hii ilikuwa imeanza kufifia kwenye miaka ya 70; 80; lakini sasa haya mambo ndiyo yame pamba moto sana kila sehemu. Viongozi wa kisiasa ndio wanao yapa nguvu badala ya kuyakemea.

Hii inaifanya Tanzania kuwa hovyo zaidi hata pengine kulko Kenya tuliko kuwa tukiona mambo haya yakiwaumiza zaidi.
Ni hivi Watanzania 80% hawaikubali CCM hata watu makini ndani ya CCM kama Warioba wako wengi watalendo..Ila hakuna alternative.
 
Viongozi wote wa kiafrika walikuwa brilliant speakers. Kutoka Marcus Garvey, Kwame Nkurumah, Malcolm X, Luther King Jr, Nyerere, Mandela nk.

Ukiwa kiongozi hujajifunza kuongea na hadhira yako ndio utumwa, wenyewe.

Kalamu, uwa maoni mazuri sana. Lakini wakati mwingine ukubali unakuwa mbishi.
Sasa hapa ubishi ni upi. Wewe binafsi unaona kuwa na "sauti" fulani ni sifa ya uongozi, mimi sioni hivyo. Tatizo ni nini?
 
Mzee mpango ni kama mwalimu wa mathematics akiingia darasani.akifundisha lazma ulale
 
Ni hivi Watanzania 80% hawaikubali CCM hata watu makini ndani ya CCM kama Warioba wako wengi watalendo..Ila hakuna alternative.
Nahofia kuweka namba, kama hiyo ya asili mia 80. Jamii yetu mahali kwingi haijawa na ufahamu wa kutoa maoni wazi bila ya kuvutwa na vitu visivyo kuwa na maana sana maishani mwao. Wewe angalia tu hata humu JF.

Lakini, ndiyo, ninakubaliana na wewe kuhusu ubovu wa CCM. Laiti kama pange tokea tukapata njia ya watu kuamua kwa haki na uhuru wote bila ya woga wowote, nami naamini kwamba CCM kwa sasa hivi inge kataliwa vibaya sana.

Lakini tatizo pia lina changiwa na kutokuwepo chama makini sana kinacho aminiwa na wananchi. CHADEMA wangeweza, lakini naona wanavurugana ndani kwa ndani, hasa viongozi wao.

lakini ngoja nikupeleke mahali tofauti kidogo na hayo niliyo eleza hapa.

Kwa hali yetu ilivyo, Tanzania kwa sasa hivi inahitaji "a strong man". Kiongozi ambaye hababaiki na anao msimamo hasa kuhusu maslahi ya nchi. Kiongozi huyu asiwe mwonevu kwa yeyote kwa sababu za kibinafsi. Kiongozi anaye heshimu taratibu na sheria. Kiongozi mkweli. Akisema kitu watu hawatilii mashaka juu yake.

Huyu ni kiongozi ambaye akipatikana kwa sasa, Tanzania itatulia; bila kujali hizo demokrasia za vyama vingi, n.k..
 
Nahofia kuweka namba, kama hiyo ya asili mia 80. Jamii yetu mahali kwingi haijawa na ufahamu wa kutoa maoni wazi bila ya kuvutwa na vitu visivyo kuwa na maana sana maishani mwao. Wewe angalia tu hata humu JF.

Lakini, ndiyo, ninakubaliana na wewe kuhusu ubovu wa CCM. Laiti kama pange tokea tukapata njia ya watu kuamua kwa haki na uhuru wote bila ya woga wowote, nami naamini kwamba CCM kwa sasa hivi inge kataliwa vibaya sana.

Lakini tatizo pia lina changiwa na kutokuwepo chama makini sana kinacho aminiwa na wananchi. CHADEMA wangeweza, lakini naona wanavurugana ndani kwa ndani, hasa viongozi wao.

lakini ngoja nikupeleke mahali tofauti kidogo na hayo niliyo eleza hapa.

Kwa hali yetu ilivyo, Tanzania kwa sasa hivi inahitaji "a strong man". Kiongozi ambaye hababaiki na anao msimamo hasa kuhusu maslahi ya nchi. Kiongozi huyu asiwe mwonevu kwa yeyote kwa sababu za kibinafsi. Kiongozi anaye heshimu taratibu na sheria. Kiongozi mkweli. Akisema kitu watu hawatilii mashaka juu yake.

Huyu ni kiongozi ambaye akipatikana kwa sasa, Tanzania itatulia; bila kujali hizo

Hi hivi Ata mkipata strong man kama Magufuli mtampigia kelele sababu ya ukabila wenu. Hamtamtambua wewe na genge lenu. Nafikiri mnataka Mbowe achukue nchi.atafanya mageuzi gani kwa akili hizi, zake?
 
Hi hivi Ata mkipata strong man kama Magufuli mtampigia kelele sababu ya ukabila wenu. Hamtamtambua wewe na genge lenu. Nafikiri mnataka Mbowe achukue nchi.atafanya mageuzi gani kwa akili hizi, zake?
LOooooh!

Sasa mimi 'Kalamu', nami nimekuwa na "genge"?

Magufuli alikuwa 'strongman' asiye kuwa na busara ndani yake. Na ni kweli kuhusu hayo ya ukabila na kuendekeza makundi, tabia mbaya kabisa aliyo kuwa nayo.
Hapana. Sizungumzii "strongman" aina ya Magufuli, ingawaje yapo mambo ambayo 'instinctively' alikuwa akiyafanya kuonekana kuwa ya maslahi ya nchi; wakati huo huo aki-'sabotage' hata uzuri huo; kwa mfano kujenga uwanja wandege kwao na kupeleka raslimali nyingi huko isivyo kuwa na taratibu.

Lakini pamoja na haya yote, inashangaza sana kwamba alikoga roho nyingi za waTanzania. Na sababu yake ni hizo kelele alizo kuwa akifanya kuhusu "wanyonge".

Anahitajika kiongozi mwenye uelewa mzuri wa haya ya 'wanyonge' lakini pia asiwe mtu wa kuburuza tu watu katika maamuzi yake.

Sasa mkuu 'lookmasin'; kama kweli unataka kuniweka kwenye 'genge', basi nitafutie genge lisilo yumbishwa na chochote kuhusu maslahi ya Tanzania. Hilo genge nitalifurahia sana.. Vinginevyo, unanivunjia tu heshima.
 
LOooooh!

Sasa mimi 'Kalamu', nami nimekuwa na "genge"?

Magufuli alikuwa 'strongman' asiye kuwa na busara ndani yake. Na ni kweli kuhusu hayo ya ukabila na kuendekeza makundi, tabia mbaya kabisa aliyo kuwa nayo.
Hapana. Sizungumzii "strongman" aina ya Magufuli, ingawaje yapo mambo ambayo 'instinctively' alikuwa akiyafanya kuonekana kuwa ya maslahi ya nchi; wakati huo huo aki-'sabotage' hata uzuri huo; kwa mfano kujenga uwanja wandege kwao na kupeleka raslimali nyingi huko isivyo kuwa na taratibu.

Lakini pamoja na haya yote, inashangaza sana kwamba alikoga roho nyingi za waTanzania. Na sababu yake ni hizo kelele alizo kuwa akifanya kuhusu "wanyonge".

Anahitajika kiongozi mwenye uelewgia mzuri wa haya ya 'wanyonge' lakini pia asiwe mtu wa kuburuza tu watu katika maamuzi yake.

Sasa mkuu 'lookmasin'; kama kweli unataka kuniweka kwenye 'genge', basi nitafutie genge lisilo yumbishwa na chochote kuhusu maslahi ya Tanzania. Hilo genge nitalifurahia sana.. Vinginevyo, unanivunjia tu heshima.
Unafikiri kwanini nchi ilimpenda?
Hivi sera, kauli zake hazikusaidia wananchi wengi kama Babu yako kijijini.
 
Back
Top Bottom