TANZIA Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

Wazungu wakisema hatuna akili tusikatae tangu saa 11 mpaka saa 2 mnauangalia tu? Hamna vituo vya polisi? hospital?
Kweli kabisa usemayo.
Tukio kama hili kwanza hata umati wa watu haitakiwi hapo zaidi ya vyombo habari, Usalama na watu wa paremedic Ambulance na mwili kuondokewa haraka iwezekanavyo Marehemu anasitiriwa!
Watu wameacha shughuli Aonasb na kwenda kushangaa waTanzania bado tuko Nyuma.
 
Atakuwa alikuwa Mwalimu huyu. Hawa jamaa tuwaangalie kwa karibu wataisha
 
Naomba huu uzi tusiuchanganye, ni uzi ambao utatusaidia wengi ukizingatia lililompata mwenzetu laweza mpata mtu yeyote.

Majura ya saa 11 alfajiri, kijana huyu alifanikiwa kuingia jengo ambalo kwa kawaida lina walinzi masaa 24.

Alifanikiwa kuingia na kupanda lifti hadi floor ya 15 , ambapo inasemekana akajirusha na kufariki hapo hapo hadi mida ya saa 2 ndipo mwili wake ukaonfolewa.

Mashuhuda wanasema alikuja na gari dogo aina ya suzuki swift ambayo aliipaki nje ya jengo hilo na kisha kuingia kwenye jengo hilo ambalo ni moja ya majengo marefu hapa tz.

Je nini kilimsibu kijana mwenzetu?

Inasemekana huyu kijana amewahi kufanya kazi kama MC?

Baadhi wanao mfahamu wanasema jumapili alikua kanisani vizuri, na wala hakuonyesha dalili zozote za msongo wa mawazo nk.

Je jina lake halisi ni nani na anaishi wapi?

RIP kijana mwwnzetu.

Jambo la kujifunza.. wanaume tujifunze kushare mambo yanayo tusibu hata kama tutaaibika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…