Pre GE2025 John Heche: Makonda anawahoji Polisi kwenye mkutano wa hadhara wa CCM kwasababu anawaona kama green guard

Pre GE2025 John Heche: Makonda anawahoji Polisi kwenye mkutano wa hadhara wa CCM kwasababu anawaona kama green guard

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Chadema ni wanafiki wakubwa. Ni viongozi wenye mwelekeo wa kimapinduzi tu ndani ya chama cha mapinduzi ndio wanaweza kufanikisha vita vya utawala bora nchini. Wananchi wameona na kushuhudia chini ya magufuli ufisadi na uzembe kupungua kwa kiwango kikubwa. Nyia ya kiliberali ya chadema imejaa unafiki mtupu. Wanasema eti utawala wa sheria wakijua mabwanyenye na fisadi wana uwezo wa kununua haki kwa wanasheria. Wananchi wanachohitaji ni utawala wa haki. Sheria ziko ila wanasheria wanageuza haki bishaa chini ya sera za kiliberali ambazo hazitufai afrika.
Wewe bila shaka kama sio waziri, mbunge wa kupita bila kupingwa au mkurugenzi wa taasisi furani kubwa, basi utakuwa mtoto wa mmoja wa kigogo
 
Pumba. Bashite hana cheo cha kiserikali. Yeye anatakiwa awawajibishe kwenye vikao vyao vya kichama tu basi.
Hapa ndo unapofeli mkuu
Kwa mfumo wa bongo kutii serikali ni kutii chama
No hard feelings.
Leo hii cdm ikikamata dola,itafanya haya haya

Kwani mpaka umefika umri wako huo huelewi kwanini kila chama kinataka kushikilia dola??
 
Katibu mwenezi nina serikalini mpaka amuhoji mtumishi wa umma!?ni kutojitambua tu una unaweza kuta alipo itwa akasimama na kumpigia kabisa salute.
Umeshawaita watumishi wa umma lakini hapo hapo unapinga wasihojiwe na huo umma wanaoutumikia?
Kama hawawajibiki inapaswa wahojiwe na wajibu kwa sababu gani hawatimizi wajibu wao wa kuwatumikia waliowaajiri.
 
Pumba. Bashite hana cheo cha kiserikali. Yeye anatakiwa awawajibishe kwenye vikao vyao vya kichama tu basi.
Fika kwenye taasisi kubwa zote
Wanapanga mipango yao kwa kufuata mambo mengi
Na kama hujajua miongoni mwa kitu kinachofuatwa ni plan za chama kinachoshikilia dola kwa muda husika

Fuatilia taasisi zote kubwa TRA,BOT,TCRA,MIFUKO etc
 
Makonda hajui JOB DISCRIPTIONS ZAKE. yeye huongea linalomjia tu. Nawashangaa wale wanaojitokeza kwenda kumsikiliza ni kina nani???
Watanzania wengi ni wapumbavu na wanaendeshwa kwa mihemko. Sisi kama nchi kuna haja ya kuangalia upya suala la mwenge.
 
Unaendelea kuamini ujinga wa Heche! Sasa kama kuna malalamiko RPC asihojiwe? Hivi Nyinyi CHADEMA ni wapuuzi sana! Polisi ipo kwa usalama wa raia na mali zao!
Kwa vile kahoji adui yenu Makonda mnabweka!
CHADEMA mnejaa chuki,unafiki na kutojua mnachotaka!
Sasa kwa akili ndogo tu, unaweza kuniambia CHADEMA imehusika vipi hapa? Hii nchi haitaendelea kamwe kwa kuwa na wapumbavu kama ninyi!

Hata kama mama mkwe wako yupo nyumbani kwako, huwezi kumuambia akutengee maji bafuni ukaoge, just tu kisa yupo kwenye nyumba yako.

Kila kitu kinahitaji utaratibu bana! Kwa sababu wewe ni baba mwenye nyumba utune tu?

Kuna wakati hata kwenye baadhi ya vyumba ndani ya nyumba yako huwezi fika hata kama nyumba umeijenga wewe na huwezi shitaki popote! Jifunze kenge wewe!
 
Makonda ndio nani? Bashite? Hilo jina la Makonda amelitoa wapi?

Mmekuwa mkitupigia kilele eti Bashite anatatua matatizo ya wananchi kwenye ziala zake.

Nimekuuliza swali dogo tu, tueleze tatizo moja tu la wananchi ambalo Bashite amelitatua ktk ziala zake. Naona unarukaruka tu

TUAMBIA MATATIZO YA WANANCHI AMBAYO BASHITE AMEYATATUA KTK ZIALA ZAKE
Alimpigia Waziri wa Maji Aweso kuhusu mota ya kusukuma maji huko Mkata na baada ya saa chache mota ikatengenezwa na wananchi wa Mkata wakapata maji.
Una swali jingine?
 
Wewe ni mpumbavu namba mbili baada ya kiongozi wako Heche!
Hebu Chadema tuambieni kama sio nyinyi kila siku mnalalsmika humu mitandaoni kwamba Polisi haifuati PGO?
Kwamba jeshi la Polisi linawabambika kesi raia nk!
Sasa li- chama la hovyo kama hili limejaa chuki saa yote mnawaza ubunge tu!

Kisa Makonda kawapeleka puta na anazidi kujiongezea umaarufu kwenye jamii kila anakopita nyinyi shwine wa Mbowe mnazidi kumsakama.
Chadema hamjitambuwi!
Hata jambo liwe zuri namna gani, lakini kama halifuati utaratibu uliopo kihalali ni ujinga na upumbavu.

Rudi darasani kaokote akili zilizosalia la sivyo kadiri siku zinavyokwenda ndo unazidi kupungua uwezo wa kufikiri, itafikia mahala utaanza kuvushwa barabara na trafiki
 
Alimpigia Waziri wa Maji Aweso kuhusu mota ya kusukuma maji huko Mkata na baada ya saa chache mota ikatengenezwa na wananchi wa Mkata wakapata maji.
Una swali jingine?
Kwa hiyo ikiharibika tena wamsubiri Makonda apite awasaidie?
 
Makonda hajui JOB DISCRIPTIONS ZAKE. yeye huongea linalomjia tu. Nawashangaa wale wanaojitokeza kwenda kumsikiliza ni kina nani???
Tabora walisombwa na mabasi ya NBS na kulikuwa na ugawaji wa pombe za kienyeji na t-shirt kupitia mabalozi na wenyekuti wa mitaa.
 
Alimpigia Waziri wa Maji Aweso kuhusu mota ya kusukuma maji huko Mkata na baada ya saa chache mota ikatengenezwa na wananchi wa Mkata wakapata maji.
Una swali jingine?

Kama hiyo motor ilisubiri simu ya Makonda kwa Aweso ndio ifanye kazi akiwa ziarani, ikiharibika tena matengenezo yatasubiri Makonda arudi huko kwenye ziara ndio itengenezwe? Hayo maigizo ndio njia ya kweli ya kutatua matatizo ya nchi?
 
Alimpigia Waziri wa Maji Aweso kuhusu mota ya kusukuma maji huko Mkata na baada ya saa chache mota ikatengenezwa na wananchi wa Mkata wakapata maji.
Una swali jingine?
Hahaa! Mnatengeneza tatizo na kulitatua ili kuwapata wadanganyika. Ccm kwa komedi hamjambo
 
Polisi walianza kujiingiza ccm, baadae wakajigeuza kuwa wanachama wa ccm. IGP kadhaa wameruhusu hilo litokee.

Leo Makonda anamuita mtu mwenye level ya RPC anamuhoji kwenye mkutano wa hadhara. Hii inatokea kwasababu Makonda anajua hawa ni wanachama wao.

Polisi wetu wanapaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na muongozo wao unaoitwa police general orders (PGOs) ni wapi Makonda na ccm wametajwa kwenye hivyo vitabu..

Kwamba jeshi la polisi lina makosa ni kweli, kwamba watu wanatekwa na serikali ya ccm na wengine kupotezwa kizembe ni kweli. Kwamba polisi wanapaswa kuwajibishwa ni kweli.

Sijwahi kuona hata IGP anawafokea RPCS hadharani.

Lakini RPC anaitwa na kuhojiwa kama mtoto mdogo bila kufuata sheria wala taratibu, huyu anawezaje kusimamia sheria na kutenda haki.

Makonda anawahoji kwenye hadhara kwasababu anawaona nyie ni green guard tu.

Tunahitaji kuunda upya chombo hiki muhimu kitakachoongozwa na watu wenye uwezo na weledi wa kusimamia sheria za Nchi.

Ule wimbo wa Mbeya unaosema anatuonna nyani tu.
 
Kama hiyo motor ilisubiri simu ya Makonda kwa Aweso ndio ifanye kazi akiwa ziarani, ikiharibika tena matengenezo yatasubiri Makonda arudi huko kwenye ziara ndio itengenezwe? Hayo maigizo ndio njia ya kweli ya kutatua matatizo ya nchi?
Mkuu tuna nchi ya ajabu sana
 
Kwani hao RPC's ni wakina nani mpaka wasihojiwe na wananchi?

Heche anataka kusema ili kuwahoji hao, kuna sheria maalum imewekwa kuonesha ni wakina nani wanaotakiwa kuwahoji RPC's?

- Kama ni hiyo PGO ndio imeainisha hayo, basi angetuambia ni kifungu kipi ndio kinasema hivyo.

Kama RPC's wamewekwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, sioni kwanini wasihojiwe na wananchi wanaowatumikia.

Wale sio mabosi wa wananchi, ni watumishi wa wananchi, na wala hawalipwi mishahara ili wakae ofisini, wanatakiwa kutoka wakasikilize kero za wananchi mitaani.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Labda utuambie pia kama ni ruksa kwa vyama vingine pia kuwahoji hao watu hadharani kwenye mikutano yao.
 
Wewe ni mpumbavu namba mbili baada ya kiongozi wako Heche!
Hebu Chadema tuambieni kama sio nyinyi kila siku mnalalsmika humu mitandaoni kwamba Polisi haifuati PGO?
Kwamba jeshi la Polisi linawabambika kesi raia nk!
Sasa li- chama la hovyo kama hili limejaa chuki saa yote mnawaza ubunge tu!

Kisa Makonda kawapeleka puta na anazidi kujiongezea umaarufu kwenye jamii kila anakopita nyinyi shwine wa Mbowe mnazidi kumsakama.
Chadema hamjitambuwi!

Punguza jazba, sio Kila mtu ni muumini wa siasa za kiki.
 
Kama hiyo motor ilisubiri simu ya Makonda kwa Aweso ndio ifanye kazi akiwa ziarani, ikiharibika tena matengenezo yatasubiri Makonda arudi huko kwenye ziara ndio itengenezwe? Hayo maigizo ndio njia ya kweli ya kutatua matatizo ya nchi?
Hizi sasa ni hisia tu, wala sio uhalisia, kwani kabla ya Makonda hapakuwepo na kero za wananchi zilizotatuliwa na viongozi wengine?

Kama Makonda anawaamsha kwa nafasi yake wanatenda, next time pakiharibika tena atatenda yule atakayekuwepo, msitake kulazimisha ionekane kama Makonda ndie mwanzo na mwisho wa kero za wananchi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Kama hiyo motor ilisubiri simu ya Makonda kwa Aweso ndio ifanye kazi akiwa ziarani, ikiharibika tena matengenezo yatasubiri Makonda arudi huko kwenye ziara ndio itengenezwe? Hayo maigizo ndio njia ya kweli ya kutatua matatizo ya nchi?
Hizi sasa ni hisia tu, wala sio uhalisia, kwani kabla ya Makonda hapakuwepo na kero za wananchi zilizotatuliwa na viongozi wengine?

Kama Makonda anawaamsha kwa nafasi yake wanatenda, next time pakiharibika tena atatenda yule atakayekuwepo, msitake kulazimisha ionekane kama Makonda ndie mwanzo na mwisho wa kero za wananchi.

Heche hajakatazwa na sheria yoyote kumpigia RPC yeyote na kumtaka maelezo kuhusu kero za wananchi wake, ni haki yake, na RPC anatakiwa kujibu kero zao, ni wajibu wake, na hata akijibu huo sio mwisho wa kero nyingine kuwepo, acheni kulia bila sababu.

Kama unayo sheria inayomkataza Heche kupiga simu kwa RPC yeyote na kumuuliza kuhusu kero za wananchi tuwekee hapa tuione, kinyume na hapo acheni kulia, nendeni field mkatende.

Sio kuimba tu sio utaratibu sio utaratibu... utaratibu gani huo usioainishwa kisheria mnaouimba?! au ndio unataka zile taratibu za kuwaacha wananchi na kero zao, mpaka kwanza wakakae kwenye vikao ndio next time arudi na majibu kwao!.

Mmekariri mambo mengi sana.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Hizo ndizo akili zinazoongoza nchi...
 
Back
Top Bottom