Uchaguzi 2020 John Mnyika: Tutawaandikia NEC wachukue hatua dhidi ya mgombea Urais wa CCM kwa kukiuka maadili ya uchaguzi

NEC ikipata barua ya Chadema halafu isipochukua hatua yoyote itampa Tundu Lissu uwanja mpana zaidi wa kupiga spana za hatari dhidi ya Magufuli, na NEC haiwezi kufanya fyoko. ndiyo tafsiri fupi na rahisi ya uzi huu!
Halafu Robert & Amsterdam atamalizia
 
Safi sana
 

Si ajabu wewe ni msomi mzuri tu, lakini huoni haya kujitoa ufahamu!

Sheria au utaratibu upo hivyo. Labda kama yangekuwa mambo ya dharula!

Lakini kwa vile Rais wetu huwa anadhani yeye ndiyo sheria, na wakushangilia kila akifanyacho hata nje ya utaratibu mpo mmojawapo ni wewe, aaaaaa anaona sawa tu. Lakini kwa wale wanaoona anaenda nje ya mstari, lazima waseme!
 
Kwanini hakufanya kabla ya kipindi hiki cha kampeni?
 
Mkuu hivi pasi na raisi pana waziri? Kama raisi ni mwenyekiti wa baraza la mawaziri, nafikiri sheria inapozuia waziri ina maanisha wadhifa, wadhifa ambao ni sehemu ya raisi.
Mkuu na zaidi ya yote hapo katiba haijamuongelea Rais inamzungumza Waziri,na sio Rais, Waziri akipewa maagizo anampa mtendaji kwa kuwa Katiba inamzuia yeye kufanya hivyo, lakini aliyeagiza ni Rais wa JMT.
 
Mmh! Sasa hawa NEC si ndiyo Magufuli mwenyewe? Sidhani kama itasikilizwa.
 
Nimeona wametajwa Wakuu wa Mikoa na Mawaziri hapo sijaona Rais katajwa hii inafanya nisielewe hoja ya Mnyika, au kuna mtu anaweza kunielewesha?
 
KInachofaika hapo ndiyo kampeni yenyewe hiyo ..... kampeni pia ni kuibua weakness ya mgombea mwingine!!
 
Hata Chadema ni tawi la CCM

Wagombea wake wa Urais wa 2010 na 2015 washarejea CCM

Hata kwny Mchakato wa Katiba Mpya Chadema kwa kushirikiana na Rafiki yao Lipumba walisusia mchakato Bungen
NEC haiko huru ni tawi la CCM
 
Ndoto za mchana hizi dah NEC hii ya kubadilisha form na kuengua wagombea imwadhibu JPM ? hampo seriously
Ili mradi wameyabainisha mapungufu ya mgombea wa CCM na yameonekana wazi, hiyo peke yake inatosha..........

Hata kama NEC watashikwa na "kigugumizi" na kutomchukulia hatua yoyote huyo mgombea wa CCM, lakini message itakuwa tayari imekuwa sent & delivered
 
NEC ikipata barua ya Chadema halafu isipochukua hatua yoyote itampa Tundu Lissu uwanja mpana zaidi wa kupiga spana za hatari dhidi ya Magufuli, na NEC haiwezi kufanya fyoko. ndiyo tafsiri fupi na rahisi ya uzi huu!

Umewaza sambamba na mimi, iwapo NEC haitachukua hatua yoyote watafanya cdm isibanwe kwa chochote, na ni njia nzuri sana ya kudhihirisha kuwa tume sio huru.
 
Delete ccm Oct 28
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…