Joseph Butiku: Vyombo vya Ulinzi na Usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini

Hapa ndio nimeelewa kidogo alichokuwa amekikusudia kukifikisha kwa Wananchi na kwa Serikali Mzee Butiku !
Mzee Butiku na Taasisi yake wameanza kuona kuwa huko tunakotaka kuelekea kama Taifa siko kabisa. !
 
Hili lilipofika linahitaji mjadala wa kitaifa labda katiba yetu inaruhusu baadhi ya watu wanao pewa dhamana kuahirisha kufikiri kizalendo, a.k.a kujizima data
 
Ina maana hata Sativa aliyesema alifikishwa kituo cha polisi oysterbay na baadae kukutwa pori la Katavi haitoshi kujua nani anahusika na matukio hayo?
 

Hawa nao wanabweka na kupiga kelele vilevile kama wengine....

Rais Samia Suluhu Hassan ameshasaidiwa kwa kuambiwa anachopaswa kufanya kwa mujibu wa katiba...

Mzee Butiku na taasisi yako, huyu Rais sisi wananchi tumeshamwambia aunde tume maalumu ya kijaji bila kuhusisha polisi wala TISS ambao nao ni watuhumiwa ili ichunguze mambo haya....

Kwani mnataka wananchi tumpe msaada upi zaidi ya yeye kutumia mamlaka yake ya kikatiba kutimiza wajibu wake....?

Mnataka wananchi tumsaidieje kwa mfano? Kwamba kila mwananchi abebe rungu na panga tuingie mitaani kuwasaka magaidi na majambazi hawa au....?

Rais hawezi kuwaagiza polisi na TISS haohao wanaotuhumiwa wajichunguze. Hili anapaswa kulijua kama anajipenda kweli....!!
 
Yaani jeshi la Polisi huwa linakuwa na majibu mepesi Kwa maswali magumu.

Eti ishu ya Lissu walidai eti mpaka dereva wa Lissu apatikane.
Na wakasema hawafanyii kazi taarifa za mtandaoni na kumtaka Lissu na dereva wake wafike polisi lakini tukio la kinyama la kada wa CDM wametoa taarifa kwa kurejea source za mitandaoni. Mtu yeyote anayeamini wanasiasa wanaosema nchi ina amani warejee tukio la Lissu. Kama mtu mashuhuri kama Lissu anapigwa risasi mchana kweupe tena kwenye eneo la serikali linalolindwa na hakuna hatua zilizochukuliwa jiulize vipi kwa mwananchi wa kawaida. Amani ipo kwa watawala na wote walioshikamana na ccm.
 
Tangu IGP Mangu amestaafu imekuwa changamto sana
 
Kwa wale waliosomea Cuba tu ,
Naomba ufafanuzi kidogo kwa kile alichokisema Mzee Butiku na kukusisitiza kwamba
Tunaye Rais mmoja tu wa Tanzania 🇹🇿
Hatuna maraisi wawili wala watatu tunaye mmoja tu !

Ambaye ndiye anayetakiwa na Katiba kuiendesha Nchi kwa mujibu wa Sheria na kuilinda Katiba ya Nchi kama alivyoapa kuilinda !

Je Taasisi yake Mzee Butiku imehisi wapo wengine huko pembeni ndio wanaoleta hizi Tafrani ???!!
 
Tusiseme hatuwajui wahalifu hao, tunawajua. Wanaishi miongoni mwetu na katika kaya zetu, wako ndani ya vyombo vyetu vya dola, wako makanisani na katika misikiti. Tunawajua, lazima serikali yetu iwajue.
Tunawajua ndio na this time tutadili nao! Hakuna damu itamwagika kizembe tena! Watalipa! Wao au wengine
 
Wakati Sheria ya Usalama wa Taifa inafanyiwa marekebisho Mwaka Jana pale Bungeni, Mhe. Lissu aliipigia sana Kelele lakini bahati mbaya hakupata sapoti ya kutosha.

Kwa kifupi hao Jamaa wamepewa Mandeti kubwa ya kufanya na kutenda mambo mengi ya gizani pasipo kuhojiwa huku Wakilindwa na Sheria hiyo mpya.

Tukiendelea kunyamaza wataendelea kutesa na kuwapoteza watu hadi wote tuishe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…