Pre GE2025 Joseph Oleshangay: Kuna watu wanataka Kuvunja Chama ili kumtengenezea Samia Njia Nyeupe Ya Ikulu

Pre GE2025 Joseph Oleshangay: Kuna watu wanataka Kuvunja Chama ili kumtengenezea Samia Njia Nyeupe Ya Ikulu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hakuanza leo.
1. Kama nakumbuka sawa sawa Lissu aliwahi kusema kuwa Mbowe hakumshikia drip baada ya kupigwa risasi bali ni Msigwa. Inawezekana ni kweli lakini aliisema kama vile Mbowe alikuwa anajipendekeza. Nikadhani ni kuteleza tu na ni hulka ya msema kweli.
2. Akaanza kuzungumzia mapungufu ya chama chake jukwaani. Alipoulizwa, akasema akasemee wapi? Insinuation ni kuwa Boss wake anayakumbatia.
3. Zikaanza tuhuma za yeye na Msigwa kutaka kufanya mapinduzi, akakaa kimya. Msibwa akawa anamtukana Mbowe, yeye kimya. Msigwa kahamia CCM, yeye kimya. Msigwa akawa anashambulia CDM na Mwenyekiti wake, yeye kimya.
4. Chadema wakatangaza kikao cha Kamati Kuu. Yeye wala hakujisumbua kuhudhuria badala yake publically akahudhuria mazishi ya mpiganaji mmoja wa CDM. Hii ni dhahiri ilikuwa kuonyesha kuwa Mbowe hajali wanachama wake.
5. Akaibua hili la kuhongwa na Abdul. Hadithi ambayo haina kichwa wala miguu.
6. Akazungumzia watu kung'ang'ania madaraka. Wote tulijua anamsema Mbowe

Kinachonisikitisha ni kuwa haikupaswa kuwa hivi. Angeweza kugombea bila kumpaka matope Boss wake. Nadhani washauri wake walimwambia kuwa ukitaka kuhakikisha kuwa nyoka amekufa inabidi umkate kichwa. Hivyo shutuma, maneno ya ovyo n.k. vingemtisha Mbowe kutangaza nia. Big miscalculation. Badala yake anaonekana kama opportunist asiyekuwa na chembe cha loyalty.

Na sasa, kama atashindwa, nafasi ya kugombea urais itakuwa hati hati. Labda ahamie ACT-WAZALENDO. Akifanya hivyo atawasaidia kupata wabunge wengi pengine hata zaidi ya CDM. Lakini yeye heshima yake itakuwa zero.

Amandla...
Naona umechanganya mambo au umekosa utulivu wakati wa kuandika:

Eti labda ahamie ACT, akihamia ACT atasababisha kupatikana wabunge wengi ACT kushinda CHADEMA, ila yeye atakosa heshima!! Aliyesababisha kupatikana wabunge wengi, atakosaje heshima? Atakosa heshima kwa nani? Aliosababisha wapate wabunge wengi kwa aliowasababishia wapate wabunge wachache?
 
Nimepoteza sana matumaini na Chadema, labda kama Lissu atashinda kitu ambacho sikioni maana Mbowe tayari atasaidiwa sana na Ccm kushinda kwa mbinu zao.

Kilichobaki tu nikuiomba Ccm ituletee mgombea yeyote wa kiume hata kama atakuwa January lakini si huyu mama.

Sikutegemea kabisa Mbowe aliyekipambania chama na watu wengi wamepoteza maisha wakikipambania chama kumbe mwenyekiti ni wa upande wa pili dah hii ni hatari sana. Bila Mungu kutupambania Ccm italitesa sana taifa hili.
Lissu pamoja na madhaifu yake lakini ni mpinzani wa kweli sana na hapendi kabisa rushwa ila haoni taabu kupambania kilicho haki yake.

Pamoja na maovu yote yaliyofanyika serikali za mitaa Mbowe haoni kama kuna shida. Natamani wanaopiga kura kumchagua mwenyekiti wakiweza wale pesa za Mbowe maana najua atatoa fungu kubwa sana kwa wajumbe wa mkutano mkuu ili ashinde na hizo pesa zitatoka kwa mama Abdul ila mwisho wa siku nilitamani wampigie kura Lissu.
 
Kongole Fundi Mchundo umemaliza kila kitu, hawa ni wanaharakati wa mitandaoni wanaomponza Lissu. Wanajifanya kum sympathy Soka siku maandamano yakiitwa wanabaki ku zoom kwenye laptop kuangalia nani kaenda.

Mbowe yupo sahihi kabisa dunia nzima inaimba maridhiano wewe unataka kutunishiana tumbo na dola. kama wanataka chama cha uanaharakati waanzishe chao.
Hahaaa bana ety kutunishiana tumbo dah OK msuli na give apparatus
 
Mbona uwezekano mkubwa mgonjwa na wewe!! Mleta mada ameweka analysis nzuri.
Analysis gani..maelezo yote tena kamilifu yametolewa, katiba ya chadema inamruhusu Mbowe kugombea na walipokubaliana kutoweka ukomo kulikuwa na sababu..vyama vya siasa na mbaya zaidi hapa Tanzania vinaoperata kwenye mazingira yanayohitaji mtu aina ya Mbowe..chama kikipata mtu wa aina hii hakiwezi kukubali hoja za kijinga ili kife! Mmeshindwa kupigia kelele katiba uwepo ukomo wa ubunge ambao wanaishi kwa kodi zenu mmepepesukia jambo dogo la chadema ambao wanajitoa kupigana kwa ajili yenu..mwenyekiti apate timu nzuri ya kumsaidia ili chama kiendelee kupigania maslahi ya nchi..na imeelezwa bayana mambo yote haamui mwenyekiti peke yake..yeye ni kamisaa tu mambo yote yanaamuliwa pamoja!
 
Mbona huyu lussi alipewa nafasi na Mbowe 2020 ashindane na jiwe, , kwani kuna shida gani kuwa na mwenyekiti na mgombea raisi ni mwingine kama huyu lussi alivyopewa?
Huyu mnyaturu hajielewi, anadhani akiwa mwenyekiti ndio atashinda uchaguzi, ni kama anasahau ilikuwaje yeye na jiwe 2020
Kiukweli tunajua na hata hawa chawa wa lissu mitandaoi wanajua kabisa 2025 hawataweza kumshinda mama
Lakini wanakaza fuvu
 
20241221_195856.jpg
 
Naona umechanganya mambo au umekosa utulivu wakati wa kuandika:

Eti labda ahamie ACT, akihamia ACT atasababisha kupatikana wabunge wengi ACT kushinda CHADEMA, ila yeye atakosa heshima!! Aliyesababisha kupatikana wabunge wengi, atakosaje heshima? Atakosa heshima kwa nani? Aliosababisha wapate wabunge wengi kwa aliowasababishia wapate wabunge wachache?
Kuna neno "pengine". Nitajie mtu mmoja aliyehama Chadema akabakia na heshima aliyokuwa nayo akiwa Chadema? Lissu akihamia ACT-Wazalendo atashutumiwa kuwa kuwa yeye ni mganga njaa. Hata kama sio kweli wako watakao amini. Na wako pia watakaoamini kuwa "amepewa" wabunge hao ili kupunguza nguvu ya CDM na kuifanya ACT-Wazalendo kuwa kambi rasmi ya upinzani.

Amandla...
 
Huu uongo ndio unaowaponza. Mbowe hakumsifia Samia bali alisema kuna mambo waliyapata kutokana na maridhiano.

Hivi mnataka kutuaminisha kuwa mlikuwa tayari kuingia barabarani kushikiza mikutano ya hadhara, kufutiwa kesi mamia ya wana Chadema? Nyinyi ambao mkiona askari ameshika fagio mnakimbilia kujifichq chooni!

Huyo mnaemsimanga amefungwa, ametungiwa kesi za ajabu, biashara zake zimefungwa n.k. lakini hakutetereka. Alipoita maandamano ya kupinga utekaji wa wakina Sato, mauaji ya Kibao na wengine mlitoa kisingizio kuwa anawachuuza watoto wa wengine wakati wa kwake wanakula bata ughaibuni. Alijitokeza yeye na binti yake, wote mkajificha. Angalau wakina Hilda walifika sehemu ya maandamano na wakina mama wengine. Aidha, wako waliozuiwa wakitoka bara ( wengi wao wakiwa wanawake).

Wanawake wa Bawacha waliandamana kwenda ubalozi wa Marekani kushinikiza Mbowe aachiwe na wengine walitiwa ndani. Nyinyi mashujaa, wanasheria mkaufyata!

Hata Lissu akishinda hamtathubutu kujitokeza kumuunga mkono katika hiyo mass mobilization. Tofauti yake na Mbowe ni kuwa mkimzenguq atawaachia nchi yenu wakati Mbowe alibaki humu humu nchini.

Badala ya kuchochea mambo ya kijinga mngewahimiza washindani washindane kwa lugha za kiungwana bila character assassination yeyote. Wakifanya hivyo itakuwa rahisi kwa wafuasi wao kuungana pamoja na atakae shinda.

Kwa kweli hamukitakii mema Chadema.

Amandla...
Mbona kama unabwabwaja tu inshu apa chadema ilikataa uchaguzi halafu chini ya uwongozi wa mbowe wameenda kuchukuwa ruzuku bado kiongozi huyu anafaa kuongoza mapambano
 
Huu uongo ndio unaowaponza. Mbowe hakumsifia Samia bali alisema kuna mambo waliyapata kutokana na maridhiano.

Hivi mnataka kutuaminisha kuwa mlikuwa tayari kuingia barabarani kushikiza mikutano ya hadhara, kufutiwa kesi mamia ya wana Chadema? Nyinyi ambao mkiona askari ameshika fagio mnakimbilia kujifichq chooni!

Huyo mnaemsimanga amefungwa, ametungiwa kesi za ajabu, biashara zake zimefungwa n.k. lakini hakutetereka. Alipoita maandamano ya kupinga utekaji wa wakina Sato, mauaji ya Kibao na wengine mlitoa kisingizio kuwa anawachuuza watoto wa wengine wakati wa kwake wanakula bata ughaibuni. Alijitokeza yeye na binti yake, wote mkajificha. Angalau wakina Hilda walifika sehemu ya maandamano na wakina mama wengine. Aidha, wako waliozuiwa wakitoka bara ( wengi wao wakiwa wanawake).

Wanawake wa Bawacha waliandamana kwenda ubalozi wa Marekani kushinikiza Mbowe aachiwe na wengine walitiwa ndani. Nyinyi mashujaa, wanasheria mkaufyata!

Hata Lissu akishinda hamtathubutu kujitokeza kumuunga mkono katika hiyo mass mobilization. Tofauti yake na Mbowe ni kuwa mkimzenguq atawaachia nchi yenu wakati Mbowe alibaki humu humu nchini.

Badala ya kuchochea mambo ya kijinga mngewahimiza washindani washindane kwa lugha za kiungwana bila character assassination yeyote. Wakifanya hivyo itakuwa rahisi kwa wafuasi wao kuungana pamoja na atakae shinda.

Kwa kweli hamukitakii mema Chadema.

Amandla...
Mbowe ni mwenyekiti wa maisha wa Chadema
 
Mbowe ni mwenyekiti wa maisha wa Chadema
..elewa na sababu za hali hiyo, hivi alipopatikana Mashinji kuwa katibu mkuu kuna mtu alitarajia huyu mtu ataishia kuwa DC wa ccm sawa na kina mchopanga? akili zenu haziko sawa, lkn mifano ipo..kwani Mbowe si binadamu? Kwa nini bado yupo chadema katikati ya misuko suko isiyoisha? Lisu hawezi kuwa km Mashinji? au Katambi, au Waitara..au Msigwa ana tofauti gani Lisu na hao..
 
Huu uongo ndio unaowaponza. Mbowe hakumsifia Samia bali alisema kuna mambo waliyapata kutokana na maridhiano.

Hivi mnataka kutuaminisha kuwa mlikuwa tayari kuingia barabarani kushikiza mikutano ya hadhara, kufutiwa kesi mamia ya wana Chadema? Nyinyi ambao mkiona askari ameshika fagio mnakimbilia kujifichq chooni!

Huyo mnaemsimanga amefungwa, ametungiwa kesi za ajabu, biashara zake zimefungwa n.k. lakini hakutetereka. Alipoita maandamano ya kupinga utekaji wa wakina Sato, mauaji ya Kibao na wengine mlitoa kisingizio kuwa anawachuuza watoto wa wengine wakati wa kwake wanakula bata ughaibuni. Alijitokeza yeye na binti yake, wote mkajificha. Angalau wakina Hilda walifika sehemu ya maandamano na wakina mama wengine. Aidha, wako waliozuiwa wakitoka bara ( wengi wao wakiwa wanawake).

Wanawake wa Bawacha waliandamana kwenda ubalozi wa Marekani kushinikiza Mbowe aachiwe na wengine walitiwa ndani. Nyinyi mashujaa, wanasheria mkaufyata!

Hata Lissu akishinda hamtathubutu kujitokeza kumuunga mkono katika hiyo mass mobilization. Tofauti yake na Mbowe ni kuwa mkimzenguq atawaachia nchi yenu wakati Mbowe alibaki humu humu nchini.

Badala ya kuchochea mambo ya kijinga mngewahimiza washindani washindane kwa lugha za kiungwana bila character assassination yeyote. Wakifanya hivyo itakuwa rahisi kwa wafuasi wao kuungana pamoja na atakae shinda.

Kwa kweli hamukitakii mema Chadema.

Amandla...
Yaani unyimwe haki zako ambazo zipo kwa mujibu wa katiba..halafu ukipewa tena uanze kufurahia?
 
Anaandika Wakili Joseph oleshangay

freemanmbowetz anaashiria maridhiano yalikwama Kwa sababu ya negative energy kutoka Chadema “team Lissu”

Kwa sehemu kubwa ya hotuba ya freemanmbowetz , suluhuSamia is just a pure soul.

Anasema wamenunua ofisi 1.6b kutokana na maridhiano wakapewa ruzuku. Ila anasema malimbikizo ya ruzuku Kwa sababu wao walikataa

Pia anasema haiwezekani kubadili uongozi katikati ya mapambano. Strongman mentality.

Pia kwa hotuba yake msamiati wa term limit haipo kwenye kamusi yake.

Kwa ujumla @freemanmbowetz hajasema lolote kuhusu kubadili strategy ya mapambano wala kujibu hoja kuwa yeye ni mteremko wa CCM kufanya yake.

Walau inaonekana, ndani ya Chadema kuna kusigana kwa muda mrefu na hii ndio sababu hata kwenye operation za Chadema, Lissu anatumia gari yake binafsi.

Pia walau ni wazi Kwa muda kuwa wakati Lissu akifanya peoples movement, wenzake wapo katikati ya movement na kushangilia mfumo wanaodai kuwatesa.

Nikiona vijana wanaharakati ambao kila siku wanasema free @DEUSDEDITHSOKA et al, wapo na @TunduALissu na waliosema @DEUSDEDITHSOKA anajitekenya wapo na mwamba (nusu-jiwe). This says much

Wale akina mama 19 waliosemekana walipelekwa bungeni na Ndugai wapo na Mbowe…….

Balile anapata wapi nafasi ya ku moderate? Balile si ni CCM kabisa na kama ana la ziada ni wakala?

Ni ngumu sana kuamini kuwa utawala wa vyama vya upinzani haipo mikononi mwa mawakala wa mfumo tawala kuigiza kuna vyama vingi.

Namna CHADEMA establishment wanavyopambana na Lissu, CHADEMA sio siku nyingi ipo kwenye mserereko.

Lissu tu kutangaza kugombea uwenyekiti, imekuwa nongwa.

Kuna maneno kuwa mwenyekiti katikati ya kampeni 2020 alisema “Lissu anadhani atamshinda Magufuli “?……..

Anyway, kuna watu wanamtengenezea @SuluhuSamia ushindi bila kupora kura kama kawaida ya CCM.
Tunamuomba FM atumie busura hajiondoe kwenye uchaguz kwa nia njema amuachie TL ili kukiokoa chama
 
Samia hagombei 2025.
Samia hatagombea ila anaitengenezea njia nyepesi ccm kushinda urais 2025 kwa kumpetimpeti mbowe na maridhiano-bandia.

Ila 2025 baada chuma kingine kutoka ccm kuingia ikulu , chadema itakuwa imeshajifia tayari wala hakuna atakaye hangaika na mbowe.
 
Tanzania hakuna upinzani me ndio mana siwaamin wanasiasa kabisa watajua na mambo yao
 
Huu uongo ndio unaowaponza. Mbowe hakumsifia Samia bali alisema kuna mambo waliyapata kutokana na maridhiano.

Hivi mnataka kutuaminisha kuwa mlikuwa tayari kuingia barabarani kushikiza mikutano ya hadhara, kufutiwa kesi mamia ya wana Chadema? Nyinyi ambao mkiona askari ameshika fagio mnakimbilia kujifichq chooni!

Huyo mnaemsimanga amefungwa, ametungiwa kesi za ajabu, biashara zake zimefungwa n.k. lakini hakutetereka. Alipoita maandamano ya kupinga utekaji wa wakina Sato, mauaji ya Kibao na wengine mlitoa kisingizio kuwa anawachuuza watoto wa wengine wakati wa kwake wanakula bata ughaibuni. Alijitokeza yeye na binti yake, wote mkajificha. Angalau wakina Hilda walifika sehemu ya maandamano na wakina mama wengine. Aidha, wako waliozuiwa wakitoka bara ( wengi wao wakiwa wanawake).

Wanawake wa Bawacha waliandamana kwenda ubalozi wa Marekani kushinikiza Mbowe aachiwe na wengine walitiwa ndani. Nyinyi mashujaa, wanasheria mkaufyata!

Hata Lissu akishinda hamtathubutu kujitokeza kumuunga mkono katika hiyo mass mobilization. Tofauti yake na Mbowe ni kuwa mkimzenguq atawaachia nchi yenu wakati Mbowe alibaki humu humu nchini.

Badala ya kuchochea mambo ya kijinga mngewahimiza washindani washindane kwa lugha za kiungwana bila character assassination yeyote. Wakifanya hivyo itakuwa rahisi kwa wafuasi wao kuungana pamoja na atakae shinda.

Kwa kweli hamukitakii mema Chadema.

Amandla...
Kwamba Mbowe kwenda kudanganywa na Samia kwako ndiyo jambo la maana? Je na alipodanganywa hayo mambo ya utekaji yalikoma? Zaidi sana tumejua kuwa kumbe hata enzi hizi za Samia wale team Mbowe hawatapata madhila maana kamanda wao analamba miguu. Hakuna chama cha upinzani wa kweli cha aina hiyo.

Jana Mbowe alionyesha dhahiri kuwa ana jambo lake Chadema yeye pamoja na hao wafuasi wake ambalo ni tofauti kabisa na sisi tunavyoamini. Mbona Slaa tulikuwa tukimuunga mkono? Jinsi ambavyo tulifanya kwa Slaa basi vivyo hivyo tungefanya kwa kiongozi aina ya Lissu. Mbowe ameshajionyesha kwa kila mtu kuwa ni nani. Hafichiki tena wala hasafishiki. Ungekaa tu chini ukafikiri tunahitaji nini kwa kipindi hiki basi ungeona kabisa Mbowe siyo mtu sahihi kutupeleka. Kama huwezi kujua zaidi ya kutaka Mbowe aendelee kujilipa fadhila basi pole.
 
Back
Top Bottom