MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Mabadiliko ya kweli kwenye nchi huletwa pale tu vijana wanapohamasika kujihusisha na siasa. Vijana wanaweza kubomoa au kujenga nchi. Kiongozi dhalimu Charles Taylor aliwatumia vijana kujiwezesha kurudi madarakani huku akiwa kamwaga damu za watu wengi wasio na hatia wakiwemo wazazi wa hao vijana. Vijana wa Liberia katika upumbavu wao wa hali ya juu waliamua kumchagua tena Charles Taylor. Vijana wa majirani zetu Zambia wao mwaka juzi 2021 wakaamua kwa pamoja kumchagua kwa kishindo Rais Hichilema na kukiondoa madarakani chama tawala cha PF kwa njia za kidemokrasia. Hiyo ni mifano miwili ya nguvu ya vijana kwenye mambo ya kisiasa.
Hapa nchini kwetu mara baada ya uchaguzi wa 2015 tumeona morali ya vijana ilishuka kabisa katika wakati wote wa uongozi wa awamu ya 5. Vijana walikosa kabisa uhuru wa kujadili mambo muhimu yanayowahusu. Hata vijana waliokuwepo kwenye uongozi (kina Sabaya) walifanya mambo ya kipuuzi sana hivyo kuzidi kuwakatisha watanzania wengi. Ilifikia hatua baadhi ya vijana kutotaka hata kujiandikisha kupiga kura. Kimsingi kwenye siasa wakabaki vijana wenye maslahi ya moja kwa moja na vyama vyao kwa mfano kina John Pumbulu wa CHADEMA na Kheri James wa CCM.
Ujio wa uongozi mpya wa Mama Samia Suluhu umeleta tena matumaini ya vijana wengi kuanza kujihusisha na siasa tena. Rais karuhusu watu kujadili mambo yao bila vikwazo wala vitisho. Mitandaoni mada nyingi zinajadiliwa huku watu wakipingana kwa hoja. Hii itahamasisha vijana wengi wenye vipaji vya uongozi na siasa waliokuwa wamekata tamaa kujiingiza kwenye siasa na kusaidia kuondoa viongozi wabovu. Hata hii katiba mpya inayoliliwa na upinzani inaweza kujadiliwa kisomi na muafaka ukapatikana. Vijana wakiamua hakuna wa kupinga. Kiukweli wanaotaka uongozi kwenye uchaguzi wa 2025 wajipange haswa maana kuna sura changa nyingi mno zitajitokeza kwenye udiwani na ubunge.
Mama Samia alishaliona hili ndo maana hata serikali yake ina vijana wengi kwenye ngazi za juu za uongozi. Tanzania kwa sasa ina Spika kijana Mheshimiwa Tulia Ackson, waziri wa fedha kijana Mwigulu, na viongozi vijana wengi sana kama kina Bashe, Polepole, Nikki wa pili, Joketi, Jenista Mhagama, Angela Kairuki, Alexander Mnyeti, Januari Makamba. Kama ilivyokuwa kwa Hichilema wa Zambia hata sisi vijana wa Tanzania tutamchagua kwa kishindo Mama Samia mwaka 2025.
Hapa nchini kwetu mara baada ya uchaguzi wa 2015 tumeona morali ya vijana ilishuka kabisa katika wakati wote wa uongozi wa awamu ya 5. Vijana walikosa kabisa uhuru wa kujadili mambo muhimu yanayowahusu. Hata vijana waliokuwepo kwenye uongozi (kina Sabaya) walifanya mambo ya kipuuzi sana hivyo kuzidi kuwakatisha watanzania wengi. Ilifikia hatua baadhi ya vijana kutotaka hata kujiandikisha kupiga kura. Kimsingi kwenye siasa wakabaki vijana wenye maslahi ya moja kwa moja na vyama vyao kwa mfano kina John Pumbulu wa CHADEMA na Kheri James wa CCM.
Ujio wa uongozi mpya wa Mama Samia Suluhu umeleta tena matumaini ya vijana wengi kuanza kujihusisha na siasa tena. Rais karuhusu watu kujadili mambo yao bila vikwazo wala vitisho. Mitandaoni mada nyingi zinajadiliwa huku watu wakipingana kwa hoja. Hii itahamasisha vijana wengi wenye vipaji vya uongozi na siasa waliokuwa wamekata tamaa kujiingiza kwenye siasa na kusaidia kuondoa viongozi wabovu. Hata hii katiba mpya inayoliliwa na upinzani inaweza kujadiliwa kisomi na muafaka ukapatikana. Vijana wakiamua hakuna wa kupinga. Kiukweli wanaotaka uongozi kwenye uchaguzi wa 2025 wajipange haswa maana kuna sura changa nyingi mno zitajitokeza kwenye udiwani na ubunge.
Mama Samia alishaliona hili ndo maana hata serikali yake ina vijana wengi kwenye ngazi za juu za uongozi. Tanzania kwa sasa ina Spika kijana Mheshimiwa Tulia Ackson, waziri wa fedha kijana Mwigulu, na viongozi vijana wengi sana kama kina Bashe, Polepole, Nikki wa pili, Joketi, Jenista Mhagama, Angela Kairuki, Alexander Mnyeti, Januari Makamba. Kama ilivyokuwa kwa Hichilema wa Zambia hata sisi vijana wa Tanzania tutamchagua kwa kishindo Mama Samia mwaka 2025.