Julius K. Nyerere: Ikulu ni pahali patakatifu, sio pango la wanyang'anyi

Julius K. Nyerere: Ikulu ni pahali patakatifu, sio pango la wanyang'anyi

Nanukuu kauli ya baba wa taifa mwl. Nyerere ya kuwa " ikulu ni mahali patakatifu,mimi sikuchaguliwa na wananchi wa tanzania kuja kupageuza kuwa pango la walanguzi"
Baba wa taifa aliona mbali sana,ikulu si mahali pa kuwaweka watu wanafiki na wababe kama Samwel sitta,fisadi- EL,mtu wa kubebwabebwa-membe,kinyonga Wassira,dhaifu-Pinda na magamba mengine yaliyojipambanu kuitaka ikulu,otherwise ikulu itakuwa ni pango la walanguzi. Hawa hawafai.
Ikulu ni mahali patakatifu.
 
Umenikuna wamepageuza kuwa pango la walanguzi,halafu wanasema bila haya kwamba wao ndio wanafaa kuendelea kuongoza watuambie walikaa wapi na mungu wakaandikiana mkataba wakuongoza tz milele?wamejitoa fahamu natamani niwepo mpaka tar 30/10/2015 mungu ataumba vipya na nchi zitageuka amen.
 
Umenikuna wamepageuza kuwa pango la walanguzi,halafu wanasema bila haya kwamba wao ndio wanafaa kuendelea kuongoza watuambie walikaa wapi na mungu wakaandikiana mkataba wakuongoza tz milele?wamejitoa fahamu natamani niwepo mpaka tar 30/10/2015 mungu ataumba vipya na nchi zitageuka amen.

hawana hatimiliki ya kuitawala nchi hii milele
 
Ndio maana akina Mbowe Ikulu wataisikia tu, Pale sio sehemu yao!
 
Mkuu kuna manabii walikuja wakaondoka mitume pia,sembuse ccm?watashindana lkn hawatashinda.
 
.... Naomba Michango Yenu Ukizingatia Sasa Hivi Hadi Akina Kingwangala, January Na Mwishoni Utawasikia Hadi Akina Chenge Wanatangaza Nia Ya Kwenda Ikulu, Huwa Najiuliza, Hivi Ikulu Kuna Biashara Gani? Sakata La Escrow Na Pembe Za Ndovu Za Rais Wa China Ndo Vimenifumbua Macho Kwamba Inawezekana Ikulu Kuna Biashara Kubwa Sana Hata Za Kuuza Sembe Ndo Maana Watu Wanapigana Vikumbo Hasa Wanaccm.
 
Ikulu ya Tanzania inakuhusu nini wewe fuatilia habari za Ikulu ya Rwanda.
 
Ni masikitiko matupu hapa Tanzania, ni aibu kubwa kwa serikali ya Tanzania na watanzania wote sababu ni sisi wenyewe ndo tuliwachagua. Kama hatutaki jifunza kwa haya yaliyotokea basi tusilaumu mafisadi. Ndiyo, Ikulu ni mahali patakatifu na ndiyo maana tumeweza watambua wezi; hawa jamaa hawakumwelewa Mwalimu J.K Nyerere aliposema Ikulu ni mahali patakatifu. Mwalimu angekuwa fisadi, haya mafisadi wangekuwa salama kwa kuwa muasisi alikuwa fisafi! haita wezekana. Pale ni patakatofu kweli kweli.
 
Suti saa meno ya tembo rushwa ya kuwahonga waandishi waipigie debe takataka lilopendekezwa na CCm
 
Ikulu ya Tanzania inakuhusu nini wewe fuatilia habari za Ikulu ya Rwanda.

hata kama ni wa DRC hazuiliwi kusema ukweli na ana haki hiyo hatakama madhalimu kama nyie mtachukia
 
Ikulu ya Tz ni kupiga pesa vinginginevyo, kama hupigi wewe ni bweges na utalaumiwa siku zote za maisha yako. Hii ndiyo tz bwanaaaaa!
 
Enzi za uhai wake mwalimu Nyerere katika moja ya hotuba zake wakati ameishang`atuka aliwahi kusema kuwa Ikulu ni mahali patakatifu,alikuwa anatoa ushauri kwa waliokuwa Ikulu na wanaotaka kwenda Ikulu akihoji kuna biashara gani Ikulu hadi watu wanatumia pesa kutaka kuingia pale .
Kilichinivutia kujadili ni utakatifu wa Ikulu hasa baada ya juzi kusikia katibu mkuu kiongozi Ombeni sefue akitoa msimamo wa Raisi aliyeko IKulu kuwa atachukua hatua baada ya vyombo vya uchunguzi kuchunguza na kuhakikisha makosa ya watuhumiwa kabla ya kutenda.
TAKUKURU imeishafanya uchunguzi,CAG tayari ameishafanya uchunguzi,na ripoti zao zimejadiliwa na Bunge,nikakumbuka katika moja ya maelezo mengi ya sakata la ESCROW katibu mkuu wa rais Mbena alitoa maelekezo ya kwamba hela zitolewe.
Katibu mkuu wa raisi hawezi agiza kutoa pesa nyingi kiasi hicho bila ruhusa ya bosi wake ambaye ni rais,nchi wahisani zimesitisha misaada hususan ya bajeti ya serikali kufuatia sakata hili.familia ya raisi nayo hapa jamvini imetuhumiwa kuhusika na uchotaji wapesa hizi pia.
Tumeona nchini CHINA mafisadi,wala rushwa wakipewa adhabu kali za vifungo hata kunyongwa kwa makosa kama haya,haishangazi kwa rais kusema hivi kwani anawezaje kumkamata katibu wake kwa kuagiza kutoa maagizo ya kutolewa pesa hizo!
Toka tupate uhuru nchi yetu imeongozwa na maraisi wote kutoka CCM Je ni yupi ambaye anaweza akasimama na kutangaza kwamba mimi niko safi kiasi cha kumkosoa rais aliyeko madarakani pindi akikosea??Ni nani? Walau Nyerere alifanya makosa lakini dhamira yake haikuwa hata mara moja kufisidi,kuiba na kutumia Ikulu kwa manufaa binafsi.Ndiyo maana alikuwa hata na jeuri ya kukemea na kutoa ushauri katika matukio yoyote muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu.
Baada ya yeye nani anaweza akasimama kukemea makosa lukuki yanayofanywa na uongozi wa nchi hii,hakuna kwa sababu hawana usafi huo.
Mwinyi? na azimio lake la Zanzibar? Au Mkapa na ANBEN na mgodi wa Kiwira,Kuuzwa kwa kutupwa kwa NBC?tena kuna mambo mengi labda uandike kitabu, Je huyu aliyekuwepo Ikulu sasa hivi,ni kashfa juu ya kashfa,kwa hawa anaotangaza kila siku kuwa wanamuenzi Nyerere mbona wamekengeuka busara zake?
Sasa hivi wanajipanga CCM kuendelea kuingia Ikulu, kuna mtuhumiwa wa Richmond lakini tukumbuke kuwa Nyerere aliwahi kusema kuwa Mke wa Kaisari hatakiwi kutuhumiwa,huyu ametuhumiwa akajiuzulu basi atuambie nani ni mhusika halisi wa kashfa hii kama si yeye. kuna yule mtetezi MEREMETA ambaye kila mwenye akili anajua kuwa ni wizi lakini yeye alisema hata afanywaje hatosema,kuna yule aliyeteka rasimu maridhawa ya katiba kama ilivyotayarishwa na tume ya raisi iliyoongozwa na jaji Warioba akapitisha rasimu ya kuwatetea wezi ikiandikwa na mtuhumiwa wa pesa za rada,au yule aliyetete kwa nguvu baada ya kuwekwa hadharani mpango wa serikali ya CCM na biashara ya PEMBE za ndovu na rafiki zao wachina ,sijui kwa ahadi ya kujengewa bandari Bagamoyo? jamani IKULU NI MAHALI PATAKATIFU!
CCM wamepageuza IKULU kutoka kuwa mahali patakatifu hadi kuwa PANGO LA WANYANG`ANYI,sehemu ya kupigia dili za kuiba.
Hili nalo watahakikisha linapita pia, mbona mengi yamepita,sakata la jairo ingekuwa China kanyongwa,Seth mwizi wa fedha za watanzania anatamba hana wasi wasi kwa sababu anajua kuwa Kuna pango lao la wanyang`anyi liko Ikulu washirika wake katoka maovu.
Na jinsi watanzania tulivyokuwa tumerogwa tutalipigia jambazi lingine liingie Ikulu la CCM natamani kuhamia mwezini
 
Na mimi nimeisikia leo ITV na imenikumbusha mbali na imenikumbusha mengi maana nilijikuta nikitokwa machozi nilipotafakali na kugundua kuwa sasa ikulu yetu imeshageuzwa ni Pango la wanyang'anyi.
Nyerere alikuwa ni nabii wa nyakati zetu!🙁

Hivi nyinyi mnajua maana ya Nabii kweli! ama kweli ujinga mzigo! na huko kulia ni kujitakia, lilia nafsi yako kijana kuna hukumu kesho sio unalilia Dinia hii yenye kupita!
 
Sikuchaguliwa na wananchi kwenda kuigeuza ikulu kuwa pango la walanguzi.je nani atasimamia kauli ya hayati babu nyerere?kikwete namimi nataka kuja kukusalimia mtani wangu hapo madhabahuni.
 
Sikuchaguliwa na wananchi kwenda kuigeuza ikulu kuwa pango la walanguzi.je nani atasimamia kauli ya hayati babu nyerere?kikwete namimi nataka kuja kukusalimia mtani wangu hapo madhabahuni.

Wewe kilaza hata kuandika hujui!
 
Back
Top Bottom