Juma Nature akataa kushiriki Wasafi Festival kisa malipo kidogo ya laki tano

Juma Nature akataa kushiriki Wasafi Festival kisa malipo kidogo ya laki tano

Dh!
Watoto wa Dotcom Bwana[emoji23][emoji23][emoji23]

Mnasema nature si lolote?[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Bila akina nature kuupambania mziki,usingefika hapo ulipo mlipoukutia nyie.
Nyie acheni kabisa.


Hivi mnaijua hakuna kulala nyie?
Hapo sijaweka mapanga ya mgambo.


Sema siyo kosa lenu,ni kwamba mmezaliwa mwaka 2000 2005 nature anatrend,nyie Bado vichanga mnanyonya maziwa,hamuelewi chochote wakati huo na hamuujui mziki.
Na ni makosa yenu kutokufuatilia.
Kwa Sasa necha hana soko Ndio Maana Ngoma zake za sasa haziihit mngekuwa ni wapenzi wa kweli wa mziki wake ungemsaidia kununua Ngoma zake na kuuzulia kwenye show zake
 
Hawawezi kumtangaza bila kukubaliana dau , kuna shida mahala na wala sio hyo 500K
Shida wasanii wanachukuliana poa,
Usikute walimtangaza bila makubaliano, niliwahi kusikia jux akimlalamikia harmonize kuwa kasema atakuwepo kwenye show, wakati yeye harmonize hajaongea chochote na jux.
Na ben paul pia alilalamika juu ya harmonize.
Ikaja baadae kuna msanii akimlalamikia jux kwa kitu kama hicho.
 
Nyie vitoto vya 2000 ulizeni kwanini juma huwa anawekwa wa mwisho ktk show? kuuliza sio ujinga
Kwenye malipo ya show wanaangalia jina kwanza ndio inadetermine value yako sio performance unayoenda kufanya ndio maana Kiba analipwa vizuri kwenye show kuliko Sir nature lakini kwenye performance nature amempita sana Kiba
 
Kwenye malipo ya show wanaangalia jina kwanza ndio inadetermine value yako sio performance unayoenda kufanya ndio maana Kiba analipwa vizuri kwenye show kuliko Sir nature lakini kwenye performance nature amempita sana Kiba
Umewahi kuhudhuria japo show mbili za juma. Kama umewahi utaelewa kwanini inakuwaga hivyo. Kama hujawahi huwezi kuelewa. Bye utanikausha koo bure.
 
Hawa watoto wanadhani Sir Nature ni boya flan hivi asiyejitambua kama wakina Chidy ndio maana wanaona laki 5 inamfaa wakati mwenzao laki 5 anaingiza ndani ya dakika kadhaa akiwa chini ya mti anakula zake kuberi au anatafuna gomba, [emoji38]

Ni sawa na sasa hivi umuite komando Jide eti apande kwenye tamasha lako umpe laki 5 kisa ni wa zamani, wakati wasanii wa siku hizi wanaringishiana Range, Komando alishaanza kuiendesha mapema kabisa miaka ya 2000,

Au umuite mtu kama Jay Moe useme unampa laki 5 kisa wa zamani, hahahaha wana utani wa ngumi.
Jay mo huwezi kumfananisha na nature hata kidogo kwasababu Jay mo anahit mpaka kwenye kizazi hichi nature soko lake lilikuwa zamani Ndio Maana latest song zake hazifanyi vizuri kwenye kizazi hichi .Waandaaji wanakuvalue kulingana na jina ulilonalo recently sio unaenda kuperform vipi jukwaani Ndio Maana Marioo huwezi kufanana kimalipo na nature Marioo lazima hela yake itakuwa ni kubwa zaidi ya nature
 
Diamond anamjua Nature vizuri. Nature mtoto wa kihuni toka Temeke kwahio masela lazma wawe shazi. Muziki wake unaakisi maisha halisi huwezi kufananisha na miziki ya Big G ya akina Mondi.
Ndio Maana diamond anapesa nyingi kuliko hata huyo asiyefanya mziki wa big G uoni huo utofauti
 
Nature hana njaa na wala dhiki amechagua kuishi maisha ya nje ya umaarufu, kipesa yupo vyema alishajipata muda sana. Ndiyo maana kila ikitajwa orodha ya wanamuziki wenye utajiri, kumi bora hakosekani na hapo hayupo active. Hiyo pesa ni dharau kwake, yaani akache miradi yake uende kumlipa kiasi hicho.

Mtu kuamua kuishi maisha yaleyale aliyokulia hata baada ya kufanikiwa, haimaanishi ni ana dhiki. Ile ndiyo staili yake hata alipokuwa akishika chat zote aliishi vilevile alivyo hivi sasa. Hawezi kukubali umpe hela anayoitoa kwenye mfuko wake wa shati.

Hiyo show mnasema analipiwa usafiri, chakula na malazi. Hayo mambo hawafanyi wasafi mpaka mseme wanataka kurudisha, wanafanya wadhamini wa show ile
Kwahiyo kwenye matajiri 10 naye yumo? Hizi story sijui mnaziokotaga wapi dah
 
Ndio Maana diamond anapesa nyingi kuliko hata huyo asiyefanya mziki wa big G uoni huo utofauti
Kipindi cha kina Juma Nature hakukuwa na mitandao. Connection za hela zilitegemea ma promoter na baraka za Clouds fm. Bila hivyo huuzi show kwahio wamepitia ugumu kuliko hao kina Mondi.

Halafu Nature hayuko kwenye maagano ya kishirikina kama huyo Domo unaemsifia.
 
Hii analysis ingekuwa sahihi endapo tu, tungekuwa tunazungumzia Twanga pepeta.
Na sio juma nature.
Tuchulie wahudhuriaji wa show ni kuanzia miaka 30 mpaka 23.
Wengi hapo wakati nature yupo kwenye peak walikuwa wanajitambua kuweza kujua mziki mzuri au mbaya.
Huwezi niambia mtoto wa miaka 5 mpaka 12 alikuwa hajitambui.
Hii sio show ya watu wenye akili sana kwamba watatumia heshima na kumbukumbu kuliko trend, mtu wa kawaida, muuza chips au bodaboda wa Morogoro mwenye miaka 24 unatarajia akiwekwa Jux hapo na akawekwa Juma Nature ataenda wapi?

Nature ana tracks kadhaa miaka hii mitano iliyopita, kuna ngoma yeyote ina viewers hata 200k YouTube? Wakati huo hayupo streaming platforms sasa mashabiki zake wengi wanamsikiliza kupitia wapi? Muda huo tulinganishe na ngoma za wabana pua wanaotrend hawakosi viewers za millions. Sasa kama unaandaa show ya rika hili la kurushiana vumbi unafanyaje hapo. Ushahidi wa kwamba Nature anauza unaupata wapi, unabaki na ushahidi kwamba aliwahi uza na ana fanbase yake ambayo sio hii ya Fiesta au Wasafi Festival.
 
Hizi nchi maskini ni tabu kwa kwenda mbele, najaribu tu kuwaza catalogue ya Sir Nature, kuanzia nyimbo zake, nyimbo za kundi mpka zile za kushirikishwa!

Kwa nchi kama US ilibidi awe anakula tu maokoto ya digital platforms na angekuwa tajiri bila hata hizo shows.
Sasa kwa mfano ukienda spotify nyimbo zake hata 10 hazifiki, na sina hakika kama acc ni yake kweli.

Hapa kwetu hata museum ya tu ya kumbukumbu ya Bongo fleva ilikotoka hakuna, hizi nyimbo unakuta hata wasanii wenyewe hawana, kwahiyo dharau za kulipana laki 5 lazima ziwepo.

Ifike muda tuupe thamani muziki wetu, Sugu ameonesha njia na Bongo Flava Honors japo katuwekea stage ya hovyo sana hata stage ya bar ina afadhali.

Hata tukiamua kutenga mji mmoja uwe ndo kitovu cha Bongo Fleva inawezekana, Leo hii ukienda Nashville, Tennessee kuna kumbukumbu zote za muziki wa country, producers, song writers na record label za Country zipo Nashville na wameupa heshima kubwa muziki wao.
mtaaram unaongea pwent sana.sema kunipqngishq ile salun miez 6 ya mqjaljbio ya biashara ndio umekataa mkuu
 
Hapana wengi ni watu wazima sema wametokea sigimbi kipindi nature anavuma wao hata redio walikuwa hawana
[/QUOT

Sawa ila Nature soko hana tena, afanye show yake tuone, labda Dar kwa watu wake Temeke.😄😄😄

Akipiga mikoani watu watashangaa haka kazee kametokea wapi😂😂😂
 
Kwa majukwaani bado sir nature ana uwezo wa hali ya juu mno ambao haujafikiwa na msanii yoyote yule.

Nature ni legend ila kiwango kikubwa cha hadhira ya sasa sokoni hakimpi nafasi ya kuwa na thamani hiyo mnayojaribu kumpa.

Huu ni ukweli wa kibiashara, kama tutaamua kuweka mapenzi na hisia pembeni.
 
Juma nature na watu kama kina inspector kwa mtu wa kale kama mimi tunaweza mtazama na kumlipa akiitisha shoo sababu nyimbo kama ugali, mzee wa busara tulizisikiliza sema ndo hivyo kuna umri huwezi fikiria matamasha na disko.
 
Back
Top Bottom