JWTZ ifanye uchunguzi dhidi ya tabia na mwenendo wa askari wake Denis Urio

JWTZ ifanye uchunguzi dhidi ya tabia na mwenendo wa askari wake Denis Urio

Kuipata haki hapa Duniani ni ngumu sana, kitu kimoja naamini ni kwamba Mungu yupo, anaona, anasikia na anajibu, nani alijua kwamba yule Bwana fulani angeondika mapema tena hata bila kukamilisha mipango yake, Mbowe atulie, akubali matokeo yatakayokuja, awe na imani Mungu yupo na wenye haki wanamuombea.
Hiyo ni fursa kwa Mbowe.
Nimejifunza kuna wakati Mungu huruhusu mabaya yakukute ili Ajitukuze kwako.
Naifurahia sana amani ya Mbowe, haonyeshi kujuta, amejaa tabasamu.
Hakika atashinda.
Ushindi mwindi mwingine hukamilishwa na vifungo, vipigo na maonevu.
Yakamilikapo mateso ndipo Shujaa na Mzee wa siku hushuka na kuishangaza dunia.
Yeye hajawahi shindwa.
Huujua mwisho kabla ya mwisho.
 
ukisikia kitu kinaitwa " Proof beyond reasonable doubt - uthibitisho usioacha shaka"haitegemei shahidi mmoja, wakati mwingine huwa unategemea circumstantial evidence ambayo ili uthibitishe unatakiwa uwe na ushahidi wa matukio yasiyokatika kwenye mnyororo wake.....hivyo kila shahidi anakuwa na kakitu kake anakuja kuthibitisha anaondoa,ninyi mtahangaika kupuyanga kwenye cross examination kuuliza maswali ya kufurahisha umma kumbe wenzenu kile walichomleta aje kuthibitisha sicho kile mnachokishambulia. ndilo linalotokea hapo kwenye kesi, hadi nawaonea huruma hao mawakili wa mbowe. hawaelewi kitu, ila wanajua kuufurahisha umma ambao hawa haujui mambo ya kisheria zaidi ya ushabiki wa kisiasa.

Sisi sio wanasheria ila tuna logic. Hayo ya kujifanya kuna mbinu za kisheria mnazibeba nyinyi mliotunga hii kesi. Hata kama mkimlazimisha jaji huyu kuwafichia aibu, bado kwenye mahakama ya rufaa itakuwa ni dakika chache tu ukweli wote utawekwa wazi.
 
Hii kesi inayoendelea mahakamani imeufungua macho umma wa Watanzania juu ya tabia ya askari huyo.

Aina ya Ushahidi ambao komando Urio ameutoa mahakamani umeacha maswali mengi sana ya umma juu ya tabia ya askari huyu lakini pia hata kuathiri taswira ya jeshi mbele ya umma.

Kuna haya mambo yafuatayo:
1. Je, jeshi lina taarifa za askari wake Denis Urio kumtafutia Mbowe walinzi ambao yeye Urio anasema walipanga kufanya uhaini? Hata hivyo mahakamani Urio kasema hakuripoti Jeshini bali karipoti kwrnye mamlaka ya kipolisi. Je, hivi ndivyo askari wa JWTZ anavyopaswa kufanya pindi anapopata taarifa za uhaini?

2. Ushahidi wa Urio una matobo mengi, kuna kila sababu ya kudhani kuwa Urio anatoa ushahidi wa uwongo ili kuwaumiza raia wasio na hatia–Hapa JWTZ haina budi kufanya uchunguzi binafsi na kujiridhisha juu ya mwenendo na tabia za askari wake huyu Denis Urio

3. Mbele ya jamii ni vigumu kwa JWTZ kujiweka pembeni katika hii kesi kwa sababu, wananchi wanapata taswira mbaya kuwa JW inatumika kisiasa kuumiza wapinzani. Kwa hiyo ipo haja kwa JWTZ kujisafisha dhidi ya tabia na mwenendo wa Denis Urio kama ulivyothibitika katika ushahidi anaoutoa mahakamani.

He is just a victim Kama wenzake in a different side...
 
Hii kesi inayoendelea mahakamani imeufungua macho umma wa Watanzania juu ya tabia ya askari huyo.

Aina ya Ushahidi ambao komando Urio ameutoa mahakamani umeacha maswali mengi sana ya umma juu ya tabia ya askari huyu lakini pia hata kuathiri taswira ya jeshi mbele ya umma.

Kuna haya mambo yafuatayo:
1. Je, jeshi lina taarifa za askari wake Denis Urio kumtafutia Mbowe walinzi ambao yeye Urio anasema walipanga kufanya uhaini? Hata hivyo mahakamani Urio kasema hakuripoti Jeshini bali karipoti kwrnye mamlaka ya kipolisi. Je, hivi ndivyo askari wa JWTZ anavyopaswa kufanya pindi anapopata taarifa za uhaini?

2. Ushahidi wa Urio una matobo mengi, kuna kila sababu ya kudhani kuwa Urio anatoa ushahidi wa uwongo ili kuwaumiza raia wasio na hatia–Hapa JWTZ haina budi kufanya uchunguzi binafsi na kujiridhisha juu ya mwenendo na tabia za askari wake huyu Denis Urio

3. Mbele ya jamii ni vigumu kwa JWTZ kujiweka pembeni katika hii kesi kwa sababu, wananchi wanapata taswira mbaya kuwa JW inatumika kisiasa kuumiza wapinzani. Kwa hiyo ipo haja kwa JWTZ kujisafisha dhidi ya tabia na mwenendo wa Denis Urio kama ulivyothibitika katika ushahidi anaoutoa mahakamani.
Mpaka bapa ilipofika ni kuwa Urio anaelekea kupoteza kazi yake. Hakuna namna ambavyo jeshi linaweza kumuaxha salama. Huyu ameshajiharibia.
 
Chadema mnajitahidi sana kupotosha ili gaidi asifungwe lakini hamtafanikiwa.

Denis Urio alipewa ruhusa na DCI aendelee kusbirikiana na Mbowe ili mradi tu awe anatoa taarifa ya kila kitu kinachoendelea.
Personally, Urio na DCI wamewasababishia sana mateso wenzake(makomandoo), hii dhambi haitawaacha salama Daima.

Ivi ilihitaji kuendelea kutafuta watu wa kuwatesa ili wamuwajibishe Mbowe! Kweli?
 
Mpaka bapa ilipofika ni kuwa Urio anaelekea kupoteza kazi yake. Hakuna namna ambavyo jeshi linaweza kumuaxha salama. Huyu ameshajiharibia.
Hii ni Tanzania baba usijekushangaa flani anaagiza apandishwe cheo.
 
Ukute baba yake denis ndiyo baba yake mbowe yaani baba wa taifa
 
He is just a victim Kama wenzake in a different side...
How bro?
Unataka kusema DCI alimlazimisha kula njama baada ya kugundua ana ukaribu na Mbowe?
Kama alilazimishwa, je aliripoti jeshini kwa wakubwa zake?
Kwangu mimi bora uniue kuliko kunilaximisha nimsingizie mtu mwingine.
Na tena ningeusema ukweli wote mahakamani ilovyokuwa regardless yatakayonipata.
Hakuna kitu kibaya kama kuhukumiwa na mahakama ya moyo wako...utakufa kwa sonono.
 
Hyo una sema wewe
Ila ndo tayari imeshatokea amekwenda moja kwa moja kwa DCI..ishu ya msingi nu kujua Kama mbowe anafahamiana na kamanda urio,na Kama walikuwa wanakaa vikao,kupigiana simu,chats na miamala ya simu.
Zaidi ya hapo tukubali tu mwenyekiti alikosea sehemu.
Una matatizo kichwani mwako,issue hapa ni responsibility iliyopo kwa taasisi hizi kufanya kazi zake kwa mujibu wa kisheria,urio ni mwajiriwa wa tpdf ilikua ni wajibu wake kuwasiliana na MI na SIO DCI.Mh.Mbowe issue yake itaamuliwa na judge anayesikiliza case yake,sio wewe ambaye tayari una uamuzi wa Mh.Mbowe eti kakosea,middle class wewe ni sehemu ya tatizo kubwa ambao Tanzania inakabiliana nalo,elimu mbovu matokeo ya shule za ajabu na mfumo ovyo wa kielimu.
 
ukisikia kitu kinaitwa " Proof beyond reasonable doubt - uthibitisho usioacha shaka"haitegemei shahidi mmoja, wakati mwingine huwa unategemea circumstantial evidence ambayo ili uthibitishe unatakiwa uwe na ushahidi wa matukio yasiyokatika kwenye mnyororo wake.....hivyo kila shahidi anakuwa na kakitu kake anakuja kuthibitisha anaondoa,ninyi mtahangaika kupuyanga kwenye cross examination kuuliza maswali ya kufurahisha umma kumbe wenzenu kile walichomleta aje kuthibitisha sicho kile mnachokishambulia. ndilo linalotokea hapo kwenye kesi, hadi nawaonea huruma hao mawakili wa mbowe. hawaelewi kitu, ila wanajua kuufurahisha umma ambao hawa haujui mambo ya kisheria zaidi ya ushabiki wa kisiasa.
Shahidi wenu muhimu ni huyu urio na huyu anapuyanga tu hana lolote analolijua sasa nenda na wewe ukapeleke uthibitisho urio hana
 
Una matatizo kichwani mwako,issue hapa ni responsibility iliyopo kwa taasisi hizi kufanya kazi zake kwa mujibu wa kisheria,urio ni mwajiriwa wa tpdf ilikua ni wajibu wake kuwasiliana na MI na SIO DCI.Mh.Mbowe issue yake itaamuliwa na judge anayesikiliza case yake,sio wewe ambaye tayari una uamuzi wa Mh.Mbowe eti kakosea,middle class wewe ni sehemu ya tatizo kubwa ambao Tanzania inakabiliana nalo,elimu mbovu matokeo ya shule za ajabu na mfumo ovyo wa kielimu.
Mfafanulie hiyo MI kuwa ni Military intelligence huyo kilazzer
 
Sasa hayo unasema wewe.
Nenda wewe Basi kawasiliane na MI.
Hamjiulizi chat,calls,na miamala ya fedha viliingia vipi kwenye simu ya kamanda urio?

Kesi ya msingi ndo ipo hapo.
Sio wapi alikwenda kutoa taarifa.
Mkishajua hivyo vitu vimetendeka vipi ndio mtajua ukweli Kama mbowe alihusika kupanga hyo mipango au ametengenezewa.
Kwa hyo ishu sio kamanda urio amekwenda kuripoti wapi.
Ishu ni kweli mbowe alimtafuta urio? alikuwa anampigia simu?alikuwa anachat naye?
Akipanga mipango yoyotte na urio?
Kesi ya msingi ndipo IPO hapo mtaelimika lini nyie?
Una matatizo kichwani mwako,issue hapa ni responsibility iliyopo kwa taasisi hizi kufanya kazi zake kwa mujibu wa kisheria,urio ni mwajiriwa wa tpdf ilikua ni wajibu wake kuwasiliana na MI na SIO DCI.Mh.Mbowe issue yake itaamuliwa na judge anayesikiliza case yake,sio wewe ambaye tayari una uamuzi wa Mh.Mbowe eti kakosea,middle class wewe ni sehemu ya tatizo kubwa ambao Tanzania inakabiliana nalo,elimu mbovu matokeo ya shule za ajabu na mfumo ovyo wa kielimu.
 
Mfafanulie hiyo MI kuwa ni Military intelligence huyo kilazzer
Na hiyo ndio inayokusanya zote kutoka URAIANI, nje ya mipaka na ndani ya mipaka. Na ndio unafanya situation analysis ya kuamua wafanye nini
 
Naona hamjaelewa,,, Urio kwa mujibu wa ushahidi wake, HAKUTAKA KUFANYA KAZI NA MBOWE, tangu 2008 mbowe ndo anamtafuta urio kumuweka sawa
Urio kapewa go ahead na DCI , kuendelea na hiyo ishu kama njia ya kumnasa mhalifu,,
Hiyo hapa kwetu Lubumbashi, inaitwanga, STING OPERATION,
kama hii ishu ni kweli, itakuwa walibugi kwenye kukamata haraka kabla ndege hajaingia tunduni,,
Kimsingi hapo sioni kesi
Hili jambo limeshughulikiwa na watu wajinga sana.
Kama Mbowe alikuwa na mipango hiyo, wangeendelea kufuatilia mpaka upatikane ushahidi wa kutosha. Wakikosa waliache kimya kimya.
Pia wangeendelea kutafuta watu wenye akili wafuatilie.
 
How bro?
Unataka kusema DCI alimlazimisha kula njama baada ya kugundua ana ukaribu na Mbowe?
Kama alilazimishwa, je aliripoti jeshini kwa wakubwa zake?
Kwangu mimi bora uniue kuliko kunilaximisha nimsingizie mtu mwingine.
Na tena ningeusema ukweli wote mahakamani ilovyokuwa regardless yatakayonipata.
Hakuna kitu kibaya kama kuhukumiwa na mahakama ya moyo wako...utakufa kwa sonono.

Usiongee tu kirahisi, haijalishi Ni jeshi gani, we have the same president and one political part "Ccm" Huyu Ni victim tu! Ni WA kuombea wala sio kusimangwa!
 
Shida mnakuja hapa na kujifanya mnajua kumbe wasindikizaji tu. unafikiri kweli jeshi halina taarifa za kutosha na mtu wao hadi anakuja kutoa ushahidi? pia, tuchukulie mfano, Mbowe ambaye alikuwa anamwita urio "homeboy", ameamua kuingia kwake ili amtafutie walinzi na akaamua kumshirikisha huyo homeboy wake uovu anaotaka kuufanya akijua kwamba urio hatamsaliti kwasababu wametoka mbali na ni homeboy, urio akafikisha taarifa ile kwa wakubwa zake, lazima wakubwa zake watamwelekeza akende polisi, na akifika polisi lazima tu watamwambia "ili tumpate mbowe na uovu anaouwaza, jifanye kushirikiana naye".

Hapo watashirikiana hadi kuwapata hao walinzi na mambo yote yaliyoendelea mbowe akiamini kuwa urio yupo upande wake kumbe mwenzake ameshakuwa pandikizi. kumbuka kuwa hayo mambo ua uovu lazima yalikuwepo kitambo na serikali ilikuwa inatafuta namna ya kureveal kupata ushahidi. mbowe akaingia king...na ndio yupo hapo anashangaashangaa tu anatokaje, anasubiri tu huruma za wananchi na serikali. ukweli halisi anaujua mbowe, na Mungu anamuona.
Tatizo linaloonekana wanakosa huo ushahidi. Labda wamewahi kabla ya kupata ushahidi wa kutosha au wameutafuta kijinga.
 
Hii kesi inayoendelea mahakamani imeufungua macho umma wa Watanzania juu ya tabia ya askari huyo.

Aina ya Ushahidi ambao komando Urio ameutoa mahakamani umeacha maswali mengi sana ya umma juu ya tabia ya askari huyu lakini pia hata kuathiri taswira ya jeshi mbele ya umma.

Kuna haya mambo yafuatayo:
1. Je, jeshi lina taarifa za askari wake Denis Urio kumtafutia Mbowe walinzi ambao yeye Urio anasema walipanga kufanya uhaini? Hata hivyo mahakamani Urio kasema hakuripoti Jeshini bali karipoti kwrnye mamlaka ya kipolisi. Je, hivi ndivyo askari wa JWTZ anavyopaswa kufanya pindi anapopata taarifa za uhaini?

2. Ushahidi wa Urio una matobo mengi, kuna kila sababu ya kudhani kuwa Urio anatoa ushahidi wa uwongo ili kuwaumiza raia wasio na hatia–Hapa JWTZ haina budi kufanya uchunguzi binafsi na kujiridhisha juu ya mwenendo na tabia za askari wake huyu Denis Urio

3. Mbele ya jamii ni vigumu kwa JWTZ kujiweka pembeni katika hii kesi kwa sababu, wananchi wanapata taswira mbaya kuwa JW inatumika kisiasa kuumiza wapinzani. Kwa hiyo ipo haja kwa JWTZ kujisafisha dhidi ya tabia na mwenendo wa Denis Urio kama ulivyothibitika katika ushahidi anaoutoa mahakamani.

Ndugu Missile of the Nation zipo undoubtful facts kadhaa zimefunuliwa na kesi hii;

1. Kuna uwezekano wa 99% huyu Denis Urio si askari wa JW bali alipandikizwa huko na kupachikwa uaskari wa JW na cheo just for a special mission huku CDF Mabeyo akiwa anafahamu fika au akiwa hafahamu kabisa kinachofanyika...

USHAHIDI:

Haya yanathibitishwa na circumstantial evidence inayomzunguka huyu shahidi, mathalani;

å Elimu ya huyu bwana kwa maelezo yake ni sekondari K.4 Haiwezekani mtu mwenye elimu level hii apate cheo cha "u - luteni" hata kama atakuwa mwanajeshi miaka 30 unless afanye K.6 kisha apate ingalau shahada ya chuo kikuu...

å Kama nilivyosema, alikuwa kule kwa kazi maalumu. Haijui basics za kawaida kabisa za kijeshi. Kaifanya hiyo kazi, kaimaliza lakini in a awful and very disgraceful end....

Hata alipokuja mahamakani kutoa huo ushahidi wake, hakutokea na hayupo kazini kitambo tu. Ametokea mafichoni...!!

2. Taasisi zetu (Executive, Judiciary & Parliament) by in large ndizo zimekuwa chanzo cha maovu ktk taifa letu. Yaani ile hali ya lawlessness katika nchi yetu inaanzia juu kwa wenye mamlaka ya kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kuja chini kwa raia Wa kawaida....

Kaatika mazingira tunadhani nini kitatokea huko mbeleni? Honestly, yeyote anaweza kuwa na correct prediction, kuwa tusipobadili hàli peacefully sasa kwaa kusema enough is enough, basi tutakuja kuibadilisha kwa kuamuliwa na wengine...!

Kwa mfano, katika sçenario hii ya mwanajeshi Denis Leo Urio, hebu tujaribu tu kufikiri hili...

Kwamba, iweje mwanajeshi mwenye mafunzo ya kulinda usalama na mipaka ya nchi anavuka mipaka ya majukumu yake na kuanza kushiriki uovu wa kuhujumu haki za raia wa kawaida huku vyombo vyenye mamlaka vikiangalia tu uchafu huu..?

Nani amchunguze nañi sasa kwa sababu the whole system is corrupted..?
Hawatafanya lolote kwa sababu inawezekana pia askari wao huyu ametumwa na JW kufanya aliyofanya. Kila taasisi imepangwa kutoa ushahidi wa uongo kwenye hii kesi.

Ni aibu sana jeshi kujiingiza kwenye hili.
 
Back
Top Bottom