JWTZ kuwatesa raia wanaovaa nguo za Jeshi ni ukatili

Wakati mwingine inashangaza sana. Hivi najiuliza nguo ya jeshi si mali ya jeshi? kwa hiyo raia nguo hizo wanazitoaga wapi?! Maana kama jeshi linafikia hatua ya kupiga marufuku uvaaji wa nguo zao basi kumbe inafikirisha kwamba wananchi wanaziiba huko jeshini?

Na kama zinaibiwa huko kisha kuja kuvaliwa mitaani basi kutakuwa na tatizo hapo. Lakini pia nimejiuliza ,hivi hapa Tanzania kuna raia anatengeneza hizo nguo?

Kama yupo maana yake akamatwe kisha achukuliwe hatua stahiki. Lakini kama raia wanakutwa na nguo zenye kufanana na za jeshi na ndio hao wanachezea kichapo basi pia tuipe lawama serikari kwa mifumo mibovu ya ku import bidhaa za madukani bila kujali kuwa wao wenyewe ndio tatizo maana wananchi wananunua madukani ambapo serikali imewakata kodi wafanya biashara.
 
Nguo zao washasema hawataki zivaliwe mitaani na Raia.
Mleta mada kwanini usiwashitaki kama huyo jamaa kaonewa?
 
Kumbuka mtoa uzi ni kosa kuvaa au kukutwa na ya jeshi polis, na majeshi mengine ni kosa ustahili Kama ufanya kazi kwenye majeshi hayo
 
Alisema eti "the head is empty and the land is mine...." [emoji1787][emoji1787]

Tuheshimu taratibu za taasisi za wengine....

Haina haja ya kuvaa hizo nguo zao...kwani usipovaa utapungukiwa na nini ?!!!

Watu wenyewe ndio hao..
ndio hivyo tena.....[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Jeshi letu lingeongeza ubunifu kidogo, lingebuni 'sare za jeshi' zinazoruhusiwa kuvaliwa na raia likaziuza kama jezi za Yanga na Simba.
Ukosefu wa ubunifu ndio uliua viwanda kama Urafiki, Sunguratex, Mwatex, Mbeya tex, Musoma tex, Morogoro Canvas nk.
[emoji1787][emoji1787]
 
Kuna wajinga wajinga watasapoti kwa kusema ni kosa kuvaa nguo ya jeshi bila kujali sheria inatamka adhabu gani ukiivaa hiyo nguo na endapo adhabu ya huyo kijana ipo kisheria.
 
hzo nguo hazina tofauti na sanda ukiondoa hayo mabaka mabaka.hazina uspecial wanaozipa wao kiasi cha kuona anayevaa kama sio wao basi ni muhalifu.
 
Sahihi sana mkuu, vita kuu ya pili ya dunia boats za raia zaidi ya 850 zilikwenda kuokoa askari wa Uingereza na allies ambao tayari walikuwa wamezungukwa,
Zaidi ya skari 336,000 waliokolewa, Operation Dynamo, inaitwa Miracle of Dunkirk, yalikuwa ni maajabu, jeshi la Hitler tayari lilikuwa karibu kuwamaliza askari hao na hawakuwa na mahala pakutokea, lakini kwa upendo wa wananchi waliamua kujitolea kwenda kuwakomboa askari hao, hata hivyo jeshi la Hitler lilijitahidi kuzuia uokozi huo lakini ndio hivyo kwa moyo waliokuwa nao wananchi wakashirikiana na jeshi hatimaye wakafanikisha operation hio ambayo haiwezi kusahaulika Miracle of Dunkirk.
 
hzo nguo hazina tofauti na sanda ukiondoa hayo mabaka mabaka.hazina uspecial wanaozipa wao kiasi cha kuona anayevaa kama sio wao basi ni muhalifu.
Yeah. They need to produce armature combat, T-shirts, shorts, bags etc to sell to the general public.
This is a big industry that can earn the army millions of money per year... Sasa wao wamekazana kulima makabeji 🤣🤣🤣na ma spinachi 🤣🤣🤣,
wakati pesa (maokoto) iko nje nje kwenye jezi.
 
Mwanakulitafuta mwanakulipata,Iko wazi sawa si vizuri Kwa wanajeshi kujichukulia sheria mkononi Kwa watu wanaokutwa na sare zao lakini upande mwingine ni nzuri Kwa ajili ya kuonya ,Kwa sababu hizo sare mara nyingine hutumiwa na watu wenye nia ovu kufanya vitu vya kiovu na inakuwa ngumu kugundua kama ni wanajeshi ama la pindi wanapopiga tukio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…