JWTZ, tulindieni heshima yetu yalindeni maslahi yetu DRC-Congo

JWTZ, tulindieni heshima yetu yalindeni maslahi yetu DRC-Congo

Naunga mkono hoja,inabidi tushirikiane na Congo kulinda amani ndani ya congo.Pia sisi Tz tuchangamkie fursa zilizopo Congo siyo wajinga wanatoka mbali kuja kuiba Congo.
Biashara na Congo ni muhimu Sana ukitoa mbali usafirishaji na bandari pia Congo wanahitaji Sana vyakula kutoka Tanzania kama mshirika muhimu lazima tufamye Jambo kumnusuru
 
Wakongo waweke mzigo mezani au watupe mgodi mmoja wakati wanajeshi wetu wanasaidia, wengine wanachimba madini na ya kuyarudisha home..!!

Miaka hii hakuna cha bure, enzi za mwalimu zilishapita..!! Ss hivi kila mtu ashinde mechi zake.!!
 
Ombi lako umelipeleka mahali sipo, Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuamua hilo.
 
Nyerere alikuwa mjinga.

Hakuangalia maslahi ya Tanzania kwenye negotiations zake na nchi husika.

A way foward now ni kufanya haya kwa kuzingatia maslahi yetu ya kiuchumi.
Unadiriki jumuiya NYERERE mjinga???
 
Kiswahili chenyewe tu hujui eti "shida yeyote"cha ajabu una mpaka ujasiri wa kumuona mwalimu JK Nyerere alikuwa mjinnga...

yale yale ya MPUMBAVU kujiona yeye ni MWEREVU saaana na wengine wote wajinga tu
Kumuona nyerere mjinga sio upumbavu. Wewe muone mwerevu mimi namuona mjinga. Ndo uhuru wa mawazo huo
 
Afande G. Mkunda

Ni muda wako wa kulinda historia na heshima ya muda mrefu iliyowekwa na watangulizi wako

Yanayoendelea DRC hatuwezi kuyaacha yaendelee, Sisi kama MABABU wa ulinzi na ukombozi katika ukanda wa east na south Africa ni fedheha kuona mgogoro huu unaendelea na Sisi tumekaa tuu bila kuchukua hatua.

Pamoja na madhaifu mengi ya jeshi la Congo, inahitaji hatua ya dharura kuokoa maisha ya watu wanaokufa bila hatia na safari hii tuende kimkakati zaidi

1. Kuwe na Mkataba wa muda mrefu wa ulinzi eneo lote lenye mgogoro -kivu, goma nk liwe chini ya ulinzi wa majeshi ya Tanzania Kwa makubaliano maalumu.

2. JWTZ iweke military base katika maeneo hayo.

3. JWTZ ifanye kandarasi ya Ku reshape jeshi la Congo ili Kuwa stabilize jeshi la Congo.

Endapo makubaliano hayo yatafikiwa basi Afande utakua umeweka historia na kudumisha yaliyofanywa na G.

Mwamunyange, akisaidiwa na Wazee wa kazi chafu B.G Mwakibolwa na Lt.G Mella

Licha za faida kiuchumi tutakazopata bado tunahitaji heshima yetu, wananchi wa Congo wanaimani kuwa JWTZ itawakomboa kutoka mkononi wa waasi.

Afande ni muda wako wa kulinda heshima na maslahi ya Tanzania DRC
Wapigwe tu hakuna namna nyingine.
 
Kwa moto wa M23 Wakienda kichwakichwa utaskia nao wamekimbilia Rwanda kuomba msaada utawaona kupitia BBC wanasachiwa ili wapokelewe
 
Enzi za kusaidia watu wengine for free nadhani tumwachie Hayati Nyerere.
Kwa sasa kwa sababu tulishaona jinsi tulivyocheleweshwa sababu ya vita ya ukombozi wa ndugu zetu wa kusini mwa Afrika, ni wakati wa kuingia makubaliano maalum na serikali ya DRC, tuwasaidie lakini watupe raslimali za kuendeleza nchi yetu pia kama malipo ya kazi ya kuwasaidia kiulinzi.
Haiwezekani Tanzania iendelee kuwa chini tu siku zote kwa sababu ya usamaria wema!
Safi sana, naungana nawe.
Mnapigania wengine wakati nchi yao ina raslimali kibao wezeshi wanazoweza kuzitumia kujikomboa.
Vita za aina hiyo lazima tulipane, yaani nipe hiki na kile ili nikusaidie, huwezi pambana mwenyewe.
 
Kwa moto wa M23 Wakienda kichwakichwa utaskia nao wamekimbilia Rwanda kuomba msaada utawaona kupitia BBC wanasachiwa ili wapokelewe
Unawajua JWTZ ww au unasikia barabarani ..?
 
Safi sana, naungana nawe.
Mnapigania wengine wakati nchi yao ina raslimali kibao wezeshi wanazoweza kuzitumia kujikomboa.
Vita za aina hiyo lazima tulipane, yaani nipe hiki na kile ili nikusaidie, huwezi pambana mwenyewe.
Ni sahihi watupe goma tuwalinde hata miaka 10
 
Safi sana, naungana nawe.
Mnapigania wengine wakati nchi yao ina raslimali kibao wezeshi wanazoweza kuzitumia kujikomboa.
Vita za aina hiyo lazima tulipane, yaani nipe hiki na kile ili nikusaidie, huwezi pambana mwenyewe.
Kweli kabisa,, huwa wanasahau hawa shida zao zikiisha.
Si unakumbuka Msumbiji na South Afrika walivyowafukuza Watanzania waliokuwa wanakaa huko hapo katikati (nakumbuka ilikuwa kwenye utawala wa Hayati JPM kama sikosei).
 
Na wengi tuliowasaidia hawajui wala kukumbuka mchango wetu wao wanawajua Nkrumah na Mandela tu although they did absolutely nothing for them.

Mubage aliandika kitabu akakiita Asante Mwalimu - The unsung hero of Africa. Mchango wa mwalimu unasahaulika pamoja na kujitolea kote. Hatutaki kurudi huko.

View attachment 3217662
Kweli Mkuu, sisi weusi hatunaga shukurani, bora kama tumeamua kusaidiana basi tusaidiane kwa hali na mali, nipe nikupe.
Ni kweli hata tukienda kwenye nchi zao, hata ile appreciation tu huwa hakuna!
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba wengine hata Tanzania hawajui iko wapi!
Hapa naongelea nchi kama SA, Namibia, Mozambique, Zimbabwe na Angola
 
Wakongo waweke mzigo mezani au watupe mgodi mmoja wakati wanajeshi wetu wanasaidia, wengine wanachimba madini na ya kuyarudisha home..!!

Miaka hii hakuna cha bure, enzi za mwalimu zilishapita..!! Ss hivi kila mtu ashinde mechi zake.!!
Safi sana, akili kama hizi ndo zinahitajika.
Hakuna kuoneana aibu
 
Ni humu humu nimewahi kuandika uzi miaka minne iliyopita kuwa kandarasi ya kuwamaliza M23 na wenzao ipewe JWTZ tu bila kuwachqnganya na wengine. Ni kazi ya mwezi mmoja tu. Siyo kuwatimuq bali kuwaua.
 
Back
Top Bottom