Doto Dotto
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 3,906
- 2,902
Jamani mbona mwenda zake anaandamwa sana kipindi hiki kulikoni?
Aachwe apumzike Kwa amani jamani dah!
Aachwe apumzike Kwa amani jamani dah!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Alikuwa rais but alikwua binadamu pia. and the way alivyo sitoshangaa, na si mara ya kwanza ku deny ushauri wa walinzi wake, multiple times alikuwa aki ignore that,Kambendera dish limeyumba! Rais ni kiongozi mkuu namba moja wa nchi kila hatua walinzi wanaye. Makamu wa Rais ni kiongozi wa pili wa nchi kila aendako walinzi wanaye. Sasa kwa tuhuma kama hizi ina maana walinzi wa pande mbili walikubaliana na kuacha hili jambo? Alafu pajama kwenye ofisi zinafata nini?
Ndeeefu!? Lakini ni 💩💩💩 matupu!Eric Kabendera ni Absalom Kibanda, Ansbert Ngurumo, Neville Meena na Jesse Kwayu katika sura tofauti za walioshindwa na marehemu.I'm The State kabatini. Leo, In the Name of President.
Wakaamua pia wayajaze yalioumiza wapinzani ili kukomba nguvu zao zitumike katika kupush agenda na iende. ?
Ndio, ndio waandishi walioandika kitabu chenye jina 'I am the State' ikiwa na maana Mimi ndio Dola wanatofauti gani na Eric Kabendera?
Absalom Kibanda, Ansbert Ngurumo, Neville Meena na Jesse Kwayu waliandika kitabu kwa pamoja wakielezea miradi iliyojengwa Chato kwa madai kwamba Wilaya hiyo ilipendelewa kuliko mikoa mingine yote nchini. Unafki huo unatufanya Watanzania tuonekane wajinga sana. Eric Kabendera ni sehemu ya watu waliokuwa kinyume na serikali ya Magufuli, kwakifupi alitumika kuihujumu kwa kisingizio cha Uanahabari wa Uandishi wa habari za Uchunguzi.
Kwa kifupi tu, katika matukio ya mauaji yaliyokuwa yakitokea kule Kibiti, na Rufiji; Eric Kabendera alihusika. Naam, alimtuma Azory Gwanda, ukimsikiliza maelezo yake kuna namna anakwepa kwepa kueleza namna alivyofahamiana na Azory Gwanda lakini anakiri kwamba alikuwa akiwasiliana nae na tangu siku anakamatwa alijua, mahali alipokamatiwa alipajua, alipopelekwa anapajua na hadi sehemu alikouliwa Azory Gwanda anapajua.
Kwamba Azory Gwanda alikuwa anatumia "kitochi/kiswaswadu" wakati wote akiwa porini kutafuta habari za kiuchunguzi dhidi ya wqliokuwa washukiwa wa ugaidi, hadithi zote hizo Eric Kabendera anazijua. Yeye ni nani? Kwakifupi ni kwamba Eric Kabendera alikuwa ni mmoja kati ya washukiwa wa Ugaidi japokuwa hakupatikana na hatia; inawezekana ikawa katika watu waliokuwa wameandaa hayo matukio walitokea ndani ya mfumo kama ambavyo yeye anakiri kuwa aliwakuta viongozi mbalimbali hadi wa vyombo vyaa ulinzi wakiwa magereza kwa tuhuma za Ugaidi; inawezekana ni kweli watu hao anafahamiana nao.
Ukimsikiliza katika maelezo yake, kuna kipande cha vijana watatu wa maeneo ya Mbweni anadai walikuwa watu wake wa karibu, alikuwa akipiga nao story mbalimbali. Baada ya muda vijana hao wakapotea. Katika kufuatilia kwake akajakugundua kuwa walipotea kwa madai walikuwa magaidi. Sio hao tu anasema ni zaidi ya watu 300 walipotea kwa kuhusishwa na ugaidi maeneo ya Kibiti na Rufiji.
Ukiunganisha dots unapata mstari ulionyooka kwamba Eric alikuwa sehemu ya ugaidi. Pesa zilizokuwa zikipitia katika akaunti yake hazikujitosheleza maelezo, alikiri mwenyewe kufanya money laundering (utakatishaji fedha). Hilo hakatai. Upelelezi wake kwamba alikuwa anaweza kufuatilia kuanzia wapi Azory Gwanda alitekwa, alienda kuhifadhiwa wapi; na nani, na akaenda kuuliwa sehemu gani, hii inaonesha Eric Kabendera hakuwa peke yake mchezoni. Alikuwa na timu; tena timu kubwa na yenye mizizi mirefu.
Ukifuatilia matukio ya Kibiti n Rufiji; Eric Kabendera alikuwa mtu wa kwanza kuyatolea taarifa za ndani kabisa. Leo anakiri kwamba aliwahi kufuatilia hadi wale washukiwa wa ugaidi, aliongea nao, akafanya mahojiano nao na kupata taarufa mbalimbali ambazo zilimsaidia kujua mengi kuhusu hayo madai ya ugaidi. Kwamba Eric anataka kusema yale matukio hayakuwa ya kweli kuhusu ugaidi. Kwamba wale Raia waliokuwa wanauawa sio kweli. Kuna mahali anajichanganya katika maelezo; unaona kabisa ule mchezo alikuwa sehemu yao isipokuwa walishindwa na vikosi vilivyopelekwa kule Kibiti na Rufiji na matokeo yake Azory Gwanda akauawa kwa maelezo yake.
Kituko kingine ni namna ambavyo ameelezea kwamba Hayati Dr Magufuli alitaka kumbaka makamu wake wa Rais akiwa amevaa Pajama usiku wa manane nyumbani kwa Makamu wake.
Kwa kifupi tu Eric ameinajisi nchi yetu; pengine kwa kujua ama kutokujua uhalisia wa umbali kutoka Ikulu hadi nyumbani kwa Makamu wa Rais ni zaidi ya 10+km. Kutoka Magogoni hadi St Peters kwa nyuma kuna umbali mrefu sana; kwamba kilomita zaidi ya 10; Hayati Magufuli alitembea na Pajama kwenda kumbaka Makamu wake; hii sio tu kwamba anaichafua mamlaka ya Ulinzi wa Rais bali amemtusi Rais aliyepo Madarakani hata kama Rais hatolijibia hili lakini tayari ameonesha dharau kubwa kwa safi nzima ya ulinzi wa Rais na Makamu wake, kwamba Walinzi wake walimsindikiza akafanye uhalifu huo? Hiki ni kituko kingine amekiandika katika kitabu chake.
Eneo jingine ni pale anaposema Kuhusu Ben Saanane, anasema alianza kuwasiliana nae kwa kipindi kirefu, anasema hadi dakika za mwisho za Ben saa nane, kabendera alijua alikua wapi, na alikua na akina nani, na kwamba aliambniwa pia kuna mwili wa mtu mmoja ulifikishwa hospitali, anasema ilimchukua mwaka mzima kujua huo mwili ulitoka wapi na ulifikaje hospitali, anasema walihoji watu 30 kwa nyakati tofauti, na kwamba mmoja wapo wa watu hao alimwambia kuwa aliyetenda jambo hilo ni bwana mkubwa na kwamba aliumia sana hadi kudondosha bastola yake baada ya kutenda tukio hilo; anasema Magufuli alipata mfadhaiko na kujutia tukio hilo. Baadae mwili huo ukaenda kutupwa Mto Rufiji. Moja ya hadithi ya hovyo zaidi kuwahi kutolewa.
Lakini yote haya ni kwa ajili ya nini? Nimeanza kueleza hapo juu kwamba mwaka 2022 walijitokea waandishi wanne wakaandika kitabu kinachoitwa "I am the state" kwamba "Mimi ni dola". Kitabu hicho kilikufa kifo cha asili maana kilibaki kjwa kama kijarida tu watu wakafungia maandazi maisha yakaendelea. Hakikuvuma wala kueleweka kwa umma.
Kitaalamu hii ya sasa tunasema watu wanapambana na kile alichoki-set HAYATI Magufuli kama standards katika utendaji kazi wake alipokuwa HAI. Kwa sababu hiyo inatengenezwa kila aina ya damage ama Character assassination. Wanataka kufuta na kuua legacy yake kabisa. Character assassination. Wamefikiria wakafikia conclusion kuwa hakuna wa kuweza kufanya kama yeye. The standards he set are too high for them to even dream about achieving them. Only solution is to tarnish his image and character so that Tanganyikans will get angry and eventually forgets all about him. Kwahiyo maswali kwamba hakuna atakayeweza kufanya kama Magufuli yatakufa. Na aliyoyafanya yote yataonekana ni ujinga. A fools man errand.
Ukijiuliza yale yaliyohojiwa kuhusu miradi iliyojengwa Chato, ni nani anaehoji kuhusu miradi inayojengwa Zanzibar na Kizimkazi kwa ujumla wake? Kwakifupi Magufuli enzi zake hakupemda siasa uchwara; na wanaomtusi leo ujue waliingia kwenye kumi na nane zake.
Kwakifu hakuna kitu cha maana alichokiandika kwenye hiki kitabu chake ambacho kina uhalisia wa ukweli. Amesema Mama yake alinunua nyjmba waliyokuwa wakiishi wakoloni wa kijerumani ambacho kilikuwa na maktaba kubwa ndani mwao; nimefuatilia huko kwao; ni uongo mtupu. Vile vinyumba huwezi kusimama hadharani ukasema kulikuwa na maktaba kubwa halafu ukatupeleka kutuonesha vibanda vya kuku ukatuaminisha waliishi wakoloni pale. Kwao ni pale Rwamishenye; hakuna hizo nyumba anazosema Mama yel alinunua nyumba kubwa yenye maktaba kubwa sana ndani.
Kwa mujibu wa Lisu Dr Slaa Beni ni kazi ya mboweWakati anamtungua Ben walinzi hao walikuwepo?
Ndugu yangu, naamini una uelewa mdogo kuhusiana na faragha za viongozi wanaolindwa.Kabendera sisi tunauelewa wa kutosha ni kweli unachuki na jpm lakini uongo huu uliouandika hauna tofauti na vitabu vya yericko nyerere mwenye elimu ya hapa na pale.
Wote tunafahamu raisi ni kiongozi wa umma na makamu wake hao wote safari yoyote hutoka na walinzi.
Pili wabapoishi huishi na wasaidizi wao! Hivi wewe unaposema JPM alitoka na pajama kwenda kwa makamu mbona kama ni picha ya kihindi!
Unataka kuaminisha umma raisi ni sawa na mkuu wa mkoa au wilaya wanaoweza kutembea bila walinzi wakiamua ebu acha kuchafua viongozi kwa maslahi yako.
Cha kushangaza serikali imekaa kimya kuhusu jambo hili.
We unaona alikuwa na maadili mema? Pia kumbuka aliwahi kusema yeye ni kichaa.Kimaadili haiwezekani na JPM kamwe asingeweza kufanya hivyo!
Wakati Mbowe anaanguka Chako ni Chako 🐼Wakati anamtungua Ben walinzi hao walikuwepo?
lakini uongo huu uliouandika hauna tofauti na vitabu vya yericko nyerere mwenye elimu ya hapa na pale.


Kawawa alikuwa Waziri mkuu wakati wa Rais Mwinyi? 🐼Ndugu yangu, naamini una uelewa mdogo kuhusiana na faragha za viongozi wanaolindwa.
Kwa uelewa wako, unaamini Rais hata akiwa anajisaidia, walinzi wanakuwa wamekizunguka choo?
Ungetoa hoja nyingine, siyo hiyo ya walinzi.
Uliwahi kusikia ile habari iliyosababisha kifo cha OCD kule temeke?
Sikutaka nieleze hii lakini kwa sababu inaonekana mpo watu wenye uelewa mdogo kuhusiana na masuala ya hawa viongozi, nalazimika kulisema:
Wakati Kawawa akiwa Waziri Mkuu, aliamua kwenda kwa siri kwa kimada, maeneo ya kuleTemeke Machinjioni. Akiwa huko, mkuu wa kituo akaambiwa na wakubwa wake kwamba mkubwa yupo maeneo hayo yaliyopo chini ya hemaya yako. Na kwamba ahakikishe PM anakuwa salama lakini hatakiwi kuisogolea nyumba, na kwamba haitakiwi afahamu kuwa wanajua yupo huko. Kwamba wao walichotakiwa kuhakikisha ni kuwa eneo lote hilo lipo salama. Ilikuwa usiku, OCD yupo nyumbani kwake. Akatoka kwa kasi kwenda kuhakikisha anasimamia aliyoambiwa. Bahati mbaya pale Temeke machinjioni, akagongana na lorry, na kupoteza maisha.
Kisa cha pili, ni kile cha Rais wa Nigeria kufia kwa kimada. Unadhani akiwa pale kwa kimada, walinzi walikuwa wamemzunguka? Wao wanachohakikisha ni kuwa anayelindwa yupo salama lakini bila ya kuingilia faragha yake.
Fuatilia kilichokuwa kikifanyika huko Zanzibar, Karume alipokuwa Rais, na pale alipokuwa anahitaji kimada, kilichokuwa kikifanyika.
Take Note of this:
It is rumoured that Sani Abacha was in the company of two Indian sex workers "imported" from Dubai who, allegedly, laced his drink, some say apple, with a poisonous substance, making the Head of State feel unwell around 4:30 a.m. and was dead by 6:15 a.m.
una uhakika wa unalolizungumza?Kimaadili haiwezekani na JPM kamwe asingeweza kufanya hivyo!
akilazimisha atafiapoMbowe hatakiwi kurudi madarakani
Wewe leta ukweli ,kama unaona Kabendera no Mwongo, leta UKWELI 🤔🤔🤔Kabendera sisi tunauelewa wa kutosha ni kweli unachuki na jpm lakini uongo huu uliouandika hauna tofauti na vitabu vya yericko nyerere mwenye elimu ya hapa na pale.
Wote tunafahamu raisi ni kiongozi wa umma na makamu wake hao wote safari yoyote hutoka na walinzi.
Pili wabapoishi huishi na wasaidizi wao! Hivi wewe unaposema JPM alitoka na pajama kwenda kwa makamu mbona kama ni picha ya kihindi!
Unataka kuaminisha umma raisi ni sawa na mkuu wa mkoa au wilaya wanaoweza kutembea bila walinzi wakiamua ebu acha kuchafua viongozi kwa maslahi yako.
Cha kushangaza serikali imekaa kimya kuhusu jambo hili.
Wewe kama POPOMA! Tuambie UKWELI ni Nini?? Kakosea wapi??Ni kitabu cha kijinga, before you read a book soma publisher.
Kama muhusika alikuwa anatumika na wazungu elewa access (opportunity wanazoweza mpa).
Yaani watu wampe access ya kwenda kufanya Phd chuo kikubwa, na media alizokuwa anaandikia wana multiple publishing firms (part of their group companies) na wameogopa kujihusisha na ule ujinga. Wangechapisha wao wangefanya na marketing pia ya kukiuuza.
Sasa hao waliokataa sio wachapishaji wenyewe ni kuogopa kuziingiza nchi zao kwenye diplomatic row, kwa ujinga ulioandikwa mule wasomaji wao are not that stupid and gullible ata kama hawaijui Tanzania (too childish).
Pili elewa psychology ya mwandishi anapotokea, binafsi wakati nasikiliza interview ya Kabendera asilimia kubwa ya mambo ambayo kayaongea ni vitu ambavyo tayari nilikuwa nishaadika humu JF.
Mengine kwenye interview ni uongo, promotion and self defence tu. Kwa wanasheria makini wakiamua wanamshtaki kwa picha tu aliyotumia; achana na maudhui ya upuuzi alioweka.
Usalama wa taifa ni mchezo wa watu wenye akili (hasa analyst), there is nothing else.
Magufuli hakuwa perfect lakini watanzania wanahitaji social reformer, akili zao bado sana.
Asilimia kubwa ya watanzania hawaelewi decisions za maisha zina consequences na kuna rules of engagement in life. Hii ni shida kubwa sana sio kwa raia wenye elimu ndogo, bali hata viongozi wenye nyadhifa kubwa serikalini.
Kumwelewa Magufuli inataka akili kubwa
anafosi tu!Mbowe hatakiwi kurudi madarakani