Kabila la kwanza hadi la mwisho nchini kwa ubora wa kiasili wa uzalishaji vyakula vyenye lishe nchini:

Kabila la kwanza hadi la mwisho nchini kwa ubora wa kiasili wa uzalishaji vyakula vyenye lishe nchini:

Mbeya kabila linalolima vyakula ni Wasafya na si Wanyakyusa wao walifanikiwa kusoma nashangaa hawapo hapo kabisa
 
Samahani tena...!!

Unaweza nuambia kwanini Wachagga wamekuwa wa kwanza kwa mambo mengi mazuri ndani ya nchi hii...???

Alafu pia nimefuatilia takwimu zako nimeona ukanda wa kaskazini mwa Tanzania umetoa makabila zaidi ndani ya 10 bora..!!!nini hasa Kisababishi/Vishababishi vikuu...????
Hao jamaa wa Kaskazini wanasaidiwa sana na milima yake mirefu iliyojitenga na yenye uwezo wa ku-regulate mvua. Kijiografia kuna mvua za aina tatu: conventional; monsoon; na orographic (relief). Katika aina zote hizo za mvua, ya uhakika ni ya orographic kwa sababu yenyewe inanyesha eneo lenye milima pekee, kumbuka mambo ya windward na leeward kwenye some la jiografia. Sasa, Kaskazini kuna milima mingi iliyojitenga ambayo imeleta neema kubwa sana kwa watu wa huko kuweza kuwa na mvua za uhakika kwa mwaka mzima. Na kwa kuwa, eneo hilo lipo karibu na Ikweta, linapata mvua za aina mbili - za vuli na masika (bi-modal). Halafu milima hiyo ni ya volcano ambayo inatoa udongo wa kiwango kikubwa cha nutrients kuliko udongo wa aina yoyote duniani. Ndiyo maana maeneo yenye udongo huo, yana vyakula vitamu sana na vyenye afya. Hata makabila yanayoishi eneo hilo, nao wanafanikiwa kutokana na vyakula bora.
Vilevile, licha ya kupata mvua za milimani (orographic), maeneo yanayozunguka mlima ni makame sana, hivyo hayaruhusu kusitawi kwa magonjwa hatari (fatal) sana kwa afya za Waafrika wanaoishi nchi za Tropiki hasa - malaria, malale (trypanosomiasis & nagana) na manjano (Yellow fever).
Hivyo watu wa Kaskazini wamejikuta wana afya nzuri ya kutoshambuliwa na magonjwa.
Hata hivyo, sifa hizo ni sawa sawa na zilizoko Nyanda za Juu Kusini. Tofauti yake ni kuwa, eneo karibia lote la Nyanda za Juu Kusini linapata mvua nyingi bila kujali kama kuna milima. Pia, huko hakuna milima iliyojitenga mbali na Mlima Rungwe, hali hiyo imesababisha baridi kali inayosababisha baadhi ya mazao kutohimili baridi hiyo. Baridi hiyo imesababishwa na mrundikano wa safu za milima mingi mingi kuanzia Kipengere, Livingstone, Uporoto hadi Udzungwa. Halafu Nyanda hiyo ina msimu mmoja pekee wa mvua (uni-modal) na kiangazi chenye baridi kali. Yote hayo yamekuwa yaki-descourage usitawi wa baadhi ya mazao muhimu hasa ndizi, pamoja na ufugaji wa ng'ombe na mbuzi, pamoja na baadhi ya matunda hasa machungwa.
Hata hivyo, kutokana na hali ya joto kali la Kyela iliyo katikati ya Ziwa Nyasa na Mlima Rungwe, imesababisha Wanyakyusa (Wangonde/Wakonde) wa Kyela kuivisha mazao yote yanayostawi kwenye joto.
Sijui kama nimekujibu. Hata hivyo sababu nyingine kuu, kuna siku yake nitaisema, siyo wakati kwa sasa.
 
Mbeya kabila linalolima vyakula ni Wasafya na si Wanyakyusa wao walifanikiwa kusoma nashangaa hawapo hapo kabisa
Nitaongezea ili niweke makabila yote. Kwa taarifa yako kadri ya uchambuzi, Wasafwa wako namba 19. Vuta subira nita-display makabila yote, coz sikutaka bandiko liwe refu sana.
 
Sasa nadhani hukuelewa maana ya kijedwali kile cha vyakula. Simaanishi kulima chakula cha aina moja tu bali aina mbalimbali za vyakula. Kuna mazao makuu ya chakula nchini kama: ndizi, mpunga, mahindi, mihogo, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, ulezi, mtama, ngano, njegere, mbaazi, maharage, kunde na njugu mawe.
Sasa, niambie ni mazao mangapi yanayolimwa hapo Iramba halafu jitahidi kulinganisha na makabila mengine ambayo uliwahi kupata nafasi ya kutembelea. Linganisha na makabila mengine ya kati yasiyopata mvua ya kutosha hasa Wagogo, Wanyamwezi, Wasukuma, Wanyaturu, Waisanzu, Wagorowa, Warangi, Wasandawe, Wabulunge, Wadatooga na Wambulu, uone kama nimeionea Unyilamba halafu tusaidiane niweze kurekebisha penye makosa.
Ama linganisha ulimaji wa mazao hayo na makabila kama Wahaya, Waha, Wakurya, Wakerewe, Wachaga, Waluguru, Wasambaa na Wanyakyusa utaona utofauti kati ya kuivisha vyakula vya kutosha na vyakula vya aina nyingi vya kutosha.
Mazao mengine ni kama KARANGA, MUHOGO, MAHARAGE, KUNDE, ALIZETI,ULEZI,NJUGU KWA WINGI SANA, MTAMA AINA MBALI MBALI NA NDIZI KATIKA BAADHI YA MABONDE KAMA KULE KISANA.
Pia vigezo vyako havijazingatia eneo kisiasa, mfano huwezi kuwa na upimaji linganifu kwa miji, majiji na wilaya na uka conclude kuwa hawa wako na A au B au C. Kuna makabila mengine maeneo yao ya asili ndio palipata fursa ya kuwa makao makuu ya mkoa toka zamani sana na hivyo resource zikawekwa hapo na hata walioendeleza hayo maeneo sio watu wa asili ya pale tu na pengine wenye asili hata wameondoka kabisa. Mfano wakwere ni wangapi waliojenga na kupaendeleza YOMBO kama sio eneo lote limevamiwa na watu wa kuja??
 
Mazao mengine ni kama KARANGA, MUHOGO, MAHARAGE, KUNDE, ALIZETI,ULEZI,NJUGU KWA WINGI SANA, MTAMA AINA MBALI MBALI NA NDIZI KATIKA BAADHI YA MABONDE KAMA KULE KISANA.
Pia vigezo vyako havijazingatia eneo kisiasa, mfano huwezi kuwa na upimaji linganifu kwa miji, majiji na wilaya na uka conclude kuwa hawa wako na A au B au C. Kuna makabila mengine maeneo yao ya asili ndio palipata fursa ya kuwa makao makuu ya mkoa toka zamani sana na hivyo resource zikawekwa hapo na hata walioendeleza hayo maeneo sio watu wa asili ya pale tu na pengine wenye asili hata wameondoka kabisa. Mfano wakwere ni wangapi waliojenga na kupaendeleza YOMBO kama sio eneo lote limevamiwa na watu wa kuja??
Asante sana kwa swali zuri. Nilichagua Yombo siyo kwa sababu imeshaendelezwa bali nilifuatilia eneo lenye rutuba ya kutosha kulinganisha na maeneo mengine ya Wakwere. Yes, Mlandizi na Chalinze Biko kwenye mabonde so wamekuwa wakifaidika na kilimo cha mpunga but kule Yombo, Wakwere walioishi huko, ni lazima walikuwa wakilima mazao ya aina nyingi kuliko Mlandizi, Chalinze ama Kibaha ama Bagamoyo. Vilevile, uwepo wa Bahari karibu ulisaidia sana kuchagua Tarafa hiyo kwa kuwa ilikuwa inaweza ku-access samaki wabichi tofauti na Chalinze, Mlandizi na Kibaha ambayo iko mbali kuweza kupata samaki wabichi kipindi cha kabla ya kuja kwa magari, pikipiki wala baiskeli.
Ila kiukweli hakuna sehemu yoyote niliyoconsider maendeleo ya mji, angalia mfano Waluguru sikuchukua Morogoro ama Wachaga kwa Moshi, au Mwanza kwa Wasukuma, ama Wasambaa kwa Lushoto. Ni miji michache sana mikubwa ya mikoa imefanikiwa kuwakilisha eneo bora la kabila.
 
Sina mashaka na kusudio lako LA hii takwimu ila mashaka yangu ni population ya wasukuma 7m hapo naona haiwezekani
 
Mimi nimevutiwa na effort iliyotumika kutengeneza hayo majedwali bila kutumia kompyuta!

Inanikumbusha mbali, lakini pia inanifikirisha sana juu ya dhana ya kujenga uchumi wa viwanda katika nchi yetu.
 
Sina mashaka na kusudio lako LA hii takwimu ila mashaka yangu ni population ya wasukuma 7m hapo naona haiwezekani
Usihofu kuhusu hilo, hii takwimu nimeitoa kwenye mtandao mkubwa duniani wa joshuaproject.net. La muhimu fuatilia idadi ya wakazi wa mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Geita kwa sensa ya mwaka 2012. Mikoa hiyo ilikuwa na wakazi zaidi ya milioni 7.3. Sasa fikiria kwa kasi ya ukuaji wa watu kwa mikoa hiyo yenye wastani wa zaidi ya asilimia 2.7%, watakuwa wangapi kwa sasa?
Bahati mbaya makabila mengine yenye asili ya mikoa hiyo - Wasumbwa, Wazinza, Wasubi, Wakerewe na Wakara, yana watu watu wachache, so hizo data ninaziamini kwa kiwango kikubwa kutokana na ongezeko kubwa la Wasukuma, hasa wale wa Simiyu.
 
Mimi nimevutiwa na effort iliyotumika kutengeneza hayo majedwali bila kutumia kompyuta!

Inanikumbusha mbali, lakini pia inanifikirisha sana juu ya dhana ya kujenga uchumi wa viwanda katika nchi yetu.
Hilo nalo neno. Maneno kuntu hayo mzazi.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Mimi nimevutiwa na effort iliyotumika kutengeneza hayo majedwali bila kutumia kompyuta!

Inanikumbusha mbali, lakini pia inanifikirisha sana juu ya dhana ya kujenga uchumi wa viwanda katika nchi yetu.
Hebu cheki ramani hiyo ya Tanzania ikionyesha idadi ya watu Sensa ya mwaka 1957.
Angalia idadi ya Wasukuma, ni watu 1,530,000. Kabila linalofuatia ni Wamakonde lenye watu 476,000 pekee ambalo idadi ya Wasukuma ni mara tatu zaidi ya Kabila pili kipindi hicho.
Sasa nadhani utaona kuwa, ongezeko la Wasukuma hadi kufikia watu milioni saba bado lilikuwa ni dogo tu ukilinganisha na makabila mengine kama Wahaya, Wagogo na Wachaga.


IMG_1561.JPG
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Asante sana kwa swali zuri. Nilichagua Yombo siyo kwa sababu imeshaendelezwa bali nilifuatilia eneo lenye rutuba ya kutosha kulinganisha na maeneo mengine ya Wakwere. Yes, Mlandizi na Chalinze Biko kwenye mabonde so wamekuwa wakifaidika na kilimo cha mpunga but kule Yombo, Wakwere walioishi huko, ni lazima walikuwa wakilima mazao ya aina nyingi kuliko Mlandizi, Chalinze ama Kibaha ama Bagamoyo. Vilevile, uwepo wa Bahari karibu ulisaidia sana kuchagua Tarafa hiyo kwa kuwa ilikuwa inaweza ku-access samaki wabichi tofauti na Chalinze, Mlandizi na Kibaha ambayo iko mbali kuweza kupata samaki wabichi kipindi cha kabla ya kuja kwa magari, pikipiki wala baiskeli.
Ila kiukweli hakuna sehemu yoyote niliyoconsider maendeleo ya mji, angalia mfano Waluguru sikuchukua Morogoro ama Wachaga kwa Moshi, au Mwanza kwa Wasukuma, ama Wasambaa kwa Lushoto. Ni miji michache sana mikubwa ya mikoa imefanikiwa kuwakilisha eneo bora la kabila.
Umetaja kama vile wachaga wote ni wa Kibosho?? Mbona hukufikiria wale wa Rombo, Machame au kule Marangu??
Ndio maana naona Data zilizotumika sio Represenatative! Sampuli za aina hii zinakuwa na mashaka katika kuamua, maana inategemea tu wewe uliona wapi pameendelea zaidi kumbe population kubwa ipo mahali pengine ambapo bado hapajaendelezwa na bado wanawakikilisha population ya kabila husika.
 
Ni nini faida kubwa ya ziada waliyonayo watu/jamii yenye ardhi au vyakula vingi na mvua nyingi au hali ya hewa iliyoitwa nzuri ?

Na ni mapungufu gani waliyonayo jamii yenye ardhi isiyo na rutuba au mvua nyingi,!!

Kuna relevance kwenye hzo faida na hasara NA hyo ardhi au Maeneo husika!!?
 
Umetaja kama vile wachaga wote ni wa Kibosho?? Mbona hukufikiria wale wa Rombo, Machame au kule Marangu??
Ndio maana naona Data zilizotumika sio Represenatative! Sampuli za aina hii zinakuwa na mashaka katika kuamua, maana inategemea tu wewe uliona wapi pameendelea zaidi kumbe population kubwa ipo mahali pengine ambapo bado hapajaendelezwa na bado wanawakikilisha population ya kabila husika.
Ndiyo maana kwenye post yangu awali nilieleza wazi kupata changamoto hasa kati ya Kibosho na Marangu. Binafsi Mimi huwa napenda sana Marangu kuliko eneo lolote la uchagani na ndilo bonde lenye msongamano mkubwa wa watu kuliko eneo la uchagani.
But kilichofanya nichague Kibosho ni yafuatayo:
  • Bonde la Kibosho na maeneo yanayoizunguka hasa Uru kuna mvua nyingi kuliko lile la Marangu.
  • Bonde la Kibosho Lina mito mingi kuliko eneo lolote la uchagani.
  • Bonde la Kibosho Lina mashamba ya mazao ya aina nyingi tofauti na Marangu ambako maeneo mengi yamefunikwa na migomba.
  • Blonde la Kibosho ndilo lililo katikati ya uchagani ikiunganisha Wamachame na Wasiha kwa upande wa kulia dhidi ya Wavunjo na Warombo kwa upande wa kushoto, pamoja na mji wa Moshi, Himo na Wa-Kahe.
Nikiri wazi, ugumu wa kuchagua ndio ulichelewesha taarifa hii kwani awali nilikuwa nachambua vigezo hivi kwa Kuzbass eneo la Marangu. Hata hivyo, kwa taarifa yako, hata ningetumia Marangu, Kibosho, Machame ama Mkuu, ilijionyesha wazi, miji yote hiyo ingewakilisha vyema Wachaga na kuperform the way Kibosho imefanya kwa kuwa maeneo hayo yana sifa zinazofanana sana.
Pia kwa Wahaya, nilisumbuka sana kuamua upi wa kuwakilisha Wahaya kati ya Bukoba, Kamachumu, Kemondo Bay (Kanazi). Vilevile kwa Wapare (Ugweno vs Usangi); Wajaluo (Utegi vs Shirati); Wakurya (Tarime vs Sirari); ni. Ni maeneo machache sana ambako sikutumia nguvu ya ziada kuchagua ukanda.
Hata hivyo, uchambuzi huu una mambo mengi ya "arms-chair thinking" yaani siyo ya kwenda field, hivyo kuna possibility kubwa ya baadhi ya vigezo nimevi-exaggerate, hivyo kwa kuwa Wewe ni wazi ni mwenye ni wa uchagani, nakuomba pamoja na wengine wa uchagani na maeneo mengine nchini mnisaidie, ni ukanda upi kiasili (achana na maeneo ya mijini) ambako umekuwa ukizalisha mazao mengi na ya aina mbalimbali?
 
Ni nini faida kubwa ya ziada waliyonayo watu/jamii yenye ardhi au vyakula vingi na mvua nyingi au hali ya hewa iliyoitwa nzuri ?

Na ni mapungufu gani waliyonayo jamii yenye ardhi isiyo na rutuba au mvua nyingi,!!

Kuna relevance kwenye hzo faida na hasara NA hyo ardhi au Maeneo husika!!?
Ipo tofauti kubwa tena sana katika maisha yetu ya tangu kuingia kwa formal education. Zamani kabla ya elimu hiyo ya darasani, wazee wetu walikuwa wakiturithisha elimu za mazingira tuliyokuwa tukitegemea kupata mahitaji yetu ya kila siku, hivyo walitufundisha kulima, kufuga na kuvua samaki kama shughuli kuu za kiuchumi. Hata hivyo, kutokana na kuja kwa elimu ya darasani, jamii zikaingizwa katika mfumo wa kupeleka watoto shuleni ambako wanafundishwa theory tangu darasa la kwanza hadi Chuo kikuu ili aitumie elimu hiyo. So, jamii zilizokuwa na watoto wenye kumbukumbu nzuri ndio zilifanikiwa kutoa wanafunzi wengi elimu za juu na hivyo kuneemeka kiajira na hence kimaisha.
Najua watu wengi, wanaamini kuwa, mafanikio ya baadhi ya jamii kutoka wasomi wengi ilitokana na upendeleo wa wakoloni kujenga miundombinu ya kutosha huko. Hili ni suala linalohitaji mjadala but sikuwahi kukubaliana na sababu hii kutokana na kuangalia mazingira ya wilayani kwetu mwaka 2000 ambako kipindi hicho kulikuwepo sekondari moja tu ya umma na moja ya binafsi but nilikuwa nikiambiwa repeatedly kuwa, Wilaya hiyo ni mojawapo ya Wilaya zenye wasomi wengi nchini.
So, ever since, nilichotaka kutoa kwa Watanzania, ni kuibadilisha hiyo fikra ili tuujue ukweli na muda wote kuanzia sekondari hadi Chuo Kikuu, nimekuwa nikifanya uchunguzi wa suala hilo na kufikia conclusion, jamii zenye uzalishaji wa kutosha wa vyakula na vya aina mbalimbali, pamoja na mazingira yasiyo na magonjwa hatari ya malaria na malale, yalikuwa ndiyo yana wasomi wengi. Nina uhakika umetembelea maeneo mengi nchini, utakuwa tusaidiane kujibu masuala haya muhimu:
  • Mchele wa kutoka wapi wenye ladha na bora kabisa hapa Tanzania? Why?
  • Ndizi za ka wapi zenye ladha bora kuliko zote Tanzania? Why?
  • Matunda (machungwa) gani matamu kuliko yote Tanzania? Why?
  • Samaki wa aina gani na kutoka wapi ni watamu kuliko wote hapa Tanzania? Why?
  • Nyama gani ya ng'ombe na kutoka wapi ni tamu kuliko nyingi nchini Tanzania? Why?
  • Nyama ya Kuku wa kutoka wapi ni tamu kuliko popote Tanzania? Why?
  • Maziwa ya kutoka wapi ndiyo matamu kuliko yote Tanzania? Why?
  • Ni wapi kuna maji safi kwa wingi kwa mwaka mzima hapa Tanzania? Why?
  • Ni wapi ambako huwa hawaugui malaria na man jana hapa Tanzania? Why?
Hayo ndiyo maswali muhimu yanayotakiwa kusumbua vichwa vyetu kama wasomi. Asante ningetamani watu Meiji up maswali hayo ili tujadili karibuni.
 
Lkn kuna maeneo au mikoa yenye ardhi isiyo na rutuba na isiyopendeza au ku reflect hiyo Dhana:mikoa hiyo ina mvua kidogo na vyakula si vingi kulingana na data zako. Mfano,mkoa wa singida ina watu wenye uwezo wa akili na kumbukumbu nzuri, wanaojiamini na kujisimamia,hawa nao sababu ni nini!?

Lkn pia ardhi na hali ya hewa ya Lushoto- Tanga na ya Kigoma haitofautiani na mikoa hyo ya Kilimanjaro na Mbeya -Tukuyu. Lkn mikoa hyo ya Kigoma na Tanga (Lushoto ) haina wasomi au wenye elimu wengi (Formal Education )kama jamii/mikoa uliyoisema!! Sasa hawa walipatwa na nini kama ardhi, vyakula na hali ya hewa ni kigezo!?

Hata mvua na hali ya hewa ya Mara-Musoma, Ruvuma, Sumbawanga, Morogoro na Katavi siyo mbaya. Kwa mantiki yako Ingefaa kuwa na matokeo au mafanikio at least 75 percent ya jamii zile unazosema, walizipata sababu ya vyakula from good soil fertility na mvua toshelezi. Nako huko kuna mvua, hali ya hewa Karibia 75percent ya mikoa unayozingatia!!
 
Ndiyo maana kwenye post yangu awali nilieleza wazi kupata changamoto hasa kati ya Kibosho na Marangu. Binafsi Mimi huwa napenda sana Marangu kuliko eneo lolote la uchagani na ndilo bonde lenye msongamano mkubwa wa watu kuliko eneo la uchagani.
But kilichofanya nichague Kibosho ni yafuatayo:
  • Bonde la Kibosho na maeneo yanayoizunguka hasa Uru kuna mvua nyingi kuliko lile la Marangu.
  • Bonde la Kibosho Lina mito mingi kuliko eneo lolote la uchagani.
  • Bonde la Kibosho Lina mashamba ya mazao ya aina nyingi tofauti na Marangu ambako maeneo mengi yamefunikwa na migomba.
  • Blonde la Kibosho ndilo lililo katikati ya uchagani ikiunganisha Wamachame na Wasiha kwa upande wa kulia dhidi ya Wavunjo na Warombo kwa upande wa kushoto, pamoja na mji wa Moshi, Himo na Wa-Kahe.
Nikiri wazi, ugumu wa kuchagua ndio ulichelewesha taarifa hii kwani awali nilikuwa nachambua vigezo hivi kwa Kuzbass eneo la Marangu. Hata hivyo, kwa taarifa yako, hata ningetumia Marangu, Kibosho, Machame ama Mkuu, ilijionyesha wazi, miji yote hiyo ingewakilisha vyema Wachaga na kuperform the way Kibosho imefanya kwa kuwa maeneo hayo yana sifa zinazofanana sana.
Pia kwa Wahaya, nilisumbuka sana kuamua upi wa kuwakilisha Wahaya kati ya Bukoba, Kamachumu, Kemondo Bay (Kanazi). Vilevile kwa Wapare (Ugweno vs Usangi); Wajaluo (Utegi vs Shirati); Wakurya (Tarime vs Sirari); ni. Ni maeneo machache sana ambako sikutumia nguvu ya ziada kuchagua ukanda.
Hata hivyo, uchambuzi huu una mambo mengi ya "arms-chair thinking" yaani siyo ya kwenda field, hivyo kuna possibility kubwa ya baadhi ya vigezo nimevi-exaggerate, hivyo kwa kuwa Wewe ni wazi ni mwenye ni wa uchagani, nakuomba pamoja na wengine wa uchagani na maeneo mengine nchini mnisaidie, ni ukanda upi kiasili (achana na maeneo ya mijini) ambako umekuwa ukizalisha mazao mengi na ya aina mbalimbali?


From Kinampanda-Iramba West
 
Back
Top Bottom