Kabla ya kuja watu weupe waafrika tuliamini uwepo wa Mungu ila hatukuamini uwepo wa shetani

Kabla ya kuja watu weupe waafrika tuliamini uwepo wa Mungu ila hatukuamini uwepo wa shetani

Jana nilibahatika kufanya maongezi na mzee moja wa zamani sana age inakimbilia kama miaka 90 now.

nilimuuliza maswali mengi sana yanayohusu imani ila tukaenda mpaka miaka ya nyuma kidogo kutokana na maelezo yake niligundua aya.

kuwa waafrika kabla ya kuja waarabu, wareno , waingereza, waberigiji, wafaransa, wahindi na wachina. waliamini uwepo wa mungu ila swala lilikuja pale kumuabudia huyo mungu.

Nini maana halisi ya neno "Mzimu"?

Mzimu ni marehemu, ambapo Kiafrika kiasili tuliamini kuwa wafu wapo karibu na Mungu hivyo tulikuwa tunaomba mizimu utusaidie maana wao wapo karibu na Mungu. Ni sawa na Wakatoliki wanavyoamini katika saints.

lakini kwenye dunia ya leo tunaamini

"Maana ya neno "Mzimu", ni Mashetani ambao ndio humuongoza kufanya maasi, wakati mtu anakata roho hao Mashetani hutoka, hao ndio "Mizimu". Mizimu ni Mashetani walio toka kwa WAFU, kutii Mizimu ni kutii Mashetani, na si kutii WAFU."

ila ukweli wa mambo ni kuwa neno SHETANI sio neno lenye asili ya kiafrica . Concept ya shetani imeletwa afrika. waafrika walikuwa hawaamini uwepo wa shetani.

Mzimu imefananishwa na shetani baada ya dini za kigeni kufika afrika ila
imani ya uwepo wa shetani imeletwa hapo mwanzo haikuwepo.

Waafrika wengi wanaamini mababu zetu hawakuamini Mungu bali mizimu. Kumbe sio kweli Mungu alikuwepo ila tuliamini ndugu zetu waliokufa walikuwa wanatuunganisha sisi na Mungu, hivyo ili maombi yako yafanikiwe unaongea na mizimu (marehemu wa ukoo wenu).

Waafrika tuliamini Mungu, ila tukaamini Mungu yuko karibu na wafu (mizimu/mababu na ndugu walokufa) ambao tuliamini wanaishi katika mibuyu na miti nk. Sio kwamba tuliabudu miti

Ndio maana dini za Kiafrika hazikuwa na wamisionari wa kusambaza kwasababu, kila mtu aliomba Mungu kupitia mizimu ya ukoo wao. Mizimu ya ukoo wa mwezako ulikuwa hakusaidii hivyo hakukuwa haja ya kusambaza dini za asili, kila mtu aliomba kikwao.

Ila watu weupe ndio wakatufunza kuwa Mungu kwa imani zetu sio sahihi. Kwahiyo wasingekuwa wao bado tungeamini Mungu kinamna yetu.

nakualika kaka Mshana Jr katika kutoa mawazo yako katika hili andiko
Hatimaye nimefika...
Kwa sehemu kubwa waafrika hatukuwa na Mungu mmoja japo kuna Mungu mmoja ndio alijulikana kama mkuu wa Miungu huyu akiwa ni mwanaume (Mungu jua) ambaye naye alikuwa na msaidizi wake mwanamke (Mungu mwezi)
Halafu ikafuata miungu mingine kulingana na hadhi zao, nguvu na nafasi zao kwenye jamiii
Hawa miungu waliombwa neema, tiba ulinzi, mvua, ukwasi, ushindi nk kwenye mambo yote ya kijamii.. Na iliaminika kwamba jamii yoyote ilipopatwa na jambo lolote baya basi mungu fulani alikasirika na taratibu za kimila zilifanyika kwenda kumuomba msamaha

Level ya tatu ni mizimu yenye nguvu ya kuweza kuwasiliana na mungu fulani.. Si kila roho ya mfu iliweza kugeuka roho ya mzimu wenye nguvu bali ni wale watu waliokuwa mashuhuri kwenye jamii kama
Wafalme
Watemi
Majemadari wa vita
Wazee wa kimila
Viongozi nknk
Hawa mafanikio yao kwenye lolote yaliunganishwa moja kwa moja na baraka za Mungu mkuu kupitia miungu mbalimbali, na hivyo kuaminika nguvu yao kwenye kufikisha ujumbe wa maombi yoyote kwa miungu kisha kwa Mungu mkuu
Maombi hayo yalifanyika sehemu maalum tu zilizoaminika kama makazi ya miungu/mizimu... Makazi hayo yakiwa ya kudumu ama kinyume chake

Level ya nne ni wazee wanaoaminika kuwa na hekima, usafi ama nguvu nyingine za ziada kwenye jamii.. Hawa walisimama kama viongozi wa kiimani kama ilivyo leo hii.. Na hawa ndio walitumika kufanya patano, kusuluhisha kesi za kijamii kutibu kiroho na kimwili nknk.. Na hawa ndio ambao wakifa hupanda level na kuwa level ya tatu

Level ya tano ni miungu/mapepo waharibifu, wenye ghadhabu, kisirani na waliojawa na hasira sana.. Hawa ni mizimu maroho yaliyogeuka kuwa na nguvu ya maangamizi kutokana na kuwa na mwisho mbaya/kikomo cha kuwa hasa kubwa likiwa mauaji ya kukusudia, mapigano, visasi nk
Hawa ndio kwa wazungu walipewa jina la shetani
 
Wazungu walikua wajanja sana ....walijua sisi waafrika tuna Mungu ndio maana wakatuletea na sanamu zao ili tuziabudu....yaani tuwaabudu wao sababu unaposoma biblia unaona kabisa kuna mistari inaonesha kua watu walioandikwa kwenye biblia walikua ni weusi......

Mfano ayubu alikua ni mweusi
Hata suleimani alikua ni mweusi ....sasa ukijiuliza kama mfalme suleiman alikua ni mweusi na Yesu ametoka kwenye kizazi hicho cha mfalme suleiman(sababu ukisoma unaona Yesu ni mbari ya daudi na daudi alikua ni baba yake suleimani, na suleiman amejisema kabisa kua yeye ni mweusi (soma wimbo ulio bora).......

Ukisoma biblia vizuri unakuja kuona hata wale waarabu pale misri ni mapandikizi ya wazungu ili kupoteza historia yetu halisi na ndio maana wakatuletea jina la afrikaa ambalo haliko kwenye biblia....je niendelee zaidi kukuonesha kua sisi ngozi nyeusi tunajidharau bure lakini sisi ni wathamani
 
Ninaendelea kidogo kukuthibitishia

Wimbo Ulio Bora 1:5
[5]Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri,
Enyi binti za Yerusalemu,
Mfano wa hema za Kedari,
Kama mapazia yake Sulemani.
I am black, but comely, O ye daughters of Jerusalem, as the tents of Kedar, as the curtains of Solomon.

Hapo juu jinsi suleimani alijithibitisha kua yeye ni mweusi....


Sasa hawa wazungu sijui kwanini wametulisha matangopori......kwa uelewa wangu natamani nije na mada kuhusu hii historia
 
Kaburini kuna nn iwapo mtu kilichompeleka ni kumbukumbu? Hawa kina petro, yohana yakobo n.k waliokufa ndo wanafaa kukumbukwa linapokuja suala la MUNGU?
Nisaidie kumuuliza ni yupi bora na mwenye thamani kwake kati ya Yohana, Petro pamoja na yakopo ukilinganisha na Babu yake aliyemzaa baba yake kisha yeye kuzaliwa. Ni yupi bora kati yao Babu yake na hao akina Petro.

Ukimuuliza historia ya asili yake hawezi kuijua ila kajifunza ya akina Yakobo na wenzie
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Umepotea ndugu.

Historia uliochimba wewe nichamtoto..

Kuna jamaa kafundisha, video ipo YouTube

kaelezea tangu jinsi gani watu waliingia ardhi ya Tanzania..
Makabila kama wanyamwezi, wahehe, wapare, wahiraki yalianzishwa vipi na kwa maana zipi,.
imani hizo za mizimu zilianza vipi tulizitoa wap...

Shule ya maana.

na Hitimisho ni.. Sisi watu wa mataifa nje na Israel mwanzo wote hatukumjua Mungu wa kweli tulifanya ibada za Sanamu na kuabudu miungu pasipo kujua (Tunaita ni zama za ujinga)

lakini sasa tupo ambao tumeijua kweli, Tunamuabudu Mungu tunae mjua, Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo.
Nisaidie hii link ya hii video
 
Nisaidie kumuuliza ni yupi bora na mwenye thamani kwake kati ya Yohana, Petro pamoja na yakopo ukilinganisha na Babu yake aliyemzaa baba yake kisha yeye kuzaliwa. Ni yupi bora kati yao Babu yake na hao akina Petro.

Ukimuuliza historia ya asili yake hawezi kuijua ila kajifunza ya akina Yakobo na wenzie
Naamini ameona swali.
 
Wazungu walikua wajanja sana ....walijua sisi waafrika tuna Mungu ndio maana wakatuletea na sanamu zao ili tuziabudu....yaani tuwaabudu wao sababu unaposoma biblia unaona kabisa kuna mistari inaonesha kua watu walioandikwa kwenye biblia walikua ni weusi......

Mfano ayubu alikua ni mweusi
Hata suleimani alikua ni mweusi ....sasa ukijiuliza kama mfalme suleiman alikua ni mweusi na Yesu ametoka kwenye kizazi hicho cha mfalme suleiman(sababu ukisoma unaona Yesu ni mbari ya daudi na daudi alikua ni baba yake suleimani, na suleiman amejisema kabisa kua yeye ni mweusi (soma wimbo ulio bora).......

Ukisoma biblia vizuri unakuja kuona hata wale waarabu pale misri ni mapandikizi ya wazungu ili kupoteza historia yetu halisi na ndio maana wakatuletea jina la afrikaa ambalo haliko kwenye biblia....je niendelee zaidi kukuonesha kua sisi ngozi nyeusi tunajidharau bure lakini sisi ni wathamani
Adam(a.s) ni mtu na Mtume wa Allah(s.w) wa kwanza. Adam(a.s) ameumbwa kwa udongo uliofinyangwa ukafanywa kuwa sanamu la mtu kisha likapuliziwa roho na kuwa mtu kamili kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:
Na (kumbuka) Mola wako alipowaambia Malaika, “Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo mkavu unaotoa sauti, wenye kutokana na matope meusi yaliyovunda.”“Basi nitakapomkamilisha na kumpulizia roho inayotokana na Mimi, basi mumuangukie kwa kumtii.” (15:28-29)


NOTE
Kumbe Adam kuumbwa kwake aliumbwa udongo mkavu,,unaotoa sauti,,WENYE KUTOKANA NA MATOPE MEUSI YALIYOVUNDA.

Hii kitu huwa inanifanya niamini kabisa sisi watu weusi tuna kitu cha ziada,,sisi ndio msingi mkuu,,sisi ndio binadamu grade one (toleo la kwanza kabisa) ila sasa sijui ni kwanini hawa wenzetu wametupiga GAP kwenye mambo mengi [emoji23][emoji23][emoji23]
 
FB_IMG_1666930412962.jpg
 
Nisaidie hii link ya hii video
Mzee nimeitafuta sanaaa hiyo part, naikosa.
Lakini aliyefundisha search anaitwa Omari Mnyeshani.
ukipata nipe mrejesho
 
Wamefuta neno mizmu wakaleta roho mtakatifu Ila n kitu kile kile
Tunavyo Omba kupitia roho mtakatifu n similar stracture na watu walivyo Omba kupitia mizmu
Mpk structure za sadaka zinafanana Ila Hawa wenye likitabu lao la kizungu wanakiita bible haijaonyesha
Pengne huwa Nahsi roho mtakatifu anavary na locality ndo maana kila koo ilikuwa na mizimu yake
Nisamehewe kama nimekufuru ni mawazo yangu na fikra zangu.
 
Nakubali sana, hata vitabu tunasoma katika shule za sekondari mfano, “Things fall apart, River’s between cha Ngugi wa thiong’ nk”, vinatupa mwangaza vizazi vya sasa kua mizimu ya koo husika ndio ilikua kiungo kati ya MUNGU na wanadamu, itawalinda na waovu.
Na jamaa na jamii zilikua katika utaratibu mzuri na maadili mema kuliko ilivyo sasa.
NAWAALIKA TUREJEE Etiopia, Afrika Yetu Asili yetu.
 
Umepotea ndugu.

Historia uliochimba wewe nichamtoto..

Kuna jamaa kafundisha, video ipo YouTube

kaelezea tangu jinsi gani watu waliingia ardhi ya Tanzania..
Makabila kama wanyamwezi, wahehe, wapare, wahiraki yalianzishwa vipi na kwa maana zipi,.
imani hizo za mizimu zilianza vipi tulizitoa wap...

Shule ya maana.

na Hitimisho ni.. Sisi watu wa mataifa nje na Israel mwanzo wote hatukumjua Mungu wa kweli tulifanya ibada za Sanamu na kuabudu miungu pasipo kujua (Tunaita ni zama za ujinga)

lakini sasa tupo ambao tumeijua kweli, Tunamuabudu Mungu tunae mjua, Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo.
Mkuu rudia tena kusoma kwa kutulia uzi huu bila shaka utaelea kilicho andikwa
 
Mungu (nguvu kuu) kila jamii ilikuwa na namna yake yakumfikia mungu (nguvu kuu) katika dunia nzima, kwetu afrika tulikuwa na njia zetu za kumfikia mungu na kutusaidia

Mizimu ni watu wema au mababu zetu waliokufa lakini katika uhai wao walikuwa watu wema walikuwa machifu,waaguzi,walinzi wa ukoo,watabiri n.k hawa watu roho zao hubaki katika ulimwengu kusaidia jamii zao husaidia kwakuwa wapo karibu sana na nguvu kuu( mungu) ndomana wakiombwa na kukumbukwa na jamii zao husaidia bila shaka lolote

Lakini pia kuna mizimu mibaya mababu zetu waliokuwa wachawi,wasaliti,walozi nao pia roho zao hua zinabaki duniani kuendeleza mambo yao waliowaachia mikoba huwaomba wawasaidie kazi zao za uchawi na ulozi na huwasaidia pia

Note: kila jamiii ina namna yake yakumfikia mungu (nguvu kuu) maamuzi ni yako kufata jamii yako ili umfikie mungu au kufata jamii nyingine wazungu,waarabu,wachina,waizraeli n.k ili umfkkie mungu(nguvu kuu)


_mzoma

Umesema vyema! Afrika ni sisi
 
Back
Top Bottom