Kafulila: Kwa miaka mitatu Rais Samia amekopa nje TZS 12.5T sawa US$ 5BL lakini amelizalishia Taifa TZS 47.5T sawa na US$19BL

Kafulila: Kwa miaka mitatu Rais Samia amekopa nje TZS 12.5T sawa US$ 5BL lakini amelizalishia Taifa TZS 47.5T sawa na US$19BL

Wewe unaelewa maana au unauliza maana?

Sijaelewa kwanini mnapenda kumtukana huyu Mama kisaikolojia huku mkifanya km mnamsifia kumbe mnaoongea matusi
Nadhani wewe unania mbaya ndio maana unasema kunalugha ya tofauti hapo
 
Kamishina wa PPP Mhe David Kafulila anasema "Wakati Rais Samia anaingia madarakani Uchumi wa Tanzania ulikuwa US$ 66BL Leo ni US$ 85BL sawa na ongezeko la US$19 wakati deni la nje ni US$ 5BL tu.

View attachment 2945755
Deni hata kama linahimilika mbona Seriakli inashindwa kulilipa hilo Deni? Ikawa Serikali haina Deni. Iweje Uchumi umeongezeka wakati Deni bado linazidi kukuwa na kuongezeka kwenda juu?
 

Kwa nini deni la taifa linaendelea kuongezeka nchini Tanzania?​

ik

CHANZO CHA PICHA,IKULU TANZANIA
Maelezo ya picha,
Rais wa Tanzania Samia Suluhu akizungumza na waziri wa fedha wa taifa hilo wakiwa Makao Makuu ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), jijini Washington DC.
Maelezo kuhusu taarifa

  • Author,Damas Kanyabwoya
  • Nafasi,Mchambuzi
  • 13 Disemba 2022
Kuongezeka kwa deni la taifa kwa kiasi cha Shilingi 21 trilioni ndani ya miezi 6 kumezua tafrani na mijadala mikali kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari nchini Tanzania.
Taarifa ya uchumi ya mwezi Novemba 2022 iliyotolewa hivi karibuni na Benki Kuu ya Tanzania inaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi Oktoba 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 90.35 trilioni.
Alipokuwa akisoma Bajeti ya Serikali mwezi Juni, Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba alisema hadi mwezi Aprili 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 69.4 trilioni.
Hii inaonyesha wazi kuwa deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20.91 trilioni kati ya Mwezi Aprili na Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa kumbukumbu za miongo miwili iliyopita za taarifa za deni la taifa kutoka Benki Kuu ya Tanzania, ongezeko la Shilingi 20 trilioni kwa muda mfupi kiasi hicho halijawahi kutokea.
Haishangazi kuwa wadau wengi wanaona ongezeko la deni hili ni kubwa sana. Suala wanalouliza katika mijadala na ambalo halijapata ufafanuzi wa kutosha ni kwa nini deni limepanda kwa kasi hiki?
Kuna wanoauliza pia kuwa pesa zilizokopwa zimeenda wapi ikiwa gharama za maisha zinazidi kupaa siku hadi siku na huduma za jamii zinadorora.
Wapo pia wanaoonyesha hofu zao kuwa kasi hii ya kupanda kwa deni la taifa inaweza kuiingiza nchi kwenye matatizo ya makubwa ya kiuchumi na kuifanya ishindwe kukopesheka.
Alipoingia madarakani hayati Rais John Magufuli, deni la taifa lilikuwa ni Shilingi 35 trilioni, kwa mujibu wa taarifa rasmi za Bunge la Tanzania.
Mwezi Aprili 2018 deni lilifikia Shilingi 49.9 trilioni, kwa mujibu wa Bajeti ya serikali iliyosomwa Bungeni. Mwaka mmoja baadae (Aprili 2019) deni la taifa likafika Shilingi 51.03 trilioni. Deni halikupungua. Likaendelea kukua na kufikia Shilingi 60.7 trilioni mwezi Aprili 2021.

Maelezo ya viongozi serikali​

Viongozi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wamejitokeza kujibu baadhi ya hoja zinazoibuliwa na wadau katika mijadala kuhusu ongezeko kubwa la deni la taifa. Lakini hakuna hata mmoja wa viongozi hao aliyetoa majibu ya kina kwa nini deni limepanda na pesa zimeenda wapi.
Akiongea na gazeti la The Citizen mwishoni mwa juma Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Emmanuel Tutuba alidai kuwa deni la taifa ni himilivu na kuwataka watanzania waondoe hofu.
“Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi. Deni la taifa lina uhimilivu wa kutosha kwa sasa, kwa baade na kwa muda mrefu,” Bwana Tutuba alisema.
w

CHANZO CHA PICHA,AFRICA-PRESS.NET
Maelezo ya picha,
Waziri wa fedha na mipango Tanzania, Mwigulu Nchemba

Waziri Nchemba yeye aliingia kwenye mtandao wa Twitter na kudai kuwa ongezeko kubwa la deni la taifa limechangiwa na sekta binafsi ambayo hivi majuzi ilikopa Shilingi 20 trilioni.
Hata hivyo alitoa mchanganuo wa deni ambao umeongeza sintofahamu badala ya kufafanua. Mchanganuo wake pia una kasoro za waziwazi za kimahesabu.
Mchanganuo wa Waziri Nchemba ulikuwa hivi; deni la serikali kuu na mashirika yake ni Shilingi 46.6 trilioni; deni la sekta binafsi ni kati ya Shilingi 17 trilioni hadi 20 trilioni; hati fungani za serikali ni Shilingi 26,600 bilioni (ambayo ni 26.6 trilioni).
Halafu Dk Nchemba akatoa jumla yote ya mchanganuo huu kuwa ni Shilingi 71.2 trilioni wakati hesabu rahisi zinaonyesha kuwa jumla ya mchanganuo wake ni Shilingi 90.2 trilioni inayoendana na taarifa ya Benki Kuu ya Oktoba ya jumla ya deni lote.
Dk Nchemba akaongeza kuwa sekta binafsi ilikopa tena hivi karibuni kiasi cha takribani Shilingi 20 trilioni, ambazo kadiri ya mahesabu yake Waziri Nchemba ndizo zimefanya deni la taifa kufikia Shilingi 91 trilioni.
Ufafanuzi wa Dk Nchemba unachangaza kwa sababu unaongeza deni badala ya kulipunguza. Mchanganuo wake unaonyesha deni limefikia Shilingi 112 trilioni badala ya Shilingi 91 trilioni inayoonyeshwa na Benki Kuu ya Tanzania. Kama ni hivyo kuna tatizo la kimahesabu na la ki-taarifa.
Yote kwa yote mchanganuo na ufafanuzi wa Dk Mwigulu bado hauelezi kwa nini deni la taifa limeongezeka kwa Shilingi 20 trilioni kati ya Aprili 2022 na Oktoba 2022.
Ni wazi kuwa hii sio mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa na mijadala mikali kuhusu deni la taifa. Wakati wa utawala wa Rais Magufuli kuongezeka kwa deni la taifa kulizua mijadala.
Wakati huo serikali ilidai kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ilikuwa ndio sababu ya kuongezeka kwa deni hilo. Hata hivyo ongezeko la deni la taifa halikuwahi kufikia kiasi kikubwa kama cha mwaka huu.
w

CHANZO CHA PICHA,TRC
Maelezo ya picha,
Serikali ya Tanzania ina miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa reli za kisasa na vituo vya umeme

Uhakiki wa deni la taifa ufanyike​

Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya miundombinu ikiwemo ya reli ya kisasa ya SGR, ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere na barabara za mwendokasi kutoka katikati ya mji wa Dar es Salaam kwenda Mbagala.
Hata hivyo serekali ya Rais Samia imeweza kupata mikopo mingi yenye riba nafuu kutoka Benki ya Dunia na Shirila la Fedha Duniani (IMF) ambayo mtangulizi wake. Mikopo hii inazidi kiasi cha dola za kimarekani 2 bilioni (zaidi ya Shilingi 4 trilioni) tangu Rais Samia aingie madarakani mwezi Machi 2021. Mikopo hii ambayo ilielekezwa kwenye shughuli za kukuza uchumi na kuboresha huduma za jamii ingetosha kabisa kuleta ahueni kwenye deni la taifa badala ya kuliongeza kwa kasi kubwa hivyo.
Kwa namna yoyote ile maelezo ya kina kutoka serikalini yanahitajika. Serikali ya Tanzania ni lazima ieleze ni kwa nini deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20 trilioni ndani ya miezi sita. Hakuna mtu nje ya serikali, hata angekuwa na utaalam kiasi gani, ambaye angeweza kuelezea ongezeko kubwa kiasi hicho.
Dk Nchemba ni mwanasiasa. Inawezekana kuna baadhi ya taarifa ambazo hajazipata kuhusu ongezeko kubwa hilo la deni la taifa. Ni wakati sasa kwa Gavana wa Benki Kuu na wataalam wake kujitokeza kutoa ufafanuzi wa kina. chanzo.BBC
 

Kwa nini deni la taifa linaendelea kuongezeka nchini Tanzania?​

ik

CHANZO CHA PICHA,IKULU TANZANIA
Maelezo ya picha,
Rais wa Tanzania Samia Suluhu akizungumza na waziri wa fedha wa taifa hilo wakiwa Makao Makuu ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), jijini Washington DC.
Maelezo kuhusu taarifa

  • Author,Damas Kanyabwoya
  • Nafasi,Mchambuzi
  • 13 Disemba 2022
Kuongezeka kwa deni la taifa kwa kiasi cha Shilingi 21 trilioni ndani ya miezi 6 kumezua tafrani na mijadala mikali kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari nchini Tanzania.
Taarifa ya uchumi ya mwezi Novemba 2022 iliyotolewa hivi karibuni na Benki Kuu ya Tanzania inaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi Oktoba 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 90.35 trilioni.
Alipokuwa akisoma Bajeti ya Serikali mwezi Juni, Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba alisema hadi mwezi Aprili 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 69.4 trilioni.
Hii inaonyesha wazi kuwa deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20.91 trilioni kati ya Mwezi Aprili na Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa kumbukumbu za miongo miwili iliyopita za taarifa za deni la taifa kutoka Benki Kuu ya Tanzania, ongezeko la Shilingi 20 trilioni kwa muda mfupi kiasi hicho halijawahi kutokea.
Haishangazi kuwa wadau wengi wanaona ongezeko la deni hili ni kubwa sana. Suala wanalouliza katika mijadala na ambalo halijapata ufafanuzi wa kutosha ni kwa nini deni limepanda kwa kasi hiki?
Kuna wanoauliza pia kuwa pesa zilizokopwa zimeenda wapi ikiwa gharama za maisha zinazidi kupaa siku hadi siku na huduma za jamii zinadorora.
Wapo pia wanaoonyesha hofu zao kuwa kasi hii ya kupanda kwa deni la taifa inaweza kuiingiza nchi kwenye matatizo ya makubwa ya kiuchumi na kuifanya ishindwe kukopesheka.
Alipoingia madarakani hayati Rais John Magufuli, deni la taifa lilikuwa ni Shilingi 35 trilioni, kwa mujibu wa taarifa rasmi za Bunge la Tanzania.
Mwezi Aprili 2018 deni lilifikia Shilingi 49.9 trilioni, kwa mujibu wa Bajeti ya serikali iliyosomwa Bungeni. Mwaka mmoja baadae (Aprili 2019) deni la taifa likafika Shilingi 51.03 trilioni. Deni halikupungua. Likaendelea kukua na kufikia Shilingi 60.7 trilioni mwezi Aprili 2021.

Maelezo ya viongozi serikali​

Viongozi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wamejitokeza kujibu baadhi ya hoja zinazoibuliwa na wadau katika mijadala kuhusu ongezeko kubwa la deni la taifa. Lakini hakuna hata mmoja wa viongozi hao aliyetoa majibu ya kina kwa nini deni limepanda na pesa zimeenda wapi.
Akiongea na gazeti la The Citizen mwishoni mwa juma Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Emmanuel Tutuba alidai kuwa deni la taifa ni himilivu na kuwataka watanzania waondoe hofu.
“Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi. Deni la taifa lina uhimilivu wa kutosha kwa sasa, kwa baade na kwa muda mrefu,” Bwana Tutuba alisema.
w

CHANZO CHA PICHA,AFRICA-PRESS.NET
Maelezo ya picha,
Waziri wa fedha na mipango Tanzania, Mwigulu Nchemba

Waziri Nchemba yeye aliingia kwenye mtandao wa Twitter na kudai kuwa ongezeko kubwa la deni la taifa limechangiwa na sekta binafsi ambayo hivi majuzi ilikopa Shilingi 20 trilioni.
Hata hivyo alitoa mchanganuo wa deni ambao umeongeza sintofahamu badala ya kufafanua. Mchanganuo wake pia una kasoro za waziwazi za kimahesabu.
Mchanganuo wa Waziri Nchemba ulikuwa hivi; deni la serikali kuu na mashirika yake ni Shilingi 46.6 trilioni; deni la sekta binafsi ni kati ya Shilingi 17 trilioni hadi 20 trilioni; hati fungani za serikali ni Shilingi 26,600 bilioni (ambayo ni 26.6 trilioni).
Halafu Dk Nchemba akatoa jumla yote ya mchanganuo huu kuwa ni Shilingi 71.2 trilioni wakati hesabu rahisi zinaonyesha kuwa jumla ya mchanganuo wake ni Shilingi 90.2 trilioni inayoendana na taarifa ya Benki Kuu ya Oktoba ya jumla ya deni lote.
Dk Nchemba akaongeza kuwa sekta binafsi ilikopa tena hivi karibuni kiasi cha takribani Shilingi 20 trilioni, ambazo kadiri ya mahesabu yake Waziri Nchemba ndizo zimefanya deni la taifa kufikia Shilingi 91 trilioni.
Ufafanuzi wa Dk Nchemba unachangaza kwa sababu unaongeza deni badala ya kulipunguza. Mchanganuo wake unaonyesha deni limefikia Shilingi 112 trilioni badala ya Shilingi 91 trilioni inayoonyeshwa na Benki Kuu ya Tanzania. Kama ni hivyo kuna tatizo la kimahesabu na la ki-taarifa.
Yote kwa yote mchanganuo na ufafanuzi wa Dk Mwigulu bado hauelezi kwa nini deni la taifa limeongezeka kwa Shilingi 20 trilioni kati ya Aprili 2022 na Oktoba 2022.
Ni wazi kuwa hii sio mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa na mijadala mikali kuhusu deni la taifa. Wakati wa utawala wa Rais Magufuli kuongezeka kwa deni la taifa kulizua mijadala.
Wakati huo serikali ilidai kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ilikuwa ndio sababu ya kuongezeka kwa deni hilo. Hata hivyo ongezeko la deni la taifa halikuwahi kufikia kiasi kikubwa kama cha mwaka huu.
w

CHANZO CHA PICHA,TRC
Maelezo ya picha,
Serikali ya Tanzania ina miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa reli za kisasa na vituo vya umeme

Uhakiki wa deni la taifa ufanyike​

Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya miundombinu ikiwemo ya reli ya kisasa ya SGR, ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere na barabara za mwendokasi kutoka katikati ya mji wa Dar es Salaam kwenda Mbagala.
Hata hivyo serekali ya Rais Samia imeweza kupata mikopo mingi yenye riba nafuu kutoka Benki ya Dunia na Shirila la Fedha Duniani (IMF) ambayo mtangulizi wake. Mikopo hii inazidi kiasi cha dola za kimarekani 2 bilioni (zaidi ya Shilingi 4 trilioni) tangu Rais Samia aingie madarakani mwezi Machi 2021. Mikopo hii ambayo ilielekezwa kwenye shughuli za kukuza uchumi na kuboresha huduma za jamii ingetosha kabisa kuleta ahueni kwenye deni la taifa badala ya kuliongeza kwa kasi kubwa hivyo.
Kwa namna yoyote ile maelezo ya kina kutoka serikalini yanahitajika. Serikali ya Tanzania ni lazima ieleze ni kwa nini deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20 trilioni ndani ya miezi sita. Hakuna mtu nje ya serikali, hata angekuwa na utaalam kiasi gani, ambaye angeweza kuelezea ongezeko kubwa kiasi hicho.
Dk Nchemba ni mwanasiasa. Inawezekana kuna baadhi ya taarifa ambazo hajazipata kuhusu ongezeko kubwa hilo la deni la taifa. Ni wakati sasa kwa Gavana wa Benki Kuu na wataalam wake kujitokeza kutoa ufafanuzi wa kina. chanzo.BBC
Nadhani ungeleta chanzo Cha taarifa yako
 

Deni la Taifa Kenya laongezeka kufikia shilingi trilioni 1.56​

16 Agosti, 2023
Muonekano wa Barabara ya Nairobi Expressway iliyojengwa na Shirika la Barabara na Madaraja la China (CRBC) Mei 8, 2022. Picha na REUTERS/Thomas Mukoya

Muonekano wa Barabara ya Nairobi Expressway iliyojengwa na Shirika la Barabara na Madaraja la China (CRBC) Mei 8, 2022. Picha na REUTERS/Thomas Mukoya
Ona maoni
Kiwango cha deni la Kenya kimefikia kiwango cha juu licha ya Rais William Ruto kuapa kupunguza azma ya kuendelea kukopa, takwimu za Hazina zinaonyesha.
Jumla ya deni la taifa limepanda na kufikia rekodi ya shilingi trilioni 1.56 ambazo ni sawa na dola bilioni 10.8 katika mwaka wa fedha uliomalizika Juni 30 na kufikia shilingi trilioni 10.1, hivyo kuvuka ukomo wa deni wa shilingi trilioni 10, kulingana na data iliyotolewa Jumanne.
“Ongezeko la deni la taifa limechangiwa na malipo ya mikopo ya nje, kushuka kwa kiwango cha ubadilishaji fedha na malipo ya deni la ndani na nje,” Hazina ilisema.
Gharama za kurejesha mikopo, haswa kwa China, zimeongezeka wakati sarafu ya Kenya katika biashara ikiwa katika rekodi ya chini sana cha takriban shilingi 144 kwa dola moja.
Gharama ya kulipa madeni katika kipindi cha mwaka uliomalizika mwezi Juni ilikuwa shilingi bilioni 391 ambapo malipo ya juu zaidi -- shilingi bilioni 107 -- yalikwenda China.
Wabunge nchini Kenya walipiga kura mwezi Juni kubadilisha kiwango cha juu cha kukopa kutoka kile kilichopangwa hadi sehemu ya pato la taifa (GDP). Baraza la Seneti bado halijapitisha marekebisho hayo.
Ruto aliingia mamlakani mwaka jana akiahidi kufufua uchumi wa nchi ambayo ina takriban watu milioni 53.
Akieleza mpango wake wa mageuzi ya kiuchumi "kuanzia chini kwenda juu", Ruto aliahidi kupunguza deni la serikali na kuanzisha sera za kuweka pesa mifukoni mwa Wakenya ambao ni maskini.
Ukuaji wa uchumi ulipungua hadi asilimia 4.8 katika kipindi cha mwaka 2022 kutoka asilimia 7.6 mwaka uliopita, na unatabiriwa kuongezeka kwa zaidi ya asilimia tano mwaka huu, kulingana na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP chanzo.VOA
 
Zinaenda kupingana na facts zipi zilizotolewa?

Punguza uzwazwa
Deni la Taifa ni jumla ya Deni la Serikali na Deni la Sekta binafsi. Pia Deni la Taifa lipo la ndani na la nje. Mfano ongezeko la dola 5bn ilikuwa la nje. Kutoka usd24bn mpaka usd29bn.. la ndani liliongezeka nadhan kutoka TSH 15+trn mpaka TSH30+trn. deni la ndan maanake lipo ktk TSH..
 
Zinaenda kupingana na facts zipi zilizotolewa?

Punguza uzwazwa
Deni la Taifa ni jumla ya Deni la Serikali na Deni la Sekta binafsi. Pia Deni la Taifa lipo la ndani na la nje. Mfano ongezeko la dola 5bn ilikuwa la nje. Kutoka usd24bn mpaka usd29bn.. la ndani liliongezeka nadhan kutoka TSH 15+trn mpaka TSH30+trn. deni la ndan maanake lipo ktk TSH..

Nadhani Kafulila alimaanisha haya.
 
Nimemsikiliza huyu Kafulila kwenye hayo mahojiano,

Nakubaliana kabisa ni kweli deni la Taifa limekua,

Lakini pia, Nimekubaliana kuwa ni kweli Uchumia wa Taifa pia umekuwa.

Hoja hapa deni limekuwa kwa kiasi gani na Uchumi umekuwa kwa kiasi gani?

Asante Kafulila
 
Back
Top Bottom