Kafulila: Lissu acha kuzipaka matope Mahakama za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa?

Kafulila: Lissu acha kuzipaka matope Mahakama za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa?

Wasalaam wana wa Mungu.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Zacharia Kafulila, amekosoa kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu A Lissu kuhusu hoja ya kesi ya kukamatwa kwa Ndege na zingine mashauli yake kushughulikiwa kwenye Mabaraza ya Usuluhishi ya kibiashara kama ICSID- international Center For Settlement of Investment Disputes.

====

Akikosoa kauli hiyo, David Zacharia Kafulila amenukuliwa kwenye mtandao wa tweeter akiandika haya " Sitaki kujadili suala la kesi, naomba nijadili suala moja tu la uelewa kuhusu ICSID na Uanachama wake kwani Tundu A Lissu amepotosha katika hilo na huenda akawafanya wasiofahamu kuamini kwamba Tanzania ni mwanachama wa ICSID kwa Sababu ya Udhaifu wa Mahakama na Serikali ya Tanzania katika kusimamia Uhuru wa Mahakama.

Tundu A Lissu alinukuliwa kupitia ClubHouse akieleza kuwa " Lazma ieleweke kuwa sababu ya mashauri haya ya mikataba baina yetu na kampuni za nje kushughulikiwa kwenye mabaraza haya ya usuluhishi wa migogoro ya biashara na uwekezaji kama ICSID inatokana na tabia ya Serikali yetu ikiwa chini ya JPM na hata Samia kuingilia mambo ya mahakama na hivyo mahakama kukosa uhuru. Hivyo mahakama zetu haziaminiki, serikali yetu haiaminiki, hatuaminiki kwasababu ya rushwa za majaji na kuingiliwa na Ikulu. ndio sababu mashauri haya yanamuliwa ICSID "

Tundu A. Lissu ambae ni M/kiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na aliyekuwa Mgombea wa Urais wa JMT aliyepata kura kiduchu sana katika Uchaguzi Mkuu uliyopita wa 2020, ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Siasa pekee ambaye familia yake yote ni Raia wa Marekani ameonekana mara zote kuwa upande wa mataifa ya nje kuliko taifa lake.

David Zacharia Kafulila anatoa mfano wa nchi kubwa kama Marekani na Uchina zikiwa nchi wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania pamoja na nchi nyingine zaidi ya 166 kumuuliza Tundu A. Lissu kuwa nchi zote hizi Mahakama zao zinaingiliwa kama ilivyo kwa Tanzania ama ni utaratibu tu wa hiari wa kiusuluhishi uliowekwa Duniani katika kuoneaha imani kwa wawekezaji hasa wa nje?

Hoja ya David Zacharia Kafulila kwa Tundu A. Lissu ni kwamba kama Tanzania Mahakama zake siyo huru ndiyo sababu kesi za migogogro ya kibiashara zinafanyikia nje kwenye tume hii ya ICSID. Je, Marekani na Uchina ambazo nazo kesi zao za migogogro ya kibiashara zinafanyikia huko huko ICSID tulikopelekwa sisi kwa hoja ya hiyo ya Lissu anataka tuamini pia kuwa Mahakama za mataifa haya pia haziko huru?

" Lissu acha kuzipaka matope Mahakamani za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa ?"

View attachment 2433362View attachment 2433363
Bahati nzuri mimi niliusikiliza huo mjadala wa TL na wenzake huko Club House (nitaweka link hapa)..

Lakini ni bahati mbaya kuwa Kafulila hata hajamwelewa Tundu Kiasi...!!

JIBU KWA SWALI LA KAFULILA NI HILI:

Ni kweli USA na CHINA ni wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania na nchi zingine 165 duniani...

Lakini ni ukweli pia kuwa, CHINA na USA mahakama zao haziingiliwi na serikali zao kama ilivyo kwa mahakama za nchi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania...

Aidha mikataba ya kimataifa (International bilateral agreements), mwekezaji mwenye mgogoro na serikali husika, ana uhuru akiona inafaa (hasa kwa kigezo cha uhuru wa mahakama ktk nchi husika) kusuluhishwa na mahakama za ndani au kwenda straight huko ICSID...

Kwa kigezo hiki, ndiyo Lissu akasema, kwa Tanzania ambapo mahakama zinafanya kazi kwa kuangalia interests za mtawala (serikali), hakuna mwekezaji aweza kuziamini mahakama zetu hata huyo Jaji au hakimu akampa haki mwekezaji ku - seize mali za serikali kama inavyofanyika huko ICSID...

Kwa lugha rahisi, ni kuwa, TL alimaanisha hakimu au Jaji wa mahakama hawezi kuhukumu against serikali...!!
 
Bahati nzuri mimi niliusikiliza huo mjadala wa TL na wenzake huko Club House (nitaweka link hapa)..

Lakini ni bahati mbaya kuwa Kafulila hata hajamwelewa Tundu Kiasi...!!

JIBU KWA SWALI LA KAFULILA NI HILI:

Ni kweli USA na CHINA ni wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania na nchi zingine 165 duniani...

Lakini ni ukweli pia kuwa, CHINA na USA mahakama zao haziingiliwi na serikali zao kama ilivyo kwa mahakama za nchi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania...

Aidha mikataba ya kimataifa (International bilateral agreements), mwekezaji mwenye mgogoro na serikali husika, ana uhuru akiona inafaa (hasa kwa kigezo cha uhuru wa mahakama ktk nchi husika) kusuluhishwa na mahakama za ndani au kwenda straight huko ICSID...

Kwa kigezo hiki, ndiyo Lissu akasema, kwa Tanzania ambapo mahakama zinafanya kazi kwa kuangalia interests za mtawala (serikali), hakuna mwekezaji aweza kuziamini mahakama zetu hata huyo Jaji au hakimu akampa haki mwekezaji ku - seize mali za serikali kama inavyofanyika huko ICSID...

Kwa lugha rahisi, ni kuwa, TL alimaanisha hakimu au Jaji wa mahakama hawezi kuhukumu against serikali...!!
Zipo Kesi kibao Tanzania tumebwagwa na wawekezaji humu humu ndani,
 
Kimsingi mahakama zetu zingeaminiwa na wawekezaji wa kimataifa, wasingelazimisha arbitration ifanyike katika mahakama za kimataifa.

Kwa hivyo, sioni alipokosea Tundu Lissu.
 
Arbitrations sio mahakama za kawaida which sits all year round. Hizi zinaitwa ADR na hearing ni private.

Uwezi kwenda kujifungulia tu case lazima iwe sehemu ya makubaliano ya mkataba. Sasa mkataba sio lazima uwe expressed ata unapoingia bilateral trade agreement ikisema mgogoro na wawekezaji wao utatatuliwa on neutral ground hapo umewapa wawekezaji uhalali wakukufungulia case arbitration yeyote. Ndio kama hao wa Swedes wamepata uhalali huo wakufungua kesi kunatokana na bilateral trade na Tanzania iliyopo.

For arbitration to be legal binding inabidi nchi zijiunge (voluntary) ili kuweza kutekeleza maamuzi yake na sio zote zimejisajili na arbitration zote. Ndio maana South Africa waliachia ndege ya ATCL kwa sababu hawakuwa wanachama wa arbitration iliyotoa maamuzi ya case husika, jamaa wakakimbilia Canada.

Surely haya mambo dispute resolution processes na contract law wanafunzi wa business management and other disciplines other than law wanafundishwa huko UDSM, it is basic knowledge kwenye dunia ya biashara maana huyo Lissu huko anajiropokea tu.
BIT ni bilateral investment treaties maana yake ni kwamba serikali A na B wanawekeana mkataba kwamba mwananchi wa A akiweza B asijeakadhulumiwa and B na mwananchi wa B akiweza A asijeakadhulumiwa. Kama atadhulumiwa mali zake anahaki ya kwenda kwenye arbitration. Viena ,The Hague,London,Singapore and Washington DC Magufuli aliamua not to renew same of the expired BIT but he forgot that most of the BITs have a sunset clause that can take up to 10 years all in all the country was doomed to fail in its endeavor to rob investors
 
Nchi ambayo haina BIT mwekezaji akienda huko anashauriwa kuwa na MIGA
Unachanganya mambo. Suala la arbitration linawekwa kwenye mkataba na taasisi itakayokubalika na pande zote mbili. Bila kipengele hicho wawekezaji hawatii saini.

Amandla...
mwekezaji akienda huko anashauriwa kiwa na MIGA
 
Arbitrations sio mahakama za kawaida which sits all year round. Hizi zinaitwa ADR na hearing ni private.

Uwezi kwenda kujifungulia tu case lazima iwe sehemu ya makubaliano ya mkataba. Sasa mkataba sio lazima uwe expressed ata unapoingia bilateral trade agreement ikisema mgogoro na wawekezaji wao utatatuliwa on neutral ground hapo umewapa wawekezaji uhalali wakukufungulia case arbitration yeyote. Ndio kama hao wa Swedes wamepata uhalali huo wakufungua kesi kunatokana na bilateral trade na Tanzania iliyopo.

For arbitration to be legal binding inabidi nchi zijiunge (voluntary) ili kuweza kutekeleza maamuzi yake na sio zote zimejisajili na arbitration zote. Ndio maana South Africa waliachia ndege ya ATCL kwa sababu hawakuwa wanachama wa arbitration iliyotoa maamuzi ya case husika, jamaa wakakimbilia Canada.

Surely haya mambo dispute resolution processes na contract law wanafunzi wa business management and other disciplines other than law wanafundishwa huko UDSM, it is basic knowledge kwenye dunia ya biashara maana huyo Lissu huko anajiropokea tu.
Umeandika hadithi isiyokuwa na content.

Unadhani kwa nini mataifa, hasa mataifa ambayo wala hayakuwa waanzilishi wa mahakama hii, huamua kuwa wanachama wa hizi mahakama za biashara?

Kwa nchi za Africa na Asia, kama hujui, ni kwamba sababu kubwa ya mataifa kujiunga na taasisi hizi ni kujenga confidence kwa wawekezaji kuwa hamwezi kuwadhulumu kwa kutumia mahakama zenu za ndani zinazoamriwa kutoa hukumu kwa matakwa ya watawala.

Mfano mmojawapo ni kwamba sisi hapo awali hatukuwa wanachama wa taasisi hii. Mkapa alipoingia madarakani, uchumi ukiwa umedorora kabisa, misaada na mikopo kutoka taasisi za fedha tumezuiwa kupewa, Rais Mkapa akaanza kufanya jitihada kubwa kuwapata wawekezaji. Sekta iliyoonekana ingeweza kuwavutia wawekezaji wa nje, ni sekta ya madini. Kwa sababu Tanzania ilikuwa na miundombinu duni kabisa, wataalam walishauri kuwa ni lazima yapatikane makapuni makubwa yenye mitaji mikubwa ndiyo yanayoweza kuwekeza kwenye sekta ya madini, makampuni yatakayokuwa na uwezo wa kujenga miundombinu yao kama umeme, maji na barabara.

Kampuni iliyoonekana kuwa na uwezo huo, kwenye top list ilikuwa Barrick Gold. Serikali ilipoiomba Barrick Gold kuja kuwekeza Tanzania, kwa kumtumia Andrew Young, rafiki wa Hayati Mwalimu Nyerere, Barrick waligoma, wakisema kuwa nchi haina investment security code, tena ikiwa na record mbaya kabisa ya kutaifisha mali za makampuni na watu binafsi mwaka 1967.

Serikali ilijitetea sana kuwa utaifishaji hautatokea, bado Barrick hawakuridhika, wakagoma kuwekeza Tanzania. Serikali ikaiomba World Bank isaidie kuishawishi Barrick. World Bank ikaiambia Serikali ya Tanzania kuwa ili kuwapa confidence Barrick, ni lazima nchi iwe mwanachama wa ICSID na WTO ili nchi ikikiuka, Barrick wawe na uwezo wa kuishtaki. Serikali ya Tanzania ikajiunga. Walivyowaendea Barrick, Barrick bado waligoma kwa maelezo kuwa Tanzania haina mali ya kufidia gharama iliyopo nje ya nchi ambayo wataichukua kama Tanzania itaenda kinyume na haki. Serikali ikalazimika kukopa dola mioni 400, na kuziweka kama bond. Baada ya hapo ndiyo Barrick wakaja kuwekeza Tanzania.

Kama hujarlewa mpaka hapo, sina la kukusaidia.
 
Yan huyu Tumbili badala ya kushauri serikali ilipe deni anakimbilia kum attack Lissu ili akumbukwe tena kwenye uteuzi, Chawa pro max pumbavu kweli
Sidhani kama anaweza kumteka Rais Samia kwa kauli za kinafiki kama hizi.
 
Umeandika hadithi isiyokuwa na content.

Unadhani kwa nini mataifa, hasa mataifa ambayo wala hayakuwa waanzilishi wa mahakama hii, huamua kuwa wanachama wa hizi mahakama za biashara?

Kwa nchi za Africa na Asia, kama hujui, ni kwamba sababu kubwa ya mataifa kujiunga na taasisi hizi ni kujenga confidence kwa wawekezaji kuwa hamwezi kuwadhulumu kwa kutumia mahakama zenu za ndani zinazoamriwa kutoa hukumu kwa matakwa ya watawala.

Mfano mmojawapo ni kwamba sisi hapo awali hatukuwa wanachama wa taasisi hii. Mkapa alipoingia madarakani, uchumi ukiwa umedorora kabisa, misaada na mikopo kutoka taasisi za fedha tumezuiwa kupewa, Rais Mkapa akaanza kufanya jitihada kubwa kuwapata wawekezaji. Sekta iliyoonekana ingeweza kuwavutia wawekezaji wa nje, ni sekta ya madini. Kwa sababu Tanzania ilikuwa na miundombinu duni kabisa, wataalam walishauri kuwa ni lazima yapatikane makapuni makubwa yenye mitaji mikubwa ndiyo yanayoweza kuwekeza kwenye sekta ya madini, makampuni yatakayokuwa na uwezo wa kujenga miundombinu yao kama umeme, maji na barabara.

Kampuni iliyoonekana kuwa na uwezo huo, kwenye top list ilikuwa Barrick Gold. Serikali ilipoiomba Barrick Gold kuja kuwekeza Tanzania, kwa kumtumia Andrew Young, rafiki wa Hayati Mwalimu Nyerere, Barrick waligoma, wakisema kuwa nchi haina investment security code, tena ikiwa na record mbaya kabisa ya kutaifisha mali za makampuni na watu binafsi mwaka 1967.

Serikali ilijitetea sana kuwa utaifishaji hautatokea, bado Barrick hawakuridhika, wakagoma kuwekeza Tanzania. Serikali ikaiomba World Bank isaidie kuishawishi Barrick. World Bank ikaiambia Serikali ya Tanzania kuwa ili kuwapa confidence Barrick, ni lazima nchi iwe mwanachama wa ICSID na WTO ili nchi ikikiuka, Barrick wawe na uwezo wa kuishtaki. Serikali ya Tanzania ikajiunga. Walivyowaendea Barrick, Barrick bado waligoma kwa maelezo kuwa Tanzania haina mali ya kufidia gharama iliyopo nje ya nchi ambayo wataichukua kama Tanzania itaenda kinyume na haki. Serikali ikalazimika kukopa dola mioni 400, na kuziweka kama bond. Baada ya hapo ndiyo Barrick wakaja kuwekeza Tanzania.

Kama hujarlewa mpaka hapo, sina la kukusaidia.
Naongezea serikali ikakubali Bima ya MIGA
 
Hivi Watanzania wanajua kwamba nchi yao ina kesi ngapi za namna hii??ambazo zitasababisha mali nyingi kukamatwa??na kwa nini waandishi wa habari hawataki kujituma na kwenda kwenye mtatandao wa hizi kesi na kuandika habari zote ili kuwaelimisha Watanzania??Au kuwaweka gizani ndio strategy ya serikali??Kwani kodi zao ndio zinatumika kulipa mambo kama haya
 
Symbion walipwa bila kushinda kesi lakini Watanzania waliambiwa nchi imeshindwa kesi
 
Wasalaam wana wa Mungu.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Zacharia Kafulila, amekosoa kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu A Lissu kuhusu hoja ya kesi ya kukamatwa kwa Ndege na zingine mashauli yake kushughulikiwa kwenye Mabaraza ya Usuluhishi ya kibiashara kama ICSID- international Center For Settlement of Investment Disputes.

====

Akikosoa kauli hiyo, David Zacharia Kafulila amenukuliwa kwenye mtandao wa tweeter akiandika haya " Sitaki kujadili suala la kesi, naomba nijadili suala moja tu la uelewa kuhusu ICSID na Uanachama wake kwani Tundu A Lissu amepotosha katika hilo na huenda akawafanya wasiofahamu kuamini kwamba Tanzania ni mwanachama wa ICSID kwa Sababu ya Udhaifu wa Mahakama na Serikali ya Tanzania katika kusimamia Uhuru wa Mahakama.

Tundu A Lissu alinukuliwa kupitia ClubHouse akieleza kuwa " Lazma ieleweke kuwa sababu ya mashauri haya ya mikataba baina yetu na kampuni za nje kushughulikiwa kwenye mabaraza haya ya usuluhishi wa migogoro ya biashara na uwekezaji kama ICSID inatokana na tabia ya Serikali yetu ikiwa chini ya JPM na hata Samia kuingilia mambo ya mahakama na hivyo mahakama kukosa uhuru. Hivyo mahakama zetu haziaminiki, serikali yetu haiaminiki, hatuaminiki kwasababu ya rushwa za majaji na kuingiliwa na Ikulu. ndio sababu mashauri haya yanamuliwa ICSID "

Tundu A. Lissu ambae ni M/kiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na aliyekuwa Mgombea wa Urais wa JMT aliyepata kura kiduchu sana katika Uchaguzi Mkuu uliyopita wa 2020, ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Siasa pekee ambaye familia yake yote ni Raia wa Marekani ameonekana mara zote kuwa upande wa mataifa ya nje kuliko taifa lake.

David Zacharia Kafulila anatoa mfano wa nchi kubwa kama Marekani na Uchina zikiwa nchi wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania pamoja na nchi nyingine zaidi ya 166 kumuuliza Tundu A. Lissu kuwa nchi zote hizi Mahakama zao zinaingiliwa kama ilivyo kwa Tanzania ama ni utaratibu tu wa hiari wa kiusuluhishi uliowekwa Duniani katika kuoneaha imani kwa wawekezaji hasa wa nje?

Hoja ya David Zacharia Kafulila kwa Tundu A. Lissu ni kwamba kama Tanzania Mahakama zake siyo huru ndiyo sababu kesi za migogogro ya kibiashara zinafanyikia nje kwenye tume hii ya ICSID. Je, Marekani na Uchina ambazo nazo kesi zao za migogogro ya kibiashara zinafanyikia huko huko ICSID tulikopelekwa sisi kwa hoja ya hiyo ya Lissu anataka tuamini pia kuwa Mahakama za mataifa haya pia haziko huru?

" Lissu acha kuzipaka matope Mahakamani za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa ?"

View attachment 2433362View attachment 2433363
Bahati nzuri mimi niliusikiliza huo mjadala wa TL na wenzake huko Club House (nitaweka link hapa)..

Lakini ni bahati mbaya kuwa Kafulila hata hajamwelewa Tundu...!!

JIBU KWA SWALI LA KAFULILA NI HILI:

Ni kweli USA na CHINA ni wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania na nchi zingine 165 duniani...

Lakini ni ukweli pia kuwa, CHINA na USA mahakama zao haziingiliwi na serikali zao kama ilivyo kwa mahakama za nchi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania...

Aidha mikataba ya kimataifa (International bilateral agreements), mwekezaji mwenye mgogoro na serikali husika, ana uhuru akiona inafaa (hasa kwa kigezo cha uhuru wa mahakama ktk nchi husika) kusuluhishwa na mahakama za ndani au kwenda straight huko ICSID...

Kwa kigezo hiki, ndiyo Lissu akasema, kwa Tanzania ambapo mahakama zinafanya kazi kwa kuangalia interests za mtawala (serikali), hakuna mwekezaji aweza kuziamini mahakama zetu hata huyo Jaji au hakimu akampa haki mwekezaji ku - seize mali za serikali kama inavyofanyika huko ICSID...

Kwa lugha rahisi, ni kuwa, TL alimaanisha hakimu au Jaji wa mahakama hawezi kuhukumu against serikali...!!
Zipo Kesi kibao Tanzania tumebwagwa na wawekezaji humu humu ndani,

Ni kweli...

Na pale iliposhindwa serikali, hukataa kutekeleza hukumu hiyo...
 
Wasalaam wana wa Mungu.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Zacharia Kafulila, amekosoa kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu A Lissu kuhusu hoja ya kesi ya kukamatwa kwa Ndege na zingine mashauli yake kushughulikiwa kwenye Mabaraza ya Usuluhishi ya kibiashara kama ICSID- international Center For Settlement of Investment Disputes.

====

Akikosoa kauli hiyo, David Zacharia Kafulila amenukuliwa kwenye mtandao wa tweeter akiandika haya " Sitaki kujadili suala la kesi, naomba nijadili suala moja tu la uelewa kuhusu ICSID na Uanachama wake kwani Tundu A Lissu amepotosha katika hilo na huenda akawafanya wasiofahamu kuamini kwamba Tanzania ni mwanachama wa ICSID kwa Sababu ya Udhaifu wa Mahakama na Serikali ya Tanzania katika kusimamia Uhuru wa Mahakama.

Tundu A Lissu alinukuliwa kupitia ClubHouse akieleza kuwa " Lazma ieleweke kuwa sababu ya mashauri haya ya mikataba baina yetu na kampuni za nje kushughulikiwa kwenye mabaraza haya ya usuluhishi wa migogoro ya biashara na uwekezaji kama ICSID inatokana na tabia ya Serikali yetu ikiwa chini ya JPM na hata Samia kuingilia mambo ya mahakama na hivyo mahakama kukosa uhuru. Hivyo mahakama zetu haziaminiki, serikali yetu haiaminiki, hatuaminiki kwasababu ya rushwa za majaji na kuingiliwa na Ikulu. ndio sababu mashauri haya yanamuliwa ICSID "

Tundu A. Lissu ambae ni M/kiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na aliyekuwa Mgombea wa Urais wa JMT aliyepata kura kiduchu sana katika Uchaguzi Mkuu uliyopita wa 2020, ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Siasa pekee ambaye familia yake yote ni Raia wa Marekani ameonekana mara zote kuwa upande wa mataifa ya nje kuliko taifa lake.

David Zacharia Kafulila anatoa mfano wa nchi kubwa kama Marekani na Uchina zikiwa nchi wanachama wa ICSID kama ilivyo kwa Tanzania pamoja na nchi nyingine zaidi ya 166 kumuuliza Tundu A. Lissu kuwa nchi zote hizi Mahakama zao zinaingiliwa kama ilivyo kwa Tanzania ama ni utaratibu tu wa hiari wa kiusuluhishi uliowekwa Duniani katika kuoneaha imani kwa wawekezaji hasa wa nje?

Hoja ya David Zacharia Kafulila kwa Tundu A. Lissu ni kwamba kama Tanzania Mahakama zake siyo huru ndiyo sababu kesi za migogogro ya kibiashara zinafanyikia nje kwenye tume hii ya ICSID. Je, Marekani na Uchina ambazo nazo kesi zao za migogogro ya kibiashara zinafanyikia huko huko ICSID tulikopelekwa sisi kwa hoja ya hiyo ya Lissu anataka tuamini pia kuwa Mahakama za mataifa haya pia haziko huru?

" Lissu acha kuzipaka matope Mahakamani za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa ?"

View attachment 2433362View attachment 2433363
Kafulila endelea na kuwakosoa Hawa Wamarekani
 
Nchi ambayo haina BIT mwekezaji akienda huko anashauriwa kuwa na MIGA

mwekezaji akienda huko anashauriwa kiwa na MIGA
Mkataba wowote una kipengele cha nini kitafanyika pakitokea disputes. Ili kuepuka kukimbilia Mahakamani, mikataba inasema hatua ya kwanza ya kuresolve disputes ni arbitration na taasisi itakayosimamia. Mara nyingi kwenye mikataba ya ujenzi ya hapa nyumbani taasisi inayotajwa ni NCC. Kwenye mikataba ya kimataifa mara nyingi taasisi inakuwa ICC. Ila kama dispute ni kati ya mwekezaji na serikali, taasisi inayohusika ni ICSID. Sina uhakika kama inakuwepo kwenye mkataba ila nadhani mwekezaji mgeni yeyote ambae anaona hajatendewa haki na serikali mwenyeji ambayo ni signatory ana haki ya kupeleka mashtaka ICSID.

Amandla...
 
Mkataba wowote una kipengele cha nini kitafanyika pakitokea disputes. Ili kuepuka kukimbilia Mahakamani, mikataba inasema hatua ya kwanza ya kuresolve disputes ni arbitration na taasisi itakayosimamia. Mara nyingi kwenye mikataba ya ujenzi ya hapa nyumbani taasisi inayotajwa ni NCC. Kwenye mikataba ya kimataifa mara nyingi taasisi inakuwa ICC. Ila kama dispute ni kati ya mwekezaji na serikali, taasisi inayohusika ni ICSID. Sina uhakika kama inakuwepo kwenye mkataba ila nadhani mwekezaji mgeni yeyote ambae anaona hajatendewa haki na serikali mwenyeji ambayo ni signatory ana haki ya kupeleka mashtaka ICSID.

Amandla...
Kipengele kinakuwa Diplomatic mwekezaji anakwenda kwenye ubalozi wake Tanzania balozi anajaribu kuwasiliana na wizara ya mambo ya nje.Wizara yetu ya mambo ya nje ilikuwa ya ajabu sana kwani nchi nyingi zilijaribu kuwasiliana nao lakini wakawa na dharau .Baada ya miezi sita mwekezaji anaambiwa na nchi yake aende The Hague akatafute haki yake usilaumu wawekezaji wengi ni wazalendo sana na wanajua ufedhuli unaofanyika Tanzania
 
Back
Top Bottom