Kafulila: Lissu acha kuzipaka matope Mahakama za Tanzania, unataka kutuambia US & China ambao nao ni wanachama wa ICSID Mahakama zao zinaingiliwa?


Kesi zilizopo na zilizotatuliwa tayari, ni za nchi mbali mbali.

Lissu ana audience yake, arbitration ni sehemu ya ADR (Alternative Dispute Resolution) hizi private hearings, run by industry experts.

ADR mara nyingi huwa zipo kwenye mkataba (through stabilisation clause) ikitokea mgogoro kuna maelewano ya pande mbili wapi ukapatiwe ufumbuzi.

Mtu kama Lissu keshajua kuna bozzos chochote anachosema wanaunga mkono na kutetea bila ya hata wao wenyewe kujiongeza.
 
Mbona mmetaka ziwafukuza akina Halima mmegonga Mwamba?

Eti Mnataka Rais atoe maelekezo mahakamani hili halipo.

Mahakama zetu ni huru sana.
Chadema imeomba Mahakama ipi iwafukuze wakina Halima? Na iwafukuze kutoka wapi?

Amandla...
 


Mwingine huyo hapo anataka kulipwa fidia ya $95 million, sasa ukiwa google arbitrators waliochaguliwa utaona ni industry experts na haya mambo ni private.

Jamaa kazi yake kuwalisha matango pori wafuasi wa CDM ambao wameamua kumuabudu gullibly.
 
Hoja ya Kafulila ni ya upeo mdogo.

1) Haelewi nani walianzisha mahakama hiyo

2) Haelewi kwa nini ilionekana kuna haja ya kuanzisha mahakama hiyo

Ukweli ni kwamba ilianzishwa baada ya kuonekana katika baadhi ya nchi ni ngumu sana kushughulikia migogoro ya biashara hasa pale inapokuwa ni dhidi ya Serikali kwa sababu katika mataifa hayo, Serikali inaweza kuingilia maamuzi yoyote yale.

Sasa ili wawekezaji wawe na uhakika wa uwekezaji wao au biashra zao kutoingiliwa na maamuzi ya uonevu yanayofanywa na Serikali na watawala, nchi inatakiwa kuwa mwanachama wa chombo hiki, ili iweze kushtakiwa na kuhukumiwa inapoenda kinyume.

Hizi sheria zetu za ajabu ajabu eti ukitaka kuishtaki Serikali kwanza upate kibali cha Serikalu, utaweza kweli kuishtaki Serikali na upate haki yako dhidi ya Serikali? Jibu ni hapana. Kwa hiyo maelezo ya Lisu ni sahihi kabisa, maana ndiyo lengo lililokusudiwa. Hii ina maana kama kampuni au mtu anaenda kuwekeza kwenye huzu Guchiro republics, na hizo nchi siyo mwanachama wa chombo hiki, unafanya hivyo at your own risk.
 
Rais juzi akiongea na mawakili wa Afrika mashariki alusemaje?

Kwamba nyie tumieni sheria zenu za nje mie nita tumia sheria zangu kuhakikisha.

Huu ndio ushahidi kwamba mahakama zetu ziko mikononi mwa dola. Na haziko huru.
Sahihi kabisa. Sisi ni Nguchiro republic. Hatuna mahakama wala bunge. Kila kitu kimo mikononi mwa Rais.

Nani mwekezaji makini mwenye akili atawekeza kwenye nchi kama hii ya kwetu, kama tysingekuwa wanacha wa ICSID, wakati anajua kabisa kwamva, ndani ya nchi hatuna mfumo wa mahakama ka mhimili. Mahakama na bunge vipo kama idara za ikulu.
 
Arbitrations sio mahakama za kawaida which sits all year round. Hizi zinaitwa ADR na hearing ni private.

Uwezi kwenda kujifungulia tu case lazima iwe sehemu ya makubaliano ya mkataba. Sasa mkataba sio lazima uwe expressed ata unapoingia bilateral trade agreement ikisema mgogoro na wawekezaji wao utatatuliwa on neutral ground hapo umewapa wawekezaji uhalali wakukufungulia case arbitration yeyote. Ndio kama hao wa Swedes wamepata uhalali huo wakufungua kesi kunatokana na bilateral trade na Tanzania iliyopo.

For arbitration to be legal binding inabidi nchi zijiunge (voluntary) ili kuweza kutekeleza maamuzi yake na sio zote zimejisajili na arbitration zote. Ndio maana South Africa waliachia ndege ya ATCL kwa sababu hawakuwa wanachama wa arbitration iliyotoa maamuzi ya case husika, jamaa wakakimbilia Canada.

Surely haya mambo dispute resolution processes na contract law wanafunzi wa business management and other disciplines other than law wanafundishwa huko UDSM, it is basic knowledge kwenye dunia ya biashara maana huyo Lissu huko anajiropokea tu.
 
Kafulila jitahidi pia kuangalia upande wa pili kwani maisha sio siasa tu kwani hata Hapi ameamua kuingia ktk kilimo.
Ukweli humweka mtu huru na mtu huru huaminiwa kwa hoja zake kwani sio za kuokoteza kwa kuwa ndo fani yake.
 
Yan huyu Tumbili badala ya kushauri serikali ilipe deni anakimbilia kum attack Lissu ili akumbukwe tena kwenye uteuzi, Chawa pro max pumbavu kweli
 
Unachanganya mambo. Suala la arbitration linawekwa kwenye mkataba na taasisi itakayokubalika na pande zote mbili. Bila kipengele hicho wawekezaji hawatii saini.

Amandla...
 
Lissu sio mtu mzuri.

Kwanza yeye watoto wake sio Watanzania.

Hata Kama atatupiganisha tukauana yeye na familia yake atabaki kuwa salama.

Tumwogope kabisa Huyu mtu kwa usalama wa Taifa letu.

Asante Mzalendo Kafulila.

Watu wengi wa tanzania unaowaamini hawana uraia wa Tanzania

Siku ukija kuwajua hutoamini macho yako, huyo lisu ni mmoja Kati ya 200+ ambao watoto wao au wao wenyewe ni raia wa inchi zingine na niviongozi wetu


Na mwingine katumbuliwa juzi Tu hapa
 
Lissu huyu huwa simwelewi kabisa

Huwezi kumwelewa kama anazungumzia kitu usichokifahamu au usichokikubali au ukiwa na chuki nae.

Ni mara nyingi chuki au kutokubalika vimekuwa ni sababu za kutochaguliwa watu wenye mawazo tofauti - sio lazima mawazo hayo tofauti yawe mabaya!!
 
Huwezi kumwelewa kama anazungumzia kitu usichokifahamu au usichokikubali au ukiwa na chuki nae.

Ni mara nyingi chuki au kutokubalika vimekuwa ni sababu za kutochaguliwa watu wenye mawazo tofauti - sio lazima mawazo hayo tofauti yawe mabaya!!
Pumzika mkuu, Usiku huu
 

Wewe ndio unalisha watu matango pori. Hiyo sio private entity ni entity inayotmbulika under international dispute resolution ndio maana kabla ya Magufuli kuingia Investment Act iliitambua hiyo mahakama, na Tanzania ni mwanachama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…