Kagera (Bukoba) mahali pa ovyo kuwahi kutembelea

Sema huna hela kilaza wewe kwa maana mwenye hela zake anajua wapi pa kulala na huwezi ona anakuja hapa kuandika kwamba nawaza pa kulala.

Hivi mpaka sasa bado unasimama na takwimu za NBS ambayo wakusanya takwimu wao ni wale tulioonyeshwa kwamba walikuwa wanajaza takwimu wanazozijua wao kwenye madodoso waliyopewa wakiwa vyumbani mwao wakati wanafanya utafiti wa matumizi ya kaya binafsi?

Kwanza unajiita Econometrician ikimaanisha una uelewa wa uchumi na takwimu sasa twambie kutokana na takwimu hizo za NBS ni variables zipi zilitumika kujustify hilo. Takwimu ni takwimu tu lakini kuzichambua na kuzielewa ni kitu kingine kabisa na hapo ndipo unakutana na hizo mambo za sijui NBS imesema, n.k.

Mwaka jana nilishiriki kwenye kisemina fulani cha utoaji wa matokeo ya sensa na matumizi yake kwa baadhi ya maeneo ambayo walikuwa wametoa matokeo.

Ni kwamba hata watumishi wa NBS wenyewe hawaelewi hizo data wanazotolea matokeo zina maana gani na zinatumikaje kwa sababu wawasilisha taarifa yapo maswali waliulizwa lakini wakashindwa na wakaishia kutwambia takwimu zipo hivyo kama zilivyo hivyo tusihoji sana.

Kuna tafiti za matumizi ya kaya binafsi ambayo yanaonyesha watu wa mkoa X wanatumia pesa kununua kila hitaji la nyumbani kutoka dukani na watu wa mkoa Y wanapata mahitaji yao shambani moja kwa moja kwa asilimia 90 na 10 ni kutoka dukani. Ukiwaangalia hawa matumizi yao ya pesa ni tofauti kabisa lakini matokeo ya NBS yanakwambia wapo kwenye kapu moja na kwamba anayepata mahitaji yake kutoka dukani kwa asilimia 10 tu ni maskini wa kipato ukilinganisha na anayepata mahitaji yake kutoka dukani kwa asilimia 100 bila kutwambia spendings zao kwenye maeneo mengine zikoje kutokana na savings wanazozifanya
 
Mshikaji wangu alibahatisha mmoja wife material kabisaa tukiwa chuoni, first year mpaka tuna maliza had now wako wote, na alimkuta sealed, ni zaid ya five years, mshikaji wangu pale kapata mtu kweli kweli, ni bahati pia.
Sio kweli kwamba Wairaq wote ni wahuni
 
Ukiingia sehemu za watu jitahidi sana upate uyaelewe maeneo kabla ya kukurupuka kuandika unachodhani ni sahihi kwa kila mtu.

Kwahiyo wewe ulitegemea tofali iuzwe shilingi ngapi kama saruji inauzwa 24,000? Hata elimu ya biashara huna achilia mbali kuifanya hiyo biashara. Pale kilimanjaro kuna kiwanda cha saruji na ipo karibu na tanga lakini tofali linauzwa hadi 1,800 wakati saruji ni 14,000 hadi 16,000 kutegemea na eneo sembuse huko? Kwahiyo kuwa jirani na geita, katoro au chato ni justification au sababu ya kuwafanya hao wauza tofali nao wauze kwa 1,000 au 1,200? Maskini wa fikra na akili wewe.

Unataka kuuza kwa 1,200 hata 1,000 anzisha project yako, tafuta wateja wauzie wala usisingizie watu. Kama bidhaa yako ina ubora watanunua kama haina huwezi pata wateja na ndiyo utakuja na haya uliyoandika hapa.

Kwanza unatakiwa kujua kwamba wao wanajenga sana tena sana kwa kutumia tofali za kuchoma na watu wanauza kwa 200, 300, 500 na 600 na wote wanauza tofali zao kwa wateja wao na huwezi sikia ulichokiandika hapa eti anzisha kiwanda uuze 1,200 wakuue. Kiazi mkubwa wewe.

Wewe sema bidhaa yako ilikataliwa kutokana na ubora hafifu na sasa unatafuta sababu ya kufichia aibu yako huku washindani wako wakipeta na kuuza tu bila shida yoyote.

Ulijiuliza au uliuliza ni kwanini majengo yao mengi yawe ya serikali au watu binafsi wanatumia sana tofali za kuchoma zinazouzwa kati ya 300, 500 au 600 ambazo zinahitaji saruji nyingi wakati wa kuzijengea?
 
Endelea kushangaa kwa maana ulijibeba na mentality ya huko ulipotoka.
Ni simple tu na hiyo ni fursa kwako ingia sokoni tafuta mfanyabiashara mdadisi na tengeneza mahusiano ya kibiashara ili nawe uanze kuagiza zinakotoka kwa bei chee uje uuze kwa bei kubwa. Sasa ukifika kule kwa kina mangi si utalia kabisa na kuja kutwambia umelala njaa?

Suala la usafiri wa bajaji kwa mji kama wa bukoba siyo sehemu yake sana na wanaofanya hawategemei hizo bajaji pekee. Movememt ya watu ni kupanda na kushuka vilima vilovyozunguka huo mji na kwa kiwango kikubwa watu hawakai hapo kati wao wanaita bondeni. Labda kwa sasa ambapo wamepunguza mwinuko wa barabara ya uganda inaweza wezesha bajaji kuongezeka upande wa hiyo barabara kuelekea rwamishenye. Vinginevyo bajaji zingekuwa zinaokotwa chini kwa kushindwa kupanda milima sababu hata magari kuna wakati wanashindwa kupanda.

Bodaboda ni usafiri namba moja na wenyeji hawalalamiki zaidi ya wa kuja lakini utashangaa unaenda mwendo mrefu anakucharge 1,500 au 2,000 wakati ungekuwa mikoa mingine kwa umbali sawa na huo ingekutoka 3,000 au 4,000. Ukitafiti utapata majibu ni kwanini daladala ziliondoka mjini na kusalia za kutoka mjini kwenda vijijini au wilaya jirani.

Kuna maeneo kama bugabo kuna daladala zinaenda huko kutokea mjini kwa 2,000 au 3,500 lakini watu wengi wako tayari kupanda bodaboda kwa 7,000 au 10,000 ila si kusubiri hiyo daladala ijae au iende inasimama kujaza abiria tena kwa kusimama.
 
Mkuu merckme nimejaribu kupitia majibu Yako Kwa Kila alieandika kwenye huu uzi na muandiko wako unasema mengi na ya Ziada kuliko maandishi Yako. Nikupongeze Kwa Kila herufi Yako iliyodhihirisha niliyoyaandika...... JIREKEBISHENI au Bakini na Ujinga wenu
 
Upo sahihi sana. Kimsingi mtoa mada ni mshamba tu. Asiyejua kutofautisha na kubadilika kutokana na mazingira
 
Kwa hiyo na takwimu za uchumi wa mkoa wenu huwa anaandaa yeye!
 
Hehe nimesoma yote, nahisi upo kwenye hamashauri za bukoba, pole sana kaka. Hapo kwenye halmashauri ndo kwenye kitovu cha huo ukabila. Sababu humo kunq comprise wazee wa baraza ambao ni typical wakabila. Anyway nimewahi kuwa na rafiki wa kihaya kipindi tupo chuo. Nlichelewa kugundua kuwa jamaa alikua rafiki kwangu sababu ya umaterial issues. Kwa maana alitamani kuwa karibu yangu sababu ya resources nlizonazo, nlipozipoteza zile resources nlihisi angekua mtu wa kumtegemea .. ooh.. bojo ndo alikua mtu wa kwanza kuzungusha maneno kwamba nimefulia nimeuza gari, nauza vitu vya ndani .. asivokua na aibu nliporudi kwenye game at a higher profile than before jamaa akawa anansumbua nkam ignore. Point of reference ni kwamba bora marafiki wachagga wanajua kuwa na staha wanapomshobokea mtu ili wapate kitu ila sio wahaya man.
 
Ni mtu wa kusikiliza akili za wengine sio kutumia za kwake...ndo maana anashindwa kuadapt.
Bukoba ukiachana na siasa...mengine ni kawaida tu....ni kutafuta gape na kuanzisha biashara.
Watu kama hao ni kutowajibu. Maana wana akili ndogo
 
Kwa kiasi fulani ulichoongea kina ukweli,lkn changamoto huwa hazikimbiwa kaka bali unakabiriana nazo,, penye uzito kuna wepesi,,mlango mmoja ukifungwa fungua mlango mwingine hapo hapo,,nilikuwa hapo kipindi fulani,kuna jamaa alipigwa vita sana lkn hakukata tamaa,anatokea huko kaskazini,nadhani wajua hawa jamaa wanavojua biashara,kwasasa anaendelea vyema na tanpoint yake,ametanuka,na kawafanya wenyeji waamke mapema kufungua biashara zao,maana walizoea kuamka hadi saa nne ati mtu ndo anafungua duka lake!!
Supermarket ilikuwa ni fidodido tu ya wahindi fulani,kwa sasa hata wenyeji wamefungua zao, midomo imefungwa watu wamechangamka sasa,majungu yanapungua japo kwa taratiibu sana.
 
Kaka nakuelewa sanaaa ila Kwa tunao jitafuta hii Sio sehemu sahihi kuwepo
 
Wasamehe bure tu - udongo uliowaumba ulikuwa wa mwisho mwisho
 
Umemfafanulia vyema mkuu. It seems ana matatizo makubwa kuliko hata hao anaowaita mashetani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…