Kagera: Watoto 10 wamefariki na 6 kujeruhiwa baada ya shule Msingi Islamic Byamungu kuwaka moto

Kagera: Watoto 10 wamefariki na 6 kujeruhiwa baada ya shule Msingi Islamic Byamungu kuwaka moto

Huu ni ubaguzi ndugu yangu, Natamani ufute hii msg yako
Mkuu sikubaliani na wewe. Kuna trend kubwa sana ya shule za kiislam kuungua moto huko Dar, Same na sasa Bukoba. Why shule za kiislam tu? Kila siku chanzo cha moto wanasema hakijulikani. Walichoma za wakubwa baada ya kuona wengi wanajiokoa wameamua kuhamia za watoto. Hili jambo sio la kuupuzwa. Serikali ikae na makundi yote ya kiislam kuona kuna nini kati yao. Inauma sana kupoteza watoto kizembe namna hii.
 
Mbona shule za kiislam tu?
Kuna kitu nyuma ya pazia sio bule.
 
Mkuu sikubaliani na wewe. Kuna trend kubwa sana ya shule za kiislam kuungua moto huko Dar, Same na sasa Bukoba. Why shule za kiislam tu? Kila siku chanzo cha moto wanasema hakijulikani. Walichoma za wakubwa baada ya kuona wengi wanajiokoa wameamua kuhamia za watoto. Hili jambo sio la kuupuzwa. Serikali ikae na makundi yote ya kiislam kuona kuna nini kati yao. Inauma sana kupoteza watoto kizembe namna hii.
Kwenye Uislam ikhtilafu zipo nazo ni za kimitizamo ya kielimu. Hizi ikhtilafu zipo tangu kipindi cha Maswahaba mpaka sasa na wala haikuwa na haijakuwa sababu ya kutoana roho ama kuleta maangamivu.

Tunatofautiana mitizamo ya kihoja kielimu kama vyanzo ama Taasisi nyengine zinavyotofautiana kihoja kuhusu masuala ya kielimu.
 
Kwenye Uislam ikhtilafu zipo nazo ni za kimitizamo ya kielimu. Hizi ikhtilafu zipo tangu kipindi cha Maswahaba mpaka sasa na wala haikuwa na haijakuwa sababu ya kutoana roho ama kuleta maangamivu.

Tunatofautiana mitizamo ya kihoja kielimu kama vyanzo ama Taasisi nyengine zinavyotofautiana kihoja kuhusu masuala ya kielimu.
Andika kiswahili basi mkuu. Samahani lakini.
 
Watoto 10 wamefariki na sita kujeruhiwa vibaya kufuatia moto ulioteketeza bweni la wavulana shule ya Msingi Islamic Byamungu iliyopo Kyerwa Mkoani Kagera. Hadi sasa chanzo moto huo hakijajulikana.

Watoto waliopoteza maisha ni wa umri wa miaka sita hadi 12.

Taarifa zaidi inakuja...


Wanafunzi 10 wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa baada ya bweni la shule yao ya Byamungu English Medium Primary School iliyoko wilayani Kyerwa kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo.

Jumla ya wanafunzi 74 walikuwepo kwenye bweni hilo ambalo chanzo cha moto hakijajulikana

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti amesitisha shughuli za malazi katika shule hiyo kwa muda.’’ Nachukua hatua nyingine za ziada, hatua ya kwanza na ya awali kabisa tunasitisha huduma za malazi katika shule hii watoto wote waliokuwa wakilala katika huduma ya hosteli au bweni huduma hiyo sasa imesitishwa mbaka itakavyoelekezwa vinginevyo’’, amesema Brigedia Jenerali Marco Gaguti alipotembelea eneo la tukio.

Amesema Sambamba na ameelekeza kamati za usalama za ngazi zote kataika mkoa wa kagera kufanya mapitio upya ya shule zinazotoa malazi, kuhakiki kwamba shule hizo kama zinavyo vibali halali vya serikali na ubora wa majengo yanayotumiwa na wanafunzi, na kuangalia mifumo ya uzimaji moto na kujiokoa inapo.

Amesisitza kuwa kama sifa hizo hazitakua zimekidhi basi hatua zichukuliwe za kufungia huduma hizo katika shule husika.

Awali Mwenyekiti wa kijiji Bw. Munaraka Muhammod aliwaomba watu walioko katibu na Itera wafike kusaidia kuuzima moto huo uliowaka kuanzia jana usiku .

Chanzo za ajali baado hakijajulikana.



Innalillahi wainna ilayhi rajiuun
 
R.I.P wadogo zetu... Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un [emoji120]
 
Shule za kiislam na Moto kulikoni? Mola wape pumziko la heri watoto hao.
 
apa tusi chengeshe maneno hapa, ni Dhahiri kabisa hujuma inahusika hapa na hii si sawa hata kidogo
 
Tatizo lipo kwa wamiliki na serikali kwani lilitolewa agizo kwa shule zote kununua vifaa vya tahadhali ya majanga ya moto na vifaa hivyo vinauzwa bei rahisi inaonekana hiyo shule haikununua hivyo vifaa na pia serikali haijafanya ukaguzi kuhakikisha kama shule zote zimetekeleza agizo lake.
Nawapo pole wote waliofiwana kupoteza mali zao.
 
KWANINI SHULE ZA WENZETU ZINAUNGUA KIASI HIKI?!! WAPENDWA SOTE TU WATANZANIA, TUSIKAE KIMYA KUHUSU HILI TUNAHITAJI TUME KUCHUNGUZA KUNA NINI NDANI?! HAIWEZEKANI HILI, MACHUNGU YA KUZAA KUSOMESHA HALAFU MWANANGU ANAKUFA KWA UZEMBE HILI HAIWEZEKANI INAUMIZA SANA SANA SANA..FIKIRIA UWE WEWE MWANAO NDO AFARIKI KWA NAMNA HII OHOOO JAMANI JAMANI JAMANIII[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji2367]
Kamati ipo ila sijui inakwama wapi kutujulisha sababu ya moto katika shule hasa za kiislamu
Maana haiwezekani iwe ajali za kawaida, sasa sijui wanasubiri nini kuwakamata watuhumiwa
 
Poleni Sana Kwa Msiba.
Majeruhi Wapone Haraka
 
Mkuu sikubaliani na wewe. Kuna trend kubwa sana ya shule za kiislam kuungua moto huko Dar, Same na sasa Bukoba. Why shule za kiislam tu? Kila siku chanzo cha moto wanasema hakijulikani. Walichoma za wakubwa baada ya kuona wengi wanajiokoa wameamua kuhamia za watoto. Hili jambo sio la kuupuzwa. Serikali ikae na makundi yote ya kiislam kuona kuna nini kati yao. Inauma sana kupoteza watoto kizembe namna hii.
Hoja za waislam kutofautiana zipo lakini hii ipo beyond na tofauti za kiimani
 
Back
Top Bottom