Iq yako ni ndogo kuliko mchangaUnamwamuru Mungu chakufanya?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Iq yako ni ndogo kuliko mchangaUnamwamuru Mungu chakufanya?
🤔 ni wapi hapo?Kahama fresh
Hayana Bima na unakuta Dereva hana Leseni na hizo kuni pia zimevunwa kiwizi.Matrekta naona Kama yamesahaulika yapo mengi sana barabarani na mengi ni mabovu
tunaomba takwimu kwanza ya waganda,barabara na idadi ya traffic ili tulinganishe na hili dude letu lenye maelfu ya kms,maelfu ya magari na malaki ya watumiaji wa vyombo,tabia zetu waafrica zinafanana.Uganda walitimua askari barabarani wakabaki wa kuhesabu mmoja mmoja tu lakini suala la ajali ni kitendawili.
Zambia unaweza kutembea kilometers 500 usikutane na askari barabarani zaidi ya watu wa uhamiaji tu na hakuna ajali za kizembe kama hapa kwetu wanapolundikana traffic kila baada ya kilomita 3.
Elimu kwa madereva na wasafiri kwa ujumla ndiyo inaweza kupunguza ajali.
Ama itumike njia ya artificial intelligence ambayo itawaondoa traffic wote barabarani kwakuwa mfumo haudai rushwa kama hawa viumbe.
Kweni huwa kuna Trafiki usiku wa manane.Kinana kashasema trafick watolewe barabarani haya ndio wanayataka Acha tuvune tulichopanda juzi nimepanda basi NBS Kutoka Tabora mpk dodoma basi halijasimamishwa ili hali lilijaza watu sana.
Pole sana chief[emoji22]So sad,hii ajari imesababisha kifo cha mdogo wangu kwenye hiyo IST,laiti ningemkamata dereva wa hilo trekta,ningemtatua malinda bila kalainishi.
Inaonekana mtu wa hiace Alikua speed 100+. Km/hrHiace ilikua imebeba watu 31.
Mpaka mchana huu wamekufa 17 (mwingine kaongezeka asubuhi hii saa nne).
Ambao wanapumulia mashine ni 14.
Mabasi ndio huwa yanavunja sheria zote za Barabarani tena mbele ya Traffic police.madereva wanasahaugi kwamba wamebeba roho za watu
Huenda hata alikuwa 80 kph lakini labda hakuona ishara yoyote na huenda huyo mwenye Lori hakuwasha double hazzard au hata kumflashia taa ili dereva wa Hiace ashtuke.Inaonekana mtu wa hiace Alikua speed 100+. Km/hr
Hilo agizo halikuwa na tatizo lolote Trafiki polisi walikuwa ni kero Mabarabarani Kinana alikuwa sahihi.Polisi waache kuisikiliza CCM
Kinana akerwa na Utitiri wa Traffic barabarani. Atoa maagizo mazito kwa Afande IGP Camilius Wambura
Chanzo cha mapato traffic wa Tanzaniawww.jamiiforums.com
Mkuu hapakuwekwa viashiria vya ajali? Huenda boda alihisi ni majambazi mnataka kumteka na hzo tochi zenu!Inanikumbusha boda boda mmoja pale mapinga.
Kuna Lori la cement limetoka kushusha likagongana na gari la maji la afya.njia ikawa imefungwa na hayo magari.ilikuwa usiku sana.yule bwana na haraka zake yuko speed balaa watu wanammulika tochi lakini wapi.asikii Wala haoni akaenda kugonga ubavuni mwa gari la cement akalala juu .na kiuno akateguka.
Tuweni makini madereva mwendo kasi haufai
Sioni sababu kama wangefuata Sheria reflectors na taa zao za kwenye Trekta na Tela lake.Kwanza tractor zingepigwa maarufuku kutembea usiku
Hata kama polisi wakifanya patrol lakini hawawezi kuwa kila sehemu gari ilipoharibika kwa wakati. Gari inapoharibika, dakika tano tu ni muhimu sana.