Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.

Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.

Watanzania nani katuroga?

Ina maana hao ndio watu wa kwanza kuchuchumalishwa?

Mkuu au na wewe ulipewa marbolo yenye wekundu wekundu?

Ndio maana tunashuhudia viongozi wetu wanafanya mauaji hadharani na kupewa adhabu ndogo tu ya kulipa pesa kidogo ila kosa hilohilo akifanya mlalahoi adhabu yake ni kifungo cha maisha.

Watanzania tuna unafiki sana.

Nchi za wenzetu hawa jamaa washenzi na wale waliopokea magunia yaliyojaa pesa ilitakiwa wapigiwe risasi mbele ya watu mchana kweupe.

Tanzania sheria zipo kuwahukumu masikini sio matajiri.


Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts".

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.
Rejea
Utetezi wa kutetea haki za binaadamu humu jf, sikuanza leo, na wala siwatetei hawa kwa sababu ni matajiri, nimepigia kelele siku nyingi na haya chini ni mabandiko yangu kutetea haki
1. Bango la "Mwizi Mkenya!" Mlimani City ni Ubaguzi!, Udhalilishaji ...

2. Watetezi Wa Kweli wa Haki za Binaadamu Tanzania ni Kina Nani ...

3. Huu ni udhalilishaji wa Polisi kuwavisha mabango watuhumiwa ...

4. Anachofanya Waziri Mkuu, sio sawa, sio haki, sio good governance ...

5. Tukio zima la wachawi wawili waliodondoka na ungo huko kahama ...

6. ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional! | JamiiForums ...

7. Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo | JamiiForums | The Home of Great ...

8. Nini hasa maana ya utu? | Page 6 | JamiiForums | The Home of Great ...

9. Swali kuhusu ma-fumanizi, na reaction za wafumaniaji ...

10. Mchawi akamatwa jijini Dar na kuuawa baada ya kudondoka na ungo ...

11. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality ...

12. Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...

13. Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? | Page 2 ...

14. TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali ...

15. Chan. Ten:Inastahili Pongezi kwa "Freedom of Expression, Watangaza ...

16. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ..

17. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...

18. Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili .

19. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

20. Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki .

21. Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote .

22. Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

23. Naibu Spika Anna Makinda ni Dikteta! |

24. Je, Huu Sio Uvunjaji wa Haki Za Msingi za Binaadamu Unaofanywa na ...

25. Kutoka Geneva: Prof Mchome atoa msimamo kuhusu mpango wa ..

26. Je, Kila utumbuaji ni wa haki, au kuna kumkomoa Kikwete .

27. Kagoda: Kamwe haitafikishwa Mahakamani! | J

28. Kitendo Cha Rev. Mtikila Kugomea Arrest!, Kinastahili Pongezi ...

29. Wito kwa Baba *****: Watendee Haki Kina ***** Wote Ili Nao Wapate ...

30. Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu wali-teswa ...
 
Well said PASKALI. Hata mimi hii hali ya kuwafolenisha watuhumiwa ili wapigwe picha na maneno ya kifedhuli yanayotolewa na walinzi wetu wa amani, ni udhalilishaji mkubwa. Hao wazee wamekaa nao, wamewahoji, wamewaleta mahakamani; kulikuwa na haja gani kuwaamrisha wachuchumae? (Singh ndo alipiga goti kabisa). Kuna wakati mwingine askari magereza huwaleta mahabusu wakiwa wamefungwa pingu hadi ndani ya vyumba vya mahakama, na kuwafungua tu pale hakimu anapokaribia kuanza session.

Ni vema kutunza utu wa mtu hata kama ni mtuhumiwa!
MBONA HII AFADHALI KULIKO KUNYEA DEBE? UMESHAWAHI KUELEZWA KUONA AU KUSIKIA JUU YA HILI? MBONA LUPANGO ZA WENZETU HAWAFANYI HAYAA WANA VYOO VYA KIBINADAMU? WAHANDISI WETU WAMESHINDWA KUWEKA VYOO SALAMA
 

Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts".

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.
Rejea
Utetezi wa kutetea haki za binaadamu humu jf, sikuanza leo, na wala siwatetei hawa kwa sababu ni matajiri, nimepigia kelele siku nyingi na haya chini ni mabandiko yangu kutetea haki
1. Bango la "Mwizi Mkenya!" Mlimani City ni Ubaguzi!, Udhalilishaji ...

2. Watetezi Wa Kweli wa Haki za Binaadamu Tanzania ni Kina Nani ...

3. Huu ni udhalilishaji wa Polisi kuwavisha mabango watuhumiwa ...

4. Anachofanya Waziri Mkuu, sio sawa, sio haki, sio good governance ...

5. Tukio zima la wachawi wawili waliodondoka na ungo huko kahama ...

6. ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional! | JamiiForums ...

7. Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo | JamiiForums | The Home of Great ...

8. Nini hasa maana ya utu? | Page 6 | JamiiForums | The Home of Great ...

9. Swali kuhusu ma-fumanizi, na reaction za wafumaniaji ...

10. Mchawi akamatwa jijini Dar na kuuawa baada ya kudondoka na ungo ...

11. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality ...

12. Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...

13. Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? | Page 2 ...

14. TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali ...

15. Chan. Ten:Inastahili Pongezi kwa "Freedom of Expression, Watangaza ...

16. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ..

17. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...

18. Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili .

19. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

20. Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki .

21. Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote .

22. Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

23. Naibu Spika Anna Makinda ni Dikteta! |

24. Je, Huu Sio Uvunjaji wa Haki Za Msingi za Binaadamu Unaofanywa na ...

25. Kutoka Geneva: Prof Mchome atoa msimamo kuhusu mpango wa ..

26. Je, Kila utumbuaji ni wa haki, au kuna kumkomoa Kikwete .

27. Kagoda: Kamwe haitafikishwa Mahakamani! | J

28. Kitendo Cha Rev. Mtikila Kugomea Arrest!, Kinastahili Pongezi ...

29. Wito kwa Baba *****: Watendee Haki Kina ***** Wote Ili Nao Wapate ...

30. Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu wali-teswa ...

Umesema ya ukweli Paskali lakini tatizo kubwa watu hapa hawatakuelewa maana wewe ulikua mtetezi wao mkubwa huko nyuma hivyo watu watadhani kuna maslahi gongana japo unaloliongelea ni la kweli. Halafu pia umesahau uzi uliouandika juu ya fedha za ESCROW siyo za umma.
 
Watanzania nani katuroga?

Ina maana hao ndio watu wa kwanza kuchuchumalishwa?

Mkuu au na wewe ulipewa marbolo yenye wekundu wekundu?

Ndio maana tunashuhudia viongozi wetu wanafanya mauaji hadharani na kupewa adhabu ndogo tu ya kulipa pesa kidogo ila kosa hilohilo akifanya mlalahoi adhabu yake ni kifungo cha maisha.

Watanzania tuna unafiki sana.

Nchi za wenzetu hawa jamaa washenzi na wale waliopokea magunia yaliyojaa pesa ilitakiwa wapigiwe risasi mbele ya watu mchana kweupe.

Tanzania sheria zipo kuwahukumu masikini sio matajiri.
Nina wasiwasi ni akili yako
 
Paskali,

Tuache unafiki. Hebu niambie ni waTanzania wangapi wanaodharirishwa tena zaidi ya hao walioambiwa kuchuchumaa and no body cares?

Tuache huu unafiki. watu wamepiga kelele jinsi wafungwa/mahabusu wanavyokuwa treated, jinsi magereza yalivyo machafu but no body cares. hata sidhani kwenye bajeti kuna mbunge anasimama kuhoji magereza yanaendeshwa vipi. Leo singa singa ameambiwa achuchumae chini unaandika thread ndeefu kwamba amedharirishwa? Human rights zinakuwa human rights for the rich and stronger but not for the poor and the wretched of the earth? Si ndiyo?

Ngoja tusubiri tuambiwe kwamba inabidi wajengewe gereza lao maana yaliyopo ni machafu.

Kaka yangu Paskali, wazungu wanasema: If the society cannot protect the weak in its midst, what makes you think that they will protect the stronger when times come?

All I can say: Tupige kelele wee..lakini Magufuli anatufundishia watoto kitu kimoja muhimu sana (it may be late for me and you) kwamba CRIME DOESNT PAY! Tufanye kazi kwa bidii tule na kuridhika na tunachopata kwa halali. Mengine ni porojo.

Masanja
Mkuu chukua Kilimanjaro moja hapo ulipo kwa bili yangu.
 
Pascal Mayalla

Mvunja sheria/katiba mkuu ni huyo huyo umsifiaye humu kila uchwao na Taasisi nyingine zote zinajifunza kwake.

Imeonekana hiyo ndiyo style pendwa ya awamu hi, acha double standards.


Yaani unajisahaulisha kabisa dhalili mbaya zisizomithilika wanazofanyiwa watuhumiwa wamakosa mbali mbali?

Wale mashekhe wanateswa na kudhalilishwa kuliko kawaida lakini hadi Leo hii "uchunguzi haujakamilika", Wale Waliotajwa na Makonda kwenye hekaya ya "dawa za kulevya" (Yule unayetaka awe Rahisi ajaye baada ya pombe), Wabunge Wa Upinzani Wanadhalilishwa mno ndani ya Bunge yote hayo huyaoni.

Sizonje anataja taja majina ya watu hovyo hovyo huku akiwa "brand" hatia mbali mbali hata kabla hawajafikishwa mahakamani, hayo uliyafumbia macho sasa wameguswa wenye nazo umekurupushika kuleta "uzi gazeti" la kupinga udhalilishaji.



Tuvumilie hii ndio style pendwa ya awamu hii kila taasisi inatafuta "kiki".
 
Kaka Pasco , nimekusoma
Katika hili andiko lako iko hoja ya msingi ,ambayo kwa bahati mbaya watu wengi hawataiona . Hii inatokana na hisia mbalimbali ambazo zimejikita katika mioyo ya watu wengi kwa sasa. Katika kipindi hiki unapojaribu kukosoa jambo fulani lazima uwe makini sana , vinginevyo unaweza kuonekana unatetea wahujumu uchumi.

Lakini kuna kitu pia nimejiuliza. Je hii ni mara ya kwanza watu kupigishwa magoti pale Kisutu? .Mbona kumbukumbu zangu zinaonesha kuwa tabia hii wamefanyiwa watu wengi sana? , je kwa nini tulikaa kimya mpaka hawa matajiri wanapigishwa magoti?

Kaka Pasco huoni kwamba watu wanaweza kutafsiri kuwa tumeongea kwa sababu labda wapendwa wetu wameguswa na hii aibu?

Nataka kusema kuwa kwa mda mrefu sasa katika jamii hii kumekuwa na tabia ya watu kudhalilishwa tena mbele ya kamera za waandishi wa habari halafu hakuna mtu anayeshituka na kukemea udhalilishaji huo. Sasa imeanza kuonekana kumdhalilisha mtu ni ushujaa katika jamii hii.

Juzi tu tumeona matukio ya walemavu wakipigwa mbele ya kamera za waandishi wa habari , hakuna mtu aliyekemea hali ile. Leo katika jamii yetu imeanza kuonekana chuki ya wazi kabisa hata katika misiba . watu wanachukiana kwa kiwango ambacho hajiwahi kuonekana katika Taifa .

Hii tabia ambayo leo mimi nina nguvu naweza kufanya chochote haitasadia taifa hili hata kidogo. Kwa kipindi hiki tumeona baadhi ya watu ambao hapo awali walipokuwa na nguvu waliweza kufanya chochote dhidi ya wenzao. Lakini leo hii na wao yanawakuta yale yale waliyowafanyia wenzao kipindi wapo madarakani. Tujifunze kukemea uovu katika jamii tusisubili yatukute sisi kwanza ndio tuseme.
 
I felt heart sick nilivyoona Mzee Rugemalila akipiga magoti na rozari yake.

Hakuna asiye mdhambi, hakuna apendaye kudharirishwa. Hakuna mkamilifu.

Wakipatikana na makosa wahukumiwe ila si busara kuwadharirisha.
 
Mbona umewaona hawa tuu?wakiuliwa watuumiwa wa ugaidi upo kimya masheikh wanapigwa picha wanadhalilishwa mbele ya haki nyie kimya why hawa??
 
HIVI KWANINI MAGU HAMTEUI JUDGE MKUU. MWAKA WA PILI SASA. MAANA ULE NAO NI MUHIMIRI WA SERIKALI AMBAO UNATAKIWA KUWA NA KIONGOZI WAKE ILI KUSAIDIA CHECK AND BALANCE
 
Sasa Kama mawazo ya nchi yameshikwa Mabashite unategemea nini ? Tupo kwenye show off tukimaliza tutarudi kwenye code of conduct.

WEZI WEZI HATA KUWAUWA SAWA..HAWANA FAIDA
 

Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts".

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.
Rejea
Utetezi wa kutetea haki za binaadamu humu jf, sikuanza leo, na wala siwatetei hawa kwa sababu ni matajiri, nimepigia kelele siku nyingi na haya chini ni mabandiko yangu kutetea haki
1. Bango la "Mwizi Mkenya!" Mlimani City ni Ubaguzi!, Udhalilishaji ...

2. Watetezi Wa Kweli wa Haki za Binaadamu Tanzania ni Kina Nani ...

3. Huu ni udhalilishaji wa Polisi kuwavisha mabango watuhumiwa ...

4. Anachofanya Waziri Mkuu, sio sawa, sio haki, sio good governance ...

5. Tukio zima la wachawi wawili waliodondoka na ungo huko kahama ...

6. ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional! | JamiiForums ...

7. Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo | JamiiForums | The Home of Great ...

8. Nini hasa maana ya utu? | Page 6 | JamiiForums | The Home of Great ...

9. Swali kuhusu ma-fumanizi, na reaction za wafumaniaji ...

10. Mchawi akamatwa jijini Dar na kuuawa baada ya kudondoka na ungo ...

11. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality ...

12. Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...

13. Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? | Page 2 ...

14. TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali ...

15. Chan. Ten:Inastahili Pongezi kwa "Freedom of Expression, Watangaza ...

16. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ..

17. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...

18. Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili .

19. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

20. Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki .

21. Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote .

22. Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

23. Naibu Spika Anna Makinda ni Dikteta! |

24. Je, Huu Sio Uvunjaji wa Haki Za Msingi za Binaadamu Unaofanywa na ...

25. Kutoka Geneva: Prof Mchome atoa msimamo kuhusu mpango wa ..

26. Je, Kila utumbuaji ni wa haki, au kuna kumkomoa Kikwete .

27. Kagoda: Kamwe haitafikishwa Mahakamani! | J

28. Kitendo Cha Rev. Mtikila Kugomea Arrest!, Kinastahili Pongezi ...

29. Wito kwa Baba *****: Watendee Haki Kina ***** Wote Ili Nao Wapate ...

30. Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu wali-teswa ...

Paskali, utawala huu unavunja kstiba, sheria, taratibu and everything you can think of.. the list is endless!
It is a pity kuwa hata Mkuu akivunja hayo, watanzania tunashangilia!
 
Back
Top Bottom